Ushujaa na ubora wa Rais Magufuli utang'ara zaidi baada ya kung'atuka madarakani 2025

Deogratias Mutungi

Senior Member
Oct 1, 2019
137
179
Salaam Wana JF

Nianze andiko hili fupi la uchambuzi kwa kutoa hongera na shukrani kwa Rais Dkt. Pombe Magufuli kuendelea kuonyesha misimamo chanya dhidi ya maslahi ya Watanzania katika mambo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kifya licha ya uwepo wa mashambulizi makali kutoka miongoni mwa Watanzania wenyewe na upande mwingine kutoka kwa wageni kwa maana ya nje ya nchi, Pengine tujiulize kwa nini Magufuli anapingwa sana? Sababu ipo wazi ni kutokana na "Misimamo yake ya utaifa na mali zake" Uadui baina ya Magufuli na mataifa ya magharibi unaanzia kwenye dhana hii, historia inatuonyesha wazi kuwa kila kiongozi wa Kiafrika na mabara mengine kama Asia na hata Amerika ya kusini aliyejaribu kuonyesha " Misimamo ya kizalendo kwa taifa lake amepitia kwenye tanuru la moto na kufitinishwa na wananchi wake kwa mbinu za hila na mfarakano wa kiuchumi".

Je kizazi cha sasa cha vijana wa Kitanzania wanazijua vyema mbinu hizi mfu za Magharibi, Bila shaka jibu ni "Wachache wenye ufahamu wa falsafa hii" Wengi ni wale wanaolishwa matango pori na kujazwa upepo kama puto bila kujua athari zake hapo badae, tunao vijana wengi wanaoendeshwa na kuamini kila tamko la magharibi liko sahihi kimantiki pasipo kuchanganua ukweli wa mambo, Mathalani wakati mataifa ya Magharibi wanaivamia Libya, Walibya waliaminishwa Gaddafi ni Kiongozi muuaji na asiyezingatia utu wa raia wake, wakaamua kuamini hivyo na leo hii libya ni "Machinjio ya binadamu" kwa sababu ya Propaganda za hovyo na za kinafiki Libya si sehemu salama tena wanatamani Gaddafi afufuke kitu ambacho akiwezekani kabisa, Kwa dhana hii, ndipo swali lisilopata jibu hadi sasa uibuka, '' Afrika ni bara la watu wa namna gani" Wenye kuuliza swali hili ni wazungu wanaotutumia katika kufarakana na sisi tunaingia katika mtego huo.

Mantiki kuu ya Andiko hili nikutaka kuwaambia kuwa rais Magufuli ni mwema na kiongozi anayeipenda nchi yake na watu wake na si kama propaganda zinavyoenezwa mitandaoni ndani na nje ya nchi, inawezekana rais ana mapungufu yake kama ilivyo kwa binadamu yoyote yule lakini dhana inayojengwa kwa sasa kuwa rais Magufuli anaizuia chanjo ya corona kuingia nchini ili watu wafe "afurahi", ni dhana potofu na ya hovyo kabisa na wala haikubaliki hata kidogo, Rais ni alama ya utaifa na kivuli cha amani, Kwa Magufuli hilo lipo wazi na amelitimiza kwa asilimia zinazokubalika, bahati mbaya ukweli huu unaposemwa wapo ambao ununa na uamua kurusha matusi badala ya hoja kinzani.

Juhudi za kuijenga Tanzania ya badae zinazofanywa na Rais Magufuli uenda tusizione leo hii lakini tukaja kuziona baada ya kumaliza muda wake hapo mwaka 2025, na ndivyo itakavyokuwa, Wakati wa Rais Mstaafu Kikwete wapo walio mtusi na Kukejeli jitihada zake za ujenzi wa Tanzania, leo hii wanamlilia na kusema "Baba tumekumic", ilikuwa hivyo kwa Nyerere, ikawa hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na hata Magufuli itakuwa hivyo, maana historia inao ukweli ndani yake. Myonge myongeni lakini haki yake mpeni, Rais Magufuli anawajibika na anadhubutu kuwakomboa Watanzania, Janga la Corona lisiwe Kigezo cha kufitinishana na kusahau mazuri ndani ya utawala wake, nina imani katika wimbi hili tutavuka salama na maisha yataendelea kama kawaida, Kwa pamoja tuijenge nchi yetu.

Deogratias Mutungi
 
Naliona kwa mtazamo tofauti. Pengine kichwa cha habari kingekuwa "Udhaifu, Madudu na Uozo wa Magufuli kuonekana baada ya 2025"

Nitakupa sababu;
1. Kipindi chake kilichoanza 2015 vyombo vya habari haviko HURU, vimetishiwa sana kiasi kwamba haviandiki mabaya na Uozo wake Kama wakati wa JK.

2. Wamebbakia kumsifu tu kwenye vyombo vyote kiasi kwamba huoni tofauti ya kusoma gazeti la Mwananchi na Uhuru. Dr Abbas ndiye Mhariri wa vyombo vyote

3. Hata wasaidizi wake yaani Mawaziri, wakuu wa mikoa na makatibu wakuu hawana fursa ya kumshauri au kumkosoa. Wakifanya hivyo anawatumbua

Nakuthibitishia kuwa hata wale unaowaona wanamsifia sana sasa hivi Kama Sheikh Alhad wa BAKWATA au RC Chalamila wa Mbeya au Makonda, atakapokuja Rais mwingine ndiyo watakuwa wa kwanza KUMKOSOA na KUMPONDA
 
Asante kwa kushiriki
1614936401854.png
 
UVCCM huwa mnaandika vitu kama kuku asiye na kichwa. Ni ugomvi upi ambao Mabeberu wanao dhidi ya Magufuli? Maana kila kukicha mnaimba kuhusu VITA YA KIUCHUMI, ni uchumi upi ambao tunao na mabeberu wanautamani wao tu ndiyo wawe nao hadi watupige vita?!
Unaishi kwenye Taifa ambalo almost 68% ni masikini wa kutupwa kabisa huku ukiwa na utajiri wa rasilimali, ina maana mabeberu wanataka kuchukua Mlima Kilimanjaro au kubeba hifadhi zetu au wanataka kuchukua Bahari na Maziwa yetu!
Msimamo upi ambao KINJEKITILE nao kuhusu Mabeberu! Hatuna hata chembe ya msimamo wa kupambana nao, tatizo nyie Lumumba mnafanya mambo kwa kupiga piga kelele, Mabeberu wao wanafanya kimya kimya kuwabana korodani zenu.
Mmezunguka weee kukubali uwepo wa COVID19 phase 2, hatimaye sasa mmeanza kuongea lugha yao baada ya kubanwa kwenye masharti ya mikopo na miongozo ya afya Duniani.
Huwa sielewi watu kama nyie kwa nini mnaona KINJEKITILE ni mkombozi wa Taifa hili, hakuna jambo tangible amefanya zaidi ya hizo WHITE ELEPHANT PROJECTS ambazo nazo ni mkono wa mabeberu.
KINJEKITILE hakupaswa hata kuwa kilanja wa Darasa, hajui ukubwa na uzito wa nafasi ya URAIS anaendesha nchi kama anaendesha familia yake nyumbani.
 
Kwel ww ni mtungi
Salaam Wana JF

Nianze andiko hili fupi la uchambuzi kwa kutoa hongera na shukrani kwa Rais Dkt. Pombe Magufuli kuendelea kuonyesha misimamo chanya dhidi ya maslahi ya Watanzania katika mambo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kifya licha ya uwepo wa mashambulizi makali kutoka miongoni mwa Watanzania wenyewe na upande mwingine kutoka kwa wageni kwa maana ya nje ya nchi, Pengine tujiulize kwa nini Magufuli anapingwa sana? Sababu ipo wazi ni kutokana na "Misimamo yake ya utaifa na mali zake" Uadui baina ya Magufuli na mataifa ya magharibi unaanzia kwenye dhana hii, historia inatuonyesha wazi kuwa kila kiongozi wa Kiafrika na mabara mengine kama Asia na hata Amerika ya kusini aliyejaribu kuonyesha " Misimamo ya kizalendo kwa taifa lake amepitia kwenye tanuru la moto na kufitinishwa na wananchi wake kwa mbinu za hila na mfarakano wa kiuchumi".

Je kizazi cha sasa cha vijana wa Kitanzania wanazijua vyema mbinu hizi mfu za Magharibi, Bila shaka jibu ni "Wachache wenye ufahamu wa falsafa hii" Wengi ni wale wanaolishwa matango pori na kujazwa upepo kama puto bila kujua athari zake hapo badae, tunao vijana wengi wanaoendeshwa na kuamini kila tamko la magharibi liko sahihi kimantiki pasipo kuchanganua ukweli wa mambo, Mathalani wakati mataifa ya Magharibi wanaivamia Libya, Walibya waliaminishwa Gaddafi ni Kiongozi muuaji na asiyezingatia utu wa raia wake, wakaamua kuamini hivyo na leo hii libya ni "Machinjio ya binadamu" kwa sababu ya Propaganda za hovyo na za kinafiki Libya si sehemu salama tena wanatamani Gaddafi afufuke kitu ambacho akiwezekani kabisa, Kwa dhana hii, ndipo swali lisilopata jibu hadi sasa uibuka, '' Afrika ni bara la watu wa namna gani" Wenye kuuliza swali hili ni wazungu wanaotutumia katika kufarakana na sisi tunaingia katika mtego huo.

Mantiki kuu ya Andiko hili nikutaka kuwaambia kuwa rais Magufuli ni mwema na kiongozi anayeipenda nchi yake na watu wake na si kama propaganda zinavyoenezwa mitandaoni ndani na nje ya nchi, inawezekana rais ana mapungufu yake kama ilivyo kwa binadamu yoyote yule lakini dhana inayojengwa kwa sasa kuwa rais Magufuli anaizuia chanjo ya corona kuingia nchini ili watu wafe "afurahi", ni dhana potofu na ya hovyo kabisa na wala haikubaliki hata kidogo, Rais ni alama ya utaifa na kivuli cha amani, Kwa Magufuli hilo lipo wazi na amelitimiza kwa asilimia zinazokubalika, bahati mbaya ukweli huu unaposemwa wapo ambao ununa na uamua kurusha matusi badala ya hoja kinzani.

Juhudi za kuijenga Tanzania ya badae zinazofanywa na Rais Magufuli uenda tusizione leo hii lakini tukaja kuziona baada ya kumaliza muda wake hapo mwaka 2025, na ndivyo itakavyokuwa, Wakati wa Rais Mstaafu Kikwete wapo walio mtusi na Kukejeli jitihada zake za ujenzi wa Tanzania, leo hii wanamlilia na kusema "Baba tumekumic", ilikuwa hivyo kwa Nyerere, ikawa hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na hata Magufuli itakuwa hivyo, maana historia inao ukweli ndani yake. Myonge myongeni lakini haki yake mpeni, Rais Magufuli anawajibika na anadhubutu kuwakomboa Watanzania, Janga la Corona lisiwe Kigezo cha kufitinishana na kusahau mazuri ndani ya utawala wake, nina imani katika wimbi hili tutavuka salama na maisha yataendelea kama kawaida, Kwa pamoja tuijenge nchi yetu.

Deogratias Mutungi
 
Hawa waliosoma syllabus za zamani fikra zao ni duni kweli kweli.Mali ipi ya afrika iliyomshinda Mzungu akiitaka.Raslimali zetu ni takataka tusipoziuza nje nani anakula dhahabu au madini pasipowauzia hao nje.Wala hawahitaji kuja ndani kusomba mali uingia ubia na wazawa kama kivuli na mali wanasomba.Ishu ya corona sisi si kisiwa wakisema Hakuna kwenda Hija bila chanjo utakwendaje.Suala la afya ni la mtu binafsi thus hata chanjo ikiwepo ni hiari sio lzm wote wachanjwe kama ilivyo clinic ni hiari umpeleke mtoto au usimpeleke.
Mliosoma zamani tabu kweli.
 
Gadafi aliuwawa na watu wake sababu akutaka kuwasilikiza kama angewaunganisha watu wake asingeuwawa.Unapowabagua watu wako na kutokuwa wamoja unajitengenezea bomu lako.
 
Back
Top Bottom