Gelion Kayombo
Senior Member
- Feb 17, 2018
- 149
- 193
Kwenye makala yetu ya leo tunaenda kujifunza na kujibu swali amabalo watu wengi hujiuliza upi ni wakati sahihi wa kufanya mazoezi kati ya asubuhi na jioni. Mara nyingi swali hili humjia mtu pindi anapoamua kuanza kufanya mazoezi ya mwili, sasa anakuwa anashindwa kuchagua wakati gani awe anafanya mazoezi hayo.
Kwanza kabisa muda sahihi wa kufanya mazoezi ya mwili hutofautiana baina ya mtu na mtu. Utofauti huu huja kutonaka na kutofautiana kwa ratiba baina ya mtu na mtu. Tofauti hii hufanya mtu fulani kufurahia kufanya mazoezi wakati wa asubuhi na mtu mwingine kufurahia kufanya mazoezi wakati wa jioni.
Ili kujibu swali la wakati gani ni sahihi kufanya mazoezi kwanza tuangalie faida za kufanya mazoezi asubuhi na faida za kufanya mazoezi jioni.
Tembelea blog hii Gelion Kayombo kujifunza makala bora zitakazo badili mtazamo wako wa maisha.
Kufanya mazoezi asubuhi hunyoosha mwili
Kufanya mazoezi asubuhi asubuhi hunyoosha mwili na kuandaa mwili kwa majukumu ya siku husika. Hii ni kwa sababu mtu akilala viungo na misuli ya mwili hulegea na kusinyaa. Hivyo kufanya mazoezi asubuhi hufanya viungo na misuli ya mwili kuwa imara.
Huchangamsha akili
Unapolala akili nayo hulala. Huchukua muda akili ya mtu kuchangamka kwa ukamilifu. Njia rahisi ya kuchangamsha akili na kuamsha akili kwa ukamilifu ni kufanya mazoezi. Wale wanaofanya mazoezi wanajua ninacho zungumza hapa.
Huunguza mafuta ambayo mwili hauyahitaji
Asubuhi ni wakati mzuri wa kuunguza mafuta ya vyakula anavyokula mtu kabla ya kulala. Mwili umemeng’enya chakula wakati mtu amelala na mafuta ambayo mwili hauyahitaji umeyahifadhi. Asubuhi ni wakati sahihi wa kuondoa mafuta hayo. Na utaweza kuondoa mafuta hayo kwa kufanya mazoezi asubuhi.
Hufanya siku ya mtu kuwa yenye furaha
Faida za kufanya mazoezi asubuhi haziishii tu wakati mtu anafanya mazoezi tu. Faida za kufanya mazoezi hudumu siku nzima. Hii ni kutokana na mwili huzalisha kemikali fulani zinahusika na kumfanya mtu ajisikie vizuri. Kemikali inayomfanya mtu ajisikie vizuri huzalishwa kwa wingi na kwa haraka pindi baada ya mtu kuchangamsha mwili kwa kufanya mazoezi.
Kufanya mazoezi jioni husaidia mtu kulala usingizi mzuri
Kwa sababu ya damu kuzunguka vizuri mwilini baada ya kufanya mazoezi husaidia mtu kulala usingizi mzuri.
Utakuwa na nishati(energy), nyingi mwilini mwako
Kufanya mazoezi jioni hufanya mwili uwe na nishati nyingi nyingi mwilini. Nishati hiyo huhusika na mtu kuamka asubuhi akiwa mchangamfu bila uchovu wowote.
Ni namna nzuri ya kumaliza siku yako
Umetoka kazini, siku yako ilikuwa imejaa kurupushani kiasi kwamba hujafurahi kabisa siku yako. Namna rahisi ya kurudisha mwili wako katika hali ya kawaida na bora ni kufanya mazoezi jioni. Mazoezi yatakuondolea msongo wa mawazo na maumivu mbalimbali uliyopitia katika siku yako.
Kuwa Na Muda Wa Kutosha Wa Kufanya Mazoezi
Ufanyaji wa mazoezi wakati wa jioni humfanya mtu kufanya mazoezi kwa kustarehe kwani anakuwa na muda wa kutosha wa kufanya mazoezi. Tofauti, na wakati wa asubuhi ambapo mtu anakuwa na mawazo ya kwenda kazini au kukabiliana na majukumu ya siku husika.
Pia ufanyaji wa mazoezi jioni unaweza kupelekea mtu kuchelewa kulala kutokana na mwili kuwa na nishati ya kutosha na kuchangamka sana.
Kwa hiyo ili kujibu swali la upi ni wakati sahihi wa kufanya mazoezi ya mwili kati ya asubuhi na jioni naweza kujibu kama ifuatavyo; Unaweza kufanya mazoezi muda wowote kati ya asubuhi au jioni. Ingawa ufanyaji wa mazoezi wakati wa asubuhi unaonesha kuwa na matokeo bora zaidi kuliko kufanya mazoezi wakati wa jioni. Faida za kufanya mazoezi wakati wa asubuhi ndiyo kama nilivyotaja kwenye makala hii. Faida nilizotaja hapa siyo peke yake, zipo na nyingine nyingi tu.
Kusoma makala nyingine zitakazo badili mtazamo wako tembelea blog hii Gelion Kayombo.
Nakutakia wakati mwema
Kwanza kabisa muda sahihi wa kufanya mazoezi ya mwili hutofautiana baina ya mtu na mtu. Utofauti huu huja kutonaka na kutofautiana kwa ratiba baina ya mtu na mtu. Tofauti hii hufanya mtu fulani kufurahia kufanya mazoezi wakati wa asubuhi na mtu mwingine kufurahia kufanya mazoezi wakati wa jioni.
Ili kujibu swali la wakati gani ni sahihi kufanya mazoezi kwanza tuangalie faida za kufanya mazoezi asubuhi na faida za kufanya mazoezi jioni.
Tembelea blog hii Gelion Kayombo kujifunza makala bora zitakazo badili mtazamo wako wa maisha.
Faida Za Kufanya Mazoezi Asubuhi
Zifuatazo ni faida za kufanya mazoezi wakati wa asubuhiKufanya mazoezi asubuhi hunyoosha mwili
Kufanya mazoezi asubuhi asubuhi hunyoosha mwili na kuandaa mwili kwa majukumu ya siku husika. Hii ni kwa sababu mtu akilala viungo na misuli ya mwili hulegea na kusinyaa. Hivyo kufanya mazoezi asubuhi hufanya viungo na misuli ya mwili kuwa imara.
Huchangamsha akili
Unapolala akili nayo hulala. Huchukua muda akili ya mtu kuchangamka kwa ukamilifu. Njia rahisi ya kuchangamsha akili na kuamsha akili kwa ukamilifu ni kufanya mazoezi. Wale wanaofanya mazoezi wanajua ninacho zungumza hapa.
Huunguza mafuta ambayo mwili hauyahitaji
Asubuhi ni wakati mzuri wa kuunguza mafuta ya vyakula anavyokula mtu kabla ya kulala. Mwili umemeng’enya chakula wakati mtu amelala na mafuta ambayo mwili hauyahitaji umeyahifadhi. Asubuhi ni wakati sahihi wa kuondoa mafuta hayo. Na utaweza kuondoa mafuta hayo kwa kufanya mazoezi asubuhi.
Hufanya siku ya mtu kuwa yenye furaha
Faida za kufanya mazoezi asubuhi haziishii tu wakati mtu anafanya mazoezi tu. Faida za kufanya mazoezi hudumu siku nzima. Hii ni kutokana na mwili huzalisha kemikali fulani zinahusika na kumfanya mtu ajisikie vizuri. Kemikali inayomfanya mtu ajisikie vizuri huzalishwa kwa wingi na kwa haraka pindi baada ya mtu kuchangamsha mwili kwa kufanya mazoezi.
Faida Za Kufanya Mazoezi Jioni
Zifuatazo ni faida za kufanya mazoezi wakati wa jioniKufanya mazoezi jioni husaidia mtu kulala usingizi mzuri
Kwa sababu ya damu kuzunguka vizuri mwilini baada ya kufanya mazoezi husaidia mtu kulala usingizi mzuri.
Utakuwa na nishati(energy), nyingi mwilini mwako
Kufanya mazoezi jioni hufanya mwili uwe na nishati nyingi nyingi mwilini. Nishati hiyo huhusika na mtu kuamka asubuhi akiwa mchangamfu bila uchovu wowote.
Ni namna nzuri ya kumaliza siku yako
Umetoka kazini, siku yako ilikuwa imejaa kurupushani kiasi kwamba hujafurahi kabisa siku yako. Namna rahisi ya kurudisha mwili wako katika hali ya kawaida na bora ni kufanya mazoezi jioni. Mazoezi yatakuondolea msongo wa mawazo na maumivu mbalimbali uliyopitia katika siku yako.
Kuwa Na Muda Wa Kutosha Wa Kufanya Mazoezi
Ufanyaji wa mazoezi wakati wa jioni humfanya mtu kufanya mazoezi kwa kustarehe kwani anakuwa na muda wa kutosha wa kufanya mazoezi. Tofauti, na wakati wa asubuhi ambapo mtu anakuwa na mawazo ya kwenda kazini au kukabiliana na majukumu ya siku husika.
Pia ufanyaji wa mazoezi jioni unaweza kupelekea mtu kuchelewa kulala kutokana na mwili kuwa na nishati ya kutosha na kuchangamka sana.
Kwa hiyo ili kujibu swali la upi ni wakati sahihi wa kufanya mazoezi ya mwili kati ya asubuhi na jioni naweza kujibu kama ifuatavyo; Unaweza kufanya mazoezi muda wowote kati ya asubuhi au jioni. Ingawa ufanyaji wa mazoezi wakati wa asubuhi unaonesha kuwa na matokeo bora zaidi kuliko kufanya mazoezi wakati wa jioni. Faida za kufanya mazoezi wakati wa asubuhi ndiyo kama nilivyotaja kwenye makala hii. Faida nilizotaja hapa siyo peke yake, zipo na nyingine nyingi tu.
Hitimisho
Wakati wowote unaweza kufanya mazoezi ya mwili kutegemeana na ratiba zako. Unaweza kufanya mazoezi asubuhi au unaweza kufanya mazoezi jioni. Ingawa kufanya mazoezi wakati wa asubuhi kuna faida nyingi kuliko wakati wa jioni. Utaweza kujijengea nidhamu binafsi haraka kama utafanya mazoezi wakati wa asubuhi.Kusoma makala nyingine zitakazo badili mtazamo wako tembelea blog hii Gelion Kayombo.
Nakutakia wakati mwema