Ushauri kuhusu ku-apply vyuo vikuu 2016/2017

Ushauri kuhusu ku-apply vyuo vikuu 2016/2017

ah sawa nimekuelewa mkuu vp kwa yule kijana aliyepata DDS HGL akiaply education anaweza akapata na una mshauri angeaply chuo gani ambacho hakina ushindani???
 
ah sawa nimekuelewa mkuu vp kwa yule kijana aliyepata DDS HGL akiaply education anaweza akapata na una mshauri angeaply chuo gani ambacho hakina ushindani???
nimeskia NIT education ipo, so aombe hapo, udomu, ruco, makumira, theofilo kisanji, archiboshop mihayo
 
Mdogowangu ana matokeo ana division 3 ya point 16
Physics E
A/mathematics E
GS E
Chemistry S
unamshauri aende chuo gani??
 
HGL nimepata DDE Napenda kuwa mwalimu ipi nzuri Bachelor of Art's Education au Education for special needs ipi itakua na soko zuri
 
Nina division two ya 12 history D,kiswahili C,English E.Vipi hapo UDSM wananichukuwa Education ?
 
mbona watanzania hampendi huambiwa ukweli. hayo maelezo yako hapo juu inaonyesha unaringa kabisa.
pia hujaombwa uje uombe ushari kwenye huu uzi sisi tunataka watu wenye nia ya dhati ya kusoma. majivuno yako baki nayo moyoni huku hadi 1 za 3 zipo wala humtishi mtu humu, we vipi
Ila we jamaa umezidi unoko bana, Mtu kakujibu vizuri we unasema unoko
 
Habari ndugu na wana JF kwa ujumla.

Nimeona nianzishe huu uzi mahususi kabisa kwa wale wanaoomba vyuo vikuu kozi mbali mbali tuwape elimu na ujanja ili waweze ingia vyuo wavipendavyo.

Pia huu uzi utashauri ubora wa chuo husika kuhusu baadhi ya kozi kwani kuna baadhi ya vyuo vina sifa kadhaa katika fani wanazofundisha.

Unachopaswa kufanya ewe unaeomba chuo utaleta matokeo yako yote ili tuyachambue ndio tukupe ushauri, pia kwa vyuo vyenye ushindani kwa kozi fulani hawa hadi matokeo ya form four wanaangalia so usiwe na hofu relax tutakushauri na hakika utashinda mapema wala hutapoteza kitu na pia uwashauri na wenzio walio karibu wapitie huu uzi ili wajifunze zaidi.

Kumbuka ufaulu wako ndo unaamua yote unapoomba kozi angalia ufaulu wako na ushindani kama idadi ni kubwa sana ya waliiomba na wewe una matokeo hafifu badilisha haraka.

Pia ni vyema kufanya maamuzi sahihi ukitegemea eti utahama chuo ni ngumu na hizi habari zinaingiliana na mkopo hivyo basi utaweza kuja kupata mkopo mwaka wa pili.

Hivyo basi jandae vizuri usiwe mbishi sikiliza ushauri wetu vizuri na sisi tumepita huko.

Pia wenzetu mliosoma diploma tunaweza wasaidia mawili matatu.
Karibuni sana.
Nina division 1.9 ya PCB yaani C C C. Kwa kozi ya MD vipi, na ni kwa Vyuo gani?
 
.
UDSM hakuna Udaktari
Mkuu una uhakika ukisemacho?! Mbona toka mwaka jana wamedahili wanachuo kwa kozi ya MD
Kama hujui kitu kaa kimya na usiwapotoshe wenzako na wala hutoonekana mjinga
 
Mkubwa nimemaliza form six PCB matokeo yangu ni haya:
Physics E
Chemistry D
Biology D.
Nina ndoto ya kusomea course za afya l, hasa udaktari!! Naombeni ushauri wakuu....
 
hayo ni matokeo ya form four tena bora umekutana na mimi nikushauri, kwa ukweli wewe una uwezo wa kawaida. sikushauri uende form six kule ni kupoteza mda tuu ila kama una amin utapata division one basi nenda na iwe ya PCB hapo utaweza kujikinga kifua na kuomba kozi ya udaktari vyuo vya serikali kama muhasi, udsm na udom. ila kwa vyuo vya private pcb za division 2 hadi 3 unaenda iwe unataka udaktari, ufamasia au maabara. ila kwenu muwe mna pesa ada ni zaidi ya million 6. kwa vyuo vya imtu, hku, kairuki huko. kampala. ila vyuo kama archibishop james songea ada ni million 3 na ushee ivi, st francis morogoro ada ni million 3 kasoro. na jua kadri miaka ivavyozidi kwenda ada nayo inapata.
kcmc na bugando ata inakaribia million 3 ila lazima uwe umefaulu vizur pcb, ushindani upo man,

ushauri wangu achana na mambo ya advance sababu unautaka udaktari. kwan zinahitajika pcb za one ila unaweza kwenda kama utakuja kusoma vyuo vya private na hela yako juu. serikali inatoa mkopo kwa hela isiyozidi million 3.1 na hapo hiyo milliom3.1 ni full yan asilimia 100% sasa wewe kubata hiyo asimilia 100% inategemea kama umekidhi mahitaji na vigezo vyao, mfano kama umesoma serikalini kuanzia msingi, olevel na advance na vipengele vyao vingine unaweza pata asilimia 100% au usipate kabisa kama seriikali haina pesa hili ni swala la bahati ndugu. kuna mayatima waliambatanisha vyeti vyao na ulemavu wa wazazi wao lakini wapi hawakupata nawengine wakafunga safari hadi hadi bodi ya mkopo na hawakusaidiwa,
so ndugu we apply chuo cha diploma tena vya serikali wewe matokeo yakmo yanaruhusu kabisa na utapata nina imani.
nimejitahidi nimekuambia yote. ukiwa na tatizo zaid nicheki usiwe na hofu
Duh! yan kumbe 100% ndo million 3.1 tu!!! Sasa kwa yule anayepata 40% au 50% au 30% anapewa sh. ngap sasa...!!!
 
dah wakuu me nataka nikapige procurement & logistic management au banking &finance IPI kati ya hizi iko poa kwa kujiajiri au kuajiriwa? Nisaidieni wakuu ..
 
Nina two ya 12 Geog D, math E na Economics C nataka kusomea BAF ya ARDHI vipi naweza kupata
 
Back
Top Bottom