Upweke umewaanza vijana mapema, Uzeeni sijui itakuwaje. Ni janga kubwa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,894
UPWEKE UMEWAANZA VIJANA MAPEMA, UZEENI SIJUI ITAKUWAJE. NI JANGA KUBWA.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Huwezi sema unafurahia maisha ukiwa pekeako. Mtu mpweke hawezi kuwa na furaha. Mpweke ni tafsiri halisi ya maiti inayoishi.

Utoto ni raha kwa sababu utoto unahusisha ushirikiano wa mtoto na watoto wenzake. Mtoto na wazazi. Mtoto na michezo. Ndio maana mtoto katika umri wa utoto Unaowajibu wa kumfanya ashirikiane na watoto wengine. Na sio uanze kumfungia ndani kama mfungwa.

Upweke ndio hufanya kijana au binti aoe. Mapenzi ni moja ya tiba ya upweke. Ukiwa na mtu mnayependana na kuelewana automatically upweke utakuwa umedhibitiwa.

Njia nyingine ya kudhibiti upweke ni kujihusisha na vikundi vya kijamii, kidini pamoja na michezo. Lakini hivi ni wakati ukiwa nje ya nyumba yako. Nyumbani ukirudi kama huna mpenzi iwe mke au mume ambaye mnapendana. Utaiona siku ni ndefu na mara nyingi utayaona maisha hayana maana.

Vijana wa sasa wapo vile uwaonavyo, ni kama hawana utulivu, wamechanganyikiwa, wengi wao ni kwa sababu ya Upweke. Upweke unaleta Sonona kama sio Depression. Upweke ni chanzo cha Kifo.

Mabinti wengi ninaowasiliana nao na ambao wanapata huduma kwangu wanakabiliwa na changamoto ya upweke. Wanaishi wenyewé. Wengi wao ni kati ya miaka 22-40. Unakuta Mwanamke amepanga chumba au nyumba anaishi mwenyewe au na watoto, hana mume.

Pia vijana nao wengi wenye umri huo wapo single. Na wanaishi vikundi vikundi kwenye Maghetto yao. Licha ya kuishi vijana kuanzia wawili lakini bado upweke unawasumbua. Hii ni kwa sababu. Wao sio familia moja.
Familia ni Mume, mke na watoto.

Kuanguka kwa taasisi ya ndoa kumeongeza Upweke ndani ya jamii. Na hii itachukuliwa kama fursa kwa wamiliki wa mitandao ya kijamii kwani Watu wengi hutumia mitandao kama sehemu ya kudhibiti upweke.

Upweke ubaya wake upo siku za Weekend kwa wale wanaofanya kazi. Lakini pia upweke huonekana Dhahiri nyakati za usiku Watu wanaporudi kupumzika majumbani kwao.
Wapo Watu ambao usiku kwao hauna faida.

Sababu nyingine kubwa ya wanaume kufa mapema zaidi ni hiihii, UPWEKE. Mtu mpweke hulazimika kufa mapema kutokana na matatizo kama ya msongo wa mawazo.
Wanawake kwa upande wao muda mwingi huweza kuutumia na watoto waliowazaa kuwalea kama kuwabembeleza, kuwaogesha, kuwalisha chakula, kupishana nao kelele, kucheza nao.
Lakini vipi kwa mwanaume?
Mwanaume zaidi ya kwenda Bar kutuliza nafsi na kuondoa upweke ambao kimsingi hauondoki hana pengine pamoja kukimbilia.

Jambo moja lazima ulielewe, Taikon kama Mastermind ninakuambia Upweke huwezi uondoa na Watu Baki. UPWEKE unaondolewa na Watu unaowapenda na unaostahili kuwapenda. Upweke unahusu Moyo. Hisia za UPENDO.
Mke au Mume ndio mtu wa kwanza kuondoa upweke wako.
Kisha Watoto wako.
Alafu Wazazi wako.
Ndipo ndugu na marafiki.

Niliwahi kufanya uchunguzi wa kuona ni namna gani mtu Baki anaweza kukuondolea upweke nikagundua kuwa ni ngumu sana. Ni kwa sababu akili italazimisha moyo u-pretend kuwa haupo pweke.

Kama utaenda Kasino ukachukua Kahaba hata wawili au watatu kwaajili ya kukuondolea upweke, utagundua ya kuwa hawawezi kufanya jambo hilo kwa sababu wao wapo kwaajili ya kujifurahisha kimwili na sio kinafsi(Moyo).

Mtu aliyempweke huweza kufanya lolote la hatari. Upweke huathiri mtu kisaikolojia na huweza msababishia mtu kukosa UTU.

Mtu akikosa anayemjali na wanaomjali moyo wa kujali wengine huanza kufa polepole. Na kama utakufa kabisa utu huondoka nafsini mwake.

Ushauri kwa vijana,
Wapende na kaa karibu na Wazazi wako. Husaidia kuondoa upweke.
Tafuta familia, mke au mume, naye huondoa upweke.
Kuwa na watoto kisha fanya wajibu wako kama mzazi kwa hao watoto.
Kukosa familia ni kukosa maana halisi ya maisha.

Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
UPWEKE UMEWAANZA VIJANA MAPEMA, UZEENI SIJUI ITAKUWAJE. NI JANGA KUBWA.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Huwezi sema unafurahia maisha ukiwa pekeako. Mtu mpweke hawezi kuwa na furaha. Mpweke ni tafsiri halisi ya maiti inayoishi.

Utoto ni raha kwa sababu utoto unahusisha ushirikiano wa mtoto na watoto wenzake. Mtoto na wazazi. Mtoto na michezo. Ndio maana mtoto katika umri wa utoto Unaowajibu wa kumfanya ashirikiane na watoto wengine. Na sio uanze kumfungia ndani kama mfungwa.

Upweke ndio hufanya kijana au binti aoe. Mapenzi ni moja ya tiba ya upweke. Ukiwa na mtu mnayependana na kuelewana automatically upweke utakuwa umedhibitiwa.

Njia nyingine ya kudhibiti upweke ni kujihusisha na vikundi vya kijamii, kidini pamoja na michezo. Lakini hivi ni wakati ukiwa nje ya nyumba yako. Nyumbani ukirudi kama huna mpenzi iwe mke au mume ambaye mnapendana. Utaiona siku ni ndefu na mara nyingi utayaona maisha hayana maana.

Vijana wa sasa wapo vile uwaonavyo, ni kama hawana utulivu, wamechanganyikiwa, wengi wao ni kwa sababu ya Upweke. Upweke unaleta Sonona kama sio Depression. Upweke ni chanzo cha Kifo.

Mabinti wengi ninaowasiliana nao na ambao wanapata huduma kwangu wanakabiliwa na changamoto ya upweke. Wanaishi wenyewé. Wengi wao ni kati ya miaka 22-40. Unakuta Mwanamke amepanga chumba au nyumba anaishi mwenyewe au na watoto, hana mume.

Pia vijana nao wengi wenye umri huo wapo single. Na wanaishi vikundi vikundi kwenye Maghetto yao. Licha ya kuishi vijana kuanzia wawili lakini bado upweke unawasumbua. Hii ni kwa sababu. Wao sio familia moja.
Familia ni Mume, mke na watoto.

Kuanguka kwa taasisi ya ndoa kumeongeza Upweke ndani ya jamii. Na hii itachukuliwa kama fursa kwa wamiliki wa mitandao ya kijamii kwani Watu wengi hutumia mitandao kama sehemu ya kudhibiti upweke.

Upweke ubaya wake upo siku za Weekend kwa wale wanaofanya kazi. Lakini pia upweke huonekana Dhahiri nyakati za usiku Watu wanaporudi kupumzika majumbani kwao.
Wapo Watu ambao usiku kwao hauna faida.

Sababu nyingine kubwa ya wanaume kufa mapema zaidi ni hiihii, UPWEKE. Mtu mpweke hulazimika kufa mapema kutokana na matatizo kama ya msongo wa mawazo.
Wanawake kwa upande wao muda mwingi huweza kuutumia na watoto waliowazaa kuwalea kama kuwabembeleza, kuwaogesha, kuwalisha chakula, kupishana nao kelele, kucheza nao.
Lakini vipi kwa mwanaume?
Mwanaume zaidi ya kwenda Bar kutuliza nafsi na kuondoa upweke ambao kimsingi hauondoki hana pengine pamoja kukimbilia.

Jambo moja lazima ulielewe, Taikon kama Mastermind ninakuambia Upweke huwezi uondoa na Watu Baki. UPWEKE unaondolewa na Watu unaowapenda na unaostahili kuwapenda. Upweke unahusu Moyo. Hisia za UPENDO.
Mke au Mume ndio mtu wa kwanza kuondoa upweke wako.
Kisha Watoto wako.
Alafu Wazazi wako.
Ndipo ndugu na marafiki.

Niliwahi kufanya uchunguzi wa kuona ni namna gani mtu Baki anaweza kukuondolea upweke nikagundua kuwa ni ngumu sana. Ni kwa sababu akili italazimisha moyo u-pretend kuwa haupo pweke.

Kama utaenda Kasino ukachukua Kahaba hata wawili au watatu kwaajili ya kukuondolea upweke, utagundua ya kuwa hawawezi kufanya jambo hilo kwa sababu wao wapo kwaajili ya kujifurahisha kimwili na sio kinafsi(Moyo).

Mtu aliyempweke huweza kufanya lolote la hatari. Upweke huathiri mtu kisaikolojia na huweza msababishia mtu kukosa UTU.

Mtu akikosa anayemjali na wanaomjali moyo wa kujali wengine huanza kufa polepole. Na kama utakufa kabisa utu huondoka nafsini mwake.

Ushauri kwa vijana,
Wapende na kaa karibu na Wazazi wako. Husaidia kuondoa upweke.
Tafuta familia, mke au mume, naye huondoa upweke.
Kuwa na watoto kisha fanya wajibu wako kama mzazi kwa hao watoto.
Kukosa familia ni kukosa maana halisi ya maisha.

Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
They Call Lonelyness a Freedom.
 
Ni Ukweli Kabisa. Chanzo Kikuu Ni Mapenzi, Tunawapenda Ambazo Hawatupendi Tukitegema Tufunge Nao Ndoa Tuanzishe Familia Lakini Mwisho Huwa Ni Maumivu. Mwanaume Una 30+ Umetoka Kazini Umechoka, Biashara Haijaenda Sawa Unafika Home Hata Wa Kusema Baba Waooo Hakuna. Wa Kukwambia Pole Na Kazi Kipenzi Hakuna. Unapumzika Unajiuliza Maswali Unajijibu Mengine Yanakosekana Majibu. Ndoa Ni Jambo Jema Sana. Ukipata Mwanamke Anayekuheshimu Na Kukutii Muoe. Vijana Tusibabaike Na Shape Na Rangi.
 
Safi sana hili jambo ni la kweli ,watu wanakuwa na hasira tu kwa sababu ya upweke.

Jamii imeamua kuhamisha furaha ya asili sasa inapatikana kwa vitu kama pesa ,hta uoe ukiwa broke kama umevaa balaa .

Hapo ndipo mkwamo ulipo wa kijamii.
Pesa ni muhimu lakini kuja mambo muhimu zaidi kuliko pesa ambayo hayauzwi na yapo natural
 
Back
Top Bottom