Ushauri kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Wizara ya Teknolojia ya Mawasiliano na Habari

isajorsergio

Platinum Member
Apr 22, 2018
4,125
6,250
Habari đź‘‹

Naomba siku ya leo nitoe ushauri na mapendekezo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kuhusu wizara hii ya teknolojia, mawasiliano na habari.

Sifahamu Dr. Faustine Ndugulile kipi kimemtatiza katika hii wizara. Sina shaka na utendaji wake lakini nadhani kutokana na yeye kuegemea zaidi katika afya maybe uelewa zaidi katika teknolojia, mawasiliano na habari sio katika wigo mpana au perspective tofauti.

Pili naona naibu waziri na katibu mkuu katika wizara hii hawashauri vyema au kufanya mapitio yenye kuhusu teknolojia, mawasiliano na habari.

USHAURI | kwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan:

1. Apitie wizara husika na kufanya mabadiliko katika nafasi za katibu mkuu wa wizara na naibu waziri kuweza kuongeza ufanisi na kasi ya utendaji.

2. Wizara husika usukwe upya kwa kujumuisha masuala ya teknolojia na mawasiliano kwa wigo mpana, ibebe dhima ya teknolojia, mawasiliano na habari kwa uzito tofauti.

3. Wizara husika ikaimiwe na naibu waziri wawili na makatibu wakuu wawili. Mmoja akihusika zaidi katika teknolojia combined na mwingine akijizatiti katika mawasiliano na habari.

MAPENDEKEZO | Kutokana na kupitia watu tofauti katika wingi huu wa watu million 60+

Naomba Rais. Mama Samia Suluhu apitie majina ya wafuatao kuweza kuchukua nafasi za Naibu Mawaziri na Katibu Wakuu.

1. Maxence Melo 2. Salim Kikeke 3. Benjamin Fernandes 4. Charles Hillary 5. Millard Ayo na 6. Mimi ili kusudi tuweze kumsaidia Dr. Faustine Ndugulile na taifa katika nyanja hizi.

Naona naweza kufanya kazi katika mtiririko na kasi ya teknolojia, mawasiliano na habari na nipo tayari kwa uapisho Jumanne hii Dodoma.

Asante.
 
Isajorsergio hebu tuwekee hapa majina yako halisi na sisi tupate kukujua na kutoa mapendeke zaidi mama wewe ulivyowataja wengine kwenye huu wako.

Pili ingekuwa vizuri kama ungedadafua zaidi mapungufu yaliyopo kwenye hiyo wizara ili tuweze kuelewa kwa undani unachomaanisha katika huu uzi wako. Maana naona ni kama malalamiko ambayo ni general sana hayapo specific kwamba tatizo ni lipi hapo wizarani.
 
Isajorsergio hebu tuwekee hapa majina yako halisi na sisi tupate kukujua na kutoa mapendeke zaidi mama wewe ulivyowataja wengine kwenye huu wako.

Pili ingekuwa vizuri kama ungedadafua zaidi mapungufu yaliyopo kwenye hiyo wizara ili tuweze kuelewa kwa undani unachomaanisha katika huu uzi wako. Maana naona ni kama malalamiko ambayo ni general sana hayapo specific kwamba tatizo ni lipi hapo wizarani.
Mapungufu katika hii wizara ni matokeo ya uelewa hafifu au uwepo wa perspective tofauti inayohusu masuala ya teknolojia, mawasiliano, habari na masuala ya kidigitali. Kupitia mapungufu haya ndio taifa zima limeshuhudia mabadiliko kandamizi katika masuala ya mawasiliano na kidigitali.

Kama nilivyowahi kuona athari za awali kupitia moja ya thread husika iliyokuwa ikieleza namna wizara na mitandao ya simu ilivyofikia makubaliano ya mabadiliko kuanzia jana April 1.

Moja ya makubaliano yaliyokuwa na mapungufu ambayo watu walishindwa kuyaona ni yaliyoeleza "Mtoa huduma atahakikisha bei za vifurushi zinazingantia bei ya chini na ya juu zilizowekwa na mamlaka." kwa kupitia bei elekezi ambayo ilitolewa kwenye barua husika ilikuwa TZS. 24.16 kwa MB ambayo clearly nilitahadharisha kwamba ni kifungo kwa watanzania na go ahead kwa watoa huduma kuendeleza ukandamizaji.

Ingelikuwa ni mkataba wa kimataifa, taifa lilikuwa linaingia katika moja mikataba mibovu kama ulivyozoeleka.
 
Back
Top Bottom