Usiombe yakukute jamani, daah!!!

Usiombe yakukute jamani, daah!!!

Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Ufunuo wa yohana : Mlango 2:22 Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake.

Mithali : Mlango 6:32 Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.

Awali ni awali hakuna awali hakuna awali mbovu.. hapa ndipo nilipogundua wanaume wengi kwanini tunakufa mapema.. kwenye hii issue mkuu nimegundua yafuatayo..

Ni Mvivu wa kufikiri ama kukishughulisha kichwa cha juu ambacho ndicho chenye ufahamu na utashi.. kichwa hiki kama ungekishirikisha vzr naamini kabisa leo tusingekuwa tunazungumza haya mambo kwa ukubwa huu..

Pia hakikisha siku zote unapoanzisha mahusiano na mtu umejitafakari vya kutosha? Na je upo tayari kwa changamoto za mbeleni.. jipime mzee baba usiache tamaa zikuendeshe kwenye maamuzi ya msingi.. hapa kumbuka moyo huwa mdanganyifu kama nilivyosema hapo awali.

Tatu unapokuwa kwenye miji ya watu acha papara mzee baba.. fanya fisibilty study then yazoe mazingira kwanza..

Kumbuka kwa maelezo yako hujatueleza ubaya wowote wa mwanamke wako wa singida isipokuwa nafsi yako inakiri kumtenda vibaya mzazi mwenzio..

Moyo wako umefungwa kwenye zinaa, umeiuza nafsi yako mwenyewe!.

Then mimi naona hata kama utaharmonize hiyo situation, maswali ya msingi na ya kujiuliza ni haya..

Kwanini amwage damu kwa kujikata?
Damu hii ina maana gani?
Nini tafsiri ya damu tena ya mtu?

Anza kutafuta njia mapema ya kuiponya nafsi yako hao wa kumwaga damu hata ukiachana naye ujue haupo salama mana kiwanja ulichoingia sicho mkuu..
Huyo akijiua ujue ndugu zake watajua umemfanyia chezo ukoo utakukalia kikao..
 
Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Ufunuo wa yohana : Mlango 2:22 Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake.

Mithali : Mlango 6:32 Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.

Awali ni awali hakuna awali hakuna awali mbovu.. hapa ndipo nilipogundua wanaume wengi kwanini tunakufa mapema.. kwenye hii issue mkuu nimegundua yafuatayo..

Ni Mvivu wa kufikiri ama kukishughulisha kichwa cha juu ambacho ndicho chenye ufahamu na utashi.. kichwa hiki kama ungekishirikisha vzr naamini kabisa leo tusingekuwa tunazungumza haya mambo kwa ukubwa huu..

Pia hakikisha siku zote unapoanzisha mahusiano na mtu umejitafakari vya kutosha? Na je upo tayari kwa changamoto za mbeleni.. jipime mzee baba usiache tamaa zikuendeshe kwenye maamuzi ya msingi.. hapa kumbuka moyo huwa mdanganyifu kama nilivyosema hapo awali.

Tatu unapokuwa kwenye miji ya watu acha papara mzee baba.. fanya fisibilty study then yazoe mazingira kwanza..

Kumbuka kwa maelezo yako hujatueleza ubaya wowote wa mwanamke wako wa singida isipokuwa nafsi yako inakiri kumtenda vibaya mzazi mwenzio..

Moyo wako umefungwa kwenye zinaa, umeiuza nafsi yako mwenyewe!.

Then mimi naona hata kama utaharmonize hiyo situation, maswali ya msingi na ya kujiuliza ni haya..

Kwanini amwage damu kwa kujikata?
Damu hii ina maana gani?
Nini tafsiri ya damu tena ya mtu?

Anza kutafuta njia mapema ya kuiponya nafsi yako hao wa kumwaga damu hata ukiachana naye ujue haupo salama mana kiwanja ulichoingia sicho mkuu..
Huyo akijiua ujue ndugu zake watajua umemfanyia chezo ukoo utakukalia kikao..
Mkuu umenigusa sana,sana sanaaa!!!
Moyo wangu umesononeka sana,na tafakuri ya suluhu inazidi kuwa complex sana!
 
Jamani,naomba kuleta mrejesho wa maswahibu yangu!

Baada ya co-worker kujikata mkono kama jaribio la kujitoa uhai wake,nilisitisha safari ya Singida.
Lakini baada ya wiki moja niliamua kutengeneza dharura ya uongo kwa kumpanga rafiki yangu anipigie simu kunipa taarifa kuwa nahitajika kwetu haraka sana!(kwetu ni mkoani)

Basi jioni moja tukiwa tunaongea (huku nikiwa na hasira sana,japo sikutaka ajue),jamaa yangu akanipigia simu,akijifanya kaka yangu,akanambia nijitahidi ndani ya siku mbili nifike nyumbani kuna mambo muhimu yanahitaji uwepo wangu.

Baada ya kumaliza mazungumzo ya simu nikamwambia huyu mpnz wangu kuwa ninahitajika nyumbani haraka,inabidi kesho nipande gari kuelekea nyumbani,hakutia shaka!

Asubuhi ya siku iliyofuata nikapanda gari kuelekea Singida kwa mama watoto wangu.

Nimefika Singida,nikakuta familia yangu ikiwa poa kabisa,nikajisemea moyoni,huyu mwanamke (wa Tanga) anataka kuniharibia familia yangu hakika,kila nikiwaangalia wanangu wanavyofurahia uwepo wangu,na vizawadi kidogo nilivyowabebea nikajisemea hakika sitakubali kuiharibu familia yangu!

Usiku wa saa tano hivi nimelala na mke wangu,sijui shetani gani alinituma kushika simu ya mke wangu,nikaichukua nikaenda sebuleni,(yeye akiwa amelala baada ya game),kufungua inbox yake,loooh!nakuta SMS za wanaume kama 4 hivi,wote wanaonyesha wame-date naye,kwa sababu kila mmoja anasifia kuhusiana na mapenzi aliyopewa!
Mmoja ameandika," Bby una K ya moto sio mchezo,natamani iwe kila siku"

Mwingine,"Kwa ulivyokuwa mtamu,ungekuwa hauna mume ningekuoa kabisa"

Baada ya hapo nikajikuta najawa na hasira mbaya,ukizingatia si mtu niliyempenda ila nililazimika kuweka maslahi yangu kando ili kulinda maslahi ya watoto wetu,(maana bila watoto kiukweli tusingekuwa pamoja mpaka sasa)

Nimeendelea kuwepo mpaka sasa,na Alhamis natarajia kurejea Tanga,ila nina hasira moyoni isiyokifani,mbaya zaidi,kila nikisoma sent items zake kwa hao jamaa,naona anaonyesha ushirikiano chanya kwao!

Kimoyo moyo nawaza nikiondoka nimpotezee moja kwa moja,maana hata hamasa ya kusex naye sina kabisa!!

Nafikiria kuachana na wote nianze upya,(maana wa Tanga nampenda lakini kwa kiasi fulani naona hanifai kuwa mke) japo najiuliza ni mwanamke gani atakayenielewa kuwa nina watoto 3 na aishi nami na kuwapenda hao watoto wangu!!!???
Ushauri zaidi jamani,vijana wenzangu epuka sana kuanzisha mahusiano na mfanyakazi mwenzako,hasa kama hauna mpango wa kumuoa,ni hatari!!
 
Ndugu zangu,ukisikia njia panda Kali ndiyo hii!!
Mwaka 2010 niliachana na mpnz wangu nliyempenda sanaaa,ktk kipindi hicho cha mpito nilikutana na msichana mmoja mkoani huko,nikamtongoza ki-maskhara sana,(sikuwa serious kwa sababu sikumpenda kwa kweli) akakubali,nikajisemea moyoni huyu nakula then simrudii tena!

Kweli,nikamla msichana yule,(alikuwa mwaka wa kwanza Chuo cha diploma huko Mkoani),kwa uzembe wetu hatukutumia kinga,baada ya miezi kadhaa akaniambia anahisi ni mjamzito,nilishtuka kweli kwa sababu sikutaka kabisa kuwa na mtoto japo sikuchukua tahadhari kuliepuka hilo. Sikuikataa bali nilimshawishi atoe ile mimba,nikamtumia mpaka pesa ya kutolea,akakataa kabisa kuitoa na pesa yangu akanirudishia!(nikamtumia tena imsaidie kwa mambo yake mengine)

Baada ya mwaka mmoja,alijifungua mtoto anafanana na mimi sanaaa,hata kukataa isingewezekana,nikakubali kulea mtoto. Miaka miwili baadaye nikaanzisha mahusiano mengine,hayakudumu kwa sababu ya huyu mama wa mtoto wangu alikuwa karibu sana nami kimawasiliano juu ya maswala ya mtoto,jambo ambalo lilimkera mpnz wangu hiyo,akaamua kuachana na mimi!

Miaka yote hiyo tulikuwa tunakaa mbali mbali na huyo mama wa mtoto wangu,kutokana na upweke nilimuita Hugo mama wa mtoto nikae naye angalau kidogo niweze kutafuta kumpenda,then tuangalie uwezekano wa kuishi pamoja.(tulikaa kama miezi mitatu hivi kwa matazamio)

Ukweli alikuwa msichana mpole asiye na makuu,nikaamua kumtambulisha nyumbani rasmi,na kutambulika kuwa Huyo ndiye mchumba wangu!(akarejea kwao)

Baada ya mwaka mmoja,nikaenda kwa wazazi wake kuomba ridhaa ya kutambulika pia,wakanipa faini ya kumzalisha binti yao,nikatozwa kiasi fulani cha pesa,baada ya hapo ikawa rasmi pande zote mbili,japo nafsi yangu haikuwa imempenda kwa kweli!!

Mwaka 2014 mimi nilipata kazi,mkoani Tanga,yeye akapangwa Singida (yeye ni mwalimu),basi akawa ananitembelea Tanga mara kadhaa na maisha yakawa yanasonga!
Nilipoanzia kazi kuna binti mmoja alihamia akitokea mkoani Dodoma,tukawa tunasaidiana kazi pale ofisini lakini kwa kweli Moyo wangu ulimpenda yule Dada sanaaa!!(nikawa najizuia sana kuwa naye karibu ili nisijihusishe naye kimapenzi) pasipo kujua kumbe na yeye alikuwa ananipenda sana ila sikuwahi kujua!

Nikawa mwepesi sana kumzungumzia mwanamke wangu(mama mtoto wangu wa Singida) mara kwa mara namuweka profile picture kuongea naye japo ukweli sikuwa na hisia naye kabisa!!!

Kumbe yule dada mgeni alikuwa anakuwa disappointed sana kuona vile,akaomba nimsaidie kutafuta nyumba kwani hakuwa mwenyeji Tanga,nikamuunganisha na mzee mwenye nyumba yangu,akapata apartment pacha na yangu,(hapo ndipo matatizo yalipoanzia)

Tukawa watu wa karibu sana,akija mama wa mtoto wangu wanaongea pamoja na kuishi kiundugu kabisa,na baadaye akiondoka mke wangu anamsifia kuwa mke wangu ni mpole sana!

Akaanza kunisaidia kupika then tunakula wote,kwa kipindi cha kama miezi sita hivi,siku moja tukiwa tunaangalia filamu sebuleni,alionekana kuwa mnyonge sana,akanambia anaomba apumzike chumbani kwangu,nikamruhusu,ilikuwa jioni sana kama saa moja hivi,alipoingia chumbani kwangu mimi nikatoka kwenda kutafuta chakula kwa sababu hatukupika siku hiyo!nilikula huko nikarudi kama saa nne usiku,nikamkuta amelala kabisa,amevua blauzia na amevaa chupi na kanga tu!(kwa kweli nilishtuka nikajikuta kama sipo sawa hivi.

Nilimwamsha lakini hakuamka,niakaingia bafuni kuoga niliporudi alikuwa bado kitandani,nikapanda kitandani nikalala,ilipofika saa saba za usiku uvumilivu ulinishinda nikaanza kumshika maziwa,mapaja,na hatimaye tukaanza romance, na kuivunja amri ya sita!(kumbe lilikuwa kosa kubwa sanaaa)

Tukaingia kwenye mahusiano na ukawa mchezo wetu wa kila siku! Akija mama mtoto wangu ana-pretend kama hakuna kinachoendelea baina yetu,mwaka 2015 miezi ya saba nikata kuvunja mahusiano na mama wa mtoto,nilimshirikisha akaniomba aje tuzungumze juu ya maamuzi hayo,akaja mwezi wa 8/2015,alikaa mwezi mmoja,tuliongea kuhusu kuvunja uhusiano,akaongea kwa Huruma sana na mchozi mengi nikaamua kuahirisha maamuzi yangu,akaondoka!

Mwezi mmoja baadaye akaniambia anahisi ni mjamzito,(mtoto wa pili),nilisononeka sana lakini sikuwa na jinsi,ilibidi nikubaliane na uhalisia,baada ya kuondoka mke wangu tukaendelea na mchezo wetu na co-worker,mara akaanza wivu hataki niongee na mama wa mtoto wangu,nikamwambia ni bora tuachane kuliko kunipa masharti ya eti nisiongee na mpnz wangu mbele yake,na nikamwambia kuwa mchumba wangu ana mimba ya pili,hakufurahia kabisa habari hiyo akaniambia anatamani pia azae,(japo aliongea kiutani utani sana!)

Heeh,mwezi January 2016 co-worker akaniambia amenasa,khaaaa!!!!nikajaribu mbinu zangu zote kumwambia atoe,akasema hawezi kutoa kama sitaki mtoto atamlea mwenyewe,(Jamani wanaume wenzangu,usithubutu kukubali kauli hii kutoka kwa mwanamke,utajuta)

Baada ya miezi kwenda nikajikuta dilemma moja mbaya,huyu wa Tanga,nampenda sana,(sijui kama ndo limbwata au mapenzi natural,nampenda sana!) Wote wana watoto,ila wa Singida anao 2 japo simpendi sana,huyu wa Tanga ana mtoto 1 (nampenda sana,lakini kikwazo kwake ni kwamba kumbe kabla ya kuja Tanga alikuwa ameacha watoto wengine 2 huko kwao,japo hakuolewa)
Kutokana na mazingira aliyopo yule mama watoto wangu wa Singida ilibidi nimnunulie jiko la gas na baadhi ya vitu,jamaa yangu alikuwa anaenda huko nikamuomba niondoke naye kwenda Singida then nichangie mafuta!
Mama yanguuuu!huyu wa Tanga ameleta janga,maana amekuwa akinizuia nisiende Singida tangu juzi,na mimi kwa misimamo yangu nikamwambia siwezi kuacha kwenda ile ni familia yangu,akaniambia ukirudi utanikuta maiti hapa ndani kwako,nikampuuza,nimetoka kununua baadhi ya vitu narudi nyumbani nimemkuta chumbani kwangu akiwa anavuja damu nyingi,(naambatanisha picha mnisamehe wenye hisia kali kuona damu)

Amejichinja mshipa mkuu wa mkono wake wa kushoto,nimepata hofu sana kwa sababu sasa nagundua nipo na mtu hatari sana,kitendo alichofanya leo kimefanya nijutie maamuzi yangu ya mwanzo kabisa,kwanini nilikubali kukaa naye karibu na kuanza naye mahusiano!
Kitendo cha kujichinja mwenyewe si kuna siku anaweza kunivizia aniue huyu mwanamke jamaniii,nawezaje kumtoka mtu huyu katika mazingira haya,na kazini tupi pamoja kila siku!!!

Jamani ndugu zangu natamani siku zirudi nyuma nibadili mfumo wa maisha ila ndo siwezi tena,naombeni mawazo yenu ndugu zangu kwa sababu uwezo wangu wa kufikiri umekoma kabisaaa!!!
Hakika tunaendelea kupata funzo la kutosha humu JF

Ila mkuu hujatuambia baada y kumzalisha huyu demu wa Tanga vp khs yule wa singida alijua hili? na alilipokea vp maana alikuwa anajua ni rafk yako tu wkt anakuja pale Tanga
 
Hakika tunaendelea kupata funzo la kutosha humu JF

Ila mkuu hujatuambia baada y kumzalisha huyu demu wa Tanga vp khs yule wa singida alijua hili? na alilipokea vp maana alikuwa anajua ni rafk yako tu wkt anakuja pale Tanga
Nilipoenda hii juzi ndo nilipanga kuongea naye kwa utulivu sana,lakini baada ya kuona usaliti niliouelezea hapo juu hakika sijaweza kumwambia chochote!
 
Ndugu zangu,ukisikia njia panda Kali ndiyo hii!!
Mwaka 2010 niliachana na mpnz wangu nliyempenda sanaaa,ktk kipindi hicho cha mpito nilikutana na msichana mmoja mkoani huko,nikamtongoza ki-maskhara sana,(sikuwa serious kwa sababu sikumpenda kwa kweli) akakubali,nikajisemea moyoni huyu nakula then simrudii tena!

Kweli,nikamla msichana yule,(alikuwa mwaka wa kwanza Chuo cha diploma huko Mkoani),kwa uzembe wetu hatukutumia kinga,baada ya miezi kadhaa akaniambia anahisi ni mjamzito,nilishtuka kweli kwa sababu sikutaka kabisa kuwa na mtoto japo sikuchukua tahadhari kuliepuka hilo. Sikuikataa bali nilimshawishi atoe ile mimba,nikamtumia mpaka pesa ya kutolea,akakataa kabisa kuitoa na pesa yangu akanirudishia!(nikamtumia tena imsaidie kwa mambo yake mengine)

Baada ya mwaka mmoja,alijifungua mtoto anafanana na mimi sanaaa,hata kukataa isingewezekana,nikakubali kulea mtoto. Miaka miwili baadaye nikaanzisha mahusiano mengine,hayakudumu kwa sababu ya huyu mama wa mtoto wangu alikuwa karibu sana nami kimawasiliano juu ya maswala ya mtoto,jambo ambalo lilimkera mpnz wangu hiyo,akaamua kuachana na mimi!

Miaka yote hiyo tulikuwa tunakaa mbali mbali na huyo mama wa mtoto wangu,kutokana na upweke nilimuita Hugo mama wa mtoto nikae naye angalau kidogo niweze kutafuta kumpenda,then tuangalie uwezekano wa kuishi pamoja.(tulikaa kama miezi mitatu hivi kwa matazamio)

Ukweli alikuwa msichana mpole asiye na makuu,nikaamua kumtambulisha nyumbani rasmi,na kutambulika kuwa Huyo ndiye mchumba wangu!(akarejea kwao)

Baada ya mwaka mmoja,nikaenda kwa wazazi wake kuomba ridhaa ya kutambulika pia,wakanipa faini ya kumzalisha binti yao,nikatozwa kiasi fulani cha pesa,baada ya hapo ikawa rasmi pande zote mbili,japo nafsi yangu haikuwa imempenda kwa kweli!!

Mwaka 2014 mimi nilipata kazi,mkoani Tanga,yeye akapangwa Singida (yeye ni mwalimu),basi akawa ananitembelea Tanga mara kadhaa na maisha yakawa yanasonga!
Nilipoanzia kazi kuna binti mmoja alihamia akitokea mkoani Dodoma,tukawa tunasaidiana kazi pale ofisini lakini kwa kweli Moyo wangu ulimpenda yule Dada sanaaa!!(nikawa najizuia sana kuwa naye karibu ili nisijihusishe naye kimapenzi) pasipo kujua kumbe na yeye alikuwa ananipenda sana ila sikuwahi kujua!

Nikawa mwepesi sana kumzungumzia mwanamke wangu(mama mtoto wangu wa Singida) mara kwa mara namuweka profile picture kuongea naye japo ukweli sikuwa na hisia naye kabisa!!!

Kumbe yule dada mgeni alikuwa anakuwa disappointed sana kuona vile,akaomba nimsaidie kutafuta nyumba kwani hakuwa mwenyeji Tanga,nikamuunganisha na mzee mwenye nyumba yangu,akapata apartment pacha na yangu,(hapo ndipo matatizo yalipoanzia)

Tukawa watu wa karibu sana,akija mama wa mtoto wangu wanaongea pamoja na kuishi kiundugu kabisa,na baadaye akiondoka mke wangu anamsifia kuwa mke wangu ni mpole sana!

Akaanza kunisaidia kupika then tunakula wote,kwa kipindi cha kama miezi sita hivi,siku moja tukiwa tunaangalia filamu sebuleni,alionekana kuwa mnyonge sana,akanambia anaomba apumzike chumbani kwangu,nikamruhusu,ilikuwa jioni sana kama saa moja hivi,alipoingia chumbani kwangu mimi nikatoka kwenda kutafuta chakula kwa sababu hatukupika siku hiyo!nilikula huko nikarudi kama saa nne usiku,nikamkuta amelala kabisa,amevua blauzia na amevaa chupi na kanga tu!(kwa kweli nilishtuka nikajikuta kama sipo sawa hivi.

Nilimwamsha lakini hakuamka,niakaingia bafuni kuoga niliporudi alikuwa bado kitandani,nikapanda kitandani nikalala,ilipofika saa saba za usiku uvumilivu ulinishinda nikaanza kumshika maziwa,mapaja,na hatimaye tukaanza romance, na kuivunja amri ya sita!(kumbe lilikuwa kosa kubwa sanaaa)

Tukaingia kwenye mahusiano na ukawa mchezo wetu wa kila siku! Akija mama mtoto wangu ana-pretend kama hakuna kinachoendelea baina yetu,mwaka 2015 miezi ya saba nikata kuvunja mahusiano na mama wa mtoto,nilimshirikisha akaniomba aje tuzungumze juu ya maamuzi hayo,akaja mwezi wa 8/2015,alikaa mwezi mmoja,tuliongea kuhusu kuvunja uhusiano,akaongea kwa Huruma sana na mchozi mengi nikaamua kuahirisha maamuzi yangu,akaondoka!

Mwezi mmoja baadaye akaniambia anahisi ni mjamzito,(mtoto wa pili),nilisononeka sana lakini sikuwa na jinsi,ilibidi nikubaliane na uhalisia,baada ya kuondoka mke wangu tukaendelea na mchezo wetu na co-worker,mara akaanza wivu hataki niongee na mama wa mtoto wangu,nikamwambia ni bora tuachane kuliko kunipa masharti ya eti nisiongee na mpnz wangu mbele yake,na nikamwambia kuwa mchumba wangu ana mimba ya pili,hakufurahia kabisa habari hiyo akaniambia anatamani pia azae,(japo aliongea kiutani utani sana!)

Heeh,mwezi January 2016 co-worker akaniambia amenasa,khaaaa!!!!nikajaribu mbinu zangu zote kumwambia atoe,akasema hawezi kutoa kama sitaki mtoto atamlea mwenyewe,(Jamani wanaume wenzangu,usithubutu kukubali kauli hii kutoka kwa mwanamke,utajuta)

Baada ya miezi kwenda nikajikuta dilemma moja mbaya,huyu wa Tanga,nampenda sana,(sijui kama ndo limbwata au mapenzi natural,nampenda sana!) Wote wana watoto,ila wa Singida anao 2 japo simpendi sana,huyu wa Tanga ana mtoto 1 (nampenda sana,lakini kikwazo kwake ni kwamba kumbe kabla ya kuja Tanga alikuwa ameacha watoto wengine 2 huko kwao,japo hakuolewa)
Kutokana na mazingira aliyopo yule mama watoto wangu wa Singida ilibidi nimnunulie jiko la gas na baadhi ya vitu,jamaa yangu alikuwa anaenda huko nikamuomba niondoke naye kwenda Singida then nichangie mafuta!
Mama yanguuuu!huyu wa Tanga ameleta janga,maana amekuwa akinizuia nisiende Singida tangu juzi,na mimi kwa misimamo yangu nikamwambia siwezi kuacha kwenda ile ni familia yangu,akaniambia ukirudi utanikuta maiti hapa ndani kwako,nikampuuza,nimetoka kununua baadhi ya vitu narudi nyumbani nimemkuta chumbani kwangu akiwa anavuja damu nyingi,(naambatanisha picha mnisamehe wenye hisia kali kuona damu)

Amejichinja mshipa mkuu wa mkono wake wa kushoto,nimepata hofu sana kwa sababu sasa nagundua nipo na mtu hatari sana,kitendo alichofanya leo kimefanya nijutie maamuzi yangu ya mwanzo kabisa,kwanini nilikubali kukaa naye karibu na kuanza naye mahusiano!
Kitendo cha kujichinja mwenyewe si kuna siku anaweza kunivizia aniue huyu mwanamke jamaniii,nawezaje kumtoka mtu huyu katika mazingira haya,na kazini tupi pamoja kila siku!!!

Jamani ndugu zangu natamani siku zirudi nyuma nibadili mfumo wa maisha ila ndo siwezi tena,naombeni mawazo yenu ndugu zangu kwa sababu uwezo wangu wa kufikiri umekoma kabisaaa!!!
Kama amethubutu kujichinja mwenyewe basi jua wazi kuwa ana uwezo pia wa kukufanyia hilo jambo muda wowote akitaka. Na siku ukisema umuache, kwake kujiua ni zoezi la dakika sifuri tu. Upande wa ushauri, sijui hata nikushaurije mana hata nikikushauri uhame unaweza ukasikia ameshajiua
 
Back
Top Bottom