Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
- Thread starter
- #61
[h=1]Usife kwanza mpenzi wangu (29).....[/h]
Siku chache baada ya Levina kumtambulisha mpenzi wake Deo kwa Cleopatra na kufanikisha kumpatia kazi kwenye ofisi ya baba yake, dhambi ya usaliti inachukua nafasi yake.
Cleopatra anatumia ushawishi wa pesa na madaraka yake kumpata Deo kirahisi na kufanikiwa kujivinjari naye. Levina anahisi kitu ingawa anakosa ushahidi. Wazazi wake bado wanamuandama wakimtaka aachane kabisa na Deo kwa kuwa hana hadhi ya kumuoa.
Je, nini kitandelea? Shuka nayo…
"Huwa unatumia kinywaji gani? Namaanisha bia gani?"
"Pombe huwa sinywi, labda soda tu."
"Leo kwa kuwa uko na mimi , naomba unywe japo kidogo uchangamshe akili," alisema Cleopatra huku akiendesha gari lake kuelekea Kunduchi Wet and Wild Hotel. Mawazoni mwake, alikuwa akipanga mengine, na aliamini ile ndiyo siku yake ya kumfaidi Deo.
"Twende tukakae kule pembeni," alisema Cleopatra kwa sauti iliyojaa mbwembwe za kimalavidavi. Akamshika mkono Deo na kumuelekeza mahali pa kukaa.
Walienda kukaa kwenye kona moja iliyokuwa imejificha, wakaanza kupiga stori huku Cleopatra akitumia uwezo wake wote kumtega Deo.
"Tuongeze raundi nyingine," alisema Cleopatra huku akimalizia chupa ya kwanza ya kilevi alichozoea kukitumia.
Japokuwa Deo hakuwa na kawaida ya kunywa pombe, kutokana na ushawishi wa Cleopatra alijikuta akipiga ‘moja moja' kukwepa kuonekana dhaifu mbele ya mrembo yule. Kadri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele, ndivyo pombe zilivyokuwa zinawakolea vichwani mwao. Wakaacha kuoneana aibu kama ilivyokuwa wakati wanaingia eneo hilo.
"Deo! Naomba nikwambie kitu."
"Niambie Cleopatra, nakusikiliza."
"Naomba usinifikirie vibaya kwa hili nitakalokueleza, nimevumilia nimeshindwa mwenzio."
"Wala usijali. Jisikie huru kuzungumza chochote."
"Deo, nakupenda Deo. Naomba uwe wangu mahabuba."
"Lakini Cleopatra, si unajua kuwa mi niko na rafiki yako Levina na ndiye aliyenikutanisha na wewe?"
"Najua sana Deo, lakini Levina ana nafasi yake, na mimi naomba unipe nafasi yangu."
"Hapana Cleopatra, sipendi kumkosea Levina, amenisaidia vingi sana."
"Nikubali Deo, itakuwa siri yetu, hakuna atakayejua."
Licha ya Deo kujivunga sana, Cleopatra aliendelea kumganda kama ruba akimtaka akubali ombi lake la kuwa wapenzi. Kwa kuwa tayari kilevi kilikuwa kimeanza kukolea ndani ya vichwa vyao, Cleopatra hakuona aibu tena na hakutaka kulaza damu, akajisogeza mwilini mwa Deo na kujilaza kifuani.
Uvumilivu ulianza kumshinda Deo, akawa haeleweki anachokiongea kama amemkubali Cleopatra au la.
"Tuondoke dear, mi nimechoka nataka kwenda kulala."
"Si utanifikisha nyumbani kwanza ndiyo wewe uelekee kwako."
"Hapana Deo, mwenzio naogopa peke yangu. Nifikishe kwanza nyumbani kwangu."
Cleopatra na Deo waliondoka eneo lile wakiwa wamekumbatiana, wakaongozana hadi kwenye gari walilokuja nalo. Deo akakaa pembeni huku Cleopatra akiwa nyuma ya usukani.
Breki ya kwanza ilikuwa nyumbani kwa Cleopatra. Walipofika tu, Cleopatra alishuka haraka haraka na kumshika Deo mkono, akawa anamvutia ndani kama kondoo anayepelekwa machinjioni.
Deo hakuwa na ujanja tena, yeye mwenyewe alishadatishwa na yote yaliyokuwa yanafanywa na Cleopatra.
Akaamua kujiachia. Dakika chache baadaye, walikuwa juu ya uwanja mkubwa wa fundi seremala, chumbani kwa Cleopatra, wakiwa na suti za kulalia.
***
Levina alikuwa chumbani kwake, akifanya usafi wa kawaida. Pingamizi la wazazi wake juu ya kumpenda Deo, lilimfanya muda mwingi awe anajifungia chumbani peke yake.
Mawazo na fikra zake zote zilikuwa juu ya Deo, alimpenda kiukweli na moyoni alijiwekea nadhiri kuwa lazima aolewe naye.
"Nimemkumbuka Deo wangu, ngoja nimcheki hewani," alijisemea Levina huku akijilaza kitandani na kuchukua simu yake ya mkononi.
Simu ya Deo ilikuwa ikiita bila kupokelewa, hali iliyomtia hofu Levina. Alirudia mara ya pili lakini hali ikawa ni ile ile. Aliendelea kujaribu mara kadhaa lakini haikupokelewa.
"Amepatwa na nini Deo wangu? Siyo kawaida yake."
Aliongea Levina huku akitafuta viatu vyake kutoka chini ya kitanda. Alishindwa kuvumilia, akahisi labda Deo amepatwa na tatizo hivyo akaamua kumfuata nyumbani kwake. Alitoka nyumbani kwao bila kuaga, akanyata hadi mlango wa nje na kuwaacha baba na mama yake wamekaa sebuleni.
Alipofika kwa Deo, alikutana na ukimya wa ajabu ambao uliashiria kuwa Deo hakuwemo ndani, hali iliyozidi kumtia hofu.
"Atakuwa wapi muda huu?" Alijiuliza Levina bila kupata majibu.
Alijaribu tena kupiga namba yake, lakini safari hii simu ya Deo ikawa haipatikani kabisa. Akahisi labda huenda amezidiwa na kazi ofisini kwao ndiyo maana amechelewa kurudi. Akaamua kumpigia simu shoga yake Cleopatra ili kujua kulikoni.
"Namba ya mteja unayempigia, haipatikani kwa sasa, jaribu tena baadaye," majibu yale kutoka kwenye simu yake ya mkononi yalimmaliza nguvu kabisa.
Akilini mwake kengele ya hatari ilishaanza kulia, akahisi huenda shoga yake anamzunguka kwa kutoka na Deo kwani tangu siku ya kwanza wakati anamtambulisha kwake, Cleopatra alionekana kumzimikia.
Hakutaka kuamini kuwa muda huo inawezekana wakawa pamoja kutokana na jinsi alivyokuwa anamuamini Deo. Kitu pekee alichoona kinafaa ilikuwa ni kurudi nyumbani kwao kupumzika kwani hakuaga wakati anaondoka, jambo ambalo alijua litawaudhi wazazi wake.
Moyoni alikuwa anaumia sana kumkosa Deo, kipenzi cha nafsi yake usiku ule, akawa hapati majibu ni wapi aliko, yuko na nani na anafanya nini. Wivu wa mapenzi uliwaka mtimani mwake.
"Ulikuwa wapi usiku wote huu?" Baba yake Levina, Mzee Msammu alimpokea kwa maswali makali.
"Na wewe Levina, mpaka nashindwa kukutetea kwa baba yako. Ulikuwa wapi saa hizi? Au ndiyo huyo ‘shamba boy' wako anakuzuzua?" Alidakia mama yake. Levina hakuwa na jibu, akainamisha kichwa chake chini.
Akilini hakuwa anajali alivyowaudhi wazazi wake kwa kuondoka bila kuaga, ila alikuwa akifikiria kwa nini Deo hayuko nyumbani kwake usiku kama ule, huku simu yake ikiwa inaita bila kupokelewa na baadaye ikawa haipatikani.
"Si tunaongea na wewe? Mbona hujibu? Kiburi siyo?"
***
Deo alishtuka kutoka kwenye usingizi mzito na kujikuta yuko mikononi mwa mwanamke tofauti na yule aliyemzoea.
"Hee! Imekuwaje tena?" Alijiuliza Deo huku akiitazama saa ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda. Ilikuwa ni tayari saa sita za usiku."
"Oooh! Shit." Alijisemea baada ya kugundua kuwa kumbe alikuwa amelala na Cleopatra kitanda kimoja, tena wote wakiwa kama walivyozaliwa. Hakutaka kuamini kama amemsaliti kirahisi namna ile mpenzi wake aliyemtoa mbali, Levina.
Je, nini kitaendelea? Usikose
Siku chache baada ya Levina kumtambulisha mpenzi wake Deo kwa Cleopatra na kufanikisha kumpatia kazi kwenye ofisi ya baba yake, dhambi ya usaliti inachukua nafasi yake.
Cleopatra anatumia ushawishi wa pesa na madaraka yake kumpata Deo kirahisi na kufanikiwa kujivinjari naye. Levina anahisi kitu ingawa anakosa ushahidi. Wazazi wake bado wanamuandama wakimtaka aachane kabisa na Deo kwa kuwa hana hadhi ya kumuoa.
Je, nini kitandelea? Shuka nayo…
"Huwa unatumia kinywaji gani? Namaanisha bia gani?"
"Pombe huwa sinywi, labda soda tu."
"Leo kwa kuwa uko na mimi , naomba unywe japo kidogo uchangamshe akili," alisema Cleopatra huku akiendesha gari lake kuelekea Kunduchi Wet and Wild Hotel. Mawazoni mwake, alikuwa akipanga mengine, na aliamini ile ndiyo siku yake ya kumfaidi Deo.
"Twende tukakae kule pembeni," alisema Cleopatra kwa sauti iliyojaa mbwembwe za kimalavidavi. Akamshika mkono Deo na kumuelekeza mahali pa kukaa.
Walienda kukaa kwenye kona moja iliyokuwa imejificha, wakaanza kupiga stori huku Cleopatra akitumia uwezo wake wote kumtega Deo.
"Tuongeze raundi nyingine," alisema Cleopatra huku akimalizia chupa ya kwanza ya kilevi alichozoea kukitumia.
Japokuwa Deo hakuwa na kawaida ya kunywa pombe, kutokana na ushawishi wa Cleopatra alijikuta akipiga ‘moja moja' kukwepa kuonekana dhaifu mbele ya mrembo yule. Kadri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele, ndivyo pombe zilivyokuwa zinawakolea vichwani mwao. Wakaacha kuoneana aibu kama ilivyokuwa wakati wanaingia eneo hilo.
"Deo! Naomba nikwambie kitu."
"Niambie Cleopatra, nakusikiliza."
"Naomba usinifikirie vibaya kwa hili nitakalokueleza, nimevumilia nimeshindwa mwenzio."
"Wala usijali. Jisikie huru kuzungumza chochote."
"Deo, nakupenda Deo. Naomba uwe wangu mahabuba."
"Lakini Cleopatra, si unajua kuwa mi niko na rafiki yako Levina na ndiye aliyenikutanisha na wewe?"
"Najua sana Deo, lakini Levina ana nafasi yake, na mimi naomba unipe nafasi yangu."
"Hapana Cleopatra, sipendi kumkosea Levina, amenisaidia vingi sana."
"Nikubali Deo, itakuwa siri yetu, hakuna atakayejua."
Licha ya Deo kujivunga sana, Cleopatra aliendelea kumganda kama ruba akimtaka akubali ombi lake la kuwa wapenzi. Kwa kuwa tayari kilevi kilikuwa kimeanza kukolea ndani ya vichwa vyao, Cleopatra hakuona aibu tena na hakutaka kulaza damu, akajisogeza mwilini mwa Deo na kujilaza kifuani.
Uvumilivu ulianza kumshinda Deo, akawa haeleweki anachokiongea kama amemkubali Cleopatra au la.
"Tuondoke dear, mi nimechoka nataka kwenda kulala."
"Si utanifikisha nyumbani kwanza ndiyo wewe uelekee kwako."
"Hapana Deo, mwenzio naogopa peke yangu. Nifikishe kwanza nyumbani kwangu."
Cleopatra na Deo waliondoka eneo lile wakiwa wamekumbatiana, wakaongozana hadi kwenye gari walilokuja nalo. Deo akakaa pembeni huku Cleopatra akiwa nyuma ya usukani.
Breki ya kwanza ilikuwa nyumbani kwa Cleopatra. Walipofika tu, Cleopatra alishuka haraka haraka na kumshika Deo mkono, akawa anamvutia ndani kama kondoo anayepelekwa machinjioni.
Deo hakuwa na ujanja tena, yeye mwenyewe alishadatishwa na yote yaliyokuwa yanafanywa na Cleopatra.
Akaamua kujiachia. Dakika chache baadaye, walikuwa juu ya uwanja mkubwa wa fundi seremala, chumbani kwa Cleopatra, wakiwa na suti za kulalia.
***
Levina alikuwa chumbani kwake, akifanya usafi wa kawaida. Pingamizi la wazazi wake juu ya kumpenda Deo, lilimfanya muda mwingi awe anajifungia chumbani peke yake.
Mawazo na fikra zake zote zilikuwa juu ya Deo, alimpenda kiukweli na moyoni alijiwekea nadhiri kuwa lazima aolewe naye.
"Nimemkumbuka Deo wangu, ngoja nimcheki hewani," alijisemea Levina huku akijilaza kitandani na kuchukua simu yake ya mkononi.
Simu ya Deo ilikuwa ikiita bila kupokelewa, hali iliyomtia hofu Levina. Alirudia mara ya pili lakini hali ikawa ni ile ile. Aliendelea kujaribu mara kadhaa lakini haikupokelewa.
"Amepatwa na nini Deo wangu? Siyo kawaida yake."
Aliongea Levina huku akitafuta viatu vyake kutoka chini ya kitanda. Alishindwa kuvumilia, akahisi labda Deo amepatwa na tatizo hivyo akaamua kumfuata nyumbani kwake. Alitoka nyumbani kwao bila kuaga, akanyata hadi mlango wa nje na kuwaacha baba na mama yake wamekaa sebuleni.
Alipofika kwa Deo, alikutana na ukimya wa ajabu ambao uliashiria kuwa Deo hakuwemo ndani, hali iliyozidi kumtia hofu.
"Atakuwa wapi muda huu?" Alijiuliza Levina bila kupata majibu.
Alijaribu tena kupiga namba yake, lakini safari hii simu ya Deo ikawa haipatikani kabisa. Akahisi labda huenda amezidiwa na kazi ofisini kwao ndiyo maana amechelewa kurudi. Akaamua kumpigia simu shoga yake Cleopatra ili kujua kulikoni.
"Namba ya mteja unayempigia, haipatikani kwa sasa, jaribu tena baadaye," majibu yale kutoka kwenye simu yake ya mkononi yalimmaliza nguvu kabisa.
Akilini mwake kengele ya hatari ilishaanza kulia, akahisi huenda shoga yake anamzunguka kwa kutoka na Deo kwani tangu siku ya kwanza wakati anamtambulisha kwake, Cleopatra alionekana kumzimikia.
Hakutaka kuamini kuwa muda huo inawezekana wakawa pamoja kutokana na jinsi alivyokuwa anamuamini Deo. Kitu pekee alichoona kinafaa ilikuwa ni kurudi nyumbani kwao kupumzika kwani hakuaga wakati anaondoka, jambo ambalo alijua litawaudhi wazazi wake.
Moyoni alikuwa anaumia sana kumkosa Deo, kipenzi cha nafsi yake usiku ule, akawa hapati majibu ni wapi aliko, yuko na nani na anafanya nini. Wivu wa mapenzi uliwaka mtimani mwake.
"Ulikuwa wapi usiku wote huu?" Baba yake Levina, Mzee Msammu alimpokea kwa maswali makali.
"Na wewe Levina, mpaka nashindwa kukutetea kwa baba yako. Ulikuwa wapi saa hizi? Au ndiyo huyo ‘shamba boy' wako anakuzuzua?" Alidakia mama yake. Levina hakuwa na jibu, akainamisha kichwa chake chini.
Akilini hakuwa anajali alivyowaudhi wazazi wake kwa kuondoka bila kuaga, ila alikuwa akifikiria kwa nini Deo hayuko nyumbani kwake usiku kama ule, huku simu yake ikiwa inaita bila kupokelewa na baadaye ikawa haipatikani.
"Si tunaongea na wewe? Mbona hujibu? Kiburi siyo?"
***
Deo alishtuka kutoka kwenye usingizi mzito na kujikuta yuko mikononi mwa mwanamke tofauti na yule aliyemzoea.
"Hee! Imekuwaje tena?" Alijiuliza Deo huku akiitazama saa ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda. Ilikuwa ni tayari saa sita za usiku."
"Oooh! Shit." Alijisemea baada ya kugundua kuwa kumbe alikuwa amelala na Cleopatra kitanda kimoja, tena wote wakiwa kama walivyozaliwa. Hakutaka kuamini kama amemsaliti kirahisi namna ile mpenzi wake aliyemtoa mbali, Levina.
Je, nini kitaendelea? Usikose