Uraia wa nchi mbili na Rasimu ya Katiba Mpya: Toa maoni yako


Heko chifu wangu. Hizo ni kama bilioni 16 katika pesa za madafu....si haba ati.

Angalau tunaanza kuelekea kwenye muafaka.....

Sasa onyesha (kwa takwimu halisi ama hata projections) pia baada ya uwepo wa uraia pacha ni kiasi gani kitaongezeka katika hiyo bilioni 160?!?

Naomba nieleweke tena kwamba, hili la uraia pacha linanigusa katika ngazi ya familia. Lakini unapokuja mjadala wa uraia pacha katika engo ya kiuchumi, naogopa kuweka hisia katika kujadili.

Katika uchumi mkubwa hapo ndipo penye shida kwangu......na hili la uchumi mkubwa ndio imekuwa hoja ya bwana Membe na wenzake akina Nyerere (yule mama wa viti maalumu wa CHADEMA).
 
Tanzania siyo kisiwa banaaa kuwa na sera za kuwaadhibu wananchi wake kwa sababu za kipuuzi za kuchukua uraia wa nchi nyingine. Nchi yetu tunapenda kukurupuka bila kuangalia mambo kwa kina na kujifunza toka kwa nchi za wenzetu ambao wamekuwa na sera hizo kwa miaka mingi. Katika baadhi ya nchi kwa mfano US, UK, Ujerumani, Canada n.k. baadhi ya ajira zimetengwa kwa ajili ya raia tu, kama si raia basi we URIE TU!! Sasa kwa nini katiba yetu imuadhibu Mtanzania ambaye analipa kodi katika nchi husika na kufuata sheria za nchi husika asifaidike katika kupata kazi kama hiyo ambayo labda itamuongezea kipato chake toka £70,000 to £120,000? Mtanzania huyu kwa mwaka labda alikuwa anatuma nyumbani £4,000 kipato chake kipya kitamuwezesha kutuma £7,000 badala ya £4,000? Pia sera za kuwekeza nchi ziko tofauti kwa mzawa na raia wa kigeni, kwanini Mtanzania mzawa aliyechukua uraia wa nchi nyingine aminywe kama mgeni badala ya kuruhusiwa kuwekeza kama raia na hivyo kumpunguzia gharama na vikwazo chungu nzima vya kuwekeza kama mgeni ukilinganisha na kuwekeza kama raia!?

Naomba usikwepe swali langu Nzi hivi unadhani nchi mbali mbali za Afrika zikiwemo za majirani wetu hazikufanya analysis ya kutathmini faida na hasara za kuruhusu uDC? Unajua fika katika tathmini hizo nchi hizo mbali mbali ziliona faida ni nyingi mno kuliko hasara na hivyo kuamua kuruhusu raia wa nchi hizo kuwa na uraia wa nchi nyingine zaidi ya ile waliyozaliwa.


Dah! Chifu wangu, hatuwezi kuamua na kufanya jambo eti kwa vile nchi fulani zimefanya.

Maana kama ndivyo, tupiganie kwa nguvu kama hizi hizi (nguvu tunazopigania suala la uraia pacha) masuala kama mifumo ya kodi, uwajibikaji, mishahara ya watumishi wa umma, mikataba ya matumizi ya maliasili n.k. Tupiganie pia haya ili yaweze kufanana na jinsi nchi zingine zinavyofanya.

Tukijadili hili suala la uraia pacha kwa misingi ya kwamba nchi zingine zimefanya, hatutafikia muafaka....
 
Last edited by a moderator:
Vyema tena. Ebu toa takwimu za Tanzania, nielimike.

Nimesema kuwa waafrika waliopo uingereza kwa wastani kila mtu anatuma nyumbani Paundi 1000. Hiyo idadi ya waafrika inajumlisha watanzania pia. Dambisa Moyo katika kitabu chake Dead Aid amegusia michango ya waafrika waliopo nje na jinsi michango yao inavyoweza kupunguza tegemeo la misaada ambayo ni kikwazo cha maendeleo.

Kama unataka kuelimika kaanze na Dead Aid by Dambisa Moyo.
 
Heko chifu wangu. Hizo ni kama bilioni 16 katika pesa za madafu....si haba ati.

Angalau tunaanza kuelekea kwenye muafaka.....

Sasa onyesha (kwa takwimu halisi ama hata projections) pia baada ya uwepo wa uraia pacha ni kiasi gani kitaongezeka katika hiyo bilioni 160?!?

Naomba nieleweke tena kwamba, hili la uraia pacha linanigusa katika ngazi ya familia. Lakini unapokuja mjadala wa uraia pacha katika engo ya kiuchumi, naogopa kuweka hisia katika kujadili.

Katika uchumi mkubwa hapo ndipo penye shida kwangu......na hili la uchumi mkubwa ndio imekuwa hoja ya bwana Membe na wenzake akina Nyerere (yule mama wa viti maalumu wa CHADEMA).

Kuna vitu huwezi kuvipima kwa thamani ya pesa. Kuna watanzania wengi wamechukua uraia wa nje hili waweze kunufaika na haki za uraia wa nchi hizo kama vile kwenda shule bure au kwa mikopo nafuu. Fani zingine walizochukua hazifundishwi katika vyuo vya Tanzania. Je Tanzania inaweza kufaidika vipi?

Katika sheria za uhamiaji za Marekani, mtu yoyote mwenye exceptional talent anakaribishwa Marekani. Hawa ndio wanaofanya uchumi wa Marekani uwe vibrant. Je unafikiri hakuna watanzania miongoni mwao?
 
Tanzania si kisiwa Mkuu Nzi, kusema kwamba hatustahili kuiga sera nzuri za majirani zetu ambazo wamefaidika nazo kwa njia moja au nyingine hakuna ubaya wowote ule. Nchi inaporufu Mtanzania kokote kule aliko duniani kufuata sheri za huko aliko ili kupata uraia ambao utamuwezesha kutozikosa nadasi zozote zile ziwe katika biashara au ajira tunajua fika kwa namna moja au nyingine Tanzania nayo itafaidika. Kuna Watanzania wenzetu walioko nje baadhi yao hadi hii leo wanaogopa kuchukua uraia wa nchi nyingi kwa sababu tu ya kuogopa kuupoteza Utanzania wao. Maamuzi kama haya huwakosesha nafasi chungu nzima za maana katika ajira ambayo ingewafaidisha wao wenyewe na nchi pia, lakini kwa sera zilizopitwa na wakati Watanzania hao wanazikosa nafasi hizo.

Kuna atukatiaupinga uDC wameda kuhusu hili kutaongeza ujmbzi nchini!!!! Mbona nchia za wenzetu ambazo uDC umeruhusiwa ujambazi haujaongezeka? Wengine wamethubutu kudai kwamba wenye uDC wakishakwapua nchini watakimbilia huko walikochukua uraia mwingine. Mbona mafisadi wote wa mabilioni akina Mkapa, Lowassa, Rostam, Chenge, Dewji, Jittu na wengine chungu nzima wamekwapua mabilioni na hawana uDC na wapo nchini wakipeta mtaani kwa raha zao!? Wakati umefika wa kuruhusu uDC bila kuendelea kutafuta sababu zisizo na misingi yoyote ile.



Heko chifu wangu. Hizo ni kama bilioni 16 katika pesa za madafu....si haba ati.

Angalau tunaanza kuelekea kwenye muafaka.....

Sasa onyesha (kwa takwimu halisi ama hata projections) pia baada ya uwepo wa uraia pacha ni kiasi gani kitaongezeka katika hiyo bilioni 160?!?

Naomba nieleweke tena kwamba, hili la uraia pacha linanigusa katika ngazi ya familia. Lakini unapokuja mjadala wa uraia pacha katika engo ya kiuchumi, naogopa kuweka hisia katika kujadili.

Katika uchumi mkubwa hapo ndipo penye shida kwangu......na hili la uchumi mkubwa ndio imekuwa hoja ya bwana Membe na wenzake akina Nyerere (yule mama wa viti maalumu wa CHADEMA).
 
Last edited by a moderator:
Kitu hicho kinafaa, na kwa TZ tumechelewa sana kuwanacho. Ila tatizo ni moja tu "Sheria tunajua kuzitunga ila usimamz wake hatuwez kuutekeleza" Matokeo yake itakuwa ni faida kwa wauza unga
 
Tanzania siyo kisiwa banaaa kuwa na sera za kuwaadhibu wananchi wake kwa sababu za kipuuzi za kuchukua uraia wa nchi nyingine. Nchi yetu tunapenda kukurupuka bila kuangalia mambo kwa kina na kujifunza toka kwa nchi za wenzetu ambao wamekuwa na sera hizo kwa miaka mingi. Katika baadhi ya nchi kwa mfano US, UK, Ujerumani, Canada n.k. baadhi ya ajira zimetengwa kwa ajili ya raia tu, kama si raia basi we URIE TU!! Sasa kwa nini katiba yetu imuadhibu Mtanzania ambaye analipa kodi katika nchi husika na kufuata sheria za nchi husika asifaidike katika kupata kazi kama hiyo ambayo labda itamuongezea kipato chake toka £70,000 to £120,000? Mtanzania huyu kwa mwaka labda alikuwa anatuma nyumbani £4,000 kipato chake kipya kitamuwezesha kutuma £7,000 badala ya £4,000? Pia sera za kuwekeza nchi ziko tofauti kwa mzawa na raia wa kigeni, kwanini Mtanzania mzawa aliyechukua uraia wa nchi nyingine aminywe kama mgeni badala ya kuruhusiwa kuwekeza kama raia na hivyo kumpunguzia gharama na vikwazo chungu nzima vya kuwekeza kama mgeni ukilinganisha na kuwekeza kama raia!?

Naomba usikwepe swali langu Nzi hivi unadhani nchi mbali mbali za Afrika zikiwemo za majirani wetu hazikufanya analysis ya kutathmini faida na hasara za kuruhusu uDC? Unajua fika katika tathmini hizo nchi hizo mbali mbali ziliona faida ni nyingi mno kuliko hasara na hivyo kuamua kuruhusu raia wa nchi hizo kuwa na uraia wa nchi nyingine zaidi ya ile waliyozaliwa.

Son;

Kuna wanyarwanda walioishi kama watanzania na kusomeshwa na Tanzania. Kagame alipochukua nchi wamerudi Rwanda. Mmoja alikuwa prof. Sasa hivi ni mkuu wa chuo na tulishamjadili hapa. Mmoja alikuwa waziri wa fedha.
 
Mna hasira eenh jua limekuchwa mliambiwa mkataa kwao mtumwa nyie hamkuelewa!!!!!!!!

Sasa huko yamebuma mnabwata nini kaeni huko mfaidi burgers na sneakers kumechisha na mashati na fulana ha ha haaaaa yana umri hayo sasa jua kumi na moja na robo mnataka kuja huku tena, huku magonjwa kibao na ajira hakuna, huduma za afya mbovu maji ya kunywa tunachemsha mtaweza wazee kaeni huko kuna life expectancy kubwa!!!!!!

Mtatukana sana tu na kama hamjasoma huko na mitaji yenu ya milioni mia na nyumba hukujenga ndio inakuwa ngumu zaid yaani!!!!!!

Hata mkikubaliwa mje mmejipanga huku sio bongo ya miaka mliyoondokea msidanganyane huko jamaa msije mkamalizia hela kwenye panda shuka ya ndege kisa una uraia wa nchi mbili! !!!!!!

Na walio na uhakika wa kipato na maisha nje wala hawana kelele za uraia ila pangu pakavu tia mchuzi ndio kelele haziishi!!!!! As if hata wakipewa huo uraia watasogeza hata ukoo wake daraja moja juu kwenye ngazi ya uchumi!!!!!

Huh? Ndo umeandika nini sasa hapo? Tafsiri tafadhali.
 
Uraia sio issue ya Kulinganisha marekani na Tanzania,tuanzie base inayowafanya wawe na nguvu kwanza sio hizi petty reasons!!!!!!

Kwa nini Mtanzania wa kuzaliwa apoteze Utanzania wake endapo atachukua uraia wa nchi nyingine?
 
Kwa nini Mtanzania wa kuzaliwa apoteze Utanzania wake endapo atachukua uraia wa nchi nyingine?

Sasa unahoji katiba tena wakati ndio tunajadili???!!!!
Si ulaghai tu kuwa na urai wa nchi mbili kutokana na sera ya uchumi wakati huo wakijadili hii katiba,sasa mnataka dual sawa ila uchumi wa nchi uko katika ujamaa,ubepari au mchanganyiko??!!!!!

Haya mambo yana basics moja wapo ni hiyo economic mode kwa uelewa wangu sasa tuanze na pillars zitazotupa uwezo wa ku support hii kitu ila kwa sasa faida yake ni negligible sababu nchi haikwami kwa kukosa hili!!!!!

Ni status tu kwa baadhi ya raia wachache ambao wala hawachangii kuimarisha uti wa mgongo wa Taifa hili,huu ni ukweli wa wazi wala haihitaji nguvu kuelewa!!!!!!!

Hili sio la msingi kwa sasa jamani ni utu na ubinadamu tu kama sio home sickness!!!!!
 
Huyu jamaa alinyimwa visa au walimpa repatriation.

Dhana tu hiyo! !!!!

Ningekuwa katika makundi hayo si ndio ningekuwa upande wenu ili yangu yatimie???!!!!!
Nina sababu na uwezo wa kuomba visa nchi yoyote na nikapewa,kwa field yangu kazi sikosi mkuu hapa ndani na huko nje pia sema jingine haya ni personal tuongelee nchi na ustawi wake!!!!!!!

Repatriation kimbizaneni nayo nyie huko,mimi niko nchini kwangu huo msamiati haupo kwenye maisha yangu! !!!!!


Wewe kwa mfano una potential gani ambayo nchi hii inaikosa sababu huna uraia???!!!!!!
 
Uraia pacha (dual nationality) utageuka kuwa janga la kitaifa kwa sababu zifuatazo:

Kwa mtazamo wangu uraia pacha ni jamii ya ufisadi mwingine kwa upande wa pili wa shilingi.
uraia pacha ni hali ya tamaa kutoridhika na ubinafsi wa wachache kwa masilahi binafsi.

Ifahamike kuwa uraia pacha haimaanishi tu kuwa na uraia wa nchi mbili tofauti bali uwezo wa mtu kuwa na uraia wa nchi nyingi awezavyo!

Pia wachache kwa kutojua au kuficha ukweli wanapotosha wengine eti watanzania walioukana uraia wao na wanaotaka kuukana uraia wao wana uchungu wa kuwa na uraia wa pili ili waje kuwekeza!

Hakuna ushahidi wowote juu ya kauli hii. ukweli ni kuwa uraia pacha ni tamaa za watu wachache kutaka kujilimbikizia uraia wa nchi nyingi wawezavyo kwa hofu kuwa nchi moja maisha yakiwa magumu kiuchumi kukimbilia kwenye nchi ya pili yenye unafuu wa maisha , au nchi yenye kodi ya chini au isiyokuwa na kodi kabisa. .

Watu hawa wachache hawana uzalendo hata kidogo. kwao uraia pacha ni hazina na akiba ya baadae hawawezi kuja na hawawezi kubakia tanzania katika kipindi kigumu kama kipindi cha mtikisiko wa kiuchumi au vita lazima watahamia na vitega uchumi vyao nchi ya pili.

Pia ifahamike kuwa wanaotaka uraia huu pacha ni raia wa tanzania wa watoto wa wakulima wenye baba mama na wajomba hapa tanzania bali ni watoto wa vibosile na matajiri wenye asili za nje kama wahindi waarabu wazungu na wengine jamii hizo.

Naomba ifahamike kuwa mimi si mbaguzi kwa rangi yatu ila kwangu mimi uraia ni lulu na kitu cha thamani kinachoambatana na uzarendo kwa nchi yako hivyo basi kama mzungu au mhindi anauzalendo na anaipenda tanzania abakie na utanzania tu na si vinginevyo.

Hakuna ushahidi kuonyesha kuwa uraia wa nchi mbili au zaidi una faida katika nchi kimaendeleo bali mazingira mazuri ya kiuwekezaji na sera za nchi ndicho kivutio kwa watu wa uraia pacha kuja kuwekeza ila kwa mzarendo yupo tayari kuwekeza hata kama mazingira ni magum .mfano china wana uraia wa nchi moja nabado raia wake ni wazarendo kuiletea china maendeleo.

Kwangu mimi uraia pacha una madhara mengi kuliko faida kwa sababu zifuatazo:

Hebu fikiria leo hii kutokee mgogoro au vita na nchi ya pili ambako huyo mtu tunaeishi nae kama mtanzania pia ni raia wa nchi hiyo je mtu huyu nani anaweza kutabiri atakuwa mzarendo katika nchi ipi? Je ni nani ajuae kama hawezi kutusaliti? Je tutabakia salama kwa kujiamini kuwa ni mwenzetu? Je nani anae jua kama nchi adui haiwezi kumtumia kama jasusi?

Pia watu wanao hitaji uraia pacha ni watoto wa vibosile wengi waliosoma nje pia watoto wa matajiri wanye asili za nje kwa kuwa wanauwezo haitaishia hapo tu bali watawapenyeza watoto wao hao kwenye system mhimu ya nchi kama tiss jwtz polisi wanasiasa mawaziri hata rais kitu ambacho kitakuwa janga kwa taifa kiusalama kama ikitokea nchi ya pili ni maadui na pia kiuchumi kutorosha mali zetu kwenda nchi ya pili ambayo mtu huyo ni raia pia.

Pia ifahamike kuwa hata nchi zilizoruhusu raia pacha kuna mgogoro mkubwa kimataifa kipindi inapotokea raia huyo amepata madhara au tatizo katika nchi nyingine swali linakuwa je ni nchi gani au ubalozi wa nchi ipi umtete au utetee masilahi yake huko nje?

Mfano mtu ana uraia pacha wa tanzania kenya na marekani mtu huyu akapata madhara akiwa china ni nchi gani inamtetea?tafakari

Litakuwa ni janga kitaifa kama uraia pacha utaruhusiwa pia inanisikitisha sana kwa wanasiasa wetu kutojua kutofautisha kati ya dual nationality na dual citizenship inapofikia swala la uraia.

Kwa mzarendo nyumbani ni nyumbani hata kama uko marekani . Huwezi kutumikia mabwana wawili sawa kwa wakati mmoja. Mkataa kwao ni mtumwa.
 
Mkuu mwitasa nashukuru kwa dawa chungu iponyayo!!!!!!!

Wao wanadhani tunawachukia,tuna wivu,roho za korosho na vitu kama hivyo!!!!!

Tanganyika yetu kwanza,uzalendo wa vitendo, miundombinu ya kuendeleza nchi na sera za kueleweka halafu hayo mengine yatakuja baadaye huko kama yana umuhimu anyways!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Dhana tu hiyo! !!!!

Ningekuwa katika makundi hayo si ndio ningekuwa upande wenu ili yangu yatimie???!!!!!
Nina sababu na uwezo wa kuomba visa nchi yoyote na nikapewa,kwa field yangu kazi sikosi mkuu hapa ndani na huko nje pia sema jingine haya ni personal tuongelee nchi na ustawi wake!!!!!!!

Repatriation kimbizaneni nayo nyie huko,mimi niko nchini kwangu huo msamiati haupo kwenye maisha yangu! !!!!!


Wewe kwa mfano una potential gani ambayo nchi hii inaikosa sababu huna uraia???!!!!!!


Mkuu umewahi kusoma uchumi? Kama ungekuwa umesoma usingeuliza mimi na potential gani. Pamoja na kuwa unalipa kodi Tanzania, kodi yako ina manufaa kwa jamii pale watanzania wengine watakapolipa kodi zao. Hivyo matumizi ya mchango wako kwa taifa una maana pale utakapojumlishwa na mchango wa watu wengine. Kwa maneno mengine individually you don't have any potentials.

Kwa mtaji huu, hata mimi binafsi sina potential yoyote. Lakini mchango wangu ukiwa ndani diaspora una potential kubwa kwa taifa. Chukua mfano NSSF, wameanzisha bima kwa watanzania walio nje. Wasingeanzisha bima hiyo kama kungekuwa na mtanzania mmoja tu nje.

Kuhusiana na field yako acheni longolongo hapa. Watanzania mnashindwa ku-complete ndani ya soko la kazi la EA. Kwa sababu ya kuogopa ushindani. Mnakuwa kikwazo ndani ya EA na hata kwa diaspora.
 
Back
Top Bottom