Aiseeee nilidhani nateseka peke yangu katika maisha kumbe tuko wengi, mimi kuna kipindi nilipitia wakati mgumu sana tena sana yaani kila nachokifanya kinagoma, sio shambani sio mtaani hadi nikahisi mwezi wa 3 mwaka huu sitatoboa, maana kila unaemuambia shida zako nae anakupa matatizo yake hali ni mbaya, unakataa tamaa nakumbuka last time nikawaza niuze hii simu, godoro na vitu vya gheto nirudi home ila nikawaza home nitaenda kufanya nini na nilishakacha tangu 2016, kuna manzi yangu alikuwa anafanya kazi Tanga alikuwa ananipiga company maana anajua hali yangu yeye kasoma afya so alivyoua chuo tu akapata pa kushika, mimi nikawa kitaaa naganga njaa mwaka jana nikachoma hela kama milioni 2 hivi katika biashara bado kidogo nijiue

huyu manzi akashtuka nimi sijui nikashangaa kanitumia 50k kaniambia njoo Ta upumzike kwanza ujipange upya, to cut the story mwaka huu mwezi wa tatu ndio nilichoka nadaiwa kodi, mara shamba nililomaga limenishinda n.k nakumbuka siku hiyo nimebaki na mb 200 nikaandika uzi nikautupia kule kwenye Jukwaa la tenda na ajira baada ya hapo bundle likakata wadau wakaanza kunicheki nikapata msaada japo bado napambana maana sina kazi ila haya maisha ukiwa lele mama unaweza ukakimbia dunia hii au unaweza ufanye mambo ya ajabu ili usurvive hali inatisha, ila nimegiundua kwamba Mungu anatupa mitihani kutupima imani yetu juu yake na anatupa mitihani ambayo tunaweza kuikabili.. pia tuishi na watu vizuri haswa watu baki maana wao ndio wanaweza kukusaidia kuliko ndugu zako talking from the experience..
Marufuku kukataa tamaa
uzi ulinisave huu hapa
Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 25, muhitimu wa shahada ya ugavi na usafirishaji mwaka 2019 (Bachelor of Logistics and Transport Management) mimi ni moja kati ya vijana ambao tumemaliza chuo na kuingia mtaani kupambana na maisha bila kurudi nyumbani na hii ni mwendelezo tu wa...
www.jamiiforums.com