Sasa wewe mleta ufafanuzi hapa ndio umeharibu kabisa. Yaani una kiri kulikuwa na kulazimishwa na kuteswa kwenda kujenga hicho kituo, lakini ukaharibu kwa kuleta ushabiki wa kumtetea mkuu wa wilaya kishamba. Kwa mfano...
1/Yaani taarifa nzima imejichanganya. Mara vijana wamekwenda kunywa pombe, mara watu wamechukuliwa Gulioni, mara Askari (service men!), Mara hawajapigwa lakini wamerushwa vichura chura nk. Ni mchanganyiko kuliko usahihisho.
2/Mleta ufafanuzi hapa husemi wewe ni nani katika ufafanuzi huu. Wewe ni mkuu wa wilaya hiyo? Wewe ni msemaji wake? Wewe ni shuhuda? Wewe ni mleta mada tu lakini una source?
3/Taarifa hii ya ufafanuzi imetolewa na upande wa mkuu wa wilaya ambayo ndio inayodaiwa kutesa watu. Nini maana ya story kuwa balanced?
4/Kama shughuli ilikuwa ni ya kujitolea, kwanini watu wasakwe, warushwe rushwe kichura, wakimbizwe masokoni, Wahukumiwe kwa kwenda kilabuni?
5/Hivi ukaidi ni nini katika tukio hili? Kama suala ni kuombwa kujitolea, na mtu akakataa kujitolea ili aendelee na shughuli zake za kutafuta pesa, kuna kosa gani hapo?