Jifunafu
Senior Member
- May 25, 2020
- 182
- 599
Ukweli kwa Sisi vijana wa Tanzania tunatakiwa kuamka sana, maana tumekuwa waathirika wakubwa kutwa nzima watu ni kubishana Simba na Tanga.Mkuu waafrica tuna matatizo ya akili kabisa, ukisikia hizo story ni tafauti na uhalisia, Jaribu kufika kwenye hizo nchi na uone uhalisia wa mazingira, Nchi za kiarabu kuna waafrica mamilioni wanaoishi. Kama hayo munayoyazungumza ingelikua ni mambo ya kawaida huko kwanini waafrica waendelee kukimbilia kila kukicha?
Tuache kuchukua matukio mawili matatu tukayakuza kama ndio mazingira ya kimaisha huko yalivo. Mana tukiamua kukuza matukio Bongo kuna matukio kibao ya kinyama sana huko uarabuni hata robo hawanusi
Uwezi kupita mtaa bila kusikia vijana Hadi wazee wakibishana kuhusu kagere mara Boko kawaje, ni upuuzi mtupu.
Na hao hao ndo unakuta ni wahanga kwenye swala la ajira na nahizo Bachala zao za kiswahili na Sanaa, Mtu akileta idea flani au suala la kutafuta fulsa nje ya Tanzania utaanza kusikia ohh mara mnaenda kutolewa Figo mara unyanyasaji huko, yani Mambo ya ajabu kabisa kutwa kulia ajira wakati furusa kimejaa nje nyingi tu
Kiufupi Mimi natokea matombo ndani huko Morogoro nipo hapa zenj zaidi ya miaka 4 Sasa, kwa hichi nacho zungumza kwa mtu aliewai kukaa Zanzibar awezi kupinga.
Vijana wengi wa kizanzibari walio na fedha wengi chimbuko lao ni Mataifa hayo ya middle east, wanafanya biashara, Kuna vijana wengine wanafanya kazi huko wanatuma fedha nyumbani na kufanya maendeleo.
Usishangae kuona kijana mdogo tu anamiliki gari za tours hata tatu ukashangaa ni kawaida tu.
Fulusa kwenye Mataifa hayo ya middle east zimejaa tele na wazanzibar wengi wako huko wanafanya kazi huko wanatuma fedha nyumbani, wakenya, waganda, wafilipino, wahindi wengi tu.
Lakni Leo kijana wakitanzania ukimwambia furusa Kama hizo stanza kuwaza mara hao matapeli mara wanatoa Figo, wakati huo Hana ajira kutwa nzima kulanda na cv ya kutafuta ajira za Post code, mtu anasafiri kutoka katavi huko kuja kugombea nafasi 5 za KAZI uhamiaji, vijana amkeni furusa tele huko.
Mfano ni huu.
Kuna rafiki yangu Mmoja ni mzanzibar yeye ni wakala wa fedha, tigo, airtel, ezypesa, mpesa, halopesa, ttclpesa, Western Union MoneyGram nk. Huyu mwamba anapesa vibaya maeneo ya mlandege jna kampuni.
Amekuwa ni mteja wangu sana ninapo PATA visenti vyangu waga nakwenda pale kutuma nyumbani.
Kila nilienda pale hususani mida your unakuta watu wengi wako foleni wakipewa fedha hasa wazee, vijana na kina mama pia, lakini nikawa najiuliza uyu jamaa mbona wateja wake wengi ni wazee kwann? Au anafanya biashara ya kukopesha fedha au anautaratibu wa kutoa Sadaka kwa makundi ya wazee lakini sikupata jibu.
Siku Moja nikapita pale majira ya saa mbili asubuhi, yeye anautaratibu wa kufungua saa4 asubui, dahhh nikakuta watu wako foleni Kama kawaida hasa watu wazima na vijana pia lakini kundi la watu wazima ndio wengi, nikajiuliza Tena sikupata jibu.
Ndipo nikasema huyu mwamba inabidi nimfanyie serious investigation nijue anajiusisha na shughuli gani mbali na kuwa yeye ni agent wa fedha.
Siku Moja nikaenda pale time za saa Tisa mchana kutuma pesa nikakuta yupo lakn jamu ilikuwa hakuna, tukasalimia pale na kupiga story mbili tatu huku akinipa huduma, pale ndo nilipata nafasi ya kumchomeka swali langu kwamba mbona wewe wateja wako wengi ni wazee alafu Kama vile naonaga wanakuja hata awafanyi muamala wakifika unaangalia kitabu na kutoa pesa anahesabu Kisha anaondoka vp unakopesaha ustadhi na Mimi niombe MKOPO?
Jamaa alicheka sana akasema hapana rafiki yangu, akafungua kabati akatoa counter book kubwa sana akaanza kunionyesha majina na kiwango Cha fedha ambacho mtu ametuma, aliendelea kufungua like book nikishaanga tu Kama vile mjusi amebanwa na mlango huku mimacho ikinitoka, hakuishia hapo hakavuta laptop yake na kunionyesha.
Akanismbia unao waona hao wanakuja hapa Kila cku ni wazi wanakuja kuchukua fedha hapa wanatumia na watoto wao wanafanya kazi middle east huko, Oman, Qatar, UAE, Kuwait nk, sijakaa sawa akaja mama Mmoja kavalia baibui lake akatusalimia pale, asalam alekuhm na sisi tukaitikia walekuh msalam taalah wabarakatu, yule jamaa akamwambia mama mama taja Jina lako mama akasema naitwa Mwanahawa kombo makame.
Jamaa akavuta laptop yake akaangalia akavuta drool akatoa baasha imeandikwa Jina na kiasi Cha fedha akampa mama, mama akauliza ni kiasi gani hiki jamaa akamjibu ni million 3 na laki 5,mama akaondoka.
Yule jamaa ndo akaniambia uyu mama kijana wake anafanya KAZI Qatar na kampuni Moja ya Kiarabu anafanya KAZI ya sales representative. Akaniambia KAZI nyingi kule ustadh wazanzibari wengi wako huko wanafanya kazi.
Zanzibar michongo ya kuzama hizo Nchi ni fasta tu kikubwa uwe na pesa tu, Mimi Kuna agent nimemtumia kumuunganishia jamaa yangu mchongo wa KAZI Dubai, na jamaa amefanikiwa kuondoka Leo hii.
Siwezi kuweka nyaraka za safari yake hapa lakn jamaa muda huu ametua kwenye aridhi nyingine tayari.
Najua Kuna wengine hapa watasema ni harufu ya upigaji lakini mwenye akili ataelewa ninachokisema.