Usahihi wa taarifa toka Nkasi

Usahihi wa taarifa toka Nkasi

Munaleta hoja isiyo na msingi. ZAHANATI wameiomba hao hao wanakijiji kutokana na shida wanayoipata... zahanati inajengwa mara moja na minada iko kila siku. Sasa unataka waichezee fursa itakayowahudumia wao wenyewe.
Istoshe walikubaliana hao wenyewe siku ya kwenda kushirikiana kuijenga sasa wanapotoroka kazi yao wenyewe unataka mkuu wa wilaya afanye nini....

Musiwe wanafiki wa kudai maendeleo huku mukishindwa kuisimamia wenyewe. Tutabaki na porojo tu.
Kwa hiyo maendeleo yaje kwa wananchi kupigwa na kufanyishwa Kazi siku ya Ibada. Utakuwa hujitambui. Wewe ungezuiwa kihudhuria Ibada uende Songambele ungeona sawa tu.?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa nakuona wa maana kwa sasa sijui ni kuweke fungu gani,unamtetea Said Mitanda kwa upuuzi huu. CRAP!
Hawana maana yoyote hawa wako tayari kutetea hata upuuzi. Mtu kwa madaraka yake anaamua kuadhibu watu kisa maendeleo kwani wale ni wafungwa? Anajitapa wananchi wamekubali kufanya Kazi Jumapili (siku ya Ibada) halafu wapuuzi wanataka tushangilie nao. Mungu alipoamuru kuabudiwa kwa siku hiyo amekuwa mdogo kuliko DC anayebadilisha siku ya Ibada kuwa siku ya Kazi. Na hili wafuasi wanashangilia tu hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Munaleta hoja isiyo na msingi. ZAHANATI wameiomba hao hao wanakijiji kutokana na shida wanayoipata... zahanati inajengwa mara moja na minada iko kila siku. Sasa unataka waichezee fursa itakayowahudumia wao wenyewe.
Istoshe walikubaliana hao wenyewe siku ya kwenda kushirikiana kuijenga sasa wanapotoroka kazi yao wenyewe unataka mkuu wa wilaya afanye nini....

Musiwe wanafiki wa kudai maendeleo huku mukishindwa kuisimamia wenyewe. Tutabaki na porojo tu.
Una uhakika wao ndo walipanga hiyo siku mkuu mbona unaleta hoja za kitoto sana hii serikali inawasikiliza raia wake kweli??

sent from my BlackBerry keyone using JamiiForums mobile app
 
Hoja ilikuwa ni walikwenda Ibadani au walikwenda kunywa pombe?
Uwe mwelewa ndo maana nakuona umedandia hoja usiyoijua. Kwa taarifa yako tukio la kupigwa wananchi lilifanyika tar.12/08/2017 siku ya Jumamosi, baada ya siku hiyo DC akaamuru wananchi waendelee na Kazi siku ya Jumapili. Ndo maana ufafanuzi wake ameutoa jumapili na anajisifu watu wanaendelea na Kazi huku akijua walitakiwa kuwa kwenye Ibada. Kuna dini yoyote inayohalalisha kuacha Ibada makusudi eti mshiriki shughuli ya maendeleo!!? Bado unmsapoti hata kwa hili!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom