Nalendwa
JF-Expert Member
- Aug 9, 2016
- 7,467
- 13,024
Ni Kweli hawajiamini. Eti wanadhani kutokuwa na ufahamu ndo heshima.
Kama unaoa mwanamke wenye elimu ndogo ili awe full time house girl na kutokuchallenge kitu chochote kwenye ndoa basi una maono mafupi na watoto wako huenda ukawanyima fursa ya kuwa na wazazi wote wawili wenye kuwasaidia kwenye mambo ya shule. Tafiti pia zinaonesha kuwa wazazi wote wawili wakiwa Wana elimu ya juu basi Hali ya familia inakuwa bora Zaidi.
Tatizo wanaume wengi mno mna uselfish fulani ya kutaka kuonekana mko juu sana na hamuwezi kukosolewa, na pia mnaona wanawake ni was sex , watoto na mambo ya nyumbani. Maono mafupi na mawazo ya kimasikini sana.
Hao uliowataja wote ni 60++ kiumri. Wametokea kizazi ambacho wanawake walikuwa hawasomeshwi sana , kwahiyo mtu mwenyewe degree kuoa la saba au diploma ilikuwa Sawa tu.
Kwa kizazi hiki na uchumi huu, hiyo combination inaleta maana Kweli? Na wanaume kuheshimu ndoa inaendana na elimu au ni tabia ya mtu?
Wewe kama mzazi huwezi kumkatisha mtoto wako was kike masomo eti ile aheshimu ndo, that makes no sense na utachekwa sana tena sana. Kuheshimu ndoa ni tabia ya mtu, na heshima ya ndoa inabidi ikae Kwa wote wawili, wanaume na wanawake. Unaogopa wasomi sababu unajua msomi anajitambua na hatokaa kwenye ndoa na wewe kama hujiheshimu. Kama wajijua ni mdhaifu, stay away from wasomi.
The whole point ya mtu ku "Question" Elimu?!..