Usafiri enzi zile Mwanza yetu

Usafiri enzi zile Mwanza yetu

jiwe la maji

JF-Expert Member
Joined
May 17, 2014
Posts
1,062
Reaction score
705
Wadau wa rock city enzi zile mnakumbuka Mwanza hapakuwa na usafiri wa vipanya kama leo. Vipanya vilikuwa Mabatini na Kirumba tu lakini Igombe kulikuwa na min bus zikiitwa Toto Tundu, Mayeji na Jalijalalam, Igoma kulikuwa na Last Boy na Mkuyuni air Jordan.
 
mwanza ya henzi hizo usafiri wa mjini tuliuita express sijui nani alituletea neno daladala magari hayakua mengi kama leo lakini kwa chai maharage tulitumia saa 1 kutoka miti mirefu mpaka igoma barabara ilikua vumbi kweli tumetoka mbali
 
halafu ikaja system hizo express za pasiansi ilikuwa mwenye gari lazima aweke video maana kama hamna video watu wanachungulia tu hawapandi,

Hahahahaha dah aisee kweli tumetoka mbali, saivi Pasiansi to Nyakato lami tu
 
Kumbe nyie wote mliotoa comment mpaka sasa hivi ni wa juzi tu. Miaka ile ilikuwa hakuna cha minibus wala nini. Tulikuwa tunapanda zile peugeot za kizamani mnarundikwa kama ndizi humu. Station wagon moja ilikuwa inaweza kubeba hadi abiria 8. Zilipotoka hizo ndio zikaja express. I love Mwanza mji niliokulia.

Tiba
 
wadau wa rock city enzi zile mnakumbu mwanza hapakua na usafiri wa vipanya kam leo vipanya vilikua mabatini na kirumba tu lakini igombe kulikua na min bus zikitwa toto tundu, mayeji na jalijalalam, igoma kulikuwa na last boy na mkuyuni air jordan

wapi Masubo.........mbona njia ya Nyakato-Mitimirefu vipanya vilikuwepo miaka ya tisisini ila vumbi lilikuwa hatari.
 
Kumbe nyie wote mliotoa comment mpaka sasa hivi ni wa juzi tu. Miaka ile ilikuwa hakuna cha minibus wala nini. Tulikuwa tunapanda zile peugeot za kizamani mnarundikwa kama ndizi humu. Station wagon moja ilikuwa inaweza kubeba hadi abiria 8. Zilipotoka hizo ndio zikaja express. I love Mwanza mji niliokulia.

Tiba

Kweli Tiba hao hawakuona yale maisuzu yakiitwa Santamaria
na baadae mtama kwa watoto enzi hizo njia ya pasiansi
 
Last edited by a moderator:
Mabasi km Amini Mungu safarini, Mwadeco, Trans Africa bus service etc ndo mabasi yetu enzi zile.
Pale kilipo kiwanda cha cocacola palikuwa na bwawa kubwa la kunyeshea ng'ombe huku tukicheza mpira wa madaso pale mnadani.
 
wadau wa rock city enzi zile mnakumbu mwanza hapakua na usafiri wa vipanya kam leo vipanya vilikua mabatini na kirumba tu lakini igombe kulikua na min bus zikitwa toto tundu, mayeji na jalijalalam, igoma kulikuwa na last boy na mkuyuni air jordan


Kwa hiyo Mkusanya Express unadhani ni gari inayokidhi haja kwenda huku?
 
Tatizo la kukaa kanyigo muda mrefu ndo hili!

Pasiansi lami imewekwa toka PAPA john Paul Hajaenda kuzimu!
Tena wakati ule alipokuja pale kilimalini ILEMELA! tayari brbr inaanza kuchongwa.

We mwanza ulifika wakati ule wa GEZA ULOLE! Na yale ma Leyland ya MWATEX!

Na wakati huo Sehemu ya starehe ni kwenye BAR ya Mzee KAFITI pale nyakato na Disco unachezea Pale Kilabuni Nyakato kwa mzee mwendesha mpika KIMPUMU!

Kukaa kijijini muda mrefu ni Hatari sana.

Teh teh teh teh!

Hahaha tatizo lako uko -ve skewed sana na comment zangu. Lami ya Pasiansi-Buzuruga kupitia nyasaka imewekwa 2011/2012 imefunguliwa nov 2012, sasa ivi kutakuwa na gari za ilemela buzuruga bile kupita mjini. Sasa we unasema lami gani? kahtaan bana duh
 
Last edited by a moderator:
Unaongelea Santamaria za KIRUMBA za JUZI Hapa!? Za wale Watoto wa Mzee AWADH?

Watu wamepanda GEZA ULOLE! Gia Tatu!
Breki TOFALI halafu dereva Mzee Joseph Yuko GONGO 24/7!

Na ukiikosa hio unadandia TRANS AFRICAN BUS ya kwenda MUSOMA ukifika nyakato au Igoma haisimami, unalegezewa tu na dereva UNAACHIA Body mwenyewe!

Unasema nini wewe!

Wacha bana.

Hahahaa aisee we kweli wa Mwanza, saivi hadi Kishiri ni mjini
 
Lake never dries= Mz town to pasiansi
Vitu laini ( Hongera bus) = Mz - Shy
Amini Mungu = Mza - Bunda
Mamba safari = Mza - Arusha
 
Za Mzee Kamese Town-Pasiansi,mwanae Ismail alikuwa schoolmate wangu na ali drive 1 wakati wa likizo mie nakuwa konda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom