Utajiri wenye uchungu

NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Nne.

Utajiri mkubwa ulikuwa mbele yake lakini hakuwa na muda wa kuuchukua, kitu pekee alichokiangalia kilikuwa ni chakula tu. Hakujua afanye nini, alibaki akizunguka kwa kwenda huku na kule, yaani apande ngazi, mara ashuke, alikuwa akijifikiria tu ni kitu gani alitakiwa kufanya kuiokoa nafsi yake.
Wakati akizunguka huku na kule katika floo hiyo ya mia moja na ishrini ndipo akakumbuka kwamba katika floo ya mia na kumi na nane kulikuwa na mgahawa wa McDonald ambao ulitumika kwa watu waliokuwa wakifanya biashara katika jengo hilo.
Akaelekea kwenye dirisha na kuchungulia, maji yaliendelea kupungua na katika kipindi hicho ndiyo yalikuwa yakienda katika floo hiyo. Hakutaka kuchelewa, akaanza kuteremka kuelekea katika floo hiyo.
Alipoifikia, kulikuwa na maji yaliyomfikia kiunoni, hakutaka kurudi nyuma, tumbo lake lilikuwa tupu hivyo pasipo kufanya harakati za kutafuta chakula, basi angeweza kufa kwa njaa na si kwa mafuriko.
Kulikuwa na vyakula mbalimbali, vyote hivyo vilikuwa vimelowanishwa na maji. Kulikuwa na pizza, bugger, sandwich na vyakula vingine lakini vyote hivyo havikutamanika hata kidogo.
Mbele kabisa macho yake yakatua katika friji moja lililokuwa limepachikwa ukutani, akaanza kulifuata huku akiwa na kiu ya kutaka kunywa hata vinywaji vilivyokuwa humo ndani, alipolifikia, akalifungua na kuangalia ndani.
Kulikuwa na vinywaji vingi, mbali na vinywaji hivyo, pia kulikuwa na biskuti. Hakutaka kuchelewa, aliona kama angekosa, haraka sana akaanza kuchukua vinywaji na biskuti hizo na kuanza kula.
Alikula kwa fujo, hakumeza kilichokuwa mdomoni, akakiweka kingine. Ulaji wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na njaa. Kula tu, alitumia muda wa dakika kumi na tano, tumbo lake likawa afadhali.
Kumbukumbu za mpenzi wake zikamjia tena, akapanda kwenye floo ile aliyotoka, yenye almasi nyingi na kutulia. Machozi yakaanza kumwagika, hakuamini kama mwisho wa siku angekosa kila kitu, yaani mtoto wake na mpenzi wake, hakika moyo wake ulimuuma mno.
“Ni lazima niondoke, siwezi kukaa hapa,” alisema James.
Kitu kilichokuwa kichwani mwake ni kwamba ilikuwa lazima achukue almasi zile na kuondoka nazo kwani bila kufanya hivyo asingeweza kuzipata tena kwani endapo maji yangepungua, ulinzi ungeimarishwa tena, ilikuwa ni bora kuzichukua kwani hata wamiliki wangekuja, wangehisi kwamba maji yalizihamisha almasi hizo.
Alichokifanya ni kurudi kulekule alipokuta chakula na kisha kuling’oa friji lile na kutoa kila kitu, kwa kutumia nguvu zake, akalibeba na kupanda nalo kwenda juu. Huko, akaufungua mlango wa chumba kile kilichokuwa na almasi, akaziangalia kwa tamaa kubwa kisha kuanza kuzitoa na kuziweka ndani ya friji lile.
Zilikuwa nyingi zenye uzito wa kilo tano ambazo kwa hesabu ya harakaharaka iliyokuja kichwani mwake, ilikuwa ni zaidi ya kupata dola bilioni hamsini, kiasi kikubwa sana cha fedha ambacho kingemfanya kuwa miongoni mwa mabilionea kumi wakubwa katika ulimwengu huu.
Alipomaliza kuzipakia, hakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka, akaingia ndani ya friji, akachukua mbao kubwa ambayo alitaka kuitumia kupigia kasi kuelekea sehemu isiyokuwa na maji.
Kwa sababu tayari giza lilianza kuingia, akajipa uhakika kwamba sehemu ambayo angekwenda ingekuwa salama kwani kote huko kulikuwa na maji, yaani Jiji la New Orleans halikuonekana, lilikuwa bahari tu.
Naye akaingia ndani ya lile friji, hakutaka kuendelea kukaa ndani ya jengo hilo, akaanza kupiga kasi huku akiwa ameutoa mlango wa friji, almasi zilikuwa humo ndani tena huku akiwa amezifunika kwa nguo.
Hakujua alipokuwa akielekea, kitu pekee alichokijua ni kwamba upande aliokuwa akielekea ni ule usiokuwa na bahari. Alikuwa akipiga kasia, tena huku kukiwa na giza tayari, hakutaka kuangalia alipotoka, macho yake yalikuwa mbele tu.
Majengo marefu ambayo nayo yalifunikwa na maji yalikuwa yakionekana vizuri machoni mwake, hali ilitisha sana, alijikuta moyo wake ukiumia na machozi kuanza kumbubujika.
Hakutaka kusubiri, aliendelea na safari yake. Safari hiyo ilianza saa moja usiku, alijikuta akienda, akipiga kasia zaidi, saa nne baadaye, bado hakuwa amefika sehemu yoyote ya nchi kavu, bado alikuwa sehemu yenyemaji mengi.
Wakati akiendelea na safari yake, ndipo alipoanza kusikia muungurumo wa helkopta, hakutaka kuomba msaada, alichokifanya ni kujifunika na zile nguo zilizokuwa zimefunika almasi na kutulia.
Aliisikia helkopta ile ikipita juu yake, hakutaka kufungua, hakutaka kuonekana kwani aliamini kwamba kama angeonekana na kuokolewa basi zile almasi ambazo alikuwa nazo zingechukuliwa na hivyo yeye kubaki mikono mitupu.
“Siwezi kutamani kuokolewa na wakati nina utajiri mkubwa...” alisema James huku akiwa chini ya nguo zile.
Aliendelea na safari yake kama kawaida. Akafika sehemu ambayo maji yake yalionekana kupita kwa kasi kidogo. Hakutaka kusumbuka kufikiria sehemu hiyo kulikuwa na nini, alijua jinsi hali ilivyokuwa hivyo akagundua kwamba sehemu hiyo kulikuwa na mto.
“Mto Mississippi...” alijikuta akijisemea.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe, japokuwa maji yalikuwa yamejaza sana lakini aligundua kwamba sehemu iliyokuwa ikipitisha maji hayo kwa kasi kulikuwa na Mto Mississippi. Hakutaka kugeuza, akataka aelekee mbele huku akijua kwamba ili kuyaokoa maisha yake na utajiri mkubwa aliokuwa nao, ilikuwa ni lazima kuvuka eneo hilo. Akapiga moyo konde.
Akaendelea kupiga kasia, japokuwa alikuwa amechoka lakini hakutaka kupumzika, hakutaka kukata tamaa, aliendelea mbele zaidi tena kwa sababu alikuwa akivuka sehemu yenye mto uliokuwa ukipeleka maji kwa kasi, hata nguvu zake za kupiga kasi ziliongezeka.
Friji likaanza kupelekwa huku na kule, hakutaka kukata tamaa, aliendelea zaidi lakini maji yale yalionekana kuwa na nguvu kubwa. Hakuacha, kama kufa, ilikuwa lazima afe lakini si kuuacha utajiri ule kupotea mikononi mwake.
Akaendelea kupiga kasia, ikafika kipindi akashindwa kabisa kuendelea, akajikuta akiacha na kuona mto huo ungempeleka wapi. Alikwenda mbele mpaka sehemu ambayo maji ya bahari ile yalipoanza kupungua na mwisho kuishia kabisa hivyo kubaki kwenye maji ya mto tu.
Pembeni yake hakukuwa na majengo yoyote, ni pori kubwa lililokuwa likizinguka mto Mississippi. Alitamani kulipeleka friji lile pembezoni mwa mto ule ikiwezekana hata kutulia katika pori hilo lakini hakuwa na nguvu za kufanya hivyo.
Aliendelea kusonga mbele huku akiwa hoi. Alichoka, usingizi ulimkamata lakini hakutaka kulala kabisa, aliendelea kusonga mbele lakini mara ghafla akaanza kusikia sauti kubwa ya maji.
Akashtuka, akaangalia mbele yake, umbali kama hatua mia moja za miguu ya binadamu akaona maji yakielekea chini, yaani kulikuwa na maporomoko ya Mto Mississippi yaliyoitwa St. Antony yaliyopo Kaskazini mwa Jiji la New Orleans.
“Mungu wangu!” alijikuta akisema.
Kitu cha kwanza kabisa kilichokuja akilini mwake ni kwamba kama angeruhusu friji hilo lidondoke katika maporomoko hayo yaliyokuwa na urefu wa mita mia moja basi ingekuwa rahisi kwake kupoteza almasi hizo kwani friji lingeanguka, wakati linafiki chini lingejipindua na hivyo almasi zote kutoka ndani ya friji.
Hakutaka kuona hilo likitokea, alihangaika sana, alipambana kuzipigania almasi hivyo, kwa nafasi aliyokuwa nayo, japokuwa alichoka lakini hakutaka kuruhusu jambo hilo litokee. Nguvu zikamjia upya, friji lilizidi kusogea kule kulipokuwa na maporomoko, alichokifanya ni kupiga kasia kurudi nyuma, tena kwa kasi, ila kutokana na nguvu za maji ya mto ule, akajikuta akifanya jambo lisilosaidia, friji lile likazidi kupelekwa kule kulipokuwa na maporomoko yale, ndoto za kuwa bilionea zikaanza kupotea kichwani mwake.
Akabakiza kama hatua thelathini tu kuyafikia maporomoko yale, maporomoko ambayo yangeupoteza utajiri aliokuwa nao ndani ya friji lile.
****
“Lord have mercy on us...” (Mungu utuhurumie...)
Hayo yalikuwa maneno machache yaliyotoka kinywani mwa mchungaji wa Kanisa la Water of Life lililokuwa Mji wa Kenner, pembezoni mwa Jiji la New Orleans. Washirika wote walitoka kanisani huku wakionekana kuwa na majonzi mazito, hali iliyokuwa ikionekana iliwatisha wote, hawakuamini kama kweli maji yalihama kutoka baharini na kulifunika jiji la New Orleans.
Hapo Kenner ilionekana kama ufukweni kwani maji yote ya bahari yaliyoifunika New Orleans, yaliishia ndani ya jiji hilo. Walipoangalia kule yalipoanzia, hakukuwa na jengo lolote lililoonekana, kote huko kulifunikwa na maji na kulifanya eneo lote kuonekana kama bahari moja kubwa.
Hilo lilionekana pigo kubwa lililowahi kuikumba nchi ya Marekani, achana na lile shambulizi la septemba 11 mwaka 2001 ambapo majengo mawili ya WTC yalipolipuka baada ya kugongwa na ndege.
Washirika hao wakarudi kanisani kwani bado walikuwa kwenye maombi mazito katika kipindi hicho cha mkesha wa mwisho wa mwaka, kilichofuatia ni kuanza kuomba, walimuomba Mungu awanusuru na kile kilichokuwa kimetokea. Siku hiyo ilikuwa ni ya huzuni kubwa, vyombo vya habari viliendelea kutangaza hali iliyokuwa ikiendelea katika Jiji la New Orleans japokuwa taarifa za awali zilisema kwamba hakukuwa na mtu aliyekufa, ila majengo na vitu vingine viliharibika sana.
Vitu vinavyoweza kuhamishwa vilihama na vingi vilionekana juu ya maji vikielea, vingi vilipelekwa na maji mpaka huko Kenner, na vitu ambavyo vilipelekwa na maji hayo mpaka Kenner lilikuwa lile friji alilowekwa mtoto.
Friji hilo lilipokuwa likifika katika sehemu hiyo pembeni ya kanisa, hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba ndani ya friji lile kulikuwa na mtoto. Kama vilivyokuwa vitu vingine, hata lile friji washirika wa kanisa hilo wakaamua kulipuuzia na wao kuingia kanisani.
Maombi yaliendelea, huku kila mmoja akiwa kwenye uwepo wa Mungu, ghafla wakaanza kusikia sauti ya mtoto ikilia. Hawakujua sauti hiyo ilitoka wapi, wakabaki wakiangaliana tu, kila mwenye mtoto, alimwangalia mtoto wake, alikuwa kimya, sasa hiyo sauti ya mtoto ilitoka wapi?
Ilikuwa ni usiku sana, saa zao zilionyesha kwamba tayari ilikuwa ni saa sita usiku, sasa sauti ya mtoto hiyo ilitokea upande gani na wakati watoto wote ndani ya kanisa walikuwa wamelala.
“Who is that baby?” (Mtoto gani huyo?) aliuliza mchungaji kwa sauti ya chini.
Mwanaume mmoja akatoka akaelekea nje, alitaka kumuona huyo mtoto aliyekuwa akilia, alipofika nje, hakuweza kuisikia sauti hiyo, alijaribu kuangalia huku na kule, ukimya mkubwa ulitawala, ni vitu vilivyoletwa na maji ya bahari ndivyo vilivyoonekana.
Akarudi ndani na kutoa taarifa kwamba hakukuwa na mtoto yoyote yule. Huku mchungaji akijiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, sauti ya mtoto huyo ikaanza kusikika tena.
Mchungaji akaamua kutoka yeye mwenyewe, mkononi mwake alikuwa na rozali na kila hatua aliyokuwa akipiga, alikuwa akimuomba Mungu. Alipofika nje, akaanza kuangalia huku na kule, bado sauti ya mtoto yule ilikuwa ikisikika lakini kila alipoangalia huku na kule, hakumuona.
“Huyo mtoto yupo wapi?” aliuliza mshirika mmoja.
“Hata mimi sijui, sauti naisikia, ila mahali alipokuwa, sijui yupo wapi,” alijibu mshirika mmoja.
Mchungaji aliendelea kusogea mpaka kulipokuwa na friji moja, humo ndipo sauti ilipotoka, kwa haraka pasipo kupoteza muda mchungaji akalifungua friji hilo, alichokutana nacho hakuamini, macho yake yakatua kwa mtoto mdogo ambaye alionekana kuzaliwa siku hiyohiyo, alikuwa wa kiume, harakaharaka akamtoa kutoka ndani ya friji hilo.
Washirika wote waliokuwa nje ya kanisa hilo ambao macho yao yalikuwa yakimwangalia mchungaji huyo walibaki kushangaa, wakasogea mpaka mchungaji alipokuwa na kuanza kumwangalia mtoto huyo.
Alikuwa mzuri wa sura lakini kila mmoja akaanza kumuonea huruma, bado mwili wake ulikuwa na damu nyingi zilizoganda. Walichokifanya ni kumchukua na kwenda naye kanisani, kitu cha kwanza kabisa walichomfanyia ni maombezi kisha kujadiliana mtu ambaye alitakiwa kumchukua mtoto huyo kwa ajili ya kumlea baada ya kutoa taarifa polisi.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mmoja, alikuwa mtu mwenye uwezo wa kifedha humo kanisani.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mwingine, mjane ambaye mtoto wake pekee alikufa baada ya kuugua ugonjwa wa polio.
Alichoamua mchungaji ni kumgawia mwanamke yule mjane mtoto huyo na kwenda kuishi naye kwani maisha ya upweke aliyokuwa akiishi waliamini kwamba mtoto huyo angempa furaha. Mwanamke yule mjane akamchukua mtoto huyo na kumpa jina la Dylan.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumapili
 
*****
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Nne.

Utajiri mkubwa ulikuwa mbele yake lakini hakuwa na muda wa kuuchukua, kitu pekee alichokiangalia kilikuwa ni chakula tu. Hakujua afanye nini, alibaki akizunguka kwa kwenda huku na kule, yaani apande ngazi, mara ashuke, alikuwa akijifikiria tu ni kitu gani alitakiwa kufanya kuiokoa nafsi yake.
Wakati akizunguka huku na kule katika floo hiyo ya mia moja na ishrini ndipo akakumbuka kwamba katika floo ya mia na kumi na nane kulikuwa na mgahawa wa McDonald ambao ulitumika kwa watu waliokuwa wakifanya biashara katika jengo hilo.
Akaelekea kwenye dirisha na kuchungulia, maji yaliendelea kupungua na katika kipindi hicho ndiyo yalikuwa yakienda katika floo hiyo. Hakutaka kuchelewa, akaanza kuteremka kuelekea katika floo hiyo.
Alipoifikia, kulikuwa na maji yaliyomfikia kiunoni, hakutaka kurudi nyuma, tumbo lake lilikuwa tupu hivyo pasipo kufanya harakati za kutafuta chakula, basi angeweza kufa kwa njaa na si kwa mafuriko.
Kulikuwa na vyakula mbalimbali, vyote hivyo vilikuwa vimelowanishwa na maji. Kulikuwa na pizza, bugger, sandwich na vyakula vingine lakini vyote hivyo havikutamanika hata kidogo.
Mbele kabisa macho yake yakatua katika friji moja lililokuwa limepachikwa ukutani, akaanza kulifuata huku akiwa na kiu ya kutaka kunywa hata vinywaji vilivyokuwa humo ndani, alipolifikia, akalifungua na kuangalia ndani.
Kulikuwa na vinywaji vingi, mbali na vinywaji hivyo, pia kulikuwa na biskuti. Hakutaka kuchelewa, aliona kama angekosa, haraka sana akaanza kuchukua vinywaji na biskuti hizo na kuanza kula.
Alikula kwa fujo, hakumeza kilichokuwa mdomoni, akakiweka kingine. Ulaji wake tu ulionyesha ni jinsi gani alikuwa na njaa. Kula tu, alitumia muda wa dakika kumi na tano, tumbo lake likawa afadhali.
Kumbukumbu za mpenzi wake zikamjia tena, akapanda kwenye floo ile aliyotoka, yenye almasi nyingi na kutulia. Machozi yakaanza kumwagika, hakuamini kama mwisho wa siku angekosa kila kitu, yaani mtoto wake na mpenzi wake, hakika moyo wake ulimuuma mno.
“Ni lazima niondoke, siwezi kukaa hapa,” alisema James.
Kitu kilichokuwa kichwani mwake ni kwamba ilikuwa lazima achukue almasi zile na kuondoka nazo kwani bila kufanya hivyo asingeweza kuzipata tena kwani endapo maji yangepungua, ulinzi ungeimarishwa tena, ilikuwa ni bora kuzichukua kwani hata wamiliki wangekuja, wangehisi kwamba maji yalizihamisha almasi hizo.
Alichokifanya ni kurudi kulekule alipokuta chakula na kisha kuling’oa friji lile na kutoa kila kitu, kwa kutumia nguvu zake, akalibeba na kupanda nalo kwenda juu. Huko, akaufungua mlango wa chumba kile kilichokuwa na almasi, akaziangalia kwa tamaa kubwa kisha kuanza kuzitoa na kuziweka ndani ya friji lile.
Zilikuwa nyingi zenye uzito wa kilo tano ambazo kwa hesabu ya harakaharaka iliyokuja kichwani mwake, ilikuwa ni zaidi ya kupata dola bilioni hamsini, kiasi kikubwa sana cha fedha ambacho kingemfanya kuwa miongoni mwa mabilionea kumi wakubwa katika ulimwengu huu.
Alipomaliza kuzipakia, hakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka, akaingia ndani ya friji, akachukua mbao kubwa ambayo alitaka kuitumia kupigia kasi kuelekea sehemu isiyokuwa na maji.
Kwa sababu tayari giza lilianza kuingia, akajipa uhakika kwamba sehemu ambayo angekwenda ingekuwa salama kwani kote huko kulikuwa na maji, yaani Jiji la New Orleans halikuonekana, lilikuwa bahari tu.
Naye akaingia ndani ya lile friji, hakutaka kuendelea kukaa ndani ya jengo hilo, akaanza kupiga kasi huku akiwa ameutoa mlango wa friji, almasi zilikuwa humo ndani tena huku akiwa amezifunika kwa nguo.
Hakujua alipokuwa akielekea, kitu pekee alichokijua ni kwamba upande aliokuwa akielekea ni ule usiokuwa na bahari. Alikuwa akipiga kasia, tena huku kukiwa na giza tayari, hakutaka kuangalia alipotoka, macho yake yalikuwa mbele tu.
Majengo marefu ambayo nayo yalifunikwa na maji yalikuwa yakionekana vizuri machoni mwake, hali ilitisha sana, alijikuta moyo wake ukiumia na machozi kuanza kumbubujika.
Hakutaka kusubiri, aliendelea na safari yake. Safari hiyo ilianza saa moja usiku, alijikuta akienda, akipiga kasia zaidi, saa nne baadaye, bado hakuwa amefika sehemu yoyote ya nchi kavu, bado alikuwa sehemu yenyemaji mengi.
Wakati akiendelea na safari yake, ndipo alipoanza kusikia muungurumo wa helkopta, hakutaka kuomba msaada, alichokifanya ni kujifunika na zile nguo zilizokuwa zimefunika almasi na kutulia.
Aliisikia helkopta ile ikipita juu yake, hakutaka kufungua, hakutaka kuonekana kwani aliamini kwamba kama angeonekana na kuokolewa basi zile almasi ambazo alikuwa nazo zingechukuliwa na hivyo yeye kubaki mikono mitupu.
“Siwezi kutamani kuokolewa na wakati nina utajiri mkubwa...” alisema James huku akiwa chini ya nguo zile.
Aliendelea na safari yake kama kawaida. Akafika sehemu ambayo maji yake yalionekana kupita kwa kasi kidogo. Hakutaka kusumbuka kufikiria sehemu hiyo kulikuwa na nini, alijua jinsi hali ilivyokuwa hivyo akagundua kwamba sehemu hiyo kulikuwa na mto.
“Mto Mississippi...” alijikuta akijisemea.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe, japokuwa maji yalikuwa yamejaza sana lakini aligundua kwamba sehemu iliyokuwa ikipitisha maji hayo kwa kasi kulikuwa na Mto Mississippi. Hakutaka kugeuza, akataka aelekee mbele huku akijua kwamba ili kuyaokoa maisha yake na utajiri mkubwa aliokuwa nao, ilikuwa ni lazima kuvuka eneo hilo. Akapiga moyo konde.
Akaendelea kupiga kasia, japokuwa alikuwa amechoka lakini hakutaka kupumzika, hakutaka kukata tamaa, aliendelea mbele zaidi tena kwa sababu alikuwa akivuka sehemu yenye mto uliokuwa ukipeleka maji kwa kasi, hata nguvu zake za kupiga kasi ziliongezeka.
Friji likaanza kupelekwa huku na kule, hakutaka kukata tamaa, aliendelea zaidi lakini maji yale yalionekana kuwa na nguvu kubwa. Hakuacha, kama kufa, ilikuwa lazima afe lakini si kuuacha utajiri ule kupotea mikononi mwake.
Akaendelea kupiga kasia, ikafika kipindi akashindwa kabisa kuendelea, akajikuta akiacha na kuona mto huo ungempeleka wapi. Alikwenda mbele mpaka sehemu ambayo maji ya bahari ile yalipoanza kupungua na mwisho kuishia kabisa hivyo kubaki kwenye maji ya mto tu.
Pembeni yake hakukuwa na majengo yoyote, ni pori kubwa lililokuwa likizinguka mto Mississippi. Alitamani kulipeleka friji lile pembezoni mwa mto ule ikiwezekana hata kutulia katika pori hilo lakini hakuwa na nguvu za kufanya hivyo.
Aliendelea kusonga mbele huku akiwa hoi. Alichoka, usingizi ulimkamata lakini hakutaka kulala kabisa, aliendelea kusonga mbele lakini mara ghafla akaanza kusikia sauti kubwa ya maji.
Akashtuka, akaangalia mbele yake, umbali kama hatua mia moja za miguu ya binadamu akaona maji yakielekea chini, yaani kulikuwa na maporomoko ya Mto Mississippi yaliyoitwa St. Antony yaliyopo Kaskazini mwa Jiji la New Orleans.
“Mungu wangu!” alijikuta akisema.
Kitu cha kwanza kabisa kilichokuja akilini mwake ni kwamba kama angeruhusu friji hilo lidondoke katika maporomoko hayo yaliyokuwa na urefu wa mita mia moja basi ingekuwa rahisi kwake kupoteza almasi hizo kwani friji lingeanguka, wakati linafiki chini lingejipindua na hivyo almasi zote kutoka ndani ya friji.
Hakutaka kuona hilo likitokea, alihangaika sana, alipambana kuzipigania almasi hivyo, kwa nafasi aliyokuwa nayo, japokuwa alichoka lakini hakutaka kuruhusu jambo hilo litokee. Nguvu zikamjia upya, friji lilizidi kusogea kule kulipokuwa na maporomoko, alichokifanya ni kupiga kasia kurudi nyuma, tena kwa kasi, ila kutokana na nguvu za maji ya mto ule, akajikuta akifanya jambo lisilosaidia, friji lile likazidi kupelekwa kule kulipokuwa na maporomoko yale, ndoto za kuwa bilionea zikaanza kupotea kichwani mwake.
Akabakiza kama hatua thelathini tu kuyafikia maporomoko yale, maporomoko ambayo yangeupoteza utajiri aliokuwa nao ndani ya friji lile.
****
“Lord have mercy on us...” (Mungu utuhurumie...)
Hayo yalikuwa maneno machache yaliyotoka kinywani mwa mchungaji wa Kanisa la Water of Life lililokuwa Mji wa Kenner, pembezoni mwa Jiji la New Orleans. Washirika wote walitoka kanisani huku wakionekana kuwa na majonzi mazito, hali iliyokuwa ikionekana iliwatisha wote, hawakuamini kama kweli maji yalihama kutoka baharini na kulifunika jiji la New Orleans.
Hapo Kenner ilionekana kama ufukweni kwani maji yote ya bahari yaliyoifunika New Orleans, yaliishia ndani ya jiji hilo. Walipoangalia kule yalipoanzia, hakukuwa na jengo lolote lililoonekana, kote huko kulifunikwa na maji na kulifanya eneo lote kuonekana kama bahari moja kubwa.
Hilo lilionekana pigo kubwa lililowahi kuikumba nchi ya Marekani, achana na lile shambulizi la septemba 11 mwaka 2001 ambapo majengo mawili ya WTC yalipolipuka baada ya kugongwa na ndege.
Washirika hao wakarudi kanisani kwani bado walikuwa kwenye maombi mazito katika kipindi hicho cha mkesha wa mwisho wa mwaka, kilichofuatia ni kuanza kuomba, walimuomba Mungu awanusuru na kile kilichokuwa kimetokea. Siku hiyo ilikuwa ni ya huzuni kubwa, vyombo vya habari viliendelea kutangaza hali iliyokuwa ikiendelea katika Jiji la New Orleans japokuwa taarifa za awali zilisema kwamba hakukuwa na mtu aliyekufa, ila majengo na vitu vingine viliharibika sana.
Vitu vinavyoweza kuhamishwa vilihama na vingi vilionekana juu ya maji vikielea, vingi vilipelekwa na maji mpaka huko Kenner, na vitu ambavyo vilipelekwa na maji hayo mpaka Kenner lilikuwa lile friji alilowekwa mtoto.
Friji hilo lilipokuwa likifika katika sehemu hiyo pembeni ya kanisa, hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba ndani ya friji lile kulikuwa na mtoto. Kama vilivyokuwa vitu vingine, hata lile friji washirika wa kanisa hilo wakaamua kulipuuzia na wao kuingia kanisani.
Maombi yaliendelea, huku kila mmoja akiwa kwenye uwepo wa Mungu, ghafla wakaanza kusikia sauti ya mtoto ikilia. Hawakujua sauti hiyo ilitoka wapi, wakabaki wakiangaliana tu, kila mwenye mtoto, alimwangalia mtoto wake, alikuwa kimya, sasa hiyo sauti ya mtoto ilitoka wapi?
Ilikuwa ni usiku sana, saa zao zilionyesha kwamba tayari ilikuwa ni saa sita usiku, sasa sauti ya mtoto hiyo ilitokea upande gani na wakati watoto wote ndani ya kanisa walikuwa wamelala.
“Who is that baby?” (Mtoto gani huyo?) aliuliza mchungaji kwa sauti ya chini.
Mwanaume mmoja akatoka akaelekea nje, alitaka kumuona huyo mtoto aliyekuwa akilia, alipofika nje, hakuweza kuisikia sauti hiyo, alijaribu kuangalia huku na kule, ukimya mkubwa ulitawala, ni vitu vilivyoletwa na maji ya bahari ndivyo vilivyoonekana.
Akarudi ndani na kutoa taarifa kwamba hakukuwa na mtoto yoyote yule. Huku mchungaji akijiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, sauti ya mtoto huyo ikaanza kusikika tena.
Mchungaji akaamua kutoka yeye mwenyewe, mkononi mwake alikuwa na rozali na kila hatua aliyokuwa akipiga, alikuwa akimuomba Mungu. Alipofika nje, akaanza kuangalia huku na kule, bado sauti ya mtoto yule ilikuwa ikisikika lakini kila alipoangalia huku na kule, hakumuona.
“Huyo mtoto yupo wapi?” aliuliza mshirika mmoja.
“Hata mimi sijui, sauti naisikia, ila mahali alipokuwa, sijui yupo wapi,” alijibu mshirika mmoja.
Mchungaji aliendelea kusogea mpaka kulipokuwa na friji moja, humo ndipo sauti ilipotoka, kwa haraka pasipo kupoteza muda mchungaji akalifungua friji hilo, alichokutana nacho hakuamini, macho yake yakatua kwa mtoto mdogo ambaye alionekana kuzaliwa siku hiyohiyo, alikuwa wa kiume, harakaharaka akamtoa kutoka ndani ya friji hilo.
Washirika wote waliokuwa nje ya kanisa hilo ambao macho yao yalikuwa yakimwangalia mchungaji huyo walibaki kushangaa, wakasogea mpaka mchungaji alipokuwa na kuanza kumwangalia mtoto huyo.
Alikuwa mzuri wa sura lakini kila mmoja akaanza kumuonea huruma, bado mwili wake ulikuwa na damu nyingi zilizoganda. Walichokifanya ni kumchukua na kwenda naye kanisani, kitu cha kwanza kabisa walichomfanyia ni maombezi kisha kujadiliana mtu ambaye alitakiwa kumchukua mtoto huyo kwa ajili ya kumlea baada ya kutoa taarifa polisi.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mmoja, alikuwa mtu mwenye uwezo wa kifedha humo kanisani.
“Naomba nikamlee mimi,” alisema mwanamke mwingine, mjane ambaye mtoto wake pekee alikufa baada ya kuugua ugonjwa wa polio.
Alichoamua mchungaji ni kumgawia mwanamke yule mjane mtoto huyo na kwenda kuishi naye kwani maisha ya upweke aliyokuwa akiishi waliamini kwamba mtoto huyo angempa furaha. Mwanamke yule mjane akamchukua mtoto huyo na kumpa jina la Dylan.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumapili
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Tano.

Kitu kilichomjia kichwani mwake ni kwamba alikuwa akienda kupoteza utajiri wote aliokuwa nao katika maporomoko yaliyokuwa mbele yake. Alijitahidi sana kupiga kasia kurudi nyuma lakini bado friji lile liliendelea kupelekwa kule kulipokuwa na maporomoko yale.
Akashindwa kujua ni kitu gani alitakiwa kufanya kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa ikilikuwa ni lazima almasi zile zitumbikie ndani ya mto na hivyo kuibuka na mikono mitupu.
“Haiwezekani....” alisema James.
Alichokifanya ni kuvua suruali yale aliyoivaa kisha kuchukua zile almasi na kuzitumbukiza ndani ya miguu ya suruali ile kisha kuifunga vilivyo. Hakuridhika, alichokifanya kama nyongeza ni kuvua fulana yake, akaichukua ile suruali na kuiingiza ndani ya fulana yake kisha kuifunga vilivyo, alipomaliza, akawa tayari kwa kutumbukia ndani ya maporomoko yale.
Friji lilizidi kusogea, akaanza kumuomba Mungu kwamba hata kama friji lile lingeanguka katika maporomoko yale basi huko chini asikutane na jiwe lolote lile ambalo lingemuumiza na hata kumuua. Wakati sala ikiendelea na hata kabla hajasema ‘Amen’ tayari friji lilifika katika maporomoko hayo na kuanza kuanguka chini.
James hakupiga kelele, alitulia ndani ya friji ambalo liliendelea kwenda chini na baada ya kufika umbali fulani, likajigeuza, James akatolewa ndani ya friji kwani tayari lilikaa juu-chini.
“Mungu nisaidie...” alisema maneno hayo, hakuwa na sentensi nyingine ambayo angeisema zaidi ya kumwambia Mungu amsaidie na kumuokoa katika hilo.
Alipotua chini, hakuwa ndani ya friji, yeye alikuwa upande mwingine na friji lilikuwa upande mwingine kabisa. Japokuwa alikuwa kwenye purukushani lakini hakuuachia mzigo wake wa almasi, aliushikilia vizuri kwani huo ndiyo ulikuwa kila kitu.
Akaulegeza mwili wake, akaanza kupelekwa na maji mpaka alipofika sehemu ambayo kulikuwa na watu wengi, hasa wasichana waliokuwa wakiogelea. Walipomuona tu, kitu cha kwanza kilikuwa ni kutoka mtoni huku wakipiga kelele, walihisi kwamba ilikuwa ni maiti.
Huko nje ya mto, walisimama na kuanza kumwangalia James ambaye bado aliulegeza mwili wake kama mtu aliyekufa hivyo kumfanya kuelea juu ya maji.
“Ni maiti au?” aliuliza msichana mmoja.
“Labda ni mhanga wa maji yaliyojaa huko New Orleans...” alijibu msichana mmoja.
Walichokifanya ni kuendelea kusimama mpaka pale James alipoanza kukurukakukuruka pale majini. Hali hiyo ikawafanya wasichana hao kugundua kwamba mtu huyo hakuwa amekufa kama walivyofikiria bali alikuwa hai kabisa.
Ingawa alikuwa amechoka lakini kwa kutumia miguu yake, James akaanza kupiga mbizi kuelekea nchi kavu, hakuchukua muda mwingi, akafika na kutulia pembeni kabisa huku akionekana kuchoka mno.
Almasi zile alizozitoa New Orleans, alikuwa nazo katika nguo ile, hakutaka mtu yeyote afahamu kilichokuwa ndani ya suruali ile. Wasichana wale waliogopa, wakati mwingine walimuona James kama mzimu ambao ulikuja kwa ajili ya kuwamaliza tu.
Hakukuwa na aliyemsogelea, wote wakajikaushia pembeni kabisa tena huku wengine wakiwa wanatetemeka.
“Where am I? (nipo wapi hapa?) aliuliza James huku akiwaangalia mmoja baada ya mwingine.
“St. Antony....” alijibu msichana mmoja huku akionekana kuwa na hofu usoni mwake.
Aliposikia hivyo, James hakutaka kubaki mahali hapo, akasimama na kuanza kuondoka zake tena huku akiwa na kipensi tu mwilini mwake. Kwa sababu ilikuwa ni alfajiri, hakutaka kuwa na haraka ya kuuza madini hayo, kitu alichokitaka ni kupata sehemu ya kuishi, hata kama ni ya muda, hiyo ingekuwa nafuu kwake.
*****
Safari yake ikaishia katika eneo lililokuwa na nyumba chache zilizojengwa kwa mpangilio mzuri. Sehemu hiyo ilionekana kama kijiji, alichokifanya ni kuifuata nyumba moja ambapo mbele kulikuwa na trekta moja kubwa, akaufuata mlango na kuanza kuugonga.
Wala haukuchukua muda mrefu, mlango ukafunguliwa na mzee mmoja aliyeshika mgobole, alipomuona James, akashtuka kwani mtu aliyesimama mbele yake alionekana kuwa dhaifu, mtu aliyechoka mno.
“Who the helll are you?” (Wewe ni nani?) aliuliza mzee yule huku akimnyooshea gobole lile.
“A Young Bilionaire...” (bilionea kijana) alijibu James huku akiuweka vizuri mzigo wake wa almasi.
Mzee yule alipomwangalia mwanaume huyo aliyejitambulisha kwa jina la Bilionea Kijana akabaki akimshangaa, kwake, mwanaume huyo alionekana kuwa dhoofu, masikini ambaye alihitaji msaada mkubwa kutoka kwake.
Akamkaribisha ndani ambapo James akahitaji kuletewa chakula kwani alikuwa amechoka mno na njaa ilimkamata. Wakati ameletewa chakula na kuanza kula, mke wa huyo mzee akafika huku akiwa na binti yake, wakabaki wakimshangaa James, alikuwa mgeni ambaye hawakuwa wakimfahamu, je kwa nini alifika hapo? Na kama alitoka sehemu, yeye alikuwa nani? Hawakuwa na jibu.
“Huyu ni nani?” aliuliza mwanamke huyo.
“Ni mtu aliyekuja kuomba msaada wa chakula, anaonekana kuchoka sana, nikaamua kumsaidia...” alijibu mzee huyo.
Wote walitulia huku wakimwangalia James ambaye alikuwa akila mfululizo hali iliyoonyesha kwamba alikuwa na njaa mno. Mzigo wake wa madini bado ulikuwa mkononi mwake, hakutaka mtu yeyote yule auguse kwani kwa kipindi hicho hiyo ndiyo ilikuwa roho yake.
“Wewe ni nani?” aliuliza mwanamke huyo.
“Naitwa Carthbert....” alidanganya James.
“Umetoka wapi?”
“Nimetoka mbali sana, ni mbali mno...”
“Ni wapi huko?” aliuliza mzee huyo.
“Harvey...nilikuwa nikiogelea mtoni, ghafla maji yakaanza kujaa, nikazama, nilipokuja kuibuka, nikaibukia huku,” aliendelea kudanganya.
“Pole sana...na nyie mlikumbwa na tsunami?”
“Kidogo sana, yaani sijajua kama wenzangu niliokuwa nikiogelea nao ni wazima au la kwani maji napo yalitukumba ingawa si sana,” alisema James.
Hakutaka kuzungumza ukweli hata kidogo. Kitu alichoogopa ni almasi zake kugundulika tu. Kwa sababu alikuwa nyumbani kwa watu hao, walichokifanya ni kumsaidia kwa kumwambia aishi nao mpaka pale ambapo angepata nafasi ya kurudi nyumbani kwake.
Hiyo ilikuwa furaha yake, hicho ndicho kitu alichokitaka, hakutaka kurudi, huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa safari yake ndefu. Katika nyumba hiyo, walikuwa watu wanne tu, yeye, mzee aliyejitambulisha kwa jina la Bellamy, mkewe Bellamy na binti yao, Claire aliyekuwa na miaka ishirini.
Akaonyeshwa chumba alichotakiwa kukaa, kwa sababu ilikuwa ni kijijini na hata nyumba zilizojengwa huko hazikuwa zile zenye ubora mkubwa, akatafuta sehemu nzuri na kuyaficha madini yale, sehemu ambayo alihakikisha kwamba kusingekuwa na mtu yeyote yule ambaye angeyaona.
Muda mwingi James alikuwa chumbani kwake, huko, alikuwa akilia tu, hakuamini kitu kilichotokea, tsunami ile iliyopiga New Orleans iliharibu kila kitu. Aliamini kwamba mpenzi wake, Catherine alifariki dunia lakini pia kitu kilichomuuma zaidi ni kwamba mtoto wake wa kwanza kabisa katika maisha yake naye alifariki dunia.
Moyo wake ulimuuma mno, alijisikia maumivu makali moyoni mwake, kuna kipindi hakuwa akilala, alikesha usiku mzima akiwa analia tu. Kwa kuwa nyumba hiyo ilikuwa na televisheni, alichokifanya ni kufuatilia kuona kama kulikuwa na mtu mwingine aliyepona katika tsunami ile.
Maji hayakuwa yamekauka vya kutosha, maghorofa yalianza kuonekana na kadiri upepo ulivyopiga ndivyo maji yalivyopungua kwa kurudi baharini. James alitia huruma, kwa kumwangalia tu ilikuwa rahisi kujua kwamba mtu huyo alikuwa kwenye matatizo makubwa.
Msichana Claire ndiye alikuwa mfariji wake, mara kwa mara alikuwa pamoja naye, alizungumza naye mambo mengi na ndiye alikuwa mtu wa kwanza kumwambia ukweli juu ya kile kilichotokea.
“Mungu wangu! Pole sana....” alisema Claire, alihuzunika, stori ya James ikaanza kumtoa machozi.
“Usijali Claire, namshukuru Mungu nipo hai japokuwa ninaumia sana,” alisema james.
“Kwa hiyo hujajua kama Catherine alinusurika au la?”
“Sijajua...”
“Na mtoto je?”
“Naye sijajua Claire...”
Kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo watu hao walivyozidi kuwa karibu. Muda mwingi msichana Claire alikuwa chumbani kwa James, huko walizungumza mengi huku msichana huyo naye akitumia muda mwingi kuelezea uhusiano wake na mwanaume wake aliyempenda lakini mwisho wa siku kuumizwa vibaya na mwanaume huyo kwa kumuoa msichana mwingine.
Wawili hao wakabaki wakifarijiana lakini mwisho wa faraja hiyo ikaishia kwenye kubadilishana mate na mwisho wa siku kujiangusha kitandani na kuanza kuvunja amri ya sita.
Hiyo ndiyo ikawa tabia yao, kila siku ilikuwa ni lazima kwa Claire kwenda chumbani kwa James na kulala naye kisiri pasipo wazazi wake kugundua lolote lile. Walijisahau, kila mmoja akajikuta akimpenda mwenzake, baada ya kukaa kwa mwezi mmoja, wakashindwa kuvumilia na mwisho wa siku mapenzi yao yakaanza kuonekana hata mbele ya wazazi wa Claire.
“Nini kinaendelea kati yenu?” aliuliza mama yake.
“Ninampenda James mama...”
“Unasemaje?”
“Ninampenda James, nataka tuoane...”
“Una uhakika unampenda?”
“Ndiyo mama! Ninampenda kwa moyo wa dhati na sidhani atafanya kama alivyofanya Stephen...James ni wa tofauti sana...” alisema Claire huku akianza kububujikwa na machozi ya hisia kali ya mapenzi.
Mama yake akaja kumwambia mzee Bellamy ambaye wala hakuwa na kipingamizi chochote kile, tena kwa sababu sehemu yenyewe ilikuwa kijijini, wanaume wachache, akakubaliana naye na hatimaye kujiweka wazi kabisa, kuwa pamoja kila sehemu huku wakionyeshana mapenzi ya mnato kama njiwa.
“James....”
“Sema mpenzi...”
“Kuna kitu nataka kukwambia.”
“Kitu gani?”
“Nahisi nina mimba...”
“Unahisi una nini?”
“Mimba....”
“Unahisi au unayo?”
“Ninayo..sijaona siku zangu, pia ninaziona dalili zote...” alisema Claire.
“Kweli?”
“Kweli tena!”
James akashindwa kuvumilia, hapohapo akamsogelea Claire na kilichofuatia ni kumkubatia kwa furaha. Baada ya kumpoteza mtoto wake ambaye mpaka kipindi hicho hakujua kama alikuwa hai au alikufa, hatimaye Mungu alimuona kwa jicho jingine kwa kumpa mimba Claire, hivyo akatarajia kupata mtoto baada ya miezi tisa. Furaha aliyokuwa nayo, haikuweza kuelezeka.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane kesho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom