Kuna kitu kinaitwa propaganda kina nguvu kubwa sana katika dunia ya leo
Nimeichukua hii habari kwa maksudi kutoka kwenye hiki ki media uchwara
Hiki ni ki media kinachomilikiwa na marafiki wa Vladimir putin hivyo media hii tangu asubuhi hadi jioni kazi ya hii media ni kuponda na kukosoa mambo yote yanayohusu West na vingi ni vya uongo au exaggerated the same time watasifu silaha za Russia 24/7
Ukiifuatilia hii media ya sputniknews.com baada ya mwezi tu unaweza kudhani marekani si chochote si lolote mbele ya Russia kwa jinsi utakavyo jazwa sumu na uongo
Mara leo watajifanya wanachambua ubovu wa ndege ya F-22 na jinsi inavyoachwa mbali na ndege za Russia, mara wataichambua Patriot missile system isivyokua chochote yaani ni full kuponda marekani
Na hii sputniknews.com ndio watu wengi hapa jukwaani hupenda kuja na habari zake
Mwisho wa siku unakua unajidanganya unajua vitu vingi kumbe ni sumu tupu
Chombo hiki huwa hakisemi mapungufu ya Russia na China kijeshi
Mfano vyombo vya habari vya magharibi naweza kusema vinafuata weledi hata kama serikali zao au majeshi ya marekani yamefanya kitu kibaya cnn ABc news zitaponda na kuisema vibaya serikali
Mapungufu ya silaha mbali mbali za america cnn watasema sana tu na mijadala mingi ya kitaalam lakini sio vyombo vya habari vya urusi
Aljazeera imejipambanua kama television huru pamoja na kumilikiwa na Qatar iliyo na ushirika na marekani lakini bado media hii ni huru
Serikali ya marekani imeilalamika media hii tangu kuanzishwa kwake wakati wa wikileaks Aljazeera haikuogopa kitu ilitoa siri zote kuhusu balozi za marekani zinavyoendesha upelelezi Duniani, ni Aljazeera pekee ndio iliyoaminiwa na Julian asange na kupewa zile leaks zote
Media hii ndio ambayo hadi sasa ndio imeripoti habari za Syria Bila upendeleo, Leo itasema mazuri ya Russia kesho itasema mabaya yake the next day itasema mabaya ya America and vice versa ndio maana hata Osama bin laden mikanda yake yote ya video aliwapa Aljazeera kwa siri aliiamini
Lakini cha kushangaza hapa jukwaani utasikia watu wa Russia wakidai Aljazeera imekua ya magharibi hivi kweli unaweza unakua kwenye TV yako kutazama sputniknews.com over Aljazeera? Ni wazi utakua umechanganyikiwa
Hii ndio nguvu ya propaganda, taarifa nyingi unazozisikia kuhusu Russia na hiyo s-400 ni exaggeration
System hiyo bado ina mapungufu mengi na maboresho yanaendelea
Imepelekwa Syria kama pambo tu lakini warusi wameshindwa kuiseti kuwa operational marekani na Israel zimekua kwa maksudi zikirusha ndege jirani kabisa na latakia kupima uwezo wa hiyo s_400 na kugundua kumbe hata imeshindwa kuwashwa kutokana na so many technical problems ndio maana Russia wakaiomba defense ministry iwaletee ndege ya su 35 ambayo ni mult role fighter jet ifanye kazi ya ku patrol mahala ambako ndege zao zinafanya mashambulizi kuzikinga na incidence kama ya uturuki zisishambuliwe na ndege zingine kazi ambayo originally ilipangwa kufanywa na s-400 ambayo hata kuwaka tu imeshindikana
Je media za Russia zimeyataja haya?
Silaha kubwa ya authoritarian regimes ni propaganda be warned
Kila MTU ana hitikadi na uwelekeo anaouamini na kwa uchambuzi wako ni dhahiri wewe ni mfuasi wa propaganda za kimagharibi, na si shangai ukikitusi chombo cha habari cha Sputniks pia unaweza kuvikataa vyombo vingine visivyo na mrengo wa kimagharibi kama RIA Novosk, RT, CCTV, idhaa ya kichina, KNCA News etc. kwakuwa umekuwa ukilishwa propaganda za kimagharibi kupitia CNN, BBC news, France 24, DW,VOA, Aljazeera, Fox news, ABC, Reuters, AP etc.....
Kwa hitikadi yako huwezi kukosoa habari yoyote inayotangazwa na vyombo vya kimangaribi. Tambua kuwa kila nchi inatumia media kutangaza mazuri yake na uwezo wake na kukosoa ama kudhihaki taifa lingine lisilounga mkono falsafa na hitikadi yake (taifa ambayo limekataa kuwa kibaraka wake). Kwahiyo kila media za mataifa makubwa inatangaza propaganda.
Huwezi ingia kwenye media za kimagharibi ukaona zinakosoa mataifa ya kimagharibi, we utasikia wakosoa afrika au maifa yenye msimano tofauti na wao (china,Urusi,Korea kaskazini, Venezuela, Bolivia, Iran, etc...)
Pia uwezi ingia kwenye media za wapinzani wa mfumo wa kimagharibi ukakuta wanasifia mataifa ya magharibi.
kwa propaganda tulizolishwa na mataifa ya kimagharibi kupitia media zao maana siku hizi wanakuja juu kila nchi ya kimagharibi imepenya afrika tena kwa lugha za kiafrika. Huku hawa wa mrengo wa kushoto warusi, wachina, wairani etc wao wawepenyeza kidogo kuleta propaganda zao. Sisi Afrika tumebaki na kuchanganywa na propaganda zao, huku wengine wakiona mrengo wa kulia (magharibi) ni sahihi na wengine wakiona mrengo wa kushoto ni sahihi, ndio maana kila siku Afrika ni mizozo, migogoro na vita.