Bila kujali kwamba tuhuma za Ben Saanane na wengine ni kweli au sio kweli naona ni busara kwa Zitto now ajitoe CHADEMA na aunde hama chake ambacho yeye atakuwa mwenyekiti na ataweza kukusanya washabiki wake wote waliopo CCM na CHADEMA na kwingineko.
Sioni ni vipi Zitto anaweza kugombea urais kwa kupitia CHADEMA sio tu 2015 lakini mwaka wowote ule.....CHADEMA will never be the party for him to vie for the presidency..hii now iko waazi mno.
Na Zitto lengo lake kuu ni kugombea urais...basi ni bora ajipange now.
Mimi naona this way it is better kwa kila mtuZitto na CHADEMA pia.
Sasa nimeelewa kwamba ,kikundi cha masalia kilikuwepo , na kilikuwa na lengo la kukidhoofisha chama na kiliundwa na Mwampamba, Juliana na kundi lao la Masalia. Bali Saanane na Mamuya walikuwa wanatumika kama Intellijensia ya chama, hawa ndiyo walikuwa wanatoa taarifa kwa uwongozi wa juu wa chama kwamba nani ni msaliti , Wenyewe masalia hawakulielewa hili walifikiri Saanane na Mamuya ni wenzao kumbe walikuwa shushu, nina Uhakika Saanane na Mamuya walichukua form za kugombea uongozi bavicha ,walikuwa wanazuga ili kutambua wanaoenda kinyume na ni wakina nani , nafikiri walifanikiwa kuwajua na kuwaripoti kwenye uongozi wa juu wa chama, ndio uongozi wa juu wa chama ukawaengua baadhi ya wagombea kwa kashfa ya Rushwa kazi aliyo ifanya Saanane na Mamuya .
ukitaka kudhibitsha hilo utakugundua kwamba mkuu Saanane alikuwa anajipendekeza kwa masalia ili kujua mipango yao yote ,na akishajua anailipoti kwenye uongozi wa juu, ndio maaana uongozi wa juu ulikuwa unachukua Taadhari juu ya vijana masalia , kiasi kwamba vijana Masalia walikuwa wanaona wanatengwa , sababu walikuwa hawaijui.kumbe ni matendo yao . yliyokuwa ynaripotiwa na Mkuu Saanane na Mamuya. Saanane amefanyakazi ya Intellejensia vilivyo.
kama ni kweli Masalia walikuwa na lengo zuri kwa nini ,wameanza kufumuka baada ya Saa nane kuweka Mambo hadharani? walitakiwa watoe ripoti juu ya hili kwenye uongozi wa chama.kitambo tu kama walikuwa na nia njema. ukisoma maelezo ya Mwampamba na Juliana utagundua kwamba hawa watu walikuwa wana fadhiliwa na Zitto wakishilikiana na kafulila, wakati huohuo walikuwa wanajua kwamba Saanane ni mwenzao, kumbe alikuwa anawapeleleza.
kila mtu angependa role model wake awe raisi lakini sio kwa njia za kinafiki na uzandiki ,mimi Role model wangu ni Profesa Safari , ningependa awe raisi lakini sio kwa manufaa binafsi ni kwa manufaa ya chama , haina haja ya kuleta unafiki , na kutumia shortcuts kila mtu ajipange Chama kimpe baraka agombee lakini sio kwa kutumia unafiki, uzindaki ,uchawi . Siiungi Mkono kundi bali naunga mkono Maslai ya chama. Mwampamba na juliana shonza hamjakomaa bado,nyinyi na akina nape naona muko sawa . Mkuu Zitto nakuheshimu sana najua wewe ni jembe,lakini kuwa mvumilivu mvumilivu hula mbivu waangalie vijana wenzako Mnyika, Lissu ,Sillnde ,Msigwa, Vincent nyerere, Mdee, wanajenga chama , Achana na Kafurila hayapo kundini alishaondoka chadema zamaini, Achana na akina Shyrose Bhanji,achana na JK, achana na Wasira ungana viongozi wenzako wa JUU MBOWE na DR. Slaa mujenge Chama ,Unafiki hautakiwi. Watanzania tunakuamini kwamba ni kijana Tunaekutegemea baadaye kama kiongozi wa chini Lakini kwa sasa sifa zako zinapungua ,zinahamia kwa Mnyika ,Vincent Nyerere na Msigwa. Achana na Propaganda za ccm na NCCR ,kijenge chama mkuu. waambie wakina Mwampamba na Juliana waache Siasa za Maji taka Warudi kwenye mstarii wakijenge Chama.
Najua Dr. Kitila aliingia Kwenye Mkumbo bila yeye kujua, Nina uhakika kwa sasa ameshajua kwamba alikuwa anakitumikia chama au Mtu. na atajirekebisha
Mimi kila siku nabishana na Tuntemeke humu ndani JF kumbe nabishana na kundi la watu?
Kuna watu walikuwa wanamponda DR. Slaa nilifikiri ni magamba kumbe ni wanachadema wenzetu, hatari sana.
Tuache Siasa chafu Tukijenge Chama, "Maslahi ya Chama mbele"
jangakuu@yahoo.com