Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,764
- 903
Mkuu, si umpeleke Hospitali nadhani utapata bingwa wa magonjwa hayo
hata mi nilishangaa sana lakini sasa naanza kuamini baada ya maelezo ya Mzizimkavu<br />
<br />
utani huu mkuu
Mwambie ajaribu kutumia Kitunguu thomu
Kitunguu swaumu tangu kale kimekuwa kikijulikana kama 'dawa ya kushangaza' na kutumiwa na watu wengi katika kutibu mafua na influenza. Miongoni mwa faida za kitunguu swaumu ni kuzuia kupatwa na magonjwa mbalimbali na maambukizo ya virusi. Hivyo kitunguu swaumu hujulikana
kama antibiotiki ya asilia. Uchunguzi umeonyesha kwamba kula kitunguu swaumu kunapunguza kushadidi ugonjwa wa influenza na hata kuzuia kupatwa na ugonjwa huo. Vilevile kula kila mara kitunguu swaumu, huzuia kupatwa na magonjwa ya moyo, kwani kitunguu swaumu huzuia damu isigande kwenye mishipa ya damu.
Halikadhalika kitunguu swaumu ambacho pia ni kiungo muhimu cha chakula kina potassium, na hivyo watu wenye ugonjwa wa shinikizo la damu wanashauriwa kula vyakula vilivyopikwa kwa kitunguu swaumu.
Si vibaya kujua kuwa katika uchunguzi uliochapishwa mwaka 2001, imeelezwa kwamba, kitunguu swaumu kina athari kubwa na nzuri pale kinapochanganywa na baadhi ya dawa nyinginezo katika kutibu Ukimwi au HIV.
Haya shime jamani kuanzia leo vyakula visikose kuungwa na kitunguu thomu, iwapo unaogopa kupatwa na influenza kama mimi!
IKIWA BADO HAJAPONA JARIBU KUWASILIANA NA MIMI KWA NJIA YA P.M. NIPO NJE YA NCHI NAWEZA KUKULETEA DAWA IKAMSAIDIA HUYO MGONJWA WAKO.
Kwa wiki sasa ninasumbuliwa na kikohozi kikavu kisicho na makohozi. Nimetumia Antibacteria na syrups sijaona dalili za kupona, naomba ushauri wenu?
Lamba asali mbichi ya nyuki wadogo, mimi huwa inanisaidia sana kwenye kikohozi kikavu sababu huwa nakohoa hadi koo lauma sana.
Kama kikohozi kina dalili hizi:
Basi hicho kikohozi ni cha allergy, siyo cha infection. Moja wapo ya dawa ambazo zinasaidia ni Phernagan syrup (scientific name: promethazine). Kunywa kijiko kimoja cha chai usiku unapolala, ikwezekana hata asubuhi. Hii dawa inaweza kuleta drowsiness.
- Kikavu
- Hakiumizi kifua
- Hakiambatani na homa
- Unasikia kuwashwa kooni
- Unakohoa zaidi asubuhi au/na usiku
Nipe feedback