utamuudhi halafu utanipa kazi ya kumbembeleza halafu anajidai alijikopesha lini kwani.?mkuu saudariHana huruma hata chembe, hapo anajidai tu.
maneno kutoka mepesiiiiiiiiiiiiiiii vitendo sasa ndo shughuli pevu,usiombe ndugu yangu!
Vipi nyoka?nani atalikata tawi?Hapo tawi likikatika simba na mamba watakimbia kwa mshtuko, huo muda ndio atumie kujiokoa.
Ni kweli mkuu,akili za jamaa zinafanana na zile za ABNUASI!Halafu hivi huyo jamaa wakati anaanza kuukata huo mti, alitegemea utaangua upande upi?
Kwa haraka naona kulikuwa na kila dalili za mti kuangukia majini na huko tayari ndio makazi ya mamba...
Mwache aliwe tu kwa kuwa hakufikiria kabla...
Teh teh teh!kuchagua aina ya kifo ni bahati?Ana bahati huyu jamaa, yaani kapewa oppotunity ya menu ya kifo achague kifo anachokipendelea
mh!mitihani ya mungu!huyu jamaa alikuwa anakata mti, ghafla bin vuu! simba akatokea ikabidi aupande mti aliokuwa anaukata. Akiwa anafikiria kimkwepa simba yule akashangaa jinyoka likubwa linamsogelea, huku akijishauri kujitupa kwenye maji akashangaa mijimamba nayo imetokelezea!!!!
Hivyo ndivyo nilivyoweza kuitafsiri hiyo picha.
Hii si sifa...ifuatayo ni listy a wanyama nilio waua shambani kwangu baada ya kuingiliwa: Sungura, Panya, chatu, koboko, kifutu, fisi, kenge, na mnyama fulani wa ajabu ila jina silijuwi. Nyoka naua sana haswa wakati wa mavuno pale Kibaha. Mimi nyoka ndiyo siogopi kabisa kwani nina elimu nao hata baadhi ya wanyama pia. Fisi aliniingilia uwani usiku baada ya kusikia harufu ya kuku wa kuchoma. Nilimvizia na kumpiga mshale wa tumbo alipogeuka nikampa mwingine wa usoni karibu na jicho. Alipoanguka kwa kusikia kizunguzungu ndipo nilipommaliza na gobole ambalo mlinzi alichelewa kuniletea. Hapa ni jeshi la mtu mmoja ndugu yangu, siogopi nasubiri simba Kidawa tu aje.
hapo ni maombi tu!!!
Wewe tena ndo utammalizia, hapo alipo ameshazimia kimya kimya.
Daaaaaaaaaahhh kumbe we ni noma aisee hasa hapo kwenye chatu em nipe tekniki za kudeal nae maanake sitakagi hata kumuwaza huyo hayawani kwamba nimekutana naye.
Mkuu Blue G sikia mwenzangu, chatu si nyoka wa kumwogopa hata siku moja kwani ni mjinga ukijuwa mbinu zake. Kwanza hana sumu, yeye huvizia mnyama au binadamu then anamkunja ili amvunje mifupa na kummeza. Usipende kusikia maneno ya watu dhidi ya chatu kwani chatu hawezi kummeza mtu mzima hata siku moja, mtu mzima nikimaanisha mtu wa futi 5'0 na kilo 75, this is too much for chatu. Hapa Afrika hatuna chatu wa kuweza meza watu wazima, chatu wa namna hii wako bara la Asia, kwa hapa Tanzania na Afrika tuna chatu wa aina mbili tu ambao ni rock python (huyu ndiye mkubwa zaidi na wanapatikana sana huko Lake Manyara, Mwanza, Tabora, Kigoma, na mapori makubwa hapa Tanzania) na hawa chatu wa Kibaha wanaopatikana kila kona ya hapa Tanzania. Sikufundishi kuua chatu, ila usiwe mwoga kwao kwani wao huogopa binadamu sana. Nyoka wa kuogopa hapa ni Koboko kwani hawa ndiyo nyoka wenye akili zaidi na wana sumu kali ile mbaya. Watanzania wanasema kwa koboko kukugonga eti mpaka asimame then aanakudunga kichwani. This is bullshit, koboko hachaguwi pa kugonga, yeye anaonga sehemu yeyote ile na sumu yake inashambulia nerves systems za aliyegongwa hivyo unakufa si chini ya nusu saa kama hutopata matibabu upesi. Fimbo tu, ndiyo dawa halisi ya koboko au tuseme kila nyoka mjanja. Kuna cha kufanya hapa ila kuandika naona nitachukua nafasi na nimeanza kuchoka kuandika. Pia kumbuka unaweza kuishi na nyoka ndani ya nyumba bila hata wewe mwenyewe kujuwa, yeye atakuwa anakuepuka kila wakati kwani anakuwa anajificha ili usimuue ila siku ya siku mkikutana face to face ndipo anakudhuru kuhofia maisha yake. Usisikilize sana masuala ya kijiweni juu ya nyoka na desturi zake, I learnt the hard way by practicing what I had learnt from school na mengi niliyoambiwa na watu vijijini ni uwongo mtupu.
jamani Mkereketwa Huyu nashukuru sana kwa maelezo yako mazuri,ila am sorry coz nina maswali mawili kuhusu chatu,je ni kweli kuwa mdomo wa chatu ni mwepesi sana hivi kwamba ukipata ujasiri wa kuushika unaupasua mara moja?na je ukilala chini chatu hana uwezo wa kukuattack kwa ajili ya kukumeza zaidi akiona huamki atakuchoma na mkia wake wenye sumu na kukunyonya ubongo?hayo ni baadhi ya mambo niliyowahi kusikia watu wakiyasema kuhusu chatu,naomba ufafanuzi wako tafadhali.