Usioe kama hauna kipato cha kueleweka

Usioe kama hauna kipato cha kueleweka

Habari zenu wakuu,

Kuoa ni zaidi ya upendo, kuoa ni majukumu na sio kuitana Babe au Mahabuba.

Kama hujajipata tafadhali nakuomba usiikimbilie Ndoa, maana utaumia na kuichukia hiyo Ndoa kilasiku kwenye maisha yako. Maisha ya ndoa yanahitaji pesa za kilasiku na hilo jukumu ni la kwako wewe Mwanaume na sio mwengine, kwahyo hakikisha kuwa unakipato cha kueleweka ili kuepusha matatizo mbeleni.

Kila mtu ana ndoto za kuwa na ukwasi kwenye maisha yake, unapooa wakati hujajipanga huenda ukashindwa kufikia hizo ndoto kwa kiasi kikubwa.

Nimeona baadhi ya vijana wenzangu wakioa lakini mwisho wa siku wanazitesa familia zao kwa Njaa, maana kilasiku wanalia shida kusaidiwa hela kulisha familia zao.

NB. KUOA NI MAJUKUMU, JIPANGE KABLA YA KUYATIMIZA HAYO MAJUKUMU.
Ushaanza kunishauri ujinga sasa naingiza vimia mia vya kandoro dayle naanzaje kusema nisioe
 
Kila raheli chief 😂
Amin ili uwe mwanaume kamili ni lazima ukabili majukumu na siyo kukwepa, mwanaume unahitaji uwe na mtoto/watoto na hao watoto wanastahili upendo wa pande mbili wako na wa mama yake ni lazima nioe mwakani Mungu akipenda

Mambo ya kuhofia kuhudumia huo ni ubinafsi , kuogopa changamoto maana yake unataka uolewe wewe
 
Bado nitachagua ndoa, muoe vijana mnaogopaje changamoto za ndoa na bado mnajiona ni wanaume timilifu,mwanaume ana sifa moja kuu ya kupambana na changamoto zinazomkabili katika maisha vijana mnaogopa ndoa najiuliza uanaume wenu ni wa faida gani
Ndoa ndio mtihan mgum unaanza kupewa cheti alafu mtihan unafuata baadae!!!
 
Jamani hizi mada za ndoa zimekua nyingi sana na zote zinawakatisha tamaa vijana.Hebu tuwaache vijana waoe hakuna jambo linalo kosa changamoto.Jamani ndoa zinachangamoto nyingi na tofauti tofauti lakini isitufanye tuogope ndoa sasa familia bora zitajengwa na kina nani km sio sisi.Njooni na mada hata za huyu shemeji yenu ataniua kwa mapishi au mahaba
Atakae katika tamaa nae anapaswa aangaliwe vzuri na arudishwe xcul akarudie somo la ‘za kuambiwa changanya na zako
 
Yaaani unamaanisha nitafute pesa kwa bidii ili nije kumfurahisha mwanamke na kuhakikisha anakuwa wangu milele wakati kuna machaguo mengi???!! Hell No.
Sio kumfurahisha Mke ni kujifurahisha wewe mwenyewe Mkuu.

Mke atakusaidia kwenye mambo mengi ukiachana na kukupa familia.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Kuishi bila mke changamoto kipato kikubwa kinaishia kuhonga,kwenda club, betting na kula mavyakula ya viwandani uchafu, kutokujali muda,

Sent from my SM-A025U using JamiiForums mobile app
Upo sahihi Mkuu, na pia kugonga wanawake na Ndom. Hili suala nalichukia sana.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Back
Top Bottom