Urusi yatwaa urais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa licha ya hasira ya Ukraine

HERY HERNHO

Member
Mar 4, 2022
70
313
Urusi imechukua kiti cha urais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa licha ya Ukraine kuwataka wanachama kuzuia hatua hiyo.

Kila baraza la wajumbe 15 huchukua nafasi ya urais kwa mwezi mmoja, kwa utaratibu wa kupokezana.

Mara ya mwisho Urusi ilikuwa na nafasi ya urais ilikuwa Februari 2022, na ndio ilianzisha uvamizi kamili wa Ukraine.

Ina maana kuwa Baraza la Usalama linaongozwa na nchi ambayo rais wake yuko chini ya hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa madai ya uhalifu wa kivita.

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu - ambayo si taasisi ya Umoja wa Mataifa - ilitoa hati ya Vladimir Putin mwezi uliopita.

Licha ya malalamiko ya Ukraine, Marekani ilisema haiwezi kuizuia Urusi kuwa mwanachama wa kudumu wa baraza kutwaa kiti cha urais.

Wajumbe wengine wa kudumu wa baraza hilo ni Uingereza, Marekani, Ufaransa na China.

Jukumu hilo mara nyingi ni la kiutaratibu, lakini balozi wa Urusi katika Umoja wa Mataifa, Vasily Nebenzia, aliliambia shirika la habari la Urusi Tass kwamba alipanga kusimamia mijadala kadhaa, ukiwemo wa udhibiti wa silaha.

Alisema atajadili "utaratibu mpya wa ulimwengu" ambao, alisema, unakuja.chanzo bbc swahili
 
NATO wanaumia balaaa !! Walikua wanataka Mrusi asipewe, Jamaa wakadinda, haunipi Urais, ni sawa na kunitoa Baraza la Usalamaz ni sawa na kunitoa Umoja wa Mataifa ambayo ni sawa na Anguko la Uhusiani wa Kimataifa Kwa Nchi zote Duniani.


NATO wameufyataa
 
Urusi imechukua kiti cha urais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa licha ya Ukraine kuwataka wanachama kuzuia hatua hiyo.

Kila baraza la wajumbe 15 huchukua nafasi ya urais kwa mwezi mmoja, kwa utaratibu wa kupokezana.

Mara ya mwisho Urusi ilikuwa na nafasi ya urais ilikuwa Februari 2022, na ndio ilianzisha uvamizi kamili wa Ukraine.

Ina maana kuwa Baraza la Usalama linaongozwa na nchi ambayo rais wake yuko chini ya hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa madai ya uhalifu wa kivita.

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu - ambayo si taasisi ya Umoja wa Mataifa - ilitoa hati ya Vladimir Putin mwezi uliopita.

Licha ya malalamiko ya Ukraine, Marekani ilisema haiwezi kuizuia Urusi kuwa mwanachama wa kudumu wa baraza kutwaa kiti cha urais.

Wajumbe wengine wa kudumu wa baraza hilo ni Uingereza, Marekani, Ufaransa na China.

Jukumu hilo mara nyingi ni la kiutaratibu, lakini balozi wa Urusi katika Umoja wa Mataifa, Vasily Nebenzia, aliliambia shirika la habari la Urusi Tass kwamba alipanga kusimamia mijadala kadhaa, ukiwemo wa udhibiti wa silaha.

Alisema atajadili "utaratibu mpya wa ulimwengu" ambao, alisema, unakuja.chanzo bbc swahili
Mi naona kama wamejipendekeza kwa Urusi ili asiwashughulikie
 
Wasingeweza kumuondoa Urusi hata iweje

Hizi nchi 5 China, Marekani, Uingereza, Ufaransa na Urusi ni wanachama wa kudumu wa Baraza la Amani la Umoja wa Mataifa (UN Security Council Membership)

Walipata hivyo viti kwa kupigiwa kura na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, kwa hiyo hakuna mwenye haki ya kumtoa uanachama mwenzake hapo. Lazima taratibu walizojiwekea zifuatwe watake wasitake

Marekani na washirika wake waliweza kumtoa Urusi kwenye ile G8 (kundi la nchi tajiri duniani) tu basi mwaka 2014 alipoivamia Crimea ikabaki G7 lakini hapo hawana ubavu huo

Na ndio mataifa pekee duniani yanaruhusiwa kumiliki silaha za nyuklia. Nchi zingine zinaruhusiwa kuwa na nyuklia kwa matumizi ya amani tu kuzalisha nishati ya umeme

Hao ni wababe wa dunia
 
Linavyo tangazwa utafikiri ni jambo kubwaaaaa. Kumbe ni utaratibu wa KUPOKEZANA KWA MWEZI MMOJA MMOJA (kama ulivyosema).
 
Linavyo tangazwa utafikiri ni jambo kubwaaaaa. Kumbe ni utaratibu wa KUPOKEZANA KWA MWEZI MMOJA MMOJA (kama ulivyosema).
Kwanini wale walinuna na kuvimba jamaa wasipewe......... Waache u lgbt kununa kwa mambo madogo tu
 
Back
Top Bottom