Ndugu, nakushauri tena uwe unanisoma kwa vituo huku ukizingatia phrases ninazotumia! Kwa mfano unasema:
Hakuna popote nilipozungumzia suala la gharama za uzalishaji na hata kama ningezungumzia reference yangu kamwe isingekuwa Tanzania ambako tayari tuna takwimu zetu wenyewe!!! Sana sana, ningekupa mfano wa Australia ambako mwakajuzi Barrick Gold walilazimika kuuza moja ya migodi yao nchini humo ili ku-recover madeni!
Hebu wasome
Reuters hapa:Sifa za Cowal Mine? Endelea:Ingekuwa sisi hapa tungesema HAIWEZEKANI, tunaibiwa!! Haiwezekani mgodi unaoingiza MATRILIONI ya Dola halafu leo waseme wanauza kwa $550 Million!
Btw, kwanini walikuwa wanauza huo migodi na mingine? Hapa tena:Aidha, kama ningetaka kutoa mfano wa production cost, ningekupa mfano wa US, kwa kujiongeza, wasome mwenye Forbes
hapa!
Narudia... sijazungumza popote suala la gharama za uzalishaji na kama papo; NIONESHE! Nilichosema ni UZALISHAJI, yaani kiwango cha madini yanayozalishwa! Na kwavile Tanzania tuna takwimu zetu wenyewe, sikuzungumzia uzalishaji wa migodi yetu bali kwenye nchi zetu! Tena sio kutoka shithole countries bali kutoka US ili upate picha ya gold production!
Kisha unadai kwamba:Zile ripoti zipi?! Narudia, kwa kufahamu sisi tuna takwimu zetu wenyewe, sijazungumzia ripoti yoyote kwa hapa Tanzania hususani kwa hao ambao tumeshasema ni wezi. Kama kuna mahali nimetaja ripoti ya Acacia, au Ripoti ya Barrick kwa migodi yake ya Tanzania, NIONESHE!
Ripoti niliyoitaja ni miongoni za zile takwimu zetu wenyewe... Ripoti ya Profesa Mruma inayosema makinikia peke yake inazalisha tani 135! Ripoti inayosema tunawadai Barrick Dola 190 Billion... pesa ambayo hata tajiri namba moja duniani, HANA!!
Hapa pia, nilitoa mfano wa migodi ya US... so, kama na US nao ni shithole wanaoibiwa na Barrick, basi sawa! Na huwa natoa mfano wa huko kwa sababu NAHISI wenzetu sio shithole wanaoweza kuibiwa kirahisi rahisi tu tena na makampuni ya nje!Mbona kama unachanganya habari hata kama ulikaa huko migodini?! Suala la tani moja ya mchanga wanayodai inatoa 1gm of gold ina uhusiano gani na ujaji wa helikopta? Au unazungumzia mchanga upi? Manake kama ni makinikia, kwanini ije helikopta mara 4 kwa wiki kuchukua dhahabu inayotokana na makinikia wakati makinikia inasafirishwa?
Na hata kama unazungumzia hayo makinikia, ni wapi umepata habari kwamba kwenye tani 1 ya mchanga kuna gram moja ya dhahabu? Hapa JF ililetwa
Ripoti ya Makinikia kutoka kwa Profesa Mruma, na kwa mujibu wa maelezo yao walisema kwamba:Sasa wewe habari za
1 g/t umezitoa wapi?!
Unajua tatizo letu Watanzania huwa tunapenda habari za kuokoteza badala ya habari kutoka reliable sources na matokeo yake, Wanasiasa kila siku wanatudanganya na Wawekezaji pia wanatudangaya!!
Na hata tunapowashitukia Wawekezaji kwamba wanatudanganya, huwa hatuna uwezo wa kuwabana kwa hoja kwa sababu hoja zetu mara nyingi huonesha wazi wala hatufahamu tunadai au tunaibiwa nini na kwa kiwango gani!!!