Ushauri kuhusu machinga: TFF wapewe ofisi mjini, Karume pageuzwe kituo cha biashara

Machinga wameandaliwa eneo la kisasa na Wachina pale Ubungo.

Kutakuwa na vizimba 10,000
Hivi kwanini maamuzi yanafanywa haraka haraka hivi?
Kuna mantiki gani kuwapeleka machinga 10,000 mahali pamoja? Ni vigezo gani vilitumiwa kufikia uamuzi huo?
Kwa misingi ya human and business re-settlement; changamoto zote za kiuchumi, kimazingira, nk kwa wadau wote zimefanyiwa kazi lini?
Au ni kuhamisha tatizo kutoka eneo A kwenda eneo B? Na kwa maana hiyo pengine linakuuzwa zaidi?

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
Kwanini soko la mitumba mchikichini lisipanuliwe kwa kujengwa ghorofa baadhi wakawekwa pale, nasema baadhi kwa sababu so wore watatosha.
 
Baada ya serikali kuhamia Dodoma kuna majengo mengi sana kule posta hayana kazi mfano wizara ya afya , wizara ya ardhi, wizara ya fedha nk.

Serikali iwapatie TFF jengo mojawapo wafanye shughuli zao kama ofisi , wawapatie na ekari kadhaa za ardhi nje ya mji kwa ajili ya kujenga uwanja wa mpira, ule uwanja ugeuzwe kituo cha kibiashara kiunganishwe na machinga complex, machinga wa kariakoo wahamie Karume uwanjani
Your a great thinker aisee
 
ile Machinga comprex iongezwe kwa kuvunja ule uwanja wa mpira pale Karume na TFF...na lile eneo la makaburi upande wa pili lihamishwe then lile eneo lote liwe stand ya daladala na lile soko la ilala mchikichini ligeuzwe parking kuubwa ya magari madogo yanayoingia kariakoo na huku machinga complex...

Wale machinga wote wa kariakoo unahamishia hapo na wale wa mchikichini hapo Tatizo linakuwa solved kirahisi kabisa..
 
Masoko yajengwe Kila mtaa maana Kila mtaa una watu wanahitaji huduma, mambo ya kulundika watu mjini haitakiwi kwa usalama wa miji na kupunguza mipango ya vikundi vibaya hasa kwa vijana wenye nguvu kutafutiwa sehemu za kukaa Bure tu zinaleta vikundi vibaya kama Sasa machinga na bodaboda inavyotaka kuwa tishio hata kwa jeshi, vijana wenye nguvu waingie kwenye kazi rasimi kama ni masoko walipie Ili wapate uchungu kutumikia Nchi na taifa Sasa vijana kuruhusiwa kufanya vitu holela na Bure hata Sheria za Mungu tunaziacha, kikubwa vijana wasiruhusiwe kukaa sehemu moja wengi bila mamlaka kuwadhibiti na kuwaongoza au kutokuwa chini ya watu wanaowaongoza itakuja kuleta shida, imagine Leo kunawatu kama Sabaya kuachwa bila kusimamiwa kama kijana ni nini kimetokea? Hata hizo sehemu za bei ndogo wapewe wazee wasiojiweza ila mambo ya kuweka mauwanja ya kukusanya vijana na watu wenye nguvu sehemu moja haitakiwi kabisa.
 
Wamikoani nao wanaamishiwa Ubungo kwa wachina?

Hili haliwezi kuwa suluhisho la tatizo hili. Tunatakiwa kubadili vijana wetu kutoka kuwa wachuuzi wa bidhaa tena nyingi zikiwa fake (maana nyingine ukiziangalia kwa jicho la ukali zinavunjika!!!) kutoka nje ya nchi kuwa vijana wazalishaji mali na wauzaji wa mali hizo hapa nchini na nje ya nchi tena kwa faida. Hili ndilo suluhuisho la tatizo hili.

Hao wachumi na wataalamu wa fani mbalimbali waandae strategies za kuwezesha vijana kuzalisha mali na kuziuza nchini na ng'ambo. Uwezekano huo upo kwa sababu Mama 'kafungua' nchi, Mama 'katangaza' nchi, na Mama kapata 'msafisha taswira' ya nchi tena lobbyist nguli wa dunia.

Kwa hiyo hakuna kisingizio cha kushindwa kufanikiwa kuwasaidia vijana.
Samahani, huyo lobbyist ni nani!? Point yako ina maana kubwa sana. Maana uzslishaji ndio utatukomboa na sio uchuuzi wa makorokoro ya wachina.
 
Tamanio langu serikali ifanye kila linalowezekana kuwawezesha vijana kuwa wazalishaji badala ya wachuuzi!
Hili linawezekana panapo nia.
 
Machinga wanavyobembelezwa kama mtoto wa mwalimu wa darasa 😄
Watoto wa magufuli hao aliowaachia wavunje sheria wazi wazi sasa samia ana kazi ya kusimamia Sheria bila ya kupepesa ama sivyo watamchafulia mipango yake ya kusafisha majiji.
 
Back
Top Bottom