US Election Coverage 2008


Sasa wewe ndio una-spin...Hillary kila siku anatamkwa kama Hillary Rodham Clinton...we mwenzetu kiziwi nini?

Julius Kambarage Nyerere, Benjamin William Mkapa, Jakaya Mrisho Kikwete, Franklin Delano Roosevelt, George W. Bush, John Fitzgerald Kennedy, Barack Hussein Obama....what's wrong with that?

Obama asitake kulikana jina lake la Hussein...kwanza kuwa Muislamu na kuitwa Hussein kuna ubaya gani?
 

Yaani wewe kazi ya ukada wa CCM inakufaa haswa! Una ushahidi wowote kuwa picha ile imetoka kwa Mama au unaamini chochote kile kinachotoka na kutamkwa na Drudge?

You are the one that's not getting it....sasa mmeanza nit-picking...sasa mnadai kuna picha inayomuonyesha Obama akiwa mweusi zaidi...hivi kuwa mweusi kuna ubaya gani? Na unajua aliyei-doctor hiyo picha? Mimi mwenyewe kuna baadhi ya picha huwa naonekana lighter na baadhi naonekana darker....na mtu kama wewe unaweza kabisa kusambaza kitu kama hicho ili kumpaka matope Mama....sasa una uhakika gani hiyo picha haijatoka kwa Obama kwa lengo la kumharibia Mama...
 
Sasa wewe ndio una-spin...Hillary kila siku anatamkwa kama Hillary Rodham Clinton...we mwenzetu kiziwi nini?

Obama asitake kulikana jina lake la Hussein...kwanza kuwa Muislamu na kuitwa Hussein kuna ubaya gani?

Weee! Nyani! Hillary hatajwi kila siku as HIllary Rodham Clinton - it is VERY rare. Ni Hilary Clinton most of the time.
Pili hajasema kuna ubaya kuitwa Hussein ame protest email iliyodai kwamba kutokana na kuwa jina lake ni Hussein he is therefore a Muslim and he is keeping it a secret in order to take over the world etc. It was a nasty email, I think hata wewe utakuwa umeipata. Kama uliangalia 60 minutes on CBS one day before the primary, kuna voter moja aliyesema wazi hatampigia kura Obama kwa sababu ni mwislam who wants to destroy America, alipoulizwa alisema alipata email yeye na marafiki zake.
So do not pretend that you do not know the background and the insinuation.
Atakapoapishwa hilo jina atalitaja tu! Na hajawahi kusema anaionea aibu or anything, he was talking about the context. Au unataka nikuweke tena quote ya Rush Limbaugh alivyofurahi Hillary kufanya kazio ya GOP maana hata Rove amesema wasimwite Obama Hussein.
 
..another myth AKA cry baby ya ku play victim wa media na nyie mnaamini tuu,Obama run good & clean campaign ndio maana anashinda ila sasa mama kaanza uchafu ambao ndio utammaliza mwenyewe kama sio Democratic party.

Koba,

Like I said that's just my thinking, well largely shaped by what the media's been pumping out really, and Gupta-esque like stories even though not negatively implicating her directly, don't do her any favors either. I would, however, hasten to agree with you on the way Obama has run his campaign, he's run a clean one so far, but unfortunately the same cannot be said of Clinton.

I remember watching Clinton make a mockery of Obama and it was a major put off really; she did a poor job at belittling Obama and a good one at embarassing herself, you could see some faces in the audience cringe, I tell you. "The sky will open, a light will shine down, all problems will go away..."

Obama isn't doing himself any favors by steadfastly rehearsing his "change we can believe in" monologue day in day out and it seems to be wearing out with time, at least that's what I think. I mean he needs to put to rest the experience issue that Clinton has been touting around, he doesn't need to run a smear campaign and he shouldn't, but just point the people in the right direction, as it were.
 

Kwani Obama kila siku anaitwa Barack Hussein Obama?
Akiitwa mara moja tu mnakuja juu...nyinyi ndio manona hilo jina kuwa ni tatizo....

Ooh by the way bado nakusubiri uje na mabaya ya GOP uliyoniahidi....ulidhan nimesahahu eehhh?
 

I agree with you Mwakilishi, except for the change we can beleive in part. I think that consistency is important because somehow he has set the tone for the campaign with the change theme and McCain and HIllary are stealing his lines and slogans. But I do agree that he does need to change the course of the conversation and ensure that he projects the image of who he really is. Lakini naona hataonekana mpaka kesho, nadhani yuko busy wanajipanga upya. 7 weeks ni mbali sana. Let's wait mpaka tutakapowaona Hillary and Barack publicly stumping.
 
Kwani Obama kila siku anaitwa Barack Hussein Obama?
Akiitwa mara moja tu mnakuja juu...nyinyi ndio manona hilo jina kuwa ni tatizo....

Ooh by the way bado nakusubiri uje na mabaya ya GOP uliyoniahidi....ulidhan nimesahahu eehhh?

Ala! Nilijua umesharudi kambini kwa mama na umeabandon idea ya kujoin GOP, ndo maana niliacha kupanga points zangu. Nitaiandika lakini sasa niko busy na issue ya Democrats ndo maana sikukamilisha arguments zangu. Let's save it for a rainy day! Kuna slow days hapa zitakuja tutaendelea na hiyo debate, au unasemaje, mkuu?
 
Nikijaribu kuangalia kotekote bila ushabiki naona yafuatayo:

Kuhusu majina hiyo ni kweli kwani si hata hiyo Obama walishajidai wamekosea eti ni Osama, ndiyo itakuwa hiyo Hussein, halafu Americans nao bwana kule wapi SC nadhani watu walihojiwa before zile primaries kuna waliosema jina lake linafafana na Osama kwa hiyo wana wasiwasi naye...go figure!

Kuhusu Hillary, her full name ambayo sijaona akiitwa wala kutajwa hivyo ni: Hillary Diane Rodham Clinton. Rodham ni jina la ukoo wake kabla ya kuolewa na Clinton so technically it's not her second name!

Anyway pamoja na yote hayo majina yasiwe issue wala yasifanywe issue, katika hili anaonewa Obama ambaye majina yake sio ya kizungu wala kimagharibi, I have a feeling nani anaitumia fursa hii kwa manufaa yake na huyo mtu wala siyo Obama!
 

Bado sijahamisha kambi. Ushindi mkubwa wa Mama juzi umenipa matumaini....kuhama kambi bado ni plan B
 

Hakuna mtu anayefanya jina la Barack Hussein Obama kuwa issue zaidi ya mashabiki wake ambao hawapendi aitwe hivyo ingawa wazazi wake wenyewe walimwita hivyo...
 
Jamani naomba mi niendelee na shughuli zangu lakini kabla ya hapo nina hii zawadi nzuuuuriiii kwa Nyani, game Theory na wenzangu tunaoendelea na mjadala humu ndani:

Picha ya Hillary, Bill and.... REZKO! 😀
[media]http://s147.photobucket.com/albums/r285/scjr63/?action=view&current=ClintonRezko.jpg[/media]

GT nisaidie kupost ili wengine waione kweny ethread hapahapa!
Story yenyewe nilishaimention lakini kwa faida ya wengine go to this link:
[media]http://www.margieburns.com/blog/_archives/2008/2/2/3501879.html[/media]
Hii trial ya Rezko akina Clinton watatamani iishe mapema.
 
...nimeanza kupata bad feelings na inaonekana mama will hand Obama/Democratic party a total destruction kama wengi walivyotabiri na nimeanza kuamini,Obama sasa its time to fight fire with fire...wake up!
 
Mimi huyu Michelle alishanichosha tangu aseme hajawahi kujivunia kuwa mmarekani hadi mume wake alipogombea urais, na hii kitu imechangia kumnyima kura mume wake huko Texas na itaendelea kuwa-cost na itawa-cost November kama watapata nomination. Wakati mwingine bora Cindy ambaye habwatuki ovyoovyo. Huyu dada kila akinyanyua mdomo ni problem, sasa sijui Obama kwa nini hamwambii yeye awe anapunga mkono na kutabasamu tu basi!

BTW kampeni maneja wa Obama hapa JF ndugu Yourname amepotelea wapi baada ya super tuesday II?
 

...hapa tunakubaliana,ni kweli huyu naye kila akifungua mdomo ni poison tuu inatoka,inabidi wamfiche kwanza maana anapunguza kura tuu
 

Ebwana Cindy McCain unamuonaje? Mi naona katulia kwelikweli....
 
Ebwana Cindy McCain unamuonaje? Mi naona katulia kwelikweli....

Nyani unanikwaza ndugu yangu nirudi kujibu maoni yako:
Cindy Mccain belongs to the wax museum! She's an addict na full of botox!
Mrs Obama, mtamsema weee but it's not true that she cost votes for Obama, in fact amemsadia sana kupata black women votes. Lakini hata hivyo hayuko visible sana at least not more than Bill. Which brings me to a light touch moment: hasira za Bill ukiweka na hasira za Michelle, hebu imagine wakifanya debate na wote wanavyojua kuchonga.... sipati picha!
 
Hakuna mtu anayefanya jina la Barack Hussein Obama kuwa issue zaidi ya mashabiki wake ambao hawapendi aitwe hivyo ingawa wazazi wake wenyewe walimwita hivyo...

Nyani Ngabu ee wewe Wamarekani si unawajua bwana?! Jina tu inaweza kuwa issue kubwa, mimi nimeona wanasema kabisa hilo jina Obama limekaa kama Osama, na hiyo Hussein inawakumbushia Saddam, yaani utadhani duniani hakuna watu wengine wenye majina hayo isipokuwa wale "maadui" wawili wa Marekani.

My take:

Kumwita kwa majina yake yote siyo hoja, si majina ni ya kwake tatizo liko wapi? Tatizo ni pale unapoyataja kana kwamba unawasisitizia watu "pamoja na mazuri anayosema kumbukeni huyu ni Hussein hana tofauti na yule mbaya wetu mkimchagua shauri yenu". Nadhani ndicho kambi ya Barack Hussein Obama inachokiona hapa, inawezekana they are justified la sivyo wanajiharibia wenyewe!
 

Aaah ndugu yangu wewe Susu....Bill na Michelle wa-debate..? Mbona bonge la mismatch hilo...

Cindy McCain katulia bana....
Tukianza kuzungumzia madawa nani atabaki? Obama mwenyewe alishakiri kutumia (hadi kuuza) madawa....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…