Hebu tuwasome wenye mamlaka wanasemaje?Rasimu ya Jaji Warioba au ya katiba?na je ni rasimu ya tume ya warioba au tume ya raisi?
"1. Kuwa tume haikutumwa kwenda kuandaa rasimu itakayopendekeza uwepo wa serikali tatu , hivyo hayo ni mambo ambayo tume ilijitungia yenyewe , na hivyo Bunge la katiba litaenda kufanya uamuzi kwa misingi ya KURA .....na kila mmoja ajiandae kupokea maamuzi ya kura , hata kama yataenda kinyume na mawazo ya tume ya Warioba .
2. Wao hawakutumwa kwenda kupunguza mambo ya Muungano bali ni kwenda kuyaongeza kama vile suala la Afya, Elimu yalipaswa kuongezwa kwenye rasimu hiyo , ila tume imeenda kuyapunguza , hivyo wanatishia uhai wa Muungano na hivyo ni mawazo ambayo hayapaswi kuungwa mkono na mtu yeyote mwenye akili timamu" Dr. Gharib Bilal