Ushauri kwa member anayeitwa Perry

Ushauri kwa member anayeitwa Perry

Yeye mwanaume kakubalije kuzaa hao watoto wote na aliyezaa naye anamdhalilisha mbele yao.

Suala la watoto tuache kulitumia kuwahukumu wanawake..... wanabeba mimba ila tendo tunafanya nao na kibaya zaidi sisi ndiyo initiator wa tendo la ndoa kwa jamii zetu.

Opinion: dada wa huyo jamaa hatamani waishi kama anavyomfanya huyu dada.
Mwanaume alimuona huyo mwanamke hana akili na hana pakwenda .. Watoto ni wake hata asipohudumia hawawezi kupata baba mwingine.. kuwa baba ni kibailojia na asili sio kuhudumia au kufunga ndoa ... Mwanamke ndiye mjinga mpka anarisk maisha yake ya kuzaa kwa mtu anayemtumia bila ya heshima ya ndoa.

Wanawake ni wajinga na hii mitazamo yao ya kujifanya wanajua sana ,ukimuambia unakosea kufanya hivi : atakuambia ':unahukumu kwani wewe ni Mungu ''

Mtu anatumika mpaka anazaa mpaka sehemu za siri zinatepeta ila bado haoni umuhimu wa ndoa ...Mwanaume hata asipohudumia watoto watabaki kuwa wake milele.
 
Hivi kumbe Perry ni mwanaume 🤦‍♀️

Hata sielewi nini kinaendelea hapa, uzi uliotajwa wa Perry niliusoma kama chai...

JF ina mambo sana, kuna mwingine juzi kati kameza kijiti, kaja jukwaani chap kuomba msaada...eeish!!
 
Hata sielewi nini kinaendelea hapa, uzi uliotajwa wa Perry niliusoma kama chai...

JF ina mambo sana, kuna mwingine juzi kati kameza kijiti, kaja jukwaani chap kuomba msaada...eeish!!

Kama member Perry ni mwanaume basi uzi wake ni chai kweli inawezekana
Lakini mtu akileta uzi usiku kama ule for some reasons huwa naamini

Yule aliyemeza kijiti sio mtu wa drama,itakuwa kweli
 
Kaka kumbuka tunaongelea mwanaume mwenye watoto watatu, aliyekaa mwezi asijue wanakula nini, anayempiga mke na kumdhalilisha mbele ya watoto wake.

Haya hataki ndoa maana kuwa na watoto sio guarantee ya ndoa. Hao watoto wanakula nini kwa mwezi?

Utasema mwanamke alijiondokea mwenyewe(kiburi) utaacha kuondoka kama unapigwa na kudhalilishwa mbele ya wanao.....
Mimi kosa hapo ni kumpiga mbele ya watoto lakini kumpiga kama alienda nje ya mstari siyo kosa,kingine kwenye mahusiano ya ndoa inafaa tujue (hasa dada zetu) ni nani wa kumtaka ushauri tunapohisi mambo hayaendi sawa,tunao watu waliotuzidi umri kwenye familia zetu huyu mwanamke angeenda kuwataka ushauri siyo kwenda kwa anaolingana nao umri ambao nao wamechanganyikiwa maisha zaidi yake.

Nina uhakika 100% ushauri arudi kwao just alipigwa vibao mbele ya watoto haukutoka kwa mtu mature enough wa kushauri mambo ya ndoa,huyu alimshirikisha rika lake aliyezalia nyumbani mwenye chembechembe za u-feminist haraka sana akamwambia wanaume wote ni mbwa arudi kwao nyumba ya kuishi hajakosa nae akarudi lakini angekuwa amemshirikisha baba mkubwa au mjomba kutoka upande wowote wa mumewe au kwao kwanza angetulizwa kisha angetafutwa mumewe akumbushwe umuhimu wa kuzuia hasira za ghafla mambo mengine akamalizie chumbani.

Umezungumzia hajui watoto wanakula nini?mwenye dada yake alisema anafanya biashara online,sijui wakati anaondoka alitamka maneno gani but siku hizi mwanamke akigombana na mumewe na akawa na 800K M-pesa utasikia ”am super woman” au ”mimi ni mpambanaji” sitashindwa kitu na shit nyingine so jamaa ameamua asubiri labda atatafutwa akishindwa kuwalea.
 
Unamaanisha hiyo story ni ya kutunga?
Binafsi sijaamini kuna mwanaume anaweza akamnunia mkewe mwezi mzima ndiyo maana nikataka kufahamu mdau ameaminije habari kama hii ya upande mmoja?
 
Kwa mwanaume falaa.
Kuna wanaume wana gubu zaidi ya mwanamke
Wewe umewahi kukutana nao au umewajua kupitia visa kama hivi?

Naamini kama kuepusha shari mwanaume anaweza akakaa kimya siku moja au mbili lakini week mwezi hapana,shida anakuwa ni mwanamke na tatizo kwenye hizi kesi wanawake hutia huruma na wanaume siyo mara zote huulizwa that's why inabaki kujulikana mwanaume ndiye mwenye gubu lakini sivyo.
 
Dogo Daby umekosea kuchukua upande mmoja kabla ya kujiridhisha na ukweli wa maelezo hata hayo ya upande mmoja tu. Usikute mwamba alijaribu kumpigia kimada wake wa miaka nane baada ya kimada kutoroka na watoto lakini kimada ambaye ni Dada yetu akakausha. Halafu usipotoshe dogo Daby hizo nchi unazosema wangekua huko jamaa angeshukiwa na mvua ya child support kwanza huyo dada yetu ndo angekamatwa Kwanza na pengine hata kuishitakiwa for kidnapping her own children. Nieleweke napinga unyanyasaji wa binadamu yeyote yule Ila ninaamini zaidi kwenye facts and fairness siyo ktk mihemuko.
 
Wewe umewahi kukutana nao au umewajua kupitia visa kama hivi?

Naamini kama kuepusha shari mwanaume anaweza akakaa kimya siku moja au mbili lakini week mwezi hapana,shida anakuwa ni mwanamke na tatizo kwenye hizi kesi wanawake hutia huruma na wanaume siyo mara zote huulizwa that's why inabaki kujulikana mwanaume ndiye mwenye gubu lakini sivyo.
Tunaishi na watu...wapo watu tena wanaume atauchuna mwrzi na ushee
 
Back
Top Bottom