Isaack Newton
JF-Expert Member
- Apr 15, 2013
- 619
- 371
Habari wakuu,
Mimii ni kijana wa miaka 23, nimemaliza kidato cha sita mwaka huu, tangu nianze masomo yangu kidato cha kwanza, mke wa baba yangu mdogo ananinyanyasa sana, na nilikua nasikiaga ndugu zangu wakisema yule mama ana roho mbaya sana, yeye hana mtoto hata mmoja, kama mnavofahamu kukosea kwa binadamu ni kawaida nikimaanisha kwamba ikitokea labda nimevunja glasi nikiwa naosha, yeye hatambui kuwa ni bahati mbaya yeye anajua moja kwa moja ni makusudi.
Huwa ananitishia kunifukuza kwake na hapa me sina baba na sijawahi kumuona machoni maana alishafariki mi nkiwa mdogo sana na nimelelewa na bibi na mama yangu hana uwezo. Siku zote anataka mi niwe nafanya kazi, kazi zenyewe hamna ila raha yake anataka uwe unashikashika hata madirisha ili aridhike, akiniona nimekaa anatafuta kisa anakuja anamwambia baba yangu mdogo kwamba simuheshimu.
Baba yangu mdogo nae ananijilia juu, nikikaa nje nasemwa, nikiangalia TV sebuleni nasemwa, nikikaa chumbani nasemwa. Jamani nifanyeje maisha haya maana nimevumilia sana jamani, mpaka marafiki zangu wananishangaa maana huyu mama hataki mimi niwatembelee marafiki zangu na hataki aone rafiki yoyote kwake. Nishaurini maana nilikua na drop academically shuleni kwa sababu ya kukaa na mawazo mengi.
Jamani naombeni ushauri wenu
Nawasilisha jamani
Mimii ni kijana wa miaka 23, nimemaliza kidato cha sita mwaka huu, tangu nianze masomo yangu kidato cha kwanza, mke wa baba yangu mdogo ananinyanyasa sana, na nilikua nasikiaga ndugu zangu wakisema yule mama ana roho mbaya sana, yeye hana mtoto hata mmoja, kama mnavofahamu kukosea kwa binadamu ni kawaida nikimaanisha kwamba ikitokea labda nimevunja glasi nikiwa naosha, yeye hatambui kuwa ni bahati mbaya yeye anajua moja kwa moja ni makusudi.
Huwa ananitishia kunifukuza kwake na hapa me sina baba na sijawahi kumuona machoni maana alishafariki mi nkiwa mdogo sana na nimelelewa na bibi na mama yangu hana uwezo. Siku zote anataka mi niwe nafanya kazi, kazi zenyewe hamna ila raha yake anataka uwe unashikashika hata madirisha ili aridhike, akiniona nimekaa anatafuta kisa anakuja anamwambia baba yangu mdogo kwamba simuheshimu.
Baba yangu mdogo nae ananijilia juu, nikikaa nje nasemwa, nikiangalia TV sebuleni nasemwa, nikikaa chumbani nasemwa. Jamani nifanyeje maisha haya maana nimevumilia sana jamani, mpaka marafiki zangu wananishangaa maana huyu mama hataki mimi niwatembelee marafiki zangu na hataki aone rafiki yoyote kwake. Nishaurini maana nilikua na drop academically shuleni kwa sababu ya kukaa na mawazo mengi.
Jamani naombeni ushauri wenu
Nawasilisha jamani