Jamani,naomba kuleta mrejesho wa maswahibu yangu!
Baada ya co-worker kujikata mkono kama jaribio la kujitoa uhai wake,nilisitisha safari ya Singida.
Lakini baada ya wiki moja niliamua kutengeneza dharura ya uongo kwa kumpanga rafiki yangu anipigie simu kunipa taarifa kuwa nahitajika kwetu haraka sana!(kwetu ni mkoani)
Basi jioni moja tukiwa tunaongea (huku nikiwa na hasira sana,japo sikutaka ajue),jamaa yangu akanipigia simu,akijifanya kaka yangu,akanambia nijitahidi ndani ya siku mbili nifike nyumbani kuna mambo muhimu yanahitaji uwepo wangu.
Baada ya kumaliza mazungumzo ya simu nikamwambia huyu mpnz wangu kuwa ninahitajika nyumbani haraka,inabidi kesho nipande gari kuelekea nyumbani,hakutia shaka!
Asubuhi ya siku iliyofuata nikapanda gari kuelekea Singida kwa mama watoto wangu.
Nimefika Singida,nikakuta familia yangu ikiwa poa kabisa,nikajisemea moyoni,huyu mwanamke (wa Tanga) anataka kuniharibia familia yangu hakika,kila nikiwaangalia wanangu wanavyofurahia uwepo wangu,na vizawadi kidogo nilivyowabebea nikajisemea hakika sitakubali kuiharibu familia yangu!
Usiku wa saa tano hivi nimelala na mke wangu,sijui shetani gani alinituma kushika simu ya mke wangu,nikaichukua nikaenda sebuleni,(yeye akiwa amelala baada ya game),kufungua inbox yake,loooh!nakuta SMS za wanaume kama 4 hivi,wote wanaonyesha wame-date naye,kwa sababu kila mmoja anasifia kuhusiana na mapenzi aliyopewa!
Mmoja ameandika," Bby una K ya moto sio mchezo,natamani iwe kila siku"
Mwingine,"Kwa ulivyokuwa mtamu,ungekuwa hauna mume ningekuoa kabisa"
Baada ya hapo nikajikuta najawa na hasira mbaya,ukizingatia si mtu niliyempenda ila nililazimika kuweka maslahi yangu kando ili kulinda maslahi ya watoto wetu,(maana bila watoto kiukweli tusingekuwa pamoja mpaka sasa)
Nimeendelea kuwepo mpaka sasa,na Alhamis natarajia kurejea Tanga,ila nina hasira moyoni isiyokifani,mbaya zaidi,kila nikisoma sent items zake kwa hao jamaa,naona anaonyesha ushirikiano chanya kwao!
Kimoyo moyo nawaza nikiondoka nimpotezee moja kwa moja,maana hata hamasa ya kusex naye sina kabisa!!
Nafikiria kuachana na wote nianze upya,(maana wa Tanga nampenda lakini kwa kiasi fulani naona hanifai kuwa mke) japo najiuliza ni mwanamke gani atakayenielewa kuwa nina watoto 3 na aishi nami na kuwapenda hao watoto wangu!!!???
Ushauri zaidi jamani,vijana wenzangu epuka sana kuanzisha mahusiano na mfanyakazi mwenzako,hasa kama hauna mpango wa kumuoa,ni hatari!!