Urais, Halima, Nassari na Kigoma

Status
Not open for further replies.
Nilikuwepo uwanjani pale lake Tanganyika Kigoma, kilichoandikwa ndicho nilichosikia pia. Videos zitawekwa hapa na zitathibitisha.
Siwezi kuwaandikia mwananchi kwani mimi silalamiki kuhusu habari hiyo. Wenye kuilalamikia habari wameandika.

Mimi ninaamini gazeti la Mwananchi ndio gazeti pekee huru la kiswahili hapa nchini. Ndio gazeti pekee ambalo umiliki wake hauna maslahi na waandishi na wahariri wake ni mahiri, hawana njaa na hawapindishwi. Ndio maana huandika ukweli muda wote na wanapokosea hawasiti kurekebisha. Ndio maana ni gazeti linasomwa kwa wingi kuliko magazeti yote nchini. Hakuna gazeti linalofikia hata nusu ya mwananchi kwa kusomwa. Hivyo Mwananchi linaaminika na umma.
Najua kuna watu wana chuki binafsi na mwananchi kama gazeti na wahariri wa mwananchi kama binaadamu. Hayo wayamalize wenyewe huko walikochukiana.

Subirini video ndio tutajua habari ile imepikwa au ni ya kweli. Kwa tuliokuwepo uwanjani tunajua nani alisema nini.

Mkuu kwa heshima zote, si uiweke hiyo video ili kuondoa utata.

Halafu mkuu, umesema hujamualika mwandishi yeyote wa habari katika tamasha lile. Nani basi kafanya hiyo recording, ni wewe mwenyewe? Kama si wewe utaipataje? Umejuaje nani karekodi matukio ya tamasha?

Kisha umesema tamasha halijaandaliwa na wewe, sasa uliwezaje kuwaalika waheshimiwa wabunge wenzako katika tamasha ambalo hukuliandaa wewe?

Naomba pia ufafanuzi, umejuaje kwamba waandishi wa gazeti la Mwananchi hawana njaa na hawapindishwi!!??
 
Anayosema Muke ya Muzungu ni kweli, je mko tayari tuwaletee audio ya mambo ya kinafiki ya zitto kama akiendelea kubisha?
 
Suala la Urais lisitupotezee muda kwani kuna mambo mengi sana ya kujadili kuhusu nchi yetu. Taharuki ambazo watu wanazipata masuala ya urais yanapotajwa zinashangaza sana.

Chama changu bado hakijatangaza rasmi mchakato wa kupata mgombea Urais. Hivi sasa chama hakina mgombea Urais mpaka hapo mchakato utakapotangazwa ambapo wanachama wataruhusiwa kuomba kupeperusha bendera ya chama. Mwanachama wa chama chetu atakaye kubalika na jamii na wajumbe wa mkutano wa uteuzi ndiye atakuwa mgombea wetu. Kwa sasa hayupo na hivyo tusipoteze muda kujadili jambo hili.

Mzee Thabiti Kombo alituachia usia tunapokuwa tunazungumza. Alisema 'weka akiba' sio akiba ya fedha, bali ya akiba ya maneno. Tuweke akiba ya maneno. Tusimalize yote.

Zitto

Sound great Zitto. Magazeti yamezzoea kutudanganya wananchi.

Kaza buti kijana, usiangalie nyuma.
 
Safi kwa kujitokeza naibu katibu wangu wa chama Zitto, leo kuna thread nimesoma humu imenishitua sana, kuna baadhi ya member wanakushutumu wewe ktk uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ulimnadi mgombea wa ccm JK badala ya Dr.Slaa, ni kweli kamanda?

sasa mkuu mbona hili jambo hata mtoto wa 4M1 atakuelezea kwani nini hujui? na unataka zitto aseme nini na wakati ni ukweli mtupu.
 
Last edited by a moderator:
Kwa maelezo haya, hatuna sababu ya kuwa na mashaka tena. Zito kujiandikia habari, kisha kuwalazimisha wanahabari kuiweka habari yake ukurusa wa mbele kwa kuwalipa fedha nyingi waandishi wa magazeti, HIYO NI HONGO. KWA HIYO ZITTO NI MTOA RUSHWA KWA MASLAHI YA KISIASA. NA SIKU ZOTE MTOA RUSHWA AKIPATA NAFASI ANAKUWA MPOKEA RUSHWA. KWA UCHAFU HUU UNAOFANYWA NA ZITO, kama baada ya uchaguzi tutaendelea kumwona Zito kwenye nafasi za juu za uongozi wa CHADEMA, sitakuwa na imani na CHADEMA tena, aheri nijue tu kuwa hatuna wa kututoa mahali tulipo. Maana uchafu huo anaoufanya Zitto ni dhahiri CHADEMA watakuwa wanaujua, na je wamechukua hatua gani?


Sasa Zitto ndugu yangu hata video bado si ungesubiri iwe tayari utuletee mazima yujue mbivu na mbichi mana tumechoka porojo??????????!!!!!!!!!!!!!!!
 
mwananchi wanasema lao
halima mdee anasema lake
joshua nassari anasema lake na
zitto nae anasema lake. Sasa tumwamini nani kati yenu?
wote wanaleta porojo tu, huyu zitto mwenyewe amekurupuka nini kuandika kabla hajaambatanisha na hiyo video ili kukata fitina? Matokeo yake anatupa ahadi kama zile za dhaifu!! Nita..nita...tumeshachoka, tupia video tumalize fitina!!!
 
Zitto anafanya sasa plan B kama alivyokuwa akitarajia kupanua mtafaruku kati ya wabunge wenziwe ,chama na wananchi

Mara zote Zitto kwa malezi yake ya uzandiki aliyokulia huwa anapenda kutumia wenziwe kuwachafua ili aweze kujinufaisha au kufifisha nyota zao Nkosamali na Machali hili wanalifahamu sana alivyotaka kuwatanguliza wavuruge NCCR walimkatalia
Wabunge wa Chadema walioalikwa na Zitto kwenda kigoma nao wakakubali wangejiuliza kwa nini wabunge wa CCM walikuwa wengi kuliko wao alikuwa anaweka picha gani

Zitto anaingiza swala la uraisi sasa hivi kubadilisha agenda ya nchi na mijadala ya kitaifa tumemzowea huyo ni kiwavi wa kisiasa tuache kuongelea muuaji na mtesaji feki wa kova,Kikwete kuhongwa na Europian union dola millioni 126 mbadala wa trillion cubic meters za gas ,Kikwete kufirisi mifuko ya jamii na kuwanyima wastaafu na wanaostahili mafao yao kulipwa

Hali mbaya ya maisha na umaskini uliozidi

Ridhiwani /Miraji kununua mtambo wa kuingilia mawasiliano ya wabunge wa CDM

Kwa sababu anajulikana inda yake ningekuwa mimi wabunge Nassari na Halima ningeishia hapa mwisho kwenye mjadala kumwacha abwabwaje tu tunamfahamu sana ni mvurugaji
 
Mimi binafsi kati ya vitu vinavyonipa shida sana kufahamu ni msimamo wa Zitto Kabwe kuhusu mwelekeo wa nchi yetu hasa kuhusiana na jinsi anavyokinzana na mambo mengi sana ndani ya chama chake.

Zitto wewe ni economist, hivyo unapaswa kukaa chini na kuanalyse mwenendo wako na misimamo yako na kufanya maamuzi. Mimi nashawishika kuamini kwamba wewe uko sehemu siyo stahili yako kulingana na tabia ambayo umekuwa nayo siku zote. Zitto nashawishika kuamini kwamba CHADEMA siyo mahali panapokufaa, kwasababu unatofautiana nao kwa mambo mengi sana. Hivyo mimi nakushauri fanya maamuzi na ujiunge CCM labda huko utatimiza ndoto zako. Nasema hivyo kwasababu naamini hata Viongozi wenzako ndani ya CDM huna imani nao, ndiyo maana historia yako imejaa mambo mengi sana kinyume na mwelekeo wa chama chenu.

Zitto, kati ya vitu ambavyo siamini kama hata wewe unaamini ni wewe kuwa na uwezo wa kuongoza nchi kama TZ kwasasa na changamoto nyingi tulizonazo. Kwa nafasi yako na uwezo wako, bado huna uwezo wa kuwa Amiri Jeshi Mkuu mwaka 2015 lkn unaweza kuwa sehemu ya timu itakayowaletea watanzania mabadiliko ya kiuchumi na kijamii kutokana na uwezo wako. Lkn ukishakuwa ndani ya timu ya utendaji, hapo 2020 na kuendelea sasa unaweza ukawa na akili na uwezo wa kutimiza ndoto yako.

Zitto, tanzania ya sasa ilipofikia inahitaji mtu mwenye msimamo na asiyeyumbayumba kama ulivyo na rangi nyingi katika utendaji (rejea yanayoendea PPF na wewe kama mwenyekiti wa kamati husika lkn umewekwa mfukoni na Urio kwasababu tu anakupa support ya pesa wkt pale kuna uozo mkubwa sana).

Zitto, kuna watu wanakupoteza na kukudanganya kwa mwamvuli wa UDINI, UKANDA NA UKABILA na wewe unaykumbatia. Hii siyo ajabu kwani propaganda ya CCM siku zote ndiyo hizo lkn wewe pia nikichunguza kwa makini nagundua kwamba unakubaliana na hizi hoja hafifu hata kama kuna kitu kikitokea, basi watu wasiseme kisa UDINI na wewe huyu mdudu mbaya wa UDINI haujawahi kuukemea kabisa kwa kuwafafanunulia watu. Na kwa mantiki hiyo tunashawishika kuamini kwamba wewe unatumia hii dhana ya udini kama mtaji kwako kwa mambo ya kipuuzi ili upate sympathy ya wale wasiotaka kushugulisha akili zao.
Pole sana kwa kutotaka kutoka ndani ya Box bila kujua gharama ya kuwa na rangi nyingi katika dunia ya leo.
TELO.
 
Nilikuwepo uwanjani pale lake Tanganyika Kigoma, kilichoandikwa ndicho nilichosikia pia. Videos zitawekwa hapa na zitathibitisha.
Siwezi kuwaandikia mwananchi kwani mimi silalamiki kuhusu habari hiyo. Wenye kuilalamikia habari wameandika.

Mimi ninaamini gazeti la Mwananchi ndio gazeti pekee huru la kiswahili hapa nchini. Ndio gazeti pekee ambalo umiliki wake hauna maslahi na waandishi na wahariri wake ni mahiri, hawana njaa na hawapindishwi. Ndio maana huandika ukweli muda wote na wanapokosea hawasiti kurekebisha. Ndio maana ni gazeti linasomwa kwa wingi kuliko magazeti yote nchini. Hakuna gazeti linalofikia hata nusu ya mwananchi kwa kusomwa. Hivyo Mwananchi linaaminika na umma.
Najua kuna watu wana chuki binafsi na mwananchi kama gazeti na wahariri wa mwananchi kama binaadamu. Hayo wayamalize wenyewe huko walikochukiana.

Subirini video ndio tutajua habari ile imepikwa au ni ya kweli. Kwa tuliokuwepo uwanjani tunajua nani alisema nini.

Basi hapo umeshamaliza kaka, tunasubiri video, na kama ni kweli halima mdee na yule dogo nasari walitamka hayo ambayo wameyakanusha basi itabidi watuombe msamaha watanzania kwa kutudanganya, maana kama wanaweza kutudanganya kitu kidogo kama hicho cha kutoa speech je mambo makubwa ya jamii yetu tutaweza kuwaamini kweli? Halima na Nasari kuweni jasiri mnaogopa nini hata kama hamkusema hayo mambo kwani kusema kua zitto anafaa kua rais kuna kosa gani, kwani mmevunja sheria? mbona yule wa ccm ambae nae kaandikwa kwenye gazeti hajakanusha? yule najua ni kisiki kwa sababu hajali aseme asiseme hakuna mtu anayeweza kumlazimisha kukanusha hiyo kauli, cha ajabu yule wa ccm amekaa kimya hajakanusha na nyie wa chadema mmekanusha yaani mmemtosa mwanachadema wenu hivi hivi...kweli wanaosema vijana wa cdm bado hawajakomaa kisiasa sasa nakubaliana nao
 
Ingependeza iwapo hiyo Full video iwekwe kabla ya editing. Hatujui nani anasema ukweli au uongo katika hilo. Vilevile, kwenye kitu kama matamasha sina hakika kama waandishi wa habari wanahitaji mialiko rasmi, unless kama kwenye hilo tamasha kulikuwa na kiingilio. Na bado mwandishi wa habari ana uwezo wa kutoa kiingilio ili kuweza kupata habari na kuhabarisha jamii nyingine ambayo haikupata nafasi ya kuhudhuria.

Ni hatua gani mtachukuwa kwa gazeti kuwachonganisha na chama pamoja na wanachama? Nilisoma barua ya Nassari kuhusu hilo gazeti akiomba apology, lakini hakueleza benchmarks, atachukuwa hatua gani iwapo gazeti litashindwa kuomba apology. Kwa wengine tukiona ujumbe kama ule wa Nassari bila ya meno tunapata wasiwasi.
Kuweni macho na kauli zenu jamani.
 
Katika gazeti la Mwananchi la tarehe 23 Julai 2012, kulikuwa na habari yenye kusomeka 'Wabunge wamsafishia Zitto njia ya Urais 2015'. Habari hii imeleta mjadala mara baada ya kutoka na kusomwa. Mjadala umekuzwa zaidi baada ya Wabunge ndugu Halima Mdee na ndugu Joshua Nassari kukanusha maneno waliyonukuliwa kusema. Napenda kusema masuala yafuatayo...


Zitto

Kwa kutunga nyimbo zisizo na melody umefanikiwa sana unajifanya eti hukushiriki kwenye maandalizi ya tamasha kwa akili ya kawaida mtu atajua unaficha ukweli ili ujitetee

Wana JF wengi wameshiriki katika kuandaa events unaweza uwaalike wewe kwa maana ya barua na simu lakini unaweza kutoa wewe lists ya wageni wa kualikwa. Kila mtu anajua unaposikiliza lazima ukubaliane na msemaji kama kweli aliyasema hayo wewe unathibitisha kwamba uliyasikia maneno waliyokusifu kuwa unapaswa kuwa raisi wahusika wanasema wewe hufai kuwa raisi na hawakukutabilia hivyo.

Unasema hukuhusika kualika waandishi wa habari lakini mfululuzi wa miaka mitano Ramadhani Semtawa anaandika habari ambazo zimeleta mtafaruku kwenye chama chako hii inaonyesha wewe huwa upo kati ya maandishi ama kuaandaa ama kuhakiki.

Unaposema wajibu wenyewe walichokisema wakati wao wamekataa hawakusema unafanya makusudi kuingiza vita ya maneno na hicho ndio kipaji chako wengi wanaokufahamu wanasema ukiona jina lako halitajwi tajwi na vyombo vya habari huwa unajitengenezea stori kwa gharama zozote zile. Huo ni udhaifu manake umeshiwa hoja za kisiasa unatumia migongo ya watu kubaki kileleni kama ulivyomponza kafulila kaanguka mweleka wa ajabu kwa sababu ya wewe kumchonganisha na chama chake, kiujumla wanao shirikiana na wewe kama hawakujui kuwa wewe ni pandikizi lilo kubuhu basi wamejipalia makaa.
 
Wengine wapo kama tomaso, hawaamini mpaka waone na kusikia bana!
 
Zitto wengine hizo facebook sio wenyeji tunaomba uiweke hiyo video humu humu! Mbivu mbichi kujulikana maana ni zama za sayansi na teknolojia. Wasiwasi wangu ni tabia ya chama chenu kukanusha hadi vitu vya kiteknolojia kama ilivyotokea kwenye suala la sms.
 
Basi hapo umeshamaliza kaka, tunasubiri video, na kama ni kweli halima mdee na yule dogo nasari walitamka hayo ambayo wameyakanusha basi itabidi watuombe msamaha watanzania kwa kutudanganya, maana kama wanaweza kutudanganya kitu kidogo kama hicho cha kutoa speech je mambo makubwa ya jamii yetu tutaweza kuwaamini kweli? Halima na Nasari kuweni jasiri mnaogopa nini hata kama hamkusema hayo mambo kwani kusema kua zitto anafaa kua rais kuna kosa gani, kwani mmevunja sheria? mbona yule wa ccm ambae nae kaandikwa kwenye gazeti hajakanusha? yule najua ni kisiki kwa sababu hajali aseme asiseme hakuna mtu anayeweza kumlazimisha kukanusha hiyo kauli, cha ajabu yule wa ccm amekaa kimya hajakanusha na nyie wa chadema mmekanusha yaani mmemtosa mwanachadema wenu hivi hivi...kweli wanaosema vijana wa cdm bado hawajakomaa kisiasa sasa nakubaliana nao
Wa CCM akanushe nini sana sana atakuja na kusema na yeye aliwasikia walisema hivyo ambaye hajakomaa kisiasa pamoja na nafasi kubwa alizo nazo kitaifa na kichama na Zitto anafanya siasa za kipoland nyakati hizo za propaganda anataka jina lake liwe juu
 
Ninachokiona hapa Zitto anawajibia Mwananchi.Ukisoma taarifa yote ya Nassari na Mdee hakuna mahali popote wanamtaja Zitto bali wanakanusha habari ya gazeti kuwalisha maneno.Sasa ningemshauri Zitto awaachie Mwananchi wathibitishe au wakanushe madhali kasema hakualika waandishi.Hiki anachokifanya Zitto nadhani ni kuanzisha vita isiyo na maana yoyote kati yake na wabunge hao wa chama chake.Huo ni ushauri wangu kwake.
 
Nilikuwepo uwanjani pale lake Tanganyika Kigoma, kilichoandikwa ndicho nilichosikia pia. Videos zitawekwa hapa na zitathibitisha.
Siwezi kuwaandikia mwananchi kwani mimi silalamiki kuhusu habari hiyo. Wenye kuilalamikia habari wameandika.

Mimi ninaamini gazeti la Mwananchi ndio gazeti pekee huru la kiswahili hapa nchini. Ndio gazeti pekee ambalo umiliki wake hauna maslahi na waandishi na wahariri wake ni mahiri, hawana njaa na hawapindishwi. Ndio maana huandika ukweli muda wote na wanapokosea hawasiti kurekebisha. Ndio maana ni gazeti linasomwa kwa wingi kuliko magazeti yote nchini. Hakuna gazeti linalofikia hata nusu ya mwananchi kwa kusomwa. Hivyo Mwananchi linaaminika na umma.
Najua kuna watu wana chuki binafsi na mwananchi kama gazeti na wahariri wa mwananchi kama binaadamu. Hayo wayamalize wenyewe huko walikochukiana.

Subirini video ndio tutajua habari ile imepikwa au ni ya kweli. Kwa tuliokuwepo uwanjani tunajua nani alisema nini.



Muambiwe nini tena Watanzania wenzangu?????????????? Hamjui kusoma......picha pia hamuoni na kutafsiri....m out......!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom