Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,278
- Thread starter
- #21
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
Sehemu ya Nne.
Utajiri mkubwa ulikuwa mbele yake lakini hakuwa na muda wa kuuchukua, kitu pekee alichokiangalia kilikuwa ni chakula tu. Hakujua afanye nini, alibaki akizunguka kwa kwenda huku na kule, yaani apande ngazi, mara ashuke, alikuwa akijifikiria tu ni kitu gani alitakiwa kufanya kuiokoa nafsi yake.
Wakati akizunguka huku na kule katika floo hiyo ya mia moja na ishrini ndipo akakumbuka kwamba katika floo ya mia na kumi na nane kulikuwa na mgahawa wa McDonald ambao ulitumika kwa watu waliokuwa wakifanya biashara katika jengo hilo.
Akaelekea kwenye dirisha na kuchungulia, maji yaliendelea kupungua na katika kipindi hicho ndiyo yalikuwa yakienda katika floo hiyo. Hakutaka kuchelewa, akaanza kuteremka kuelekea katika floo hiyo.
Alipoifikia, kulikuwa na maji yaliyomfikia kiunoni, hakutaka kurudi nyuma, tumbo lake lilikuwa tupu hivyo pasipo kufanya harakati za kutafuta chakula, basi angeweza kufa kwa njaa na si kwa mafuriko.
Kulikuwa na vyakula mbalimbali, vyote hivyo vilikuwa vimelowanishwa na maji. Kulikuwa na pizza, bugger, sandwich na vyakula vingine lakini vyote hivyo havikutamanika hata kidogo.
Mbele kabisa macho yake yakatua katika friji moja lililokuwa limepachikwa ukutani, akaanza kulifuata huku akiwa na kiu ya kutaka kunywa hata vinywaji vilivyokuwa humo ndani, alipolifikia, akalifungua na kuangalia ndani.
Kulikuwa na vinywaji vingi, mbali na vinywaji hivyo, pia kulikuwa na biskuti. Hakutaka kuchelewa, aliona kama angekosa, haraka sana akaanza kuchukua vinywaji na biskuti hizo na kuanza kula.
Alikula kwa fujo, hakumeza kilichokuwa mdomoni, akakiweka kingine. Ulaji wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na njaa. Kula tu, alitumia muda wa dakika kumi na tano, tumbo lake likawa afadhali.
Kumbukumbu za mpenzi wake zikamjia tena, akapanda kwenye floo ile aliyotoka, yenye almasi nyingi na kutulia. Machozi yakaanza kumwagika, hakuamini kama mwisho wa siku angekosa kila kitu, yaani mtoto wake na mpenzi wake, hakika moyo wake ulimuuma mno.
“Ni lazima niondoke, siwezi kukaa hapa,” alisema James.
Kitu kilichokuwa kichwani mwake ni kwamba ilikuwa lazima achukue almasi zile na kuondoka nazo kwani bila kufanya hivyo asingeweza kuzipata tena kwani endapo maji yangepungua, ulinzi ungeimarishwa tena, ilikuwa ni bora kuzichukua kwani hata wamiliki wangekuja, wangehisi kwamba maji yalizihamisha almasi hizo.
Alichokifanya ni kurudi kulekule alipokuta chakula na kisha kuling’oa friji lile na kutoa kila kitu, kwa kutumia nguvu zake, akalibeba na kupanda nalo kwenda juu. Huko, akaufungua mlango wa chumba kile kilichokuwa na almasi, akaziangalia kwa tamaa kubwa kisha kuanza kuzitoa na kuziweka ndani ya friji lile.
Zilikuwa nyingi zenye uzito wa kilo tano ambazo kwa hesabu ya harakaharaka iliyokuja kichwani mwake, ilikuwa ni zaidi ya kupata dola bilioni hamsini, kiasi kikubwa sana cha fedha ambacho kingemfanya kuwa miongoni mwa mabilionea kumi wakubwa katika ulimwengu huu.
Alipomaliza kuzipakia, hakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka, akaingia ndani ya friji, akachukua mbao kubwa ambayo alitaka kuitumia kupigia kasi kuelekea sehemu isiyokuwa na maji.
Kwa sababu tayari giza lilianza kuingia, akajipa uhakika kwamba sehemu ambayo angekwenda ingekuwa salama kwani kote huko kulikuwa na maji, yaani Jiji la New Orleans halikuonekana, lilikuwa bahari tu.
Naye akaingia ndani ya lile friji, hakutaka kuendelea kukaa ndani ya jengo hilo, akaanza kupiga kasi huku akiwa ameutoa mlango wa friji, almasi zilikuwa humo ndani tena huku akiwa amezifunika kwa nguo.
Hakujua alipokuwa akielekea, kitu pekee alichokijua ni kwamba upande aliokuwa akielekea ni ule usiokuwa na bahari. Alikuwa akipiga kasia, tena huku kukiwa na giza tayari, hakutaka kuangalia alipotoka, macho yake yalikuwa mbele tu.
Majengo marefu ambayo nayo yalifunikwa na maji yalikuwa yakionekana vizuri machoni mwake, hali ilitisha sana, alijikuta moyo wake ukiumia na machozi kuanza kumbubujika.
Hakutaka kusubiri, aliendelea na safari yake. Safari hiyo ilianza saa moja usiku, alijikuta akienda, akipiga kasia zaidi, saa nne baadaye, bado hakuwa amefika sehemu yoyote ya nchi kavu, bado alikuwa sehemu yenyemaji mengi.
Wakati akiendelea na safari yake, ndipo alipoanza kusikia muungurumo wa helkopta, hakutaka kuomba msaada, alichokifanya ni kujifunika na zile nguo zilizokuwa zimefunika almasi na kutulia.
Aliisikia helkopta ile ikipita juu yake, hakutaka kufungua, hakutaka kuonekana kwani aliamini kwamba kama angeonekana na kuokolewa basi zile almasi ambazo alikuwa nazo zingechukuliwa na hivyo yeye kubaki mikono mitupu.
“Siwezi kutamani kuokolewa na wakati nina utajiri mkubwa...” alisema James huku akiwa chini ya nguo zile.
Aliendelea na safari yake kama kawaida. Akafika sehemu ambayo maji yake yalionekana kupita kwa kasi kidogo. Hakutaka kusumbuka kufikiria sehemu hiyo kulikuwa na nini, alijua jinsi hali ilivyokuwa hivyo akagundua kwamba sehemu hiyo kulikuwa na mto.
“Mto Mississippi...” alijikuta akijisemea.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe, japokuwa maji yalikuwa yamejaza sana lakini aligundua kwamba sehemu iliyokuwa ikipitisha maji hayo kwa kasi kulikuwa na Mto Mississippi. Hakutaka kugeuza, akataka aelekee mbele huku akijua kwamba ili kuyaokoa maisha yake na utajiri mkubwa aliokuwa nao, ilikuwa ni lazima kuvuka eneo hilo. Akapiga moyo konde.
Akaendelea kupiga kasia, japokuwa alikuwa amechoka lakini hakutaka kupumzika, hakutaka kukata tamaa, aliendelea mbele zaidi tena kwa sababu alikuwa akivuka sehemu yenye mto uliokuwa ukipeleka maji kwa kasi, hata nguvu zake za kupiga kasi ziliongezeka.
Friji likaanza kupelekwa huku na kule, hakutaka kukata tamaa, aliendelea zaidi lakini maji yale yalionekana kuwa na nguvu kubwa. Hakuacha, kama kufa, ilikuwa lazima afe lakini si kuuacha utajiri ule kupotea mikononi mwake.
Akaendelea kupiga kasia, ikafika kipindi akashindwa kabisa kuendelea, akajikuta akiacha na kuona mto huo ungempeleka wapi. Alikwenda mbele mpaka sehemu ambayo maji ya bahari ile yalipoanza kupungua na mwisho kuishia kabisa hivyo kubaki kwenye maji ya mto tu.
Pembeni yake hakukuwa na majengo yoyote, ni pori kubwa lililokuwa likizinguka mto Mississippi. Alitamani kulipeleka friji lile pembezoni mwa mto ule ikiwezekana hata kutulia katika pori hilo lakini hakuwa na nguvu za kufanya hivyo.
Aliendelea kusonga mbele huku akiwa hoi. Alichoka, usingizi ulimkamata lakini hakutaka kulala kabisa, aliendelea kusonga mbele lakini mara ghafla akaanza kusikia sauti kubwa ya maji.
Akashtuka, akaangalia mbele yake, umbali kama hatua mia moja za miguu ya binadamu akaona maji yakielekea chini, yaani kulikuwa na maporomoko ya Mto Mississippi yaliyoitwa St. Antony yaliyopo Kaskazini mwa Jiji la New Orleans.
“Mungu wangu!” alijikuta akisema.
Kitu cha kwanza kabisa kilichokuja akilini mwake ni kwamba kama angeruhusu friji hilo lidondoke katika maporomoko hayo yaliyokuwa na urefu wa mita mia moja basi ingekuwa rahisi kwake kupoteza almasi hizo kwani friji lingeanguka, wakati linafiki chini lingejipindua na hivyo almasi zote kutoka ndani ya friji.
Hakutaka kuona hilo likitokea, alihangaika sana, alipambana kuzipigania almasi hivyo, kwa nafasi aliyokuwa nayo, japokuwa alichoka lakini hakutaka kuruhusu jambo hilo litokee. Nguvu zikamjia upya, friji lilizidi kusogea kule kulipokuwa na maporomoko, alichokifanya ni kupiga kasia kurudi nyuma, tena kwa kasi, ila kutokana na nguvu za maji ya mto ule, akajikuta akifanya jambo lisilosaidia, friji lile likazidi kupelekwa kule kulipokuwa na maporomoko yale, ndoto za kuwa bilionea zikaanza kupotea kichwani mwake.
Akabakiza kama hatua thelathini tu kuyafikia maporomoko yale, maporomoko ambayo yangeupoteza utajiri aliokuwa nao ndani ya friji lile.
****
“Lord have mercy on us...” (Mungu utuhurumie...)
Hayo yalikuwa maneno machache yaliyotoka kinywani mwa mchungaji wa Kanisa la Water of Life lililokuwa Mji wa Kenner, pembezoni mwa Jiji la New Orleans. Washirika wote walitoka kanisani huku wakionekana kuwa na majonzi mazito, hali iliyokuwa ikionekana iliwatisha wote, hawakuamini kama kweli maji yalihama kutoka baharini na kulifunika jiji la New Orleans.
Hapo Kenner ilionekana kama ufukweni kwani maji yote ya bahari yaliyoifunika New Orleans, yaliishia ndani ya jiji hilo. Walipoangalia kule yalipoanzia, hakukuwa na jengo lolote lililoonekana, kote huko kulifunikwa na maji na kulifanya eneo lote kuonekana kama bahari moja kubwa.
Hilo lilionekana pigo kubwa lililowahi kuikumba nchi ya Marekani, achana na lile shambulizi la septemba 11 mwaka 2001 ambapo majengo mawili ya WTC yalipolipuka baada ya kugongwa na ndege.
Washirika hao wakarudi kanisani kwani bado walikuwa kwenye maombi mazito katika kipindi hicho cha mkesha wa mwisho wa mwaka, kilichofuatia ni kuanza kuomba, walimuomba Mungu awanusuru na kile kilichokuwa kimetokea. Siku hiyo ilikuwa ni ya huzuni kubwa, vyombo vya habari viliendelea kutangaza hali iliyokuwa ikiendelea katika Jiji la New Orleans japokuwa taarifa za awali zilisema kwamba hakukuwa na mtu aliyekufa, ila majengo na vitu vingine viliharibika sana.
Vitu vinavyoweza kuhamishwa vilihama na vingi vilionekana juu ya maji vikielea, vingi vilipelekwa na maji mpaka huko Kenner, na vitu ambavyo vilipelekwa na maji hayo mpaka Kenner lilikuwa lile friji alilowekwa mtoto.
Friji hilo lilipokuwa likifika katika sehemu hiyo pembeni ya kanisa, hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba ndani ya friji lile kulikuwa na mtoto. Kama vilivyokuwa vitu vingine, hata lile friji washirika wa kanisa hilo wakaamua kulipuuzia na wao kuingia kanisani.
Maombi yaliendelea, huku kila mmoja akiwa kwenye uwepo wa Mungu, ghafla wakaanza kusikia sauti ya mtoto ikilia. Hawakujua sauti hiyo ilitoka wapi, wakabaki wakiangaliana tu, kila mwenye mtoto, alimwangalia mtoto wake, alikuwa kimya, sasa hiyo sauti ya mtoto ilitoka wapi?
Ilikuwa ni usiku sana, saa zao zilionyesha kwamba tayari ilikuwa ni saa sita usiku, sasa sauti ya mtoto hiyo ilitokea upande gani na wakati watoto wote ndani ya kanisa walikuwa wamelala.
“Who is that baby?” (Mtoto gani huyo?) aliuliza mchungaji kwa sauti ya chini.
Mwanaume mmoja akatoka akaelekea nje, alitaka kumuona huyo mtoto aliyekuwa akilia, alipofika nje, hakuweza kuisikia sauti hiyo, alijaribu kuangalia huku na kule, ukimya mkubwa ulitawala, ni vitu vilivyoletwa na maji ya bahari ndivyo vilivyoonekana.
Akarudi ndani na kutoa taarifa kwamba hakukuwa na mtoto yoyote yule. Huku mchungaji akijiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, sauti ya mtoto huyo ikaanza kusikika tena.
Mchungaji akaamua kutoka yeye mwenyewe, mkononi mwake alikuwa na rozali na kila hatua aliyokuwa akipiga, alikuwa akimuomba Mungu. Alipofika nje, akaanza kuangalia huku na kule, bado sauti ya mtoto yule ilikuwa ikisikika lakini kila alipoangalia huku na kule, hakumuona.
“Huyo mtoto yupo wapi?” aliuliza mshirika mmoja.
“Hata mimi sijui, sauti naisikia, ila mahali alipokuwa, sijui yupo wapi,” alijibu mshirika mmoja.
Mchungaji aliendelea kusogea mpaka kulipokuwa na friji moja, humo ndipo sauti ilipotoka, kwa haraka pasipo kupoteza muda mchungaji akalifungua friji hilo, alichokutana nacho hakuamini, macho yake yakatua kwa mtoto mdogo ambaye alionekana kuzaliwa siku hiyohiyo, alikuwa wa kiume, harakaharaka akamtoa kutoka ndani ya friji hilo.
Washirika wote waliokuwa nje ya kanisa hilo ambao macho yao yalikuwa yakimwangalia mchungaji huyo walibaki kushangaa, wakasogea mpaka mchungaji alipokuwa na kuanza kumwangalia mtoto huyo.
Alikuwa mzuri wa sura lakini kila mmoja akaanza kumuonea huruma, bado mwili wake ulikuwa na damu nyingi zilizoganda. Walichokifanya ni kumchukua na kwenda naye kanisani, kitu cha kwanza kabisa walichomfanyia ni maombezi kisha kujadiliana mtu ambaye alitakiwa kumchukua mtoto huyo kwa ajili ya kumlea baada ya kutoa taarifa polisi.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mmoja, alikuwa mtu mwenye uwezo wa kifedha humo kanisani.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mwingine, mjane ambaye mtoto wake pekee alikufa baada ya kuugua ugonjwa wa polio.
Alichoamua mchungaji ni kumgawia mwanamke yule mjane mtoto huyo na kwenda kuishi naye kwani maisha ya upweke aliyokuwa akiishi waliamini kwamba mtoto huyo angempa furaha. Mwanamke yule mjane akamchukua mtoto huyo na kumpa jina la Dylan.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumapili
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
Sehemu ya Nne.
Utajiri mkubwa ulikuwa mbele yake lakini hakuwa na muda wa kuuchukua, kitu pekee alichokiangalia kilikuwa ni chakula tu. Hakujua afanye nini, alibaki akizunguka kwa kwenda huku na kule, yaani apande ngazi, mara ashuke, alikuwa akijifikiria tu ni kitu gani alitakiwa kufanya kuiokoa nafsi yake.
Wakati akizunguka huku na kule katika floo hiyo ya mia moja na ishrini ndipo akakumbuka kwamba katika floo ya mia na kumi na nane kulikuwa na mgahawa wa McDonald ambao ulitumika kwa watu waliokuwa wakifanya biashara katika jengo hilo.
Akaelekea kwenye dirisha na kuchungulia, maji yaliendelea kupungua na katika kipindi hicho ndiyo yalikuwa yakienda katika floo hiyo. Hakutaka kuchelewa, akaanza kuteremka kuelekea katika floo hiyo.
Alipoifikia, kulikuwa na maji yaliyomfikia kiunoni, hakutaka kurudi nyuma, tumbo lake lilikuwa tupu hivyo pasipo kufanya harakati za kutafuta chakula, basi angeweza kufa kwa njaa na si kwa mafuriko.
Kulikuwa na vyakula mbalimbali, vyote hivyo vilikuwa vimelowanishwa na maji. Kulikuwa na pizza, bugger, sandwich na vyakula vingine lakini vyote hivyo havikutamanika hata kidogo.
Mbele kabisa macho yake yakatua katika friji moja lililokuwa limepachikwa ukutani, akaanza kulifuata huku akiwa na kiu ya kutaka kunywa hata vinywaji vilivyokuwa humo ndani, alipolifikia, akalifungua na kuangalia ndani.
Kulikuwa na vinywaji vingi, mbali na vinywaji hivyo, pia kulikuwa na biskuti. Hakutaka kuchelewa, aliona kama angekosa, haraka sana akaanza kuchukua vinywaji na biskuti hizo na kuanza kula.
Alikula kwa fujo, hakumeza kilichokuwa mdomoni, akakiweka kingine. Ulaji wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na njaa. Kula tu, alitumia muda wa dakika kumi na tano, tumbo lake likawa afadhali.
Kumbukumbu za mpenzi wake zikamjia tena, akapanda kwenye floo ile aliyotoka, yenye almasi nyingi na kutulia. Machozi yakaanza kumwagika, hakuamini kama mwisho wa siku angekosa kila kitu, yaani mtoto wake na mpenzi wake, hakika moyo wake ulimuuma mno.
“Ni lazima niondoke, siwezi kukaa hapa,” alisema James.
Kitu kilichokuwa kichwani mwake ni kwamba ilikuwa lazima achukue almasi zile na kuondoka nazo kwani bila kufanya hivyo asingeweza kuzipata tena kwani endapo maji yangepungua, ulinzi ungeimarishwa tena, ilikuwa ni bora kuzichukua kwani hata wamiliki wangekuja, wangehisi kwamba maji yalizihamisha almasi hizo.
Alichokifanya ni kurudi kulekule alipokuta chakula na kisha kuling’oa friji lile na kutoa kila kitu, kwa kutumia nguvu zake, akalibeba na kupanda nalo kwenda juu. Huko, akaufungua mlango wa chumba kile kilichokuwa na almasi, akaziangalia kwa tamaa kubwa kisha kuanza kuzitoa na kuziweka ndani ya friji lile.
Zilikuwa nyingi zenye uzito wa kilo tano ambazo kwa hesabu ya harakaharaka iliyokuja kichwani mwake, ilikuwa ni zaidi ya kupata dola bilioni hamsini, kiasi kikubwa sana cha fedha ambacho kingemfanya kuwa miongoni mwa mabilionea kumi wakubwa katika ulimwengu huu.
Alipomaliza kuzipakia, hakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka, akaingia ndani ya friji, akachukua mbao kubwa ambayo alitaka kuitumia kupigia kasi kuelekea sehemu isiyokuwa na maji.
Kwa sababu tayari giza lilianza kuingia, akajipa uhakika kwamba sehemu ambayo angekwenda ingekuwa salama kwani kote huko kulikuwa na maji, yaani Jiji la New Orleans halikuonekana, lilikuwa bahari tu.
Naye akaingia ndani ya lile friji, hakutaka kuendelea kukaa ndani ya jengo hilo, akaanza kupiga kasi huku akiwa ameutoa mlango wa friji, almasi zilikuwa humo ndani tena huku akiwa amezifunika kwa nguo.
Hakujua alipokuwa akielekea, kitu pekee alichokijua ni kwamba upande aliokuwa akielekea ni ule usiokuwa na bahari. Alikuwa akipiga kasia, tena huku kukiwa na giza tayari, hakutaka kuangalia alipotoka, macho yake yalikuwa mbele tu.
Majengo marefu ambayo nayo yalifunikwa na maji yalikuwa yakionekana vizuri machoni mwake, hali ilitisha sana, alijikuta moyo wake ukiumia na machozi kuanza kumbubujika.
Hakutaka kusubiri, aliendelea na safari yake. Safari hiyo ilianza saa moja usiku, alijikuta akienda, akipiga kasia zaidi, saa nne baadaye, bado hakuwa amefika sehemu yoyote ya nchi kavu, bado alikuwa sehemu yenyemaji mengi.
Wakati akiendelea na safari yake, ndipo alipoanza kusikia muungurumo wa helkopta, hakutaka kuomba msaada, alichokifanya ni kujifunika na zile nguo zilizokuwa zimefunika almasi na kutulia.
Aliisikia helkopta ile ikipita juu yake, hakutaka kufungua, hakutaka kuonekana kwani aliamini kwamba kama angeonekana na kuokolewa basi zile almasi ambazo alikuwa nazo zingechukuliwa na hivyo yeye kubaki mikono mitupu.
“Siwezi kutamani kuokolewa na wakati nina utajiri mkubwa...” alisema James huku akiwa chini ya nguo zile.
Aliendelea na safari yake kama kawaida. Akafika sehemu ambayo maji yake yalionekana kupita kwa kasi kidogo. Hakutaka kusumbuka kufikiria sehemu hiyo kulikuwa na nini, alijua jinsi hali ilivyokuwa hivyo akagundua kwamba sehemu hiyo kulikuwa na mto.
“Mto Mississippi...” alijikuta akijisemea.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe, japokuwa maji yalikuwa yamejaza sana lakini aligundua kwamba sehemu iliyokuwa ikipitisha maji hayo kwa kasi kulikuwa na Mto Mississippi. Hakutaka kugeuza, akataka aelekee mbele huku akijua kwamba ili kuyaokoa maisha yake na utajiri mkubwa aliokuwa nao, ilikuwa ni lazima kuvuka eneo hilo. Akapiga moyo konde.
Akaendelea kupiga kasia, japokuwa alikuwa amechoka lakini hakutaka kupumzika, hakutaka kukata tamaa, aliendelea mbele zaidi tena kwa sababu alikuwa akivuka sehemu yenye mto uliokuwa ukipeleka maji kwa kasi, hata nguvu zake za kupiga kasi ziliongezeka.
Friji likaanza kupelekwa huku na kule, hakutaka kukata tamaa, aliendelea zaidi lakini maji yale yalionekana kuwa na nguvu kubwa. Hakuacha, kama kufa, ilikuwa lazima afe lakini si kuuacha utajiri ule kupotea mikononi mwake.
Akaendelea kupiga kasia, ikafika kipindi akashindwa kabisa kuendelea, akajikuta akiacha na kuona mto huo ungempeleka wapi. Alikwenda mbele mpaka sehemu ambayo maji ya bahari ile yalipoanza kupungua na mwisho kuishia kabisa hivyo kubaki kwenye maji ya mto tu.
Pembeni yake hakukuwa na majengo yoyote, ni pori kubwa lililokuwa likizinguka mto Mississippi. Alitamani kulipeleka friji lile pembezoni mwa mto ule ikiwezekana hata kutulia katika pori hilo lakini hakuwa na nguvu za kufanya hivyo.
Aliendelea kusonga mbele huku akiwa hoi. Alichoka, usingizi ulimkamata lakini hakutaka kulala kabisa, aliendelea kusonga mbele lakini mara ghafla akaanza kusikia sauti kubwa ya maji.
Akashtuka, akaangalia mbele yake, umbali kama hatua mia moja za miguu ya binadamu akaona maji yakielekea chini, yaani kulikuwa na maporomoko ya Mto Mississippi yaliyoitwa St. Antony yaliyopo Kaskazini mwa Jiji la New Orleans.
“Mungu wangu!” alijikuta akisema.
Kitu cha kwanza kabisa kilichokuja akilini mwake ni kwamba kama angeruhusu friji hilo lidondoke katika maporomoko hayo yaliyokuwa na urefu wa mita mia moja basi ingekuwa rahisi kwake kupoteza almasi hizo kwani friji lingeanguka, wakati linafiki chini lingejipindua na hivyo almasi zote kutoka ndani ya friji.
Hakutaka kuona hilo likitokea, alihangaika sana, alipambana kuzipigania almasi hivyo, kwa nafasi aliyokuwa nayo, japokuwa alichoka lakini hakutaka kuruhusu jambo hilo litokee. Nguvu zikamjia upya, friji lilizidi kusogea kule kulipokuwa na maporomoko, alichokifanya ni kupiga kasia kurudi nyuma, tena kwa kasi, ila kutokana na nguvu za maji ya mto ule, akajikuta akifanya jambo lisilosaidia, friji lile likazidi kupelekwa kule kulipokuwa na maporomoko yale, ndoto za kuwa bilionea zikaanza kupotea kichwani mwake.
Akabakiza kama hatua thelathini tu kuyafikia maporomoko yale, maporomoko ambayo yangeupoteza utajiri aliokuwa nao ndani ya friji lile.
****
“Lord have mercy on us...” (Mungu utuhurumie...)
Hayo yalikuwa maneno machache yaliyotoka kinywani mwa mchungaji wa Kanisa la Water of Life lililokuwa Mji wa Kenner, pembezoni mwa Jiji la New Orleans. Washirika wote walitoka kanisani huku wakionekana kuwa na majonzi mazito, hali iliyokuwa ikionekana iliwatisha wote, hawakuamini kama kweli maji yalihama kutoka baharini na kulifunika jiji la New Orleans.
Hapo Kenner ilionekana kama ufukweni kwani maji yote ya bahari yaliyoifunika New Orleans, yaliishia ndani ya jiji hilo. Walipoangalia kule yalipoanzia, hakukuwa na jengo lolote lililoonekana, kote huko kulifunikwa na maji na kulifanya eneo lote kuonekana kama bahari moja kubwa.
Hilo lilionekana pigo kubwa lililowahi kuikumba nchi ya Marekani, achana na lile shambulizi la septemba 11 mwaka 2001 ambapo majengo mawili ya WTC yalipolipuka baada ya kugongwa na ndege.
Washirika hao wakarudi kanisani kwani bado walikuwa kwenye maombi mazito katika kipindi hicho cha mkesha wa mwisho wa mwaka, kilichofuatia ni kuanza kuomba, walimuomba Mungu awanusuru na kile kilichokuwa kimetokea. Siku hiyo ilikuwa ni ya huzuni kubwa, vyombo vya habari viliendelea kutangaza hali iliyokuwa ikiendelea katika Jiji la New Orleans japokuwa taarifa za awali zilisema kwamba hakukuwa na mtu aliyekufa, ila majengo na vitu vingine viliharibika sana.
Vitu vinavyoweza kuhamishwa vilihama na vingi vilionekana juu ya maji vikielea, vingi vilipelekwa na maji mpaka huko Kenner, na vitu ambavyo vilipelekwa na maji hayo mpaka Kenner lilikuwa lile friji alilowekwa mtoto.
Friji hilo lilipokuwa likifika katika sehemu hiyo pembeni ya kanisa, hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba ndani ya friji lile kulikuwa na mtoto. Kama vilivyokuwa vitu vingine, hata lile friji washirika wa kanisa hilo wakaamua kulipuuzia na wao kuingia kanisani.
Maombi yaliendelea, huku kila mmoja akiwa kwenye uwepo wa Mungu, ghafla wakaanza kusikia sauti ya mtoto ikilia. Hawakujua sauti hiyo ilitoka wapi, wakabaki wakiangaliana tu, kila mwenye mtoto, alimwangalia mtoto wake, alikuwa kimya, sasa hiyo sauti ya mtoto ilitoka wapi?
Ilikuwa ni usiku sana, saa zao zilionyesha kwamba tayari ilikuwa ni saa sita usiku, sasa sauti ya mtoto hiyo ilitokea upande gani na wakati watoto wote ndani ya kanisa walikuwa wamelala.
“Who is that baby?” (Mtoto gani huyo?) aliuliza mchungaji kwa sauti ya chini.
Mwanaume mmoja akatoka akaelekea nje, alitaka kumuona huyo mtoto aliyekuwa akilia, alipofika nje, hakuweza kuisikia sauti hiyo, alijaribu kuangalia huku na kule, ukimya mkubwa ulitawala, ni vitu vilivyoletwa na maji ya bahari ndivyo vilivyoonekana.
Akarudi ndani na kutoa taarifa kwamba hakukuwa na mtoto yoyote yule. Huku mchungaji akijiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, sauti ya mtoto huyo ikaanza kusikika tena.
Mchungaji akaamua kutoka yeye mwenyewe, mkononi mwake alikuwa na rozali na kila hatua aliyokuwa akipiga, alikuwa akimuomba Mungu. Alipofika nje, akaanza kuangalia huku na kule, bado sauti ya mtoto yule ilikuwa ikisikika lakini kila alipoangalia huku na kule, hakumuona.
“Huyo mtoto yupo wapi?” aliuliza mshirika mmoja.
“Hata mimi sijui, sauti naisikia, ila mahali alipokuwa, sijui yupo wapi,” alijibu mshirika mmoja.
Mchungaji aliendelea kusogea mpaka kulipokuwa na friji moja, humo ndipo sauti ilipotoka, kwa haraka pasipo kupoteza muda mchungaji akalifungua friji hilo, alichokutana nacho hakuamini, macho yake yakatua kwa mtoto mdogo ambaye alionekana kuzaliwa siku hiyohiyo, alikuwa wa kiume, harakaharaka akamtoa kutoka ndani ya friji hilo.
Washirika wote waliokuwa nje ya kanisa hilo ambao macho yao yalikuwa yakimwangalia mchungaji huyo walibaki kushangaa, wakasogea mpaka mchungaji alipokuwa na kuanza kumwangalia mtoto huyo.
Alikuwa mzuri wa sura lakini kila mmoja akaanza kumuonea huruma, bado mwili wake ulikuwa na damu nyingi zilizoganda. Walichokifanya ni kumchukua na kwenda naye kanisani, kitu cha kwanza kabisa walichomfanyia ni maombezi kisha kujadiliana mtu ambaye alitakiwa kumchukua mtoto huyo kwa ajili ya kumlea baada ya kutoa taarifa polisi.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mmoja, alikuwa mtu mwenye uwezo wa kifedha humo kanisani.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mwingine, mjane ambaye mtoto wake pekee alikufa baada ya kuugua ugonjwa wa polio.
Alichoamua mchungaji ni kumgawia mwanamke yule mjane mtoto huyo na kwenda kuishi naye kwani maisha ya upweke aliyokuwa akiishi waliamini kwamba mtoto huyo angempa furaha. Mwanamke yule mjane akamchukua mtoto huyo na kumpa jina la Dylan.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumapili