Usioe kama hauna kipato cha kueleweka

Usioe kama hauna kipato cha kueleweka

PESA SIO SULUHISHO LA KILA KITU ILA NI MUHIMU MNO TUWE NAZO,


Pesa haihakikishi kwamba ndoa yako inakuwa na amani bali inahakikisha amani yote inayotokana na pesa inakuwepo/inapatikana.


Hivyo kabla ya pesa mtu anatakiwa ahakikishe amani zisizoletwa na pesa zinakuwepo kwa kumchagua mke/mume bora

1. Tafuta pesa
2. Chagua mke bora


Hapo maisha utakuwa umewin
 
Habari zenu wakuu,

Kuoa ni zaidi ya upendo, kuoa ni majukumu na sio kuitana Babe au Mahabuba.

Kama hujajipata tafadhali nakuomba usiikimbilie Ndoa, maana utaumia na kuichukia hiyo Ndoa kilasiku kwenye maisha yako. Maisha ya ndoa yanahitaji pesa za kilasiku na hilo jukumu ni la kwako wewe Mwanaume na sio mwengine, kwahyo hakikisha kuwa unakipato cha kueleweka ili kuepusha matatizo mbeleni.

Kila mtu ana ndoto za kuwa na ukwasi kwenye maisha yake, unapooa wakati hujajipanga huenda ukashindwa kufikia hizo ndoto kwa kiasi kikubwa.

Nimeona baadhi ya vijana wenzangu wakioa lakini mwisho wa siku wanazitesa familia zao kwa Njaa, maana kilasiku wanalia shida kusaidiwa hela kulisha familia zao.

NB. KUOA NI MAJUKUMU, JIPANGE KABLA YA KUYATIMIZA HAYO MAJUKUMU.
Mtu anaoa anaanza kupiga mizinga mke kajifungua asaidiwe,usipomsaidia anakuchukia

Vijana oeni kimkakati
 
Hongera mkuu, kusema ulikuwa huna kazi kabisa sio kweli umetuongopea


Wanawake wa hivyo ni ngumu mno kuwapata 1/100
Kipindi naingia kwenye ndoa nilipitia kipindi kigumu kidogo, maana sikuwa na pesa ya kujikimu kikamilifu. Lakini kupitia mke wangu alinipa nguvu na msukumo zaidi wa kupambana.

Sijutii kuwahi kuoa mkuu.
 
Kuiipanga hiyo ni kanuni lazima uwe nacho cha kuweza kuweka mambo ya familia yaende

Ila sasa mambo ya kuogopa ndoa mtu hodari ni yule anaepambana na changamoto na kuzipatia majibu kuogopa kuzikabili ni uoga usio wa kujenga,
Ila Waoga ndio wanaodumu 😀😀
 
Zamani kuanza maisha ya Ndoa ilikuwa rahisi sawa sawa kabisa na maisha ya kuanza ya kujitegemea kwa kijana aliyemaliza form 4.

Ila miaka hii maisha ya Ndoa yamekua mtihani kuanza na pengine yamegharamishwa kushinda hata biashara.

Yaani kijana anayemaliza chuo na hana kazi ni rahisi sana kwake kuanzisha biashara na ikafanikiwa ndani ya miaka 5 ila ni ngumu sana kuanzisha mahusiano serious ambayo yatapiga hatua za kimsingi baada ya miaka 5.

Atapata hasara sana na ataingia gharama kubwa sana plus maumivu na stress.


Miaka ya nyuma unaenda kuanzia maisha kwenye chumba uswazi na huna hata godoro unakutana na mwanamke anakupa thamani ukiwa hivyo na anakupa heshima ya mume hadi unaanza kununua godoro, mara sufuria, mara mnahama makazi hadi mnahamia kwenu anakuwa na wewe kama kepteni wake.

Hawa wasasa masharti kibao na hakuna anachokisaidia kwenye harakati za kujenga familia utadhani umeambatana na mtoto wa miaka 5 kazi kukuletea stress, utulivu zero, hana adabu, hajui matumizi sahihi ya pesa zako, hana mchango wa kifedha, ukimpa sehemu ya kushika azungushe mtaji analeta ujuaji na kuharibu, akipata kazi analeta ligi za usupa woman, full kero.
 
Bado nitachagua ndoa, muoe vijana mnaogopaje changamoto za ndoa na bado mnajiona ni wanaume timilifu,mwanaume ana sifa moja kuu ya kupambana na changamoto zinazomkabili katika maisha vijana mnaogopa ndoa najiuliza uanaume wenu ni wa faida gani
Unajua msiwe mnajitoa ufahamu kwenye hizi mada. Ni wapi hawa vijana wamesema wanaogopa changamoto za ndoa?

Shida iliyopo ni kuwa taasisi ya ndoa miaka hii inafanyiwa mzaha sana. Misingi na utaratibu wa kuitumikia inasemwa upande m'moja tu wa mwanaume ila mwanamke uzembe au ujinga wake eneo la ndoa huwa inachukuliwa poa sana kiasi kwamba ni wazi jamii imechagua kuwa bubu katika kuwawajibisha watoto wa kike na kumkazia wa kiume kuwa yeye ndie anatakiwa kusimama.

Watoto wa kiume wananunua magari, wanafanya biashara, wanasaidia familia zao, wanahonga mademu, washindwe kumudu ndoa kwenye eneo gani?

Shida ni mabinti kwa sasa hawapo tayari kuolewa wanahisi wanakwenda kifungoni na utumwani, ila wakifika miaka 30 ndoa inaanza kuwa muhimu kama sio ufala ni nini hapo?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Wapo Mkuu, kama umeshindwa kumpata waambie Wazazi au Ndugu wakutafutie.

NB. USIANGALIE MATAKO SANA!

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Tako muhimu, mambo ya kupapasa goma lako usiku unakuta tako ni zero level ni sawa na kulala na mwanaume mwenzako. Tako lina umuhimu sana mzee liheshimiwe.
 
Mkuu huyo "kujipata" unakua tayari umeshafanya mawasiliano naye akakujulisha kuwa tarehe fulani ama mwaka fulani utakuja ujipate?

Maisha yana mengi mkuu mambo mengine huja mbele kwa mbele kikubwa ni kuweka malengo, kukazana na kuomba Mungu akupe mwanamke bora na mwenye chachu ya kusonga mbele kimaisha.
 
Upo sahihi Mkuu, ila kujipanga ni lazima.

UNAWEZAJE KUOA UKIWA HAUNA HATA KITANDA AU MSOSI WAKO MWENYEWE UNAKUPIGA CHENGA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Mwanamke anayekupenda akikukuta hauna kitanda atakusaidia kupata godoro kwanza kitanda kitachongwa baadae. Na kama akishindwa kabisa atalala unapolala nyie si ni mwili m'moja bwana.

Unachokula na yeye atakula. Kama ni sahani moja ya chipsi mtakula nyote, kama ni mkate utam'megea nusu na wewe nusu mtulize njaa. Kama ni soda mtapunguziana.

Nini point ya kuwa mwili m'moja kama hamtaki kushare kila kitu.

Mwanaume akipata hela ndio ashare na mkewe ila shida ateseke nazo mwenyewe?

Huu ufala wa kumuonea boy child tuuache mwaka 2023,kuanzia 2024 boy child atapewa support anayohitaji kuwa imara na girl child atamsaidia boy child kufikia malengo na kushare nae changamoto na mafanikio kwenye maisha.

Lets end victimization ya girl child and looking down and belittling the boy child.
 
Watu wengi hawajui hilo, pesa zinaisha hata nguvu za kufanya kazi zinaisha pia. Msingi wa ndoa unapaswa kujengwa kwenye utu na sio vitu!
Hawa ndio wakishafika uzee wanasema wanawake wao wamewabadilikia au wamekengeuka kumbe shida ni namna walianza nao. Mwanamke unamvuta kwa mali au vitu vinavyohusiana na pesa then unategemea atakupenda hadi utu uzimani?
 
Habari zenu wakuu,

Kuoa ni zaidi ya upendo, kuoa ni majukumu na sio kuitana Babe au Mahabuba.

Kama hujajipata tafadhali nakuomba usiikimbilie Ndoa, maana utaumia na kuichukia hiyo Ndoa kilasiku kwenye maisha yako. Maisha ya ndoa yanahitaji pesa za kilasiku na hilo jukumu ni la kwako wewe Mwanaume na sio mwengine, kwahyo hakikisha kuwa unakipato cha kueleweka ili kuepusha matatizo mbeleni.

Kila mtu ana ndoto za kuwa na ukwasi kwenye maisha yake, unapooa wakati hujajipanga huenda ukashindwa kufikia hizo ndoto kwa kiasi kikubwa.

Nimeona baadhi ya vijana wenzangu wakioa lakini mwisho wa siku wanazitesa familia zao kwa Njaa, maana kilasiku wanalia shida kusaidiwa hela kulisha familia zao.

NB. KUOA NI MAJUKUMU, JIPANGE KABLA YA KUYATIMIZA HAYO MAJUKUMU.
Mkuu ulipaswa useme kwamba mnaotaka kuoa basi oa mwanamke wa size yako.


Hawa wanawake wana size kama ilivyo kiatu au nguo,
Ukivaa kikikubana sana shida au kikubwa sn shida.

Ila ukipata wa size yako utastarehe na dunia.

Ndoa sio kipato nakataa.

Ndoa ni size ya muoji na muolewaji.
 
Back
Top Bottom