Usafiri wa Ungo !

Usafiri wa Ungo !

Kuhusu hii trick am sure unaweza kupata videos kibao youtube lakini soma hapa jinsi ya kufanya hii trick am sure kesho watakukoma ukienda Pub lazima wakuite Uri Geller

Cool Spoon Bending Illusions

Kwahio mkuu chochote kile cha ajabu mtu anachofanya trick ni kwamba amefanyaje na hatujagundua kafanyaje sio kwamba kuna miracles zimetokea

By the way unajua ile trick ya wahindi ya kupiga filimbi na kamba inapanda peke yake ?, hata ila ni illusion tu ambayo watu wameshajua jinsi ya kufanya.., cha muhimu ni kuwa na right equipments na preparation za kutosha

Addition information jinsi Uri anavyofanya:-
Please just take time to visit Uri Uri Geller - This website could change your life!
Pasco.
 
habari zenu,
natumaini weekend inaenda vyema hapo ulipo....leo nilikuwa naangalia taarifa ya habari nikaona watu kadhaa wa familia moja wamedondoka na ungo sehemu flani hapa nchini kwetu tanzania (thread yenye habari zaidi jf hii hapa)...maswali yakaanzia hapo kutoka kwa niliokuwa nao,naomba niwashirikishe ili kama kuna anayefahamu atujulishe.
1.is it scientifically proved kwamba ungo unapaa?....kwanini tusijaribu kufanya utafiti tuhakikishe hii mambo,maana wengine(mimi personally) naona hili swala la kupanda ungo ni mulugo.
2.je hizi ungo zinavyopaa,zina route yake?....kama kulivyo na anga la kimataifa,anga la ndege ndogo etc.
3.je radar inaweza ikaona hizi ungo?
4.ungo unafananaje----kwa mwenye picha tafadhali aweke
5.je zinatumia nishati gani?
6.zipo aina tofauti za ungo?ni ngapi?




Wengine mtaanza kuponda hii thread,ila naamini itatusaidia wengine kupata uelewa kuhusu haya mambo yakoje yakoje,na kama ni kweli au stori tu......sisi ni waafrika,na mambo haya yapo kwetu,nitafurahi kujua kiundani kuhusu haya kwa jf.ni haayo tu kwa leo



cc: watu8 , chimbuvu babav nicas mtei bujibuji zinduna filipo mtambuzi mbuzimzee the boss puppy @lara1 preta erickb52 charminglady mwali ndoa

jibu la no.5. Nishati inayotumika ni damu ya binadamu aliyekufa si zaidi ya wiki moja.
 
Kama kweli wanaweza kusafiri kwa ungo wapewe nafasi kutuonesha.

Kwa shart la wakiweza watawezeshwa mafweza ili kuboresha usafiri huu kwa kuanzisha " tanzania nyungo air lines'' na wakishindwa ni adhabu kali ya kutafuna na kumeza nyungo kumi kila mmoja ili wakome uzushi!
 
...tatizo letu kubwa ni kupenda kujidharau na kuamini kwaba hakuna jema linaloweza kutoka kwa muafrika. tatizo letu lingine ni kutopenda kujisumbua na kutafiti kama kweli hili la kuruka na ungo linawezekana ama la na mengine mengi ambayo ni unexplainable.
Mwaka mzima utasikia watu wameanguka na ungo na kukamatwa halafu kimyaa! husikii anayewahoji kutaka kujua wanatumia mbinu gani kuruka nk. Tnakalia kuponda tu kwamba haiwezekani huku tukisahau kuwa 'No Research, No Right To Speak'.
Toka mambo haya yaanze, nani ambaye angalau amejisumbua tu kutafuta ukweli wa issue hii?

Cha ajabu ni kwamba anaweza akaja mzungu hapa akajichimbia kimya huko Usukumani ama Sumbawanga halafu akapata siri za jinsi ya kuruka na ungo....Halafu shangaa jinsi tutakavyomshangilia na kumuita Mvumbuzi wa tekinolojia ya kuruka na Ungo!!!
Jamani, kuna mengi sana dunia hii ambayo hatuyafahamu. Tusijikwamishe kwa kukataa moja kwa moja kwamba Hayapo ama Hayawezekani. Tuyape benefit of doubt na kuyafanyia utafiti wa kina ili tujiridhishe.
After all tunaambiwa kuwa binadamu anatumia asilimia ndogo sana ya uwezo wa ubongo wake.
 
...tatizo letu kubwa ni kupenda kujidharau na kuamini kwaba hakuna jema linaloweza kutoka kwa muafrika. tatizo letu lingine ni kutopenda kujisumbua na kutafiti kama kweli hili la kuruka na ungo linawezekana ama la na mengine mengi ambayo ni unexplainable.
Mwaka mzima utasikia watu wameanguka na ungo na kukamatwa halafu kimyaa! husikii anayewahoji kutaka kujua wanatumia mbinu gani kuruka nk. Tnakalia kuponda tu kwamba haiwezekani huku tukisahau kuwa 'No Research, No Right To Speak'.
Toka mambo haya yaanze, nani ambaye angalau amejisumbua tu kutafuta ukweli wa issue hii?

Cha ajabu ni kwamba anaweza akaja mzungu hapa akajichimbia kimya huko Usukumani ama Sumbawanga halafu akapata siri za jinsi ya kuruka na ungo....Halafu shangaa jinsi tutakavyomshangilia na kumuita Mvumbuzi wa tekinolojia ya kuruka na Ungo!!!
Jamani, kuna mengi sana dunia hii ambayo hatuyafahamu. Tusijikwamishe kwa kukataa moja kwa moja kwamba Hayapo ama Hayawezekani. Tuyape benefit of doubt na kuyafanyia utafiti wa kina ili tujiridhishe.
After all tunaambiwa kuwa binadamu anatumia asilimia ndogo sana ya uwezo wa ubongo wake.

Tatizo letu wewe na nani?

Wengine mbona tusha commission uchunguzi?

Umesoma hapa?

https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/390623-usafiri-wa-ungo.html#post5539639
 
...Tatizo langu mimi na watanzania wengine ambao idadi yao ni ngumu kuipata.
... nimeingia hapo 'umesoma hapa?', nikajikuta nimerudi tena hapa kwenye uzi huu! sijui ndio uchunguzi wenyewe?

Attention to detail, attention to detail.

Link imekupeleka kwenye a specific post ya Mtanzania anayetaka uchunguzi.

Kwa hiyo kama wewe na Watanzania wengine mna tatizo la kutotaka uchunguzi, kuna wengine tunataka uchunguzi na tushalisema hilo kabla ya post yako.

Kwa hiyo you better distinguish that not every Tanzanian is as challenged when it comes to verification as you make it out to be.

Bila uchunguzi wala namba.

Unakandya Watanzania kutopenda uchunguzi bila kufanya uchunguzi wala kuwa na a balancing anecdote, less a supporting statistic.

You are not living up to your own standard.

You need a dose of your own medicine.

Wengine hatuwezi kupinga moja kwa moja bila uchunguzi kwani tushamsoma Arthur C. Clarke kitambo na tukamuelewa aliposema "any sufficiently advanced technology is indistinguishable from magic".

Soma hapa

http://en.wikipedia.org/wiki/Clarke's_three_laws
 
Kama kweli wanaweza kusafiri kwa ungo wapewe nafasi kutuonesha.
Ni rahisi tu, Ili mradi ukubali kumtoa mtoto wako wa kwanza, mama yako mzazi, au mke wako wa kwanza. kubali tukuoneshe, utaweza tu
 

Jamani, kuna mengi sana dunia hii ambayo hatuyafahamu. Tusijikwamishe kwa kukataa moja kwa moja kwamba Hayapo ama Hayawezekani. Tuyape benefit of doubt na kuyafanyia utafiti wa kina ili tujiridhishe.
After all tunaambiwa kuwa binadamu anatumia asilimia ndogo sana ya uwezo wa ubongo wake.

Ni kweli mkuu mambo mengi hatuyafahamu lakini hata kama sijaona siwezi kukubali kwamba maji yanaweza kupanda mlima vile vile siwezi kukubali kwamba kuna chombo cha kawaida tu kwa kutumia mizizi kina-defy gravity..

Ndio maana nikafanya uchunguzi mdogo tu, nikaona kwamba sio Bongo tu, hata huko kwa hao wazungu kuna watu walisadikika kwamba wanapaa kwa kutumia mifagio au magic carpets (na kumbe wengi ya hawa wachawi walikuwa katika kutumia madawa yao kuna dawa mtu ukitumia una-hallucinate.., kwahio hawa jamaa wakadhani wanapaa kumbe wala..)

Kwenye issue ya alleviation aliyoitoa Pasco, nikacheki pia nikamuonyesha kwamba that is a known trick na ukigoogle online unaweza na wewe ukajifunza (its just magic tricks).., kuhusu kupinda vyuma na kina Uri Geller pia nikamuonyesha kwamba its just magic tricks..

Tutakuwa tumewakosea sasa wazazi na ndugu zetu waliotupeleka shule kama tutaamini mambo tu kwa majibu mepesi ya (black magic) bila kujiuliza hii kitu inafanywaje.., kwahio mkuu kama mtu anapaa na ungo basi huo sio ungo bali labda ni balloon lenye gas kama helium au hydrogen ambayo ni nyepesi kuliko oxygen..

Sio kwamba tunabisha bure bali tunakaa kukubali mambo ambayo ni impossible mpaka pale tutakapo-prove otherwise..

"When your remove all the impossibles, whatever remains however improbable its the answer.." kwahio ukimuona magician anafanya kitu ambacho hakiwezekani fahamu kwamba ni illusion
 
Ni rahisi tu, Ili mradi ukubali kumtoa mtoto wako wa kwanza, mama yako mzazi, au mke wako wa kwanza. kubali tukuoneshe, utaweza tu

Definition yako ya "rahisi" na yangu hazifanani naona.
 
haya mambo yanakuwaje mkuu maana nahisi ni kama hayawezekani!

hizi ni story tu, na hazipo Africa tu, hata ulaya zamani kutokana na hadithi kulikuwa na myth kwamba wanasafiri kwa kutumia ufagio, kama vile wasukuma na fisi na wakerewe na mamba..., its just a load of BS

mamba.jpg

Hiki kinachoonekana hapa sio fuvu la mamba kama unavyoliona, hili ni gari liendalo kasi kubwa. Kwa mujibu wa mtaalamu wa kutoa uchawi (Kazi ambayo Maji Marefu ndio alioanza nayo) alisema kwamba gari hili linaongezeka ukubwa kulingana na idadi ya watu. Mafuta yake ni damu za watu, Wamiliki wa gari hili wamekiri kwamba ni gari ambalo wanalitumia katika shughuli zao, na wamelinunua kwa gharama ya mamilioni ya shilingi kutoka kijiji cha Mkata huko Handeni Tanga. Gari hili lina uwezo wa kusafiri kutoka kijiji cha Kwakombo (Km kama 6 hivi kutoka Korogwe Mjini) kwenda Tanga Mjini (umbali wa km 92) kwa sekunde 6. Pia gari hili huweza kutoka Korogwe Tanga hadi Dar es Salaam kwa dk 25 tu. Mkuu wa Wilaya Korogwe alitafutwa siku ilipotolewa hii gari ili aonyeshwe demo ya namna gari inavyofanya kazi na yeye mwenyewe akiwa mmoja wa abiria lakini hakupatikana. . Hili ni tukio la kweli ambalo halina hata wiki mbili kuanzia leo 26/1 limetokea katika kijiji cha Kwakombo. Km 6 toka Korogwe mjini.
 
View attachment 81121

Hiki kinachoonekana hapa sio fuvu la mamba kama unavyoliona, hili ni gari liendalo kasi kubwa. Kwa mujibu wa mtaalamu wa kutoa uchawi (Kazi ambayo Maji Marefu ndio alioanza nayo) alisema kwamba gari hili linaongezeka ukubwa kulingana na idadi ya watu. Mafuta yake ni damu za watu, Wamiliki wa gari hili wamekiri kwamba ni gari ambalo wanalitumia katika shughuli zao, na wamelinunua kwa gharama ya mamilioni ya shilingi kutoka kijiji cha Mkata huko Handeni Tanga. Gari hili lina uwezo wa kusafiri kutoka kijiji cha Kwakombo (Km kama 6 hivi kutoka Korogwe Mjini) kwenda Tanga Mjini (umbali wa km 92) kwa sekunde 6. Pia gari hili huweza kutoka Korogwe Tanga hadi Dar es Salaam kwa dk 25 tu. Mkuu wa Wilaya Korogwe alitafutwa siku ilipotolewa hii gari ili aonyeshwe demo ya namna gari inavyofanya kazi na yeye mwenyewe akiwa mmoja wa abiria lakini hakupatikana. . Hili ni tukio la kweli ambalo halina hata wiki mbili kuanzia leo 26/1 limetokea katika kijiji cha Kwakombo. Km 6 toka Korogwe mjini.

wewe ulishapanda hili gari mkuu au ni kwa mujibu wa maji marefu ?

Pia tunajua mafuta kwenye gari yanachomwa na ile pressure inafanya mzunguko gari linakwenda, binadamu tunakula chakula ambacho kinayeyushwa kutoa nguvu, sasa unataka kusema huenda damu ina nguvu za nishati zaidi ? alafu hili gari linatumia chakula kingine kama mamba wengine au lenyewe ni damu tu,
 
haya mambo yanakuwaje mkuu maana nahisi ni kama hayawezekani!

wewe ulishapanda hili gari mkuu au ni kwa mujibu wa maji marefu ?

Pia tunajua mafuta kwenye gari yanachomwa na ile pressure inafanya mzunguko gari linakwenda, binadamu tunakula chakula ambacho kinayeyushwa kutoa nguvu, sasa unataka kusema huenda damu ina nguvu za nishati zaidi ? alafu hili gari linatumia chakula kingine kama mamba wengine au lenyewe ni damu tu,

Tunalo tatizo la watu kama wewe wanao kurupuka. Hii ni shida kwa Watanzania tulio wengi. Ni hivi:-

1. Sijakwambia popote kuwa Maji Marefu ameshiriki kwenye zoezi la kutoa hili gari.
2. Mimi nimefanikiwa kuwa shuhuda wa hili tukio, sijasema kuwa nimewahi kuanda hili gari,
3. Hizo habari za pressure na force sijui density na mass vyote huyo mganga hajaeleza, hii sio pure science ila ni
pseudo- sayansi.
 
Tunalo tatizo la watu kama wewe wanao kurupuka. Hii ni shida kwa Watanzania tulio wengi. Ni hivi:-

1. Sijakwambia popote kuwa Maji Marefu ameshiriki kwenye zoezi la kutoa hili gari.
2. Mimi nimefanikiwa kuwa shuhuda wa hili tukio, sijasema kuwa nimewahi kuanda hili gari,
3. Hizo habari za pressure na force sijui density na mass vyote huyo mganga hajaeleza, hii sio pure science ila ni
pseudo- sayansi.

Hivi hapo juu nimesema umeniambia au nimekuuliza ? wewe kama shuhuda una uwezekano mkubwa wa kupata majibu ambayo mimi niliyo mbali sikuyasikia. (wewe mwenyewe umemtaja Maji Marefu na mimi nikakuuliza kama umeshuhudia au umesikia toka kwa Maji Marefu)

Kujua kwamba kitu bila nishati hakiwezi kufanya kazi ni mpaka uwe mwanasayansi ?, mganga leo akikueleza kwamba binadamu anaweza kuishi bila kupumua kwa masaa 24, utasema ni sawa sababu hii ni pseudo - sayansi.
 
Hivi hapo juu nimesema umeniambia au nimekuuliza ? wewe kama shuhuda una uwezekano mkubwa wa kupata majibu ambayo mimi niliyo mbali sikuyasikia. (wewe mwenyewe umemtaja Maji Marefu na mimi nikakuuliza kama umeshuhudia au umesikia toka kwa Maji Marefu)

Kujua kwamba kitu bila nishati hakiwezi kufanya kazi ni mpaka uwe mwanasayansi ?, mganga leo akikueleza kwamba binadamu anaweza kuishi bila kupumua kwa masaa 24, utasema ni sawa sababu hii ni pseudo - sayansi.

Heri ya mwaka mpya
 
Kama kweli wanaweza kusafiri kwa ungo wapewe nafasi kutuonesha.
HIvi mimi naona vitu kama hivyo ni ushirikina maana in reality it cant be!halafu ukiangalia ni washikaji kabisa umri wao bado!na mjue kuna implication ya vitu kama hivyo ili ungo uende pengine wanahitaji kafara vitoto vichanga nk.
 
Mimi mwenyewe nilipata mashaka kama yako.
Hainiingii akilini hakuna kitu kama hiyo hao inapaswa polisi wafanye kazi yao vizuri bila kuongozwa wala kuhadaiwa na vyombo vya habari,kwani kwa kufanya hivyo watagundua jambo inaewezekana kabisa hawa jamaa ni majambazi ama wahalifu wa namna flani na walikuwa katika shughuli za kutekeleza uhalifu wao basi walipotokewa na polisi Saa nane usiku ndo wakawa na story ambayo ingeweza kuwahofisha polisi waliowakamata waache kuwafuatilia kwa undani na badala yake washughulike na mambo ya uchawi na kushangaa mtu kusafiri kwa ungo hapo inakuwa tayari wameshawatoa nje ya mada husika,ni sawa na kurusha jiwe kichakani mbwa anakimbilia jiwe wakati wewe unafanya mambo mengine tena si ajabu hata huko singida wanakodai wametoka ikifuatiliwa itagundulika hakuna anayewafahamu ktk eneo hilo na kama wanafahamika historia yao ya maisha inaweza kuwa tofauti na tunavyofikiri ama kuaminishwa na vyombo vya habari.naishauri ITV wafuatilie habari hii kwa kina isiishie hapo tena wafanye hivyo haraka ili kutuondolea mashaka sisi tunaopata mashaka juu ya jambo hili kwani sitegemei kama ulimwengu tunamoishi ni ulimwengu wa mambo hayo tena
 
Gari hili lina uwezo wa kusafiri kutoka kijiji cha Kwakombo (Km kama 6 hivi kutoka Korogwe Mjini) kwenda Tanga Mjini (umbali wa km 92) kwa sekunde 6. Pia gari hili huweza kutoka Korogwe Tanga hadi Dar es Salaam kwa dk 25 tu(km 272)

How possible is this?
 
Back
Top Bottom