KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,601
Kwa kuwa tunatumia jukwaaa ili kushauriana na kushauri, kutoa maoni na mapendekezo na hata kutoa onyo na karipio basi acha Leo nitoe ushauri kwa CHADEMA jambo ambalo ni nadra kweli kulifanya.
Kwa kuwa nilitumia jukwaaa hili kumshauri ndugu yangu Abdul Nondo ambaye ni Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT juu ya wazo la kufanya maandamano yasiyo na kikomo kuelekea ikulu. Katika Uzi wenye "title" , " ACT achaneni na migomo na maandamano kama CHADEMA, Jikiteni kwenye mipango na mikakati ya muda mrefu". Pengine ACT walipitia Uzi ule na kuachana na suala lile na badala yake ACT ni waumini Wazuri wa mijadala. Afya ya demokrasia na siasa safi ni mijadala.
Leo pia napenda kutumia jukwaaa hili hili kutoa ushauri Kwa CHADEMA na huu ndio ushauri wangu MDHIBITI MDUDE NYAGALI KABLA UVUMILIVU WA RAIS SAMIA HAUJAFIKA MWISHO NA CHAMA KUJUTIA.
Kwanza kabisa, kitendo Cha kumpa Rais Samia siku 30 za kuachana na mkataba wa uwekezaji wa bandari ni kitendo kilichokosa nidhamu na heshima Kwa vyombo vya Dola Kwa maana ya Mahakama na Bunge. Kutaka Rais asitishe suala lililoamriwa na Mahakama na kukubaliwa na Bunge ni kutaka kuaminisha watu kwamba Bunge na Mahakama haviko huru.
Pili, kutaka kufanya maandamano yasiyo na kikomo ni tafsiri ya kutaka kuanzisha fujo. Hiko kibali Cha kufanya maandamano yasiyo na kikomo yatatokana na sheria Gani? Katiba inatafsiriwa na katiba ,haki ya maandamano ni haki ya kikatiba lakini tafsiri ya haki inapatikana kwenye sheria.
Tatu, Mdude Nyagali amekuwa akitumia lugha za kudhalilisha na kukashifu jambo ambalo Leo Rais amelizungumzia kwenye mkutano wa vyama vya siasa amesema kwamba " Ruhusa ya mikutano ya hadhara haikutolewa ili kutukana na kusema dini za wengi". Ni wazi Rais anakerwa na kauli za Mdude Nyagali.
Tambueni Rais Samia ni mvumilivu lakini Uvumilivu wake unaweza mwisho siku moja, msimfikishe huko. Mdhibitini Mdude Nyagali kabla Uvumilivu wa Rais Samia haujafika mwisho na huu ndio ushauri wangu kwenu
Kwa kuwa nilitumia jukwaaa hili kumshauri ndugu yangu Abdul Nondo ambaye ni Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT juu ya wazo la kufanya maandamano yasiyo na kikomo kuelekea ikulu. Katika Uzi wenye "title" , " ACT achaneni na migomo na maandamano kama CHADEMA, Jikiteni kwenye mipango na mikakati ya muda mrefu". Pengine ACT walipitia Uzi ule na kuachana na suala lile na badala yake ACT ni waumini Wazuri wa mijadala. Afya ya demokrasia na siasa safi ni mijadala.
Leo pia napenda kutumia jukwaaa hili hili kutoa ushauri Kwa CHADEMA na huu ndio ushauri wangu MDHIBITI MDUDE NYAGALI KABLA UVUMILIVU WA RAIS SAMIA HAUJAFIKA MWISHO NA CHAMA KUJUTIA.
Kwanza kabisa, kitendo Cha kumpa Rais Samia siku 30 za kuachana na mkataba wa uwekezaji wa bandari ni kitendo kilichokosa nidhamu na heshima Kwa vyombo vya Dola Kwa maana ya Mahakama na Bunge. Kutaka Rais asitishe suala lililoamriwa na Mahakama na kukubaliwa na Bunge ni kutaka kuaminisha watu kwamba Bunge na Mahakama haviko huru.
Pili, kutaka kufanya maandamano yasiyo na kikomo ni tafsiri ya kutaka kuanzisha fujo. Hiko kibali Cha kufanya maandamano yasiyo na kikomo yatatokana na sheria Gani? Katiba inatafsiriwa na katiba ,haki ya maandamano ni haki ya kikatiba lakini tafsiri ya haki inapatikana kwenye sheria.
Tatu, Mdude Nyagali amekuwa akitumia lugha za kudhalilisha na kukashifu jambo ambalo Leo Rais amelizungumzia kwenye mkutano wa vyama vya siasa amesema kwamba " Ruhusa ya mikutano ya hadhara haikutolewa ili kutukana na kusema dini za wengi". Ni wazi Rais anakerwa na kauli za Mdude Nyagali.
Tambueni Rais Samia ni mvumilivu lakini Uvumilivu wake unaweza mwisho siku moja, msimfikishe huko. Mdhibitini Mdude Nyagali kabla Uvumilivu wa Rais Samia haujafika mwisho na huu ndio ushauri wangu kwenu