kutokana na aibu iliyotufika kambi ya upinzani katika kikao cha bajeti kilichomalizika jana, kwa kutengeneza bajeti mbovu na isiyoeleweka, mpaka wabunge wa CCM kuifananisha na bajeti ya Harusi, hii inaonesha kuwa kambi ya upinzani bado hatujajipanga kuongoza serikali na ilhali kambi ya upinzani tunao wachumi wazuri mf. Prof Lipumba kulikuwa na ugumu gani kumshirikisha katika kuandaa Bajeti mbadala? au ndio ubinafsi ule ule unaofanywa na ccm dhidi ya kutowashirikisha wapinzani, Prof kahigi kalisema hili wakati akichangia, serikali inaona ugumu gani kumtumia Prof Lipumba? na upinzani nasi tunafanya yale yale, je? kwa hali hii watanzani tutapata Maendeleo?