Mafanikio ya sekta ya kazi na ajira Tanzania.
Kwenye sekta hii pamoja malalamiko ya ukosefu wa ajira lakini kuna hatua kubwa ya maendeleo iliyofikiwa na hasa ukizingatia kuwa hakuna sehemu yoyote duniani usiyosikia kelele hizi hata kwa hao mataifa makubwa kelele hizi nipo, lakini pia majirani zetu wanakimbila Tanzania kufatuta ajira kwa kuamini kuna nafuu ya kupata ajira jambo ambalo ni kweli.
Kwa mujibu wa takwimu za shirika la kazi duniani ILO na shirika la UNDP
Ugiriki matatizo ya ajira ni 92%
Spain matatizo ya ajira ni 55%
Italia matatizo ya ajira ni 38%
S.Afica matatizo ya ajira ni 40%
Kenya matatizo ya ajira ni 40%
Baadhi ya mafanikio ni kama yafuatayo:
- Vijana waoajiriwa ni 9,056,217 sawa na %80.6 ya vijana nguvu kazi yote ya vijana waliostahili kuajiriwa kwenye sekta rasmi na isiyo rasmi.
- Katika 2011/2012 jumla ya ajira 250,678 zilipatikana
- Katika mwaka 2013 inatarajiwa kutengenezwa ajira 800,000 kutokana na miradi ya TASAF, Ujenzi na barabara, maeneo ya uwekezaji (TIC), mamlaka ya ukanda wa uchumi(EPZA), kilimo, mawasiliano, viwanda, elimu, nishati, afya na utumishi kuu n.k.
- Fidia kwa watumishi wa umma baada ya kuumia kazini mwaka wa fedha uliokwisha jumla ya watumishi 176 walilipwa shilingi 19,999,000 kama fidia
- Vita dhidi ya ajira kwa watoto na mazingira hatarishi kazini, jumla ya watoto 22,243 wametolewa katika utumikishwaji na kupatiwa mafunzo ya fani mbalimbali ikiwemo elimu ya msingi watotot 8,402 elimu ya MEMKWA watoto 1,428 na elimu ya ufundi watoto 12,413
- Kuimarisha taarifa za ajira, ujasiliamali na utambuzi wa fursa za kujiajiri
- Ajira kwa wageni imedhibitiwa