Usalama wa taifa umevamiwa?

Griss

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2025
Posts
337
Reaction score
1,945
Watu wengi wanafikiri usalama ni kulala na kuamka mzima.

Lakini usalama ni zaidi ya hapo

Nawaambia nchi haipo salama kwa Sasa.

Hakuna usalama wa ajira yaani kwa Sasa mpaka utoe rushwa ya pesa,Ngono au uwe Mtoto wa kiongozi ndio upate ajira au cheo.

Usalama wa kiafya haupo Kama ndugu yako anakufa anadaiwa milioni moja wanashikilia maiti Muhimbili.

Usalama wa uraia wako haupo kwa sababu mtu anaweza kutoka Rwanda, Burundi, Congo au Oman na kuja akaanza kuwa Chawa wa kiongozi mwisho wa siku anakuwa waziri mkuu

Ukiwa mzalendo na mzawa unaweza kuundiwa zengwe la kuambiwa si uraia Kama ilivyokuwa kwa wapili na watu kibao.

Wako wapi wengine Kama yule Nasari, Wenje, Zitto, kafilulila, Mdee walioibuka from no where?

Wakawa wabunge now bila pesa hakuna ubunge? Ingawa walikuja kukengeuka lakini tumeshindwa ku groom wapya?

Kiongozi ambaye ajaandaliwa na TISS kutoka sekondari na jkt anawezaje kuwa mzalendo wa kulinda rasilimali za nchi?

Kiongozi anayepewa pesa na mtu akatafute cheo akikipata atamtumikia mtu au watu?

TISS imelala ni lini tena tutapata kiongozi bure aje kututumikia bure?

Kiufupi usalama wa taifa umevamiwa na umekufa!.
 
kuna mtu mmoja namfahamu siyo raiya kabisa
amenunua kiwanja tena dar es slaam hakuna anayejali
ana mpaka NIDA
Je mtanzani anaweza kupata NIDA RWANDA?
KUNUNUA ARDHI JE?
USALMA WA CCM WAPO TU WANAKULA MATIKITI
Wakivaa v tshirt vya taifa stars na zile kapero zenye bendera ya taifa wanafikiri wamemaliza
usalama wa taifa anakubali kudai madeni ya bar tena akijitambulisha kabisa kwamba anatokea MAKUMBUSHO? kweli
 
Ni kweli kabisa
 
Haya ya rushwa haya jaanza leo.
Tangu wakati wa Mzee Ruksa , na yakapanda chati wakati wa kapa na kikwete.
Magufuli alijaribu kuyapunguza lakini hakuweza.
Samia hana ubavu kuya punguza sababu cabinet yake ni ya wale walo ingia serikalini kwa Rushwa.
Sasa tu ngoje uchaguzi huu utakavyokuwa na serikali atakavyo simamia.

Kwa sasa atakuwa mkali sana maana hii ni awamu yake ya mwisho na anataka kuandika historia
 
Hao uliowataja wamegoma kushiriki uchaguzi watakuaje Wabunge Sasa?
 
Sio kweli, awamu ya mwisho ndio awamu ya kila mtu kujiandalia pensheni yake..
 
Katakana wahuni
 
Nilikuja mbio nikidhani Makumbusho imevamiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…