Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 10,422
- 18,056
Kwenye hotuba yake ya kwanza akiapishwa Rais Samia mnamo 19/03/2021 alitamka kuwa magazeti yafunguliwe, wananchi waikosoe Serikali kwa mujibu wa sheria. Akasisitiza na kesi za kubambikizwa zifutwe. Akakemea Kodi za DHULUMA zikusanywazo na TRA, na kuikemea TAKUKURU na Polisi kwa kuwanyanyasa watu bila makosa.
Kweli tukaanza kuona nuru mpya baada ya siku chache. Ikawa kama ni kupindua kabisa mambo ya ukatili na uuaji ambayo yalitamalaki wakati wa Magufuli.
Kesi ya Akwilina ikapinduliwa na Mahakama ya Rufaa, yule Mdude CHADEMA wa Mbozi maarufu kwa matusi naye akashinda kesi
Mara tukaanza kusikia kauli za matusi kwenye mikutano ya CHADEMA. Mfano ni ile kauli ya Mdude siku 4 tu baada ya kuachiwa alisikika akiongea Jukwaani Barracuda Tabata kuwa "Mwambieni huyo Mama yenu, nitamnyoa kwa wembe uleule niliotumia kumnyoa mtangulizi wake"
Alitamka maneno mbele ya Mbowe na viongozi wengine wa CDM na hawakumchukulia hatua mpaka leo.
Kwa mtazamo wangu Serikali imeona pengine bado hatuna busara katika kutumia uhuru wa maoni. Tunaleta matusi badala ya kutoa maoni.
Kweli tukaanza kuona nuru mpya baada ya siku chache. Ikawa kama ni kupindua kabisa mambo ya ukatili na uuaji ambayo yalitamalaki wakati wa Magufuli.
Kesi ya Akwilina ikapinduliwa na Mahakama ya Rufaa, yule Mdude CHADEMA wa Mbozi maarufu kwa matusi naye akashinda kesi
Mara tukaanza kusikia kauli za matusi kwenye mikutano ya CHADEMA. Mfano ni ile kauli ya Mdude siku 4 tu baada ya kuachiwa alisikika akiongea Jukwaani Barracuda Tabata kuwa "Mwambieni huyo Mama yenu, nitamnyoa kwa wembe uleule niliotumia kumnyoa mtangulizi wake"
Alitamka maneno mbele ya Mbowe na viongozi wengine wa CDM na hawakumchukulia hatua mpaka leo.
Kwa mtazamo wangu Serikali imeona pengine bado hatuna busara katika kutumia uhuru wa maoni. Tunaleta matusi badala ya kutoa maoni.