Namna ya kula embe dodo kistaarabu

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,680
59,799
EcUeyRbWsAIpgwJ.png


Embe dodo ni aina ya maembe ambayo ni matamu sana. Watu wengi hawajui namna ya kula tunda hili kwa raha na kistaarabu.

Leo katika uzi huu nitaeleza namna ya kula embe hili.

UTANGULIZI
Embe dodo linaweza kuliwa likiwa limeiva au likiwa bichi. Na wakati mwingine embe dodo likiwa bado changa linatumiwa kwa kutengeneza chachandu au mboga. Kwa upande wa matumizi ya chakula embe hili linamatumizi mengi sana.

Embe hili ukila kwa pupa unaweza uchajichafua mdomo au kuchafua nguo zako kabisa. Maana likia limeiva vizuri, embe hili huwa linatoa juisi nyingi. Kwa hiyo ukila kwa pupa unaweza kujikuta unachafuka bila sababu.

Uzuri nchi yetu ya Tanzania embe dodo linapatikana kila mkoa. Na kuna sehemu embe hili huwa linakuwa na nyuzi nyuzi nyingi. Kwa upande wa Afya nyuzi nyuzi hizi husaidia kusaga chakula tumboni.

Embe hili unaweza ukalila kwa kunyonya na baadae ukala maganda yake hakuna shida kabisa. Lakini unaweza ukalikata kata kwa kisu na kuweka kwenye sahani safi na kula.

MUDA GANI UNAFAA KULA EMBE DODO?
Inategemea unakula embe la namna gani. Maana nimesema hapo awali kwamba embe dodo linaweza kuliwa likiwa limeiva, likiwa bichi au likiwa changa.

Embe dodo likiwa changa: Embe hili likiwa changa mara nyingi linakuwa na uchachu na uteute mwingi. Kwa hiyo siyo vyema kula embe dodo likiwa changa. Embe dodo changa linatumiwa kutengeneza chachandu au mboga.

Unatakiwa uchume embehilo vizuri kisha ulioshe na maji safi. Halafu weka kwenye chombo safi. Kisha ondoa maganda yake taratibu. Kama unataka kutengeneza chachandu katakata vipande vidogo vodogo. Changanya na pili pili. Weka chumvi kwa mbali. Kisha injika kwenye jiko. Pika kwa taratibu mpaka uone embe hilo limelainika.


Nitaendelea......
 
Naendelea....

Nilikuwa naongelea muda wa kula embe dodo. Kutokana na ushauri wa wataalamu mbalimbali; embe dodo linaweza kuliwa wakati wowote. Lakini linatakiwa kuliwa kistaarabu. Maana kuna watu wengine wapo hata kwenye daladala utamuona kashika mkononi embe na kuanza kulila bila hata kutoa maganda yake. Hii ya kula ovyo ovyo inaweza kusababisha matatizo kwa watu wengine maana wengine hawapendi kumuona mtu akiwa anakula embe dodo.

EMBE DODO CHANGA
Kama nilivyo sema hapo awali si vizuri kula embe dodo changa ni muhimu kusubiri likomae. Lakini kuna watu ambao wanaweza kula embe hili likiwa changa. Ni muhimu sasa kuwaeleza namna iliyo bora ya kula.

Kwaza embe hili huwezi ukalila hivi hivi, kwa sababu utamu wake bado haupo. Ila kwa sababu ya tamaa ya kusikia harufu ya maembe wengi huwa wanatamani kula.
Embe hili linafaa sana kwa mboga na kutengeneza chachandu. Lakini ukiona kuwa huna muda wa kutengeneza chachandu au mbonga; unaweza ukatumia chunvi. Japo wakati embe hili likiwa changa huwa alina maji hata kidogo. Kwahiyo litakuwa gumu na wakati mwingine linaweza kukuletea matatizo kwenye meno.

Kwa tamaduni zetu za Kitanzania; watu wakikuona unakula embe dodo changa watakushangaa sana. Ni vizuri ukalichuma embe hilo kwa kificho na kupeleka nyumbani kwaajili ya kuliandaa vizuri.
Hata hapo nyumbani kuna watu wanaweza kukushangaa wakikuona unakula embe dodo changa. Kwa hiyo jitahidi kulificha sana.

Nitaendelea.....
 
EMBE DODO BICHI

Embe dodo mbichi huwa linaukakasi sana. Ukiona mwenzako analitafuna kwa mbaali nawewe utajisikia kama kuna kitu kinapita kwenye meno. Embe hili linakuwa limekomaa lakini bado ni bichi. Embe hili ukilibonyeza linakuwa gumu, halibonyezeki wa urahisi.

Kwa mujibu wa tamaduni zetu za kitanzania embe hili linaweza kuliwa bila wasi wasi. Yapo mengine yanauzwa sokoni unaweza kuamua kulinunua na kulila hivyo hivyo au kulivundika liivye ili baadae ulile.

>Embe dodo bichi kulivundika: Unaweza ukaamua kuchuma au kununua embe dodo bichi ukalivundika kwaajili ya kula baadae. Lakini unatakiwa ulivundike sehemu ambayo wengine wanaopenda embe dodo wasilione.
Kama utaamua kulivundika hakikisha sehemu ulilolivundika ni salama kabisa. Maana unaweza kuliweka sehemu siku hiyo hiyo wengine wakaliona na kulila wakati likiwa bichi.

Nashauri kama embe ni moja tu na umelipata kwa taabu ni vyema ukalila wakati huohuo likiwa bichi kuliko kulivundika na hujui litaiva lini. Maana unaweza ukachelewa ukalikuta limeza na halifai tena kwa kuliwa. Au wengine wanaweza kuliona na kulila ukakosa.
 
Embe dodo likiwa limeiva
Embe dodo likiwa limeiva kisawa sawa ni tamu mno. Sasa ustaarabu wa kilila ndio unatakiwa ufundishwe. Wale warafi na wasiojua namna ya kulila embe dodo unaweza kuwakuta wanalibinya mbinya na kulibonda mbonda kisha linakuwa tepe tepe. Wanatoboa kitundu na kisha wanaanza kulinyonya. Hakika huu sio ustaarabu wa ulaji wa embe dodo.

Kwanza kabisa embe dodo ni vyema ukalipata kwa kununua au kuchuma kwenye mti. Kisha lioshe na maji safi. Wengine wanapendelea kula na maganda yake. Lakini mimi nashauri ule na maganda yake ikiwa maganda bado ni ya kijani.

Ukitaka kula na maganda yake; osha chmbo chako vizuri na uwe umeendaa kisu cha kukatia katia nacho lazima kiwe safi. Kata kata vipande vidogo vidogo. Weka kwenye sahani safi. Kisha chukua umma, chukua kipande kimoja kimoja taratibu. Nashauri unatakiwa uwe na tissue paper au lesso maana wakati mweingine embe hili linaweza kuwa limeiva sana likatoa maji maji.

Ukiwa unataka kula bila maganda. Ondoa maganda ya embe dodo taratibu na siyo kwa pupa. Kisha kata kata vipande vidogo vidogo. Endelea kuweka vipande hivyo kwenye sahani safi. Kisha chukua umma au vijiti vya kuchukulia kipande kimoja kimoja.

Kokwa la embe dodo haliliwi. Unaweza ukalihifadhi kwaajili ya kupanda ili uoteshe dodo jingine.
 
Back
Top Bottom