Utata: Embe lisilo na kokwa!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Swali nawaulieni,
Magwiji mnijibuni,
Nimetingwa akilini,
Jibu sijalibaini,
Embe lisilo na kokwa, ni embe au kimbembe!?
 
Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.

Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamung'unywa kwa nidhamu,Kung'atwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe
 
Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.

Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamung’unywa kwa nidhamu,Kung’atwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe
we ni mubaya bana, unatisha, haya mm - mjibu huyu.
 
Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.

Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamung’unywa kwa nidhamu,Kung’atwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe

Naam!
 
Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.

Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamung’unywa kwa nidhamu,Kung’atwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe

He!! si haba, malenga wetu tunao humu, big up
 
heshima kwako mkuu,
mkuu usipo kokotoa hii shahiri mimi utakuwa umeniacha mbali sana
 
Babu yangu Mwanakijiji,katu usitingwe akilini
Watakuja wengi wajibuji,na majibu yaso kifani
Haihitaji kumpa mtu mji,ili upate jibu akilini
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Embe lisilo na kokwa,kamwe haliwezi tokea
Hata ukienda Rukwa,lenye kokwa watakuelea
Embe lilo na kokwa,vizuri mtini labembea
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Amani kweli umenena,kuhusu kokwa lilo laini
Kwa hakika umenikuna,kwa wako ubeti makini
Kokwa laini lililotuna,embe lake ni tamu jamani
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Embe lililo na kokwa,kwa nafasi linanyonywa
Laliwa pasi kumenywa,na maganda lameng'enywa
Hilo embe lisilo na kokwa,hata bure huwezi pewa
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe
 
Babu yangu Mwanakijiji,katu usitingwe akilini
Watakuja wengi wajibuji,na majibu yaso kifani
Haihitaji kumpa mtu mji,ili upate jibu akilini
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Embe lisilo na kokwa,kamwe haliwezi tokea
Hata ukienda Rukwa,lenye kokwa watakuelea
Embe lilo na kokwa,vizuri mtini labembea
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Amani kweli umenena,kuhusu kokwa lilo laini
Kwa hakika umenikuna,kwa wako ubeti makini
Kokwa laini lililotuna,embe lake ni tamu jamani
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Embe lililo na kokwa,kwa nafasi linanyonywa
Laliwa pasi kumenywa,na maganda lameng’enywa
Hilo embe lisilo na kokwa,hata bure huwezi pewa
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe

Mkuu kumbe nawe uko!, safi sana
 
Kuna embe nalo tamu, kwa ndani lajaa miiba
Lipo taangia adamu, muumba alipotuumba
Embe hili ni adimu, ukilipata watamba
Ng`ong`o nalo ni embe, naomba msisahau

Embe lisilo na kokwa, si tija wala wala kimbembe
Kwani vingapi vya kokwa, vyafaa kuitwa embe?
Halifai kwa kunyonywa, bali utapata shibe
Ng`ong`o nalo ni embe, naomba msisahau

Ni maarufu mtaani, Wajuvi wataliomba
Likizubaa mkononi, Wenzio wanalilamba
Likipakwa chumvini, Vidole utajilamba
Ng`ong`o nalo ni embe, Naomba msisahau

Wandugu muwe makini, na dodo chini ya mbuyu
lazima tilie walakini, usije okota kibuyu
zoazoa jalalani, muachie mbayu wayu
Ng`ong`o nalo ni embe, naomba msisahau
 
Malenga mmenishika,kusema japo kidogo
Kuna embe nakumbuka,nilitafuna kigogo
Kwa kweli nilistuka,japo sikua mdogo
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani

Kwa hamu nilivutika, kulitia mdomoni
Mkeka akatandika,mwenyeji wangu chumbani
Mkono akanishika,akanivuta kwa shani
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani

Hili embe lajificha,kulila siwe papara
Nlikula usiku kucha,tena sio la duara
Mwenzenu sipati picha,embe si masihara
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani?

Nlibaki nalitafuta,kokwale siku kucha
Ulimi nikauvuta,nikatumia na kucha
Mwenyeji akajivuta,akanipa lote bucha
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani
 
Swali nawaulieni,
Magwiji mnijibuni,
Nimetingwa akilini,
Jibu sijalibaini,
Embe lisilo na kokwa, ni embe au kimbembe!?


Mimi siyo mshairi
Kumshinda mshiiri
Vile yeye kasafiri
Kwa niaba nitakiri
Embe hilo siyo siri
Ukila uwe msiri
Embe lisilo na kokwa, si kimbembe ni embe.

Ninajua utabisha
Kwa niya ya kunitisha
Kuniita napotosha
Na akili kunichosha
Sihitaji kujikosha
Ukweli utakutosha
Embe lisilo na kokwa, si kimbembe ni embe.

Linapatikana Pwani
Kibandani si dukani
Halijawekwa juani
Limefichwa barazani
Lapewa ugredi wani
Usiniulize kwa nini
Embe lisilo na kokwa, si kimbembe ni embe.

Muuzaji mwenye nyumba
Apenda kugomba gomba
Ila usije yumba
Kwa hiyo yake kasumba
Usije sema waomba
Kwani ataanza gomba
Embe lisilo na kokwa, si kimbembe ni embe.

Nitampigia simu
Endapo italazimu
Vile ninamfahamu
Hawezi kuwa mgumu
Kumbuka yana msimu
Kuweka order muhimu
Embe lisilo na kokwa, si kimbembe ni embe.

Hutakiwi kuongeza
Moja litatosheleza
Vinginevyo kujikweza
Utajuta endekeza
Kiasi inapendeza
Hasa wakati wa kiza
Embe lisilo na kokwa, si kimbembe ni embe.

Sasa lini utakuja
Liandaliwe hilo moja
Onyo! Usijelifuja
Likageuka kioja
Embe moja kwa mmoja
Usije fanya ‘Umoja'
Embe lisilo kokwa, si kimbembe ni embe.
 
Malenga mmenishika,kusema japo kidogo
Kuna embe nakumbuka,nilitafuna kigogo
Kwa kweli nilistuka,japo sikua mdogo
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani

Kwa hamu nilivutika, kulitia mdomoni
Mkeka akatandika,mwenyeji wangu chumbani
Mkono akanishika,akanivuta kwa shani
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani

Hili embe lajificha,kulila siwe papara
Nlikula usiku kucha,tena sio la duara
Mwenzenu sipati picha,embe si masihara
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani?

Nlibaki nalitafuta,kokwale siku kucha
Ulimi nikauvuta,nikatumia na kucha
Mwenyeji akajivuta,akanipa lote bucha
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani

Kuuliza si ujinga, Ulilia Mkuranga?
Maana pwani kwa vibwanga, wanajua kuvipanga
Mzinga utauchonga, lapwani likishanoga
Si Dodo wala sindano, mwenzetu ulilokula

Chumbani si sebuleni, mgeni ulitengewa
Ukawekwa mtegoni, bila hiyana wanaswa
Taratibu safarini, katika kusaka kokwa
Si Dodo wala sindano, mwenzetu ulilokula

Mwenyeji kwa ujasili, mkekani makusudi
Embe lake kama mwali, pekeyo kakukabidhi
Kwa kucha pia ulimi, binamu ulifaidi
Si Dodo wala sindano, mwenzetu ulilokula
 
Back
Top Bottom