WISDOM SEEDS
JF-Expert Member
- Jun 1, 2011
- 841
- 282
Ushauri ulioutoa wangepaswa kuulipia lakini wewe umefanya favour, thanks for that!
Mwenye masikio na asikie ushauri huu wa BURE.
Mwenye masikio na asikie ushauri huu wa BURE.
Mwenyew nshaachaga kuisikilza hiyo radio station long time ago!hata'sikumbuk tena sauti zao!manake ni kichefuchefu
Habari yako msomaji!
KWA WAMILIKI WA RADIO CLOUDS FM.
Mimi Radio Producer napenda kuandika ushauri wangu kwako/kwenu wamiliki wa clouds Fm. Ni ushauri tu ukiupenda karibu, ukiona kawaida hakuna shida, silipwi wala sikulipi!
............................
3. Kwa sababu 1. Lugha- mara nyingi lugha inayotumika hasa kiswahili cha wadada hao na wakaka hao hakiendani na na wala hakiwezi kusimamia goal iende sawa. Kama mna malengo mfano ya kuielimisha vijana, unadhani kwa hali ya lugha inayotumika unajenga nini? Uharibifu mkubwa wa utamaduni wa mtanzania kwa matumizi mabaya ya lugha ya kiswahili. Nyinyi kama chombo cha habari mlitakiwa kuwa mstari wa mbele kuwafundisha vijana kutumia lugha vizuri zaidi ili tuwe na taifa lenye nguvu na utamaduni wa kupendeza!
Acheni kutumia lugha mbaya/mtaani/chafu/uchochezi, acheni kutumia hisia zenu mnapokuwa hewani, angalieni format yenu, goal yenu na targeted audience wenu, angalieni uwezo wa watangazaji wenu hakika mtajenga taifa!
Asanteni kwa kusoma.
Radio Producer
UK.
Hapo hata mimi nakuunga mkono kwa kweli kuna baadhi ya watangazaji wanaboa sana kama yule sijui ndio anaejiita Diva?.... Haeleweki anaongea kiswahili ama English? Mimi simfahamu kabisaa!! Hivi huyu Dada target audience yake ni kundi gani? Hii lugha anaongea wanaomfahamu ni masharobaro na masista duu ambao ni wachache kwenye jamii yetu, kwa hiyo utakuta mtu anabadilisha station na hawa cloudsfm waelewe mtangazaji kama huyu anawapunguzia audience rating. Kama alifanya interview ya kuajiriwa kweli alitumia lugha pumba kama hii tunayomsikia akiongea redioni?
Na ndio ninavofanya, nilipohisi simuelewi nilibadili station, isipokuwa haya yalikuwa maoni yangu na nafikiri hapa nina uhuru wa kutoa maoni ama? Mbona mkali mkuu ama una hisa Clouds?Kama huelewi anachoongea basi ujue wewe si mlengwa wake. Badilisha tu stesheni usikilize upendacho. Redio zipo nyingi siku hizi.
Hata wewe huna nia ya kujenga bali ni chuki iliyosababishwa na madonda ya uchaguzi. Unataka tuamini Clouds ni redio mbaya eti kwa kuwa hawafuati seti fulani ya standards ulizo ziweka wakati ni dhahiri kati ya radio zaidi ya arobaini hapa nchini wao wanaongoza kwa kila kitu. Waambie na hao unaowatumikia hata wangekuwa ni malaika bado wasingekubalika na watu wote, mawazo hayo ya kutaka kumtusi au kumpa sifa mbaya kila aliyetofauti na mitazamo yao ni ya kidikteta na hayawezi kuvumiliwa na ndio maana watu waliwakataa na wataendelea kuwa kataa milele amina.
jamani hata mie nilikuwa na ushauri wa muhimu sana kwa clouds fm..maana ndio radio pekee inayopendwa kwa nguvu zote na vijana na wazee wa kesho...basi tunaona pia ni busara kuwashauri ili hilo "taifa la kesho" liwe kweli taifa la tanzania la kesho.. na sio taifa la watanzania wa-mbele wa kesho kina new-lil wizzy kina gucci mainne, kina lady gaga kina nik minaj, kina drake etc...
na hii clouds tv ndio kabsaaaa... hata watoto wa shule na waalimu wooote wanatupia-swagga kiasi kwamba dent na ticha full minyukano ya swagga... si ndo dogo janja akatia maguu kwa wajeda wa hapo makongo akaleta swagga acha achezee mikonzi ya mjeda ticha wake..
anyway..NIPENI NAMBA YA JK WA CLOUDS NIMPE MPANGO-MKAKATI WA KUTUZALISHIA VIJANA TAIFA LA KESHO LA KINA nyerere, che-guevara, patric lumumba, kwame nkrumah, mugabe, gaddafi, malcom x, rosa park, mkwawa, kinjekitile ngwale, etc.... NI MAONI TUU WADAU NOTHING PERSONAL
Mbona hwa Clouds wanasema wapo online lakini hawasikiki?
Sawia kabisa. Wanafiki wakubwa hawa. Kule kwenye jukwaa la ngono hakuna uthibitishaji wa umri. Unachofanya ni kujiunga tu na JF halafu unamtumia Invisible PM kumuomba kujiunga.
Kwa hiyo kabisa naweza kuwa na umri wa miaka 15 na nikawa niko kule. Halafu wapo hapa wanaongelea maadili. Wanashangaza sana hawa watu. Halafu ni maadili gani, kwa mfano, ya kubandika picha za watu halafu na kuanza kuwachamba?
Kama wanazungumzia maadili waanzie kwanza hapahapa. Wamshauri Max afungilie mbali lile jukwaa la ngono. Wakimaliza hapo, wawe wanazichunga threads zote zinazokashifu watu kwa sababu kashfa na zenyewe si sehemu ya maadili bora.
Ushauri ulioutoa wangepaswa kuulipia lakini wewe umefanya favour, thanks for that!
Mwenye masikio na asikie ushauri huu wa BURE.
M naamin clouds n moja ya redio zenye vijana wny ubunifu na vipaj ndan yao, ila tatizo lipo kwa baadh ya watangazaja ambao hawafuat maadil sahihi ya utangazaja ambpo wanafikia ha2a ya kutukana hadharan, ktu ambacho knaleta matabaka ya aina ya wasikilizaj. kna kile kpnd cha raha za roho, wamesogeza muda il kuwapa nafas wny rika sahih kusikiliza, ni uamuz sahh japo lugha wanaitumia imepitiliza uki compare na pillow talk cha times. All in all, wanapaswa kupunguza uhuru mkubwa kwa presenters wao il kuepeuka matatizo km hayo. hongeren clouds kwa kaz nzuri.
hii radio ilikuwa nzuri sana miaka ya nyuma,lakini mabadiliko yameanza siku si nyingi sana zilizopita,naona wamegundua hilo ndo maana wamechukua watu wawili kutoka radio one,tuwape nafasi tuone itakuwaje!
Mkuu jaribu kusikiliza na kutazama clip hizi za vipindi vya BBC. Tena wewe uko huko UK nadhani unajua zaidi yangu. Hii BBC nadhani ni kama TBC lakini wana vipindi vyenye maneno kama hayo. Sasa wewe ukishangaa Clouds inabidi nikushangae wewe.
Inabidi ujue customer wanataka nini sio kila kipindi kiwe too official au tooo formal. Tutaboreka.
Russel Howard Good knews.
Top gear
Hiyo ni mifano so clouds wana matatizo madogo madogo kama ilivyo TBC, ITV, radio one na wengine . Sio mtaalam wa radio lakini ukniuliza station gani zinahitaji reform nitaanza na TBC
Kila kituo cha redio kinakuwa na walengwa wake. Na kila kipindi huwa na walengwa wake pia.
Clouds FM si redio ya umma. Si redio ya umma kwa maana ya kwamba heitegemei ruzuku ya serikali kujiendesha. Kwa kiasi kikubwa inategemea hela za wadhamini wa vipindi na matangazo mengine ya biashara.
Sasa kama mtu ana matatizo na redio hiyo kwa nini wasipeleke ushahidi huko kwa wahusika walio na dhamana ya kutoa mwongozo wa kisheria na taratibu kuhusiana na vyombo vya habari?
Kutokukipenda kituo cha redio kwa sababu ya vipindi vyake ni jambo moja, na kusema eti wanavunja maadili au sijui wanakiuka sheria ni jambo jingine. Kwanza maadili hayaangozwi na sheria. Miiko ya fani ndo huongozwa na sheria. Mtu kama unaona Clouds FM wanavunja sheria basi kusanya vielelezo vyako na vipeleke TCRA.
Ukivipeleka huko na vikapuuzwa na wewe kwenye moyo wa moyo wako unaona kabisa una hoja nzuri basi anzisha kampeni kubwa yak u-raise awareness kuhusiana na hayo unayoyapinga dhidi Clouds. Unaweza ukaandika mabango na kwenda mbele ya ofisi za TCRA au ukaitisha maandamano dhidi ya Clouds yatakayoanzia, kwa mfano, kutoka ofisi za TCRA hadi pale Mikocheni kwenye ofisi za Clouds.
Si mnajidai mna nia njema? Si mnajidai mna hoja yenye mshiko? Basi kama hayo yote ni kweli sidhani kama itawawia vigumu kufanya hayo. Kuishia kulialia hapa JF haisaidii sana. Sasa sana mnaishia kuonekana wafa maji tu.
Hapo hata mimi nakuunga mkono kwa kweli kuna baadhi ya watangazaji wanaboa sana kama yule sijui ndio anaejiita Diva?.... Haeleweki anaongea kiswahili ama English? Mimi simfahamu kabisaa!! Hivi huyu Dada target audience yake ni kundi gani? Hii lugha anaongea wanaomfahamu ni masharobaro na masista duu ambao ni wachache kwenye jamii yetu, kwa hiyo utakuta mtu anabadilisha station na hawa cloudsfm waelewe mtangazaji kama huyu anawapunguzia audience rating. Kama alifanya interview ya kuajiriwa kweli alitumia lugha pumba kama hii tunayomsikia akiongea redioni?
Kama huelewi anachoongea basi ujue wewe si mlengwa wake. Badilisha tu stesheni usikilize upendacho. Redio zipo nyingi siku hizi.