Ushauri: Nanyanyaswa na mke wa baba yangu mdogo

Ushauri: Nanyanyaswa na mke wa baba yangu mdogo

samahani mkuu,naomba nikuulize swali moja la msingi, unanishauri nkapange, je ntapanga vip wakati sina kipato,na mbali na kipato jana nimetoka kuongea na baba yangu mdogo nikamwambia kwamba kwa kipindi hiki naomba nitafte kazi yyte ya kuniingizia kipato na kazi nilishapata kiwanda flani hivi, cha kusikitisha nikakataliwa, na mi sio kwamba nimvivu, napenda sana kazi iwe ya aina yoyote ambayo ni halali.

Dah
Sasa na wewe hapa umeniudhi,yaani umemsikiliza baba ako umeacha kazi na unajua maisha yako hayasomeki plus kazi zilivyo ngumu sikuhizi?
.u a not serious
 
Pole sana,vumilia tu,iko siku utafanikiwa kimaisha.umeweza kuvumilia tangu form one,ushindwe last minutes umeshamaliza form six? imebakia muda kidogo tuuu utaenda chuo mwanangu.wewe cha msingi vumilia,maisha ya kuishi kwa watu ni magumu sana,yataka moyo.kwani huwezi kuishi bila kwenda kwa marafiki au kuangalia tv? TV yake kama hataki,usiangalie, ishi atakavyo yeye,iko siku utanunua vya kwako,na iko siku atakuja kukuomba msaada huko mbele ya safari.wapo watu wananyanyaswa hata hawasomeshwi,wewe shukuru mungu umemaliza form six. cha muhimu usije ukapata tamaa ukaacha kuendelea kusoma ili utafute kazi,utachemsha!
Huyo mwanamke mkatili sana,usimjibu vibaya,Ubaya wake atalipwa na Mungu.
 
Umekua wewe sasa ukapange. Una drop masomo gani na hali ushamaliza form six???

Mie nimeishi na tuvijana tunato jiona tumekuwa, tuvivuuu mno, kujidai maisha ya movie, rimoti inakuwa kama extensio ya mb.o zao.

Na nikiangalia umelelewa na 'bibi', nahisi wewe ni janga. Mwanamme haogopi kazi, tena zenyewe za kufuta madirisha? Ingekuwa kumwaga zege??
Kwenye red lazima umekumbushwa mabaya sana hadi kufikia hapo
 
kujimudu naweza mkuu sema tatzo linakuja kwamba hawataki mi nianze kuchakalika na ukiangalia wenzangu niliomaliza nao sa hv wanahangaika me niliwaomba nianze kuhangaika na maisha nikakataliwa kata kata na mkuu mpk nimekuja kuomba ushauri kwenu ujue hayo yote uliyoyasema nishayajarbu lkn ndo vile.
Pole kwa matatizo unayopitia lakini siku zote yafaa ujue kuwa mtu unayemuona mbaya ndio anayekutengenezea maisha mazuri ya baadae,hizo changamoto zitakuja kukuletea mafanikio ingawa kwa sasa unaona unateseka,kuna watoto wanapata kila kitu lakini huja haribikiwa baadae kwa kukimbilia mambo makubwa wasiyoyaweza,kama kufanya kazi utakuja tu fanya cha msingi kwa sasa jielekeze kwenye masomo.
Kwa umri ulionao yafaa ujue kuepuka kila aina ya vitina na manyanyaso toka kwa huyo mama yako ila uvumilivu tu ndio utakuvusha hasa ukiacha vile vitu ambavyo wao hawataki uvifanye.
 
Nilikua kidato cha tano niliacha, Ataanzaje kupanga? hajaamua , siku akichoka hiyo hali atajua tu pesa inatafutwaje na watu hua wanapanga vipi

Mkuu usipende kukariri maisha hayana formula eti sababu wewe ulifanikiwa kwa style yako na mwingine nae afuate hizo mbinu zako atafanikiwa, si sawa hata kidogo.

Dogo hiyo ndio mitihani ya dunia ni lazima ujifunze kuishi na binadamu wa aina yoyote. Hayo unayopitia sio mateso ila ni mafunzo kwa maisha yako ya baadae. Waswahili wanasema mtumikie Tahiti upate maradi wako. Piga hizo kazi anazotaka bila kusubiri kuambiwa, jitahidi kuwa makini unavyofanya kazi za nyumbani kuepusha kuharibu mali zake, kama shida ni TV usiangalie, ukitaka kutoka muage, jitahidi kuwa naye karibu, usimchukie, mwombe msamahani kama anakoroma umekosea kitu, mpende zaidi, usipende kubishana nae, jenga ukaribu na urafiki nae, mweleze ni jinsi gani unampenda kwa kuishi nae, mwambie yeye ndo anakufundisha maisha na wewe usichukulie negave kila unaloambiwa. Nakuhakikishia ukifanya hayo utaishi nae kama mzazi wako na atakupenda. Hata ukienda chuo wakumbuke na uwajali maana wao ndo wamekusaidia ukafikia hatua hiyo. Kuwa nae karibu kuliko hata baba yako mdogo utaona atakavyo kuwa anakusifu kwa uchapaji kazi. We jitie ubwege tu faida yake utaiona. Pia yana mwisho hayo vumilia tu
 
Watoto wengi wanaolelewa na mama wengine huhisi ananyanyaswa lakini si ukweli ni mawazo yako tu.

Huyo mama anakufundisha uwe unajitegemea lakini huelewi.

Utakuja kumkumbuka na kuona kuwa uliyoyapata kwake yanakusaidia sana kimaisha, utapopata akili kwani sasa hivi ingawa una miaka 23 lakini akili zako, kwa jinsi ulivyoandika, ni kama za mtoto wa miaka 12.
 
Mkuu usipende kukariri maisha hayana formula eti sababu wewe ulifanikiwa kwa style yako na mwingine nae afuate hizo mbinu zako atafanikiwa, si sawa hata kidogo.

Dogo hiyo ndio mitihani ya dunia ni lazima ujifunze kuishi na binadamu wa aina yoyote. Hayo unayopitia sio mateso ila ni mafunzo kwa maisha yako ya baadae. Waswahili wanasema mtumikie Tahiti upate maradi wako. Piga hizo kazi anazotaka bila kusubiri kuambiwa, jitahidi kuwa makini unavyofanya kazi za nyumbani kuepusha kuharibu mali zake, kama shida ni TV usiangalie, ukitaka kutoka muage, jitahidi kuwa naye karibu, usimchukie, mwombe msamahani kama anakoroma umekosea kitu, mpende zaidi, usipende kubishana nae, jenga ukaribu na urafiki nae, mweleze ni jinsi gani unampenda kwa kuishi nae, mwambie yeye ndo anakufundisha maisha na wewe usichukulie negave kila unaloambiwa. Nakuhakikishia ukifanya hayo utaishi nae kama mzazi wako na atakupenda. Hata ukienda chuo wakumbuke na uwajali maana wao ndo wamekusaidia ukafikia hatua hiyo. Kuwa nae karibu kuliko hata baba yako mdogo utaona atakavyo kuwa anakusifu kwa uchapaji kazi. We jitie ubwege tu faida yake utaiona. Pia yana mwisho hayo vumilia tu

Umeelewa alichoeleza kwenye post? Ulichofanya hapa n sawa na kuamua kutumia Sox kama gloves

Mfano niliompa sio ili autumie bali ajifunze kutokana nao

Huyo mwanamke hafanyi hayo anayoyafanya labda kwasababu huyu jamaa hafanyi kaz , huyo mwanamke anafanya hvyo ili atimize furaha yake , furaha yake nikuona huyu jamaa anateseka

Huyu n mtu mzima , nidhamu ya woga aachene nayo , katika umri huo kuna ulaliza gan wa kukaa na mzazi? Unamiaka 23 na ndevu unanyoa alafu kuna mtu anakusumbua kisa anakuweka mjini

Na kwa upande wa pili , hili n somo kwake , atakuja kuelewa baada ya kuondoka hapo kama mm nilivyoelewa baada ya kuondoka
 
nimepitia makubwa zaidi ya hayo ukijua unachotafutaa hakuna shida we fanya wanavyotaka af usinungunike be happy... akitukana. akisema. we mwache aseme ilmradi shule wamekupeleka hakuna shida zaid
i zingatia usifanye vitu asivyovipenda km hataki marafiki we kaa nao mbali utakutana nao shule na tuition. kazana kwenye masomo yako ipo cku atakuja kukuomba msamaha. binafsi namshukuru sana kwa kunifundisha maisha.
 
Unanyanyaswa kwa kukubali kunyanyaswa
ignore her..fanya yako....
mchukulie mgonjwa wa akili
na acha mazoea ya kucheka nae wala kuzungumza nae akijichekesha
kunja sura tu kutwa ukimuona huku unaendelea na masomo yako.....
usiguse tv yake...
The Boss, haya ulioandika ndio ya muhimu, mimi niliyatekeleza hayo kwa kipindi cha miaka mitano hadi naenda A'level, na toka hapo nimesimama mwenyewe nikiwa mwanaume wa familia, hadi dingi yangu mdogo na mkewe wananiogopa hadi sasa kwa nilivyokuwa kauzu....
 
Last edited by a moderator:
kujimudu naweza mkuu sema tatzo linakuja kwamba hawataki mi nianze kuchakalika na ukiangalia wenzangu niliomaliza nao sa hv wanahangaika me niliwaomba nianze kuhangaika na maisha nikakataliwa kata kata na mkuu mpk nimekuja kuomba ushauri kwenu ujue hayo yote uliyoyasema nishayajarbu lkn ndo vile.

ushauri unaopewa hapa wengi wanasema anza kujitegemea, na wewe unasema unakataliwa kujitegemea sasa unataka ushauriwe nini?? ni hivi kama una wenzio tayari weanajitegemea ongea nao muwe mnashare ghetto. wakikubali tafuta kibarua anza kufanya ujiingizie kipato,baba yako mdogo mpe taarifa hamna anachoweza kufanya zaidi ya kukufukuza,akikufukuza unaenda kujishikiza kwa rafiki zako hadi ukae sawa. ukifaulu form 6 unaingia zako chuo maisha yanaanzia hapo,naamini hutaleta mchezo ukiingia chuo.
 
Umeelewa alichoeleza kwenye post? Ulichofanya hapa n sawa na kuamua kutumia Sox kama gloves

Mfano niliompa sio ili autumie bali ajifunze kutokana nao

Huyo mwanamke hafanyi hayo anayoyafanya labda kwasababu huyu jamaa hafanyi kaz , huyo mwanamke anafanya hvyo ili atimize furaha yake , furaha yake nikuona huyu jamaa anateseka

Huyu n mtu mzima , nidhamu ya woga aachene nayo , katika umri huo kuna ulaliza gan wa kukaa na mzazi? Unamiaka 23 na ndevu unanyoa alafu kuna mtu anakusumbua kisa anakuweka mjini

Na kwa upande wa pili , hili n somo kwake , atakuja kuelewa baada ya kuondoka hapo kama mm nilivyoelewa baada ya kuondoka

Ndo maana uliacha shule ukiwa kidata cha tano kwa ajili ya kufanya maamuzi yasiokua na subira. Kuwa na ndevu haimaniishi hnajiweza kwa kila kitu
 
Ndo maana uliacha shule ukiwa kidata cha tano kwa ajili ya kufanya maamuzi yasiokua na subira. Kuwa na ndevu haimaniishi hnajiweza kwa kila kitu

Na ninafurahia uamuz wangu , what am earning sasa hv, hata prof hapati , wenzangu wataka hitimu na degree zao watakuta nishawaandalia kaz , watafanya kaz ofisin kwangu , Hapa ndipo uamuz wangu utaonekana ulikua wa busara au la , usiogope maisha , life is full of options , elimu inakuja kama option pia
 
Watoto wengi wanaolelewa na mama wengine huhisi ananyanyaswa lakini si ukweli ni mawazo yako tu.

Huyo mama anakufundisha uwe unajitegemea lakini huelewi.

Utakuja kumkumbuka na kuona kuwa uliyoyapata kwake yanakusaidia sana kimaisha, utapopata akili kwani sasa hivi ingawa una miaka 23 lakini akili zako, kwa jinsi ulivyoandika, ni kama za mtoto wa miaka 12.

Hapana mkuu sio hivo huyu mama ana roho ya ubinafsi, lakini sipingi hoja yako ila naongelea kwa upande wangu kwamba yeye hapendi kumuona ndugu yyte aje, nahata kama akija atacheka nae siku mbili tu siku ya tatu anamuuliza anaondoka lini.Mkuu kuna ndugu ambao pia walipata kuishi nae lakini wakashindwa kuvumilia maana ikitokea mme wake amesafiri shida mtakazo pata ni balaa, kwa mfano kuna kipndi mzee alisafiri nikaanza kuumwa malaria mpk masikio yakaziba, nikamuomba hela akasema hana na sikutaka kumpigia simu mzee maana angeona nimemdharau mke wake ikanibidi niombe hela kwa rafiki yangu nikanunua mseto, na sometime ikitokea nataka kuosha gari yake, anasema "nilikuambia uoshe?" nisipo iosha napo nasemwa na mzee akirudi lazima amwambia kitu chochote ambacho kitamfanya mzee akasilike ili nae anijie juu, sa mkuu hii hali sio manyanyaso?
 
Na ninafurahia uamuz wangu , what am earning sasa hv, hata prof hapati , wenzangu wataka hitimu na degree zao watakuta nishawaandalia kaz , watafanya kaz ofisin kwangu , Hapa ndipo uamuz wangu utaonekana ulikua wa busara au la , usiogope maisha , life is full of options , elimu inakuja kama option pia

Ni kweli mkuu yani huwa inafika wakati najiuliza kwanini kila siku mimi tu, majirani wanaona mimi nina maisha mazuri xanaa maana wakiona mgorofa na Range zipo ndani basi wanajua mambo safi ni bora niishi maisha ya kawaida lakini sio kuishi kwa hofu siku zote maana daily nikiitwa najua naenda kusemwa tu maana me sinaga story nae.
 
Ni kweli mkuu yani huwa inafika wakati najiuliza kwanini kila siku mimi tu, majirani wanaona mimi nina maisha mazuri xanaa maana wakiona mgorofa na Range zipo ndani basi wanajua mambo safi ni bora niishi maisha ya kawaida lakini sio kuishi kwa hofu siku zote maana daily nikiitwa najua naenda kusemwa tu maana me sinaga story nae.

Kaa chini , tuliza akil yako , Fanya uamuz , ukichanganya kdgo na haya uliyoyapata humu naamn utatoka na uamuz sahihi
 
Pole kijana! Kwanza si kweli una miaka 23 labda kama utatimiza hiyo miaka mwakani!

Kwanza wewe ni mdogo halafu una hisia za kunyanyaswa ndio maana unaona kila unacho fanyiwa ni manyanyaso! Kwanza unatakiwa kujua unapo kuwa kwa mtu unatakiwa kuwa mpole na usiwe mbishi na utimize wajibu wako!

Sasa unacho takiwa kufanya ni hivi!

Kwanza usiwe mbishi...kuwa msikivu na mpole....!
Ukiamka asubuhi hakikisha umefanya usafi wote muhimu ikiwezekana osha vyombo,fagia nyumba na nje ya nyumba!

Ongeza umakini katika kila unacho fanya...ili kuepuka kuonekana mzembe na unafanya makusudi!
Nina hakika una ubishi lakini punguza na uwe una sikiliza hasa unapo ongea na mtu mzima!

Swala la kupenda kuangalia TV punguza ukimaliza kazi zake wewe jikite kwenye kusoma ....deal na vitabu tuu usipende kukutwa unaangalia Tv unaonekana huna kazi za kufanya!

Swala la kukataliwa kufanya kazi pengine ni kutokana na kutoaminiwa na pia umri wako..hakikisha una badilika na una jenga kuaminiwa na wakikuamini wata kuruhusu kufanya kazi au hutakuwa na sababu ya kuomba kufanya kazi bali utawaaga tuu!

Jaribu kutimiza wajubu wako na uondokane na kuona una nyanyaswa na uchukulie kuwa unapo gombezwa ni kwamba kuna sehemu umeshindwa kutimiza wajibu wako!

Ondoa hisia za kunyanyaswa na utimize wajibu wako!
 
Pole sana,vumilia tu,iko siku utafanikiwa kimaisha.umeweza kuvumilia tangu form one,ushindwe last minutes umeshamaliza form six? imebakia muda kidogo tuuu utaenda chuo mwanangu.wewe cha msingi vumilia,maisha ya kuishi kwa watu ni magumu sana,yataka moyo.kwani huwezi kuishi bila kwenda kwa marafiki au kuangalia tv? TV yake kama hataki,usiangalie, ishi atakavyo yeye,iko siku utanunua vya kwako,na iko siku atakuja kukuomba msaada huko mbele ya safari.wapo watu wananyanyaswa hata hawasomeshwi,wewe shukuru mungu umemaliza form six. cha muhimu usije ukapata tamaa ukaacha kuendelea kusoma ili utafute kazi,utachemsha!
Huyo mwanamke mkatili sana,usimjibu vibaya,Ubaya wake atalipwa na Mungu.

Ni kweli kabisa mkuu nilikua na ndugu yangu pia niliyeanza nae form one, kiukweli yeye alishindwa kuvumilia akaamua kuondoka na akaacha shule akiwa form two maana alikua akiambiwa kuosha vyombo,kupika,kudeki,au kutumwa sehem kwa mguu anaona ni kazi siyo. Me nilivumilia yote naosha vyombo mpaka leo, sema sasa huwa inafika hamala nakuwa na mawazo sana maana huwa anamsema vibaya mpk mama yangu mzazi ila huwa simwambii chochote maana nikisema nimwambie ntakuwa nimesababisha mambo mengine, yani mkuu nataman hata siku zikimbie ili nikiwa chuo atleast ntakuwa mbali nae.
 
Mkuu usipende kukariri maisha hayana formula eti sababu wewe ulifanikiwa kwa style yako na mwingine nae afuate hizo mbinu zako atafanikiwa, si sawa hata kidogo.

Dogo hiyo ndio mitihani ya dunia ni lazima ujifunze kuishi na binadamu wa aina yoyote. Hayo unayopitia sio mateso ila ni mafunzo kwa maisha yako ya baadae. Waswahili wanasema mtumikie Tahiti upate maradi wako. Piga hizo kazi anazotaka bila kusubiri kuambiwa, jitahidi kuwa makini unavyofanya kazi za nyumbani kuepusha kuharibu mali zake, kama shida ni TV usiangalie, ukitaka kutoka muage, jitahidi kuwa naye karibu, usimchukie, mwombe msamahani kama anakoroma umekosea kitu, mpende zaidi, usipende kubishana nae, jenga ukaribu na urafiki nae, mweleze ni jinsi gani unampenda kwa kuishi nae, mwambie yeye ndo anakufundisha maisha na wewe usichukulie negave kila unaloambiwa. Nakuhakikishia ukifanya hayo utaishi nae kama mzazi wako na atakupenda. Hata ukienda chuo wakumbuke na uwajali maana wao ndo wamekusaidia ukafikia hatua hiyo. Kuwa nae karibu kuliko hata baba yako mdogo utaona atakavyo kuwa anakusifu kwa uchapaji kazi. We jitie ubwege tu faida yake utaiona. Pia yana mwisho hayo vumilia tu

Yani mkuu hivo vitu mkuu huwa navifanya sana, kwa mfano kwenye suala la kufanya kazi bila kuambiwa, unaweza fanya kazi yake, cha kushangaza anakuja kukuambia "je nilikuambia ufanye"? Mfano niliosha gari yake siku moja akaja akaniuliza " nilikuambia uoshe? Au mama yako ndo anakutuma ufanye vitu vya kijinga jinga, " nikimuomba msamaha anakwambia " hakuna cha msamaha wala cha nini hapa"
 
Back
Top Bottom