TinyMonster
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 242
- 154
Jamani kuna ugonjwa wa kikohozi kikavu sasa hivi umeibuka Dar, fatilia kwenye mikusanyiko ya watu sasa hivi utagundua watu wengi wanapiga "starter" kali kama mara 2 au mara 3 kila baada ya dakika 5. Kwa wale ambao imeshawatokea (Nikiwa mmoja wao) ugonjwa huu unatesa sana muda wa kulala. Utakuta siku nzima unafanya kazi vizuri tu lakini ukishalala unajikuta unakohoa vibaya sana, bila kutoa hata makohozi na unaendelea hivyo mpaka asubuhi.
Sijajua kama tatizo ni uchavuzi wa hali ya hewa Dar au ni nini lakini watu wa Idara ya afya inabidi waangalie hiki kitu tusijekuwa wahanga wa sumu bila kujitambua. Na kwa yeyote anaefahamu tiba yake naomba atujuze manake dawa za kawaida kama koflyn, coldrill hazifanyi kazi kabisa.
Sijajua kama tatizo ni uchavuzi wa hali ya hewa Dar au ni nini lakini watu wa Idara ya afya inabidi waangalie hiki kitu tusijekuwa wahanga wa sumu bila kujitambua. Na kwa yeyote anaefahamu tiba yake naomba atujuze manake dawa za kawaida kama koflyn, coldrill hazifanyi kazi kabisa.