Kwa mara ya kwanza rasimu iliyo kabidhiwa kwa Rais imependekeza uraia wa inchi 2.
wananzuoni mnasemaje kuhusu hili?
Hebu tuwekee vifungu vya rasimu vyenye kuainisha na kubainisha jambo hili...
Kwa mara ya kwanza rasimu iliyo kabidhiwa kwa Rais imependekeza uraia wa inchi 2.
wananzuoni mnasemaje kuhusu hili?
Utanganyika wetu kwanza........................ Tanzania baadaye
Mimi ni Mtanganyika, tatizo ni kwamba tunakumbatia sana hawa wa kutoka nchi nyingine ambao hawana uchungu na nchi hii wanakuja kuchota na kwenda zao, lakini hawa watanzania wana uchungu na nchi yao, kilichowafanya waingie uraia wa nchi hizo ni kufuata sheria wasiishi isivyo halali. Lakini wanachohangaika na masuala ya maisha na uchumi, wengi wanachohangaika ni kuchuma kisha warudi huku homeland.
Maneno yao tu hayo kuwa wanataka kurudi mkuu mioyoni mwao wanajua kwa tofauti walizoziona huku hawawezi kuishi tena na ndio maana wanataka uraia wa huko wabaki nao ili yakigoma huku waondoke zao tena!!!!!!!!
Iwe mtu akitaka kurudi aukane wa huko apewe hiyo hati kwa probation then apewe uraia!!!!!
Hivi hao wa nje ndio wanaweza kubadili hali ya nchi kuliko tuliomo humu????!!!!
Kifungu husika kinasema kuwa "Bila kuathiri masharti yalipo kwenye Sura hii, mtu yoyoye mwenye asili au nasaba ya Tanzania na ambaye ameacha kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano kwa kupata uraia wa nchi nyingine, atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano, atakuwa na hadhi kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi."
Hiki kifungu kimepachikwa tuu na hakitoi hadhi yoyote kwa sababu kinasema wazi kuwa hadhi hiyo itaainishwa katika sheria za nchi.
Pia kitu cha kushangaza ni kuwa hata kama sheria hizo za nchi zitakuja kutambua uraia wa nchi mbili, itakuwa na maana kuwa mtu mwenye uraia wa Marekani, kwa mfano, atatambuliwa kama raia wa Tanzania atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano tuu.
Kwa maana hiyo, huyo mtu hatatambuliwa kama raia wa Tanzania kama atakukuwa katika nchi nyingine kama Kenya na Uganda. Huyo raia hata-enjoy benefits za East African Community kama Watanzania wengine kama akiwa katika nchi wanachama.
Zamani nipokuwa sijabahatika kutembea nchi za nje na kuishi huko nilifikiri na kuwaza kwa mtazamo wako huo, lakini nilipobahatika kufika huko pamoja na kutobadili uraia wa nchi yangu, nimepata kuelewa hali yalisi ya nchi ambako mtu hawana njia ye yote ya kupata ajira na ili aweze kufanikiwa analazimika kuwa na vibali vya kazi ambavyo havitolewi bure ila kwa taratibu za uhamiaji ambazo kuna ndoana zinazowafanya wengi walazimike kunasa ili kuendesha maisha.
Kwa bahati nzuri wengi nilioonana nao na kujadiliana kutoka nchi kadhaa hasa za bara la Ulaya na Marekani wanalilia kwao na kwamba kinachowaweka huko ni kupata cho chote cha kuja kusimamisha vema maisha na familia zao. Kama kuna wanaoona huko ni peponi ni wa kizazi cha Lulu ambao wamefika huko wakati bado bongoni mwao hawajakomaa kupima kwenye mizani mbivu na mbichi.
Mpaka sasa nina ushahidi wa wengi wao kile wanachokipata ni kuja kuwekeza kidogo kidogo home kwa vile mfano pesa nchi za huko mabenki hayana riba nzuri, mfano Marekani interest utapata 0.025% kwa mwaka, na hiyo huishia kwao kwa visingizio mbalimbali wakati bongoland unaanzia na 3% and up. Utaona wengi wao wanaamua kuja kuweka pesa zao kwenye mabanki ya huku nyumbani.
Uwekezaji nao upo kwa sana, kuna wengi wanaoingiza bidhaa toka huko kwao kwa vile wengi wetu huwa vigumu kupata visa vya Ulaya na Marekani. Kuna manufa mengi tu ila tu wengi wenye mitazamo finyu wanaona upande mmoja wa sarafu bila kuigeuza kuangalia taswira ya sarafu hiyo upande wa pili.
Ni mawazo tu yako hayo na hao uliowahoji na suala hapa sio nani katembea wapi na wapi labda kama inabidi kuleta pasi ili kushindania nani msafiri zaid!!!!!!
Hivi kwa akili yako unadhani inahitaji mtu kwenda ulaya magharibi na marekani ya kaskazini kujua kuwa uraia wa nchi mbili ni siasa zaid kuliko uchumi na uhalisia????!!!!
Hebu nitajie Raia walioukana Utanzania na wapo nje wana mitaji ya kusukuma nchi hii lakini wamekwama kwa kigezo cha uraia!!!!
Ukiweka na aina ya biashara wanazotaka kuja kufanya utaelimisha wengi pia!!!!!
nimepata kuelewa hali yalisi ya nchi ambako mtu hawana njia ye yote ya kupata ajira na ili aweze kufanikiwa analazimika kuwa na vibali vya kazi ambavyo havitolewi bure ila kwa taratibu za uhamiaji ambazo kuna ndoana zinazowafanya wengi walazimike kunasa ili kuendesha maisha.
Kwa bahati nzuri wengi nilioonana nao na kujadiliana kutoka nchi kadhaa hasa za bara la Ulaya na Marekani wanalilia kwao na kwamba kinachowaweka huko ni kupata cho chote cha kuja kusimamisha vema maisha na familia zao. Kama kuna wanaoona huko ni peponi ni wa kizazi cha Lulu ambao wamefika huko wakati bado bongoni mwao hawajakomaa kupima kwenye mizani mbivu na mbichi.
Mpaka sasa nina ushahidi wa wengi wao kile wanachokipata ni kuja kuwekeza kidogo kidogo home kwa vile mfano pesa nchi za huko mabenki hayana riba nzuri, mfano Marekani interest utapata 0.025% kwa mwaka, na hiyo huishia kwao kwa visingizio mbalimbali wakati bongoland unaanzia na 3% and up. Utaona wengi wao wanaamua kuja kuweka pesa zao kwenye mabanki ya huku nyumbani.
Uwekezaji nao upo kwa sana, kuna wengi wanaoingiza bidhaa toka huko kwao kwa vile wengi wetu huwa vigumu kupata visa vya Ulaya na Marekani. Kuna manufa mengi tu ila tu wengi wenye mitazamo finyu wanaona upande mmoja wa sarafu bila kuigeuza kuangalia taswira ya sarafu hiyo upande wa pili.
Jibu hoja nizoainisha kujenga utetezi si mipasho. Rudia kusoma tena uone nini nimekiongelea katika hoja zangu na ujaribu kujenga utetezi kwa hoja zangu kwamba hao hawaji kuwekeza home, kwamba yaliyowasibu kupoteza uraia wao ni kuhalalisha haki katika nchi vinginevyo wangeishi isivyo halali na kuacha uraia wa nchi nyingine si dhambi. Kwamba wanawekeza hapa homeland na hivyo kusaidia ajira kwa vijana. Hizo ndizo hoja nilizoainisha unatakiwa ulete zako kuzipiku zangu.
Ili wahujumu wakimbie kiurahisi au??!!!!