Ushauri kwa Halima Mdee

Ushauri kwa Halima Mdee

Usimpangie vyama vya siasa viko vingi siyo tu chadema .Chadema ya sasa inaongozwa na mazwazwa
Nimeshuhudia wimbi la Wabunge wenzako waliotoka CHADEMA wakihamia Vyama vingine. Mimi nakushauri narudia tena nakushauri usije ukachukua uamuzi wa kuhamia Chama kingine. Wewe umetoka mbali na CHADEMA tangu kuanzishwa kwa Chama hicho. Umekulia humo, umekijenga Chama hicho mpaka kikafikia hatua ya kuwa Chama Kikuu cha upinzani. CHADEMA sasa hivi ni Chama tishio na kina wanachama wapatao millioni 16 na kinapendwa na wananchi.

Kama CHADEMA hakitaingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi nakushauri Mhe. wewe vumilia na miaka mitano siyo mbali na CHADEMA itarudi kwa kasi ya kutisha. Niamini come 2030 CHADEMA inaweza kuwa Chama Dola.

Mhe. Mdee wewe vumilia achana na kuhama CHADEMA Oktoba 2030 wewe ndo utakuwa Mhe. Waziri wa Sheria na Katiba.
 
Hamna mwanasiasa alieniuma kama yule dogo wa arumeru joshua nassari. Dogo alikuwa ana potential kubwa sana kuja kuwa giant wa siasa za Tanzania... sema ndio hivyo tamaa za vyeo zikamuingia leo hii hata hajulikani yupo wapi!
ajulikan halipo, wewe mwenzako anachapa kaz unakuja kusema ajulikan, si amechukua na form leo au. unadhan amepoteana km wewe huku ujielewi
 
Halima labda ajaribu bahati yake ya ubunge via CCM au CHAUMMA
 
Aende tu na yeye mi ms*nge kama mwenye kiti wa chama atacho amia
 
Avumilie akiwa CHAMA gani? Hapo alipo yupo tu, Aende tu CCM akaendeleze kuijinga nchi
 
..namshauri astaafu siasa.

..uamuzi wa kwenda bungeni bila ridhaa ya chama chake, hawezi kuukwepa, au kuurekebisha.
Chama chake kipi tena? Chadema wameisha mtimua na sidhani kama wana nia nae. Uzuri bado ana options. Ajiunge na ACT-WAZALENDO au Chaumma. Wote hao ni wapinzani. Lakini hata akienda CCM anaweza kuwa Mpina mwengine. Au anaweza kuwa mwana harakati huru. Options ziko nyingi tu.

Amandla...
 
Hama hama ya vyama inapotezaga watu makini sana kwenye uwanja wa siasa kama wakina matiko na Bulaya Wakikosa Ubunge jua ndo bye bye kwenye siasa za Tanzania labda wakumbukwe kwenye UDC na RC basi ila kisiasa ndo wameenda kujimaliza bora wangetulia miaka mitano ipite Mbona Masele wa shinyanga alivumilia now karudi kwenye Game
Hata wakipata ubunge thamani yao itakuwa imeshuka sana. Na huko waliko itabidi wawe chawa kuliko chawa original.

Legacy yao wameiharibu na itakuwa vigumu sana kuikarabati.

Amandla...
 
Chama chake kipi tena? Chadema wameisha mtimua na sidhani kama wana nia nae. Uzuri bado ana options. Ajiunge na ACT-WAZALENDO au Chaumma. Wote hao ni wapinzani. Lakini hata akienda CCM anaweza kuwa Mpina mwengine. Au anaweza kuwa mwana harakati huru. Options ziko nyingi tu.

Amandla...

..labda chaumma au act kutamfaa zaidi.

..lakini wabunge 19 wana kazi ya ziada kurudisha imani ya wapenda mabadiliko waliyopewa wakati wakiwa chadema.

..nadhani wananchi bado wanatamani kusikia toka kwa wabunge 19 hatua kwa hatua kwa utaratibu gani walifika bungeni.
 
Nimeshuhudia wimbi la Wabunge wenzako waliotoka CHADEMA wakihamia Vyama vingine. Mimi nakushauri narudia tena nakushauri usije ukachukua uamuzi wa kuhamia Chama kingine. Wewe umetoka mbali na CHADEMA tangu kuanzishwa kwa Chama hicho. Umekulia humo, umekijenga Chama hicho mpaka kikafikia hatua ya kuwa Chama Kikuu cha upinzani. CHADEMA sasa hivi ni Chama tishio na kina wanachama wapatao millioni 16 na kinapendwa na wananchi.

Kama CHADEMA hakitaingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi nakushauri Mhe. wewe vumilia na miaka mitano siyo mbali na CHADEMA itarudi kwa kasi ya kutisha. Niamini come 2030 CHADEMA inaweza kuwa Chama Dola.

Mhe. Mdee wewe vumilia achana na kuhama CHADEMA Oktoba 2030 wewe ndo utakuwa Mhe. Waziri wa Sheria na Katiba.
Halima kwa sasa sio mwanachama wa CHADEMA. Alishafukuzwa yeye na wale wenzie 18 ambao wanatengeneza kile kinachitwa covid 19.
Anachopaswa kufanya ni kuomba radhi na aombe tena uanavhama upya. Anaweza akakubaliwa au kukataliwa. Kwa alivuo sasa na misimamo ya mwenyekiti, ushauri wako hauna maana.
 
CHADEMA sasa hivi ni Chama tishio na kina wanachama wapatao millioni 16 na kinapendwa na wananchi.
We unaota kweli, chama kinajifia we unasema eti tishio, kinamtisha nani? Hiyo njia ndio waliopitishwa nccr na cuf na hakuna alie survive. Ccm ni dude hatari sana.
 
kwahiyo sio Covid 19 tena, au mmesau mlivyokuwa mnamkejeli, hiv unafaham halima ccm ndio umemfariji mpaka hapo alipo na anajua mwoyoni mwake. labda mzee wa busara km Mbowe arudi ila sio huyu mtu asiyekuwa na hekima wala busara na mropokaji. ndio maana hata hakuna mtu anayemsaidia huko maakaman maana hana shukrani sana akitoka anaanza na yule aliyemsaidia bila hata kuwa na aibu
Lisu hahitaji kusaidiwa, katafute hao mnaowasaidiaga ndio uwatishe.
 
We unaota kweli, chama kinajifia we unasema eti tishio, kinamtisha nani? Hiyo njia ndio waliopitishwa nccr na cuf na hakuna alie survive. Ccm ni dude hatari sana.
Mlifanikiwa zamani, kizazi hiki mmeukalia. Na kwa kukusaidia tu, CUF ilikufa baada ya Maalim Seif kuihama. Cdm inaweza kupotea mtu mwenye misimamo kama Lisu akiondoka, na kikaongozwa na mtu kama Mbowe.
 
Ajaribu kilimo na ufugaji miaka 20 bungeni inamtosha atafute na mme aolewe
 
Nimeshuhudia wimbi la Wabunge wenzako waliotoka CHADEMA wakihamia Vyama vingine. Mimi nakushauri narudia tena nakushauri usije ukachukua uamuzi wa kuhamia Chama kingine. Wewe umetoka mbali na CHADEMA tangu kuanzishwa kwa Chama hicho. Umekulia humo, umekijenga Chama hicho mpaka kikafikia hatua ya kuwa Chama Kikuu cha upinzani. CHADEMA sasa hivi ni Chama tishio na kina wanachama wapatao millioni 16 na kinapendwa na wananchi.

Kama CHADEMA hakitaingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi nakushauri Mhe. wewe vumilia na miaka mitano siyo mbali na CHADEMA itarudi kwa kasi ya kutisha. Niamini come 2030 CHADEMA inaweza kuwa Chama Dola.

Mhe. Mdee wewe vumilia achana na kuhama CHADEMA Oktoba 2030 wewe ndo utakuwa Mhe. Waziri wa Sheria na Katiba.
Na matusi mliyomtukana miaka yote hii mitano unaisemea.
 
Mlifanikiwa zamani, kizazi hiki mmeukalia. Na kwa kukusaidia tu, CUF ilikufa baada ya Maalim Seif kuihama. Cdm inaweza kupotea mtu mwenye misimamo kama Lisu akiondoka, na kikaongozwa na mtu kama Mbowe.
Mbona tayari ccm wameshafanikiwa kuiua chadema, chadema kwisha habari yake, wenye akili wote wameshaondoka chadema yamebakia manyumbu tu yanadanganyana, mnaimba no reform no election wakati watu wanachukua fomu kushiriki uchaguzi.
 
Mbona tayari ccm wameshafanikiwa kuiua chadema, chadema kwisha habari yake, wenye akili wote wameshaondoka chadema yamebakia manyumbu tu yanadanganyana, mnaimba no reform no election wakati watu wanachukua fomu kushiriki uchaguzi.
Nasema hivi, kama mlifanikiwa basi ni zamani. Kwa sasa kizazi kimeamka. Watu kuchukua fomu ndio dalili za cdm kufa? Ccm inatakiwa iiue cdm kwenye uwanja wa siasa na box la kura. Vyombo vya dola havitakaa viweze kwa kizazi kilichoamka.
 
Back
Top Bottom