Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,860
- 12,293
Habari zenu wanaJF wenzangu,
Kama ilivyo desturi ya watanzania wenzetu ambao 90% ni ya wale waliokimbia shule, hivyo kujikuta wanaangukia katika mikono ya wanasiasa uchwara ambao sasa hivi wanawatumia vijana hao kwa malengo yao (wanasiasa) na familia.
Wanasiasa hao wamekuwa wakiwatumia vijana hao kwa kuwatumia vijibando kidogo kwenye PM zao, na wengine kuahidiwa ahadi hewa ya kupitishwa kugombea ubunge, uenyekiti wa serikali za mitaa nk, huku wengine wakijikuta wanakua bendera fuata upepo kwa kufuata upepo wa kundi linalotumiwa data PM, na lile la kuahidiwa ubunge nk bila hao wafuata upepo kuambulia chochote.
Ni hivi kundi hilo halina tofauti na lile lililomuandama waziri mkuu wa kwanza wa serikali ya awamu ya nne, ndugu Edward Lowasa mwaka 2008, ila mbinu inayotumika sasa ni tofauti na ile ya 2008.
Wakati mwaka 2008 ilitumika njia ya kumchafua waziri mkuu huyo, na kumtengenezea fitina yeye na chama chake kwa faida ya chama fulani cha upinzani kilichotengeneza uchafuzi huo. Sasa wamekuja na style nyingine kwa lengo lile lile la kumtengenezea waziri mkuu wa sasa mizengwe na fitina mbali mbali ili ijengeke dhana kuwa waziri mkuu huyo wa sasa hapatani au hapendwi na mwenyekiti wa chama chake au boss wake hivyo yeye waziri mkuu ajiuzulu kutokana na dhana hiyo na hivyo kutengeneza tena fitina na mgawanyiko ndani ya chama na serikali kwa ujumla kama ilivyokuwa miaka ile ya Lowasa.
Huu ni mpango uliosukwa na kile kile chama kinachoongoza kwa siasa za majitaka, ila njia huwa tofauti katika kufikia malengo yao.
Wametumwa vijana mitandaoni kumvunja nguvu waziri mkuu kupitia thread zao, kwa kujifanya wanampenda na kuchukizwa na kile wanachodai anafanyiwa waziri mkuu, lkn ukweli ni kwamba hawampendi na wala hawana huruma nae. Lengo kuu ni kumtengenezea hisia za kuona kuwa anachukiwa, hivyo aamue kujiuzulu mapema na baadae utokee mvurugano chamani, jamaa wamwite aende kwao kuwa mgombea wao, au ikishindikana basi waone mfurugano ambao baadae unaweza kuwafaidisha wao kisiasa.
Namshauri waziri mkuu awapuuze watu hao, kwani wengi wanatumiwa kwa malengo maalum, japo kuna wengine wanaandika tu ilimrqdi wajitafutie na wao jina haoa mitandaoni kupitia upepo huu wa waziri mkuu ulioanzishwa sasa hivi.
Raisi Samia ana imani nae na anamkubali kwa utendaji wake mzuri wa kazi. Kama angekuwa hamtaki kwa sheria hii ambayo wapinzani wanasema inampa "umungu mtu" raisi, basi angekuwa ameshatumbuliwa kama walivyotumbuliwa kina Bashiru, Pole pole nk na maisha yangeendelea kama yanavyoendelea now.
Utendaji wake unaoibeba serikali, na kufanya wapinzani wa serikali wakose hoja, hivyo wanatafuta njia ya kuhakikisha watendaji wazuri wanatoka kupitia vihoja vya kipuuzi puuzi kama hivi ili wabaki wale wataoharibu na wao iwe rahisi kuwakabili katika uchaguzi mkuu wa 2025. Ukiangalia wanaojenga hoja ya upepo huu ni wale wale vijana wa upande wa pili ambao wanafahamika kwa malengo yao na mipango yao.
Chama hicho kwa sasa ni kama hakina mgombea uraisi wa maana na mwenye ushawishi, hivyo kinachofanyika ni kuangalia namna gani watatengeneza fitina ambazo zitasaidia waziri mkuu kukosana na chama chake na kuhamia katika chama chao ili awe mgombea haswa baada ya kugundua kwamba waziri mkuu huyo hana makando kando na mara nyingi watu huoenda kumpongeza kwa hatua mbali mbali anazochukua dhidi ya waharibifu wa sheria za nchi.
Washaona yule anaeishi na wazungu hawezi kuuzika tena kwa wananchi ukizingatia hana chochote cha kuwaonesha watu kuwa alifanya wakati alipopewa dhamana ya ubunge kwa zaidi ya miaka 10.
Kama ilivyo desturi ya watanzania wenzetu ambao 90% ni ya wale waliokimbia shule, hivyo kujikuta wanaangukia katika mikono ya wanasiasa uchwara ambao sasa hivi wanawatumia vijana hao kwa malengo yao (wanasiasa) na familia.
Wanasiasa hao wamekuwa wakiwatumia vijana hao kwa kuwatumia vijibando kidogo kwenye PM zao, na wengine kuahidiwa ahadi hewa ya kupitishwa kugombea ubunge, uenyekiti wa serikali za mitaa nk, huku wengine wakijikuta wanakua bendera fuata upepo kwa kufuata upepo wa kundi linalotumiwa data PM, na lile la kuahidiwa ubunge nk bila hao wafuata upepo kuambulia chochote.
Ni hivi kundi hilo halina tofauti na lile lililomuandama waziri mkuu wa kwanza wa serikali ya awamu ya nne, ndugu Edward Lowasa mwaka 2008, ila mbinu inayotumika sasa ni tofauti na ile ya 2008.
Wakati mwaka 2008 ilitumika njia ya kumchafua waziri mkuu huyo, na kumtengenezea fitina yeye na chama chake kwa faida ya chama fulani cha upinzani kilichotengeneza uchafuzi huo. Sasa wamekuja na style nyingine kwa lengo lile lile la kumtengenezea waziri mkuu wa sasa mizengwe na fitina mbali mbali ili ijengeke dhana kuwa waziri mkuu huyo wa sasa hapatani au hapendwi na mwenyekiti wa chama chake au boss wake hivyo yeye waziri mkuu ajiuzulu kutokana na dhana hiyo na hivyo kutengeneza tena fitina na mgawanyiko ndani ya chama na serikali kwa ujumla kama ilivyokuwa miaka ile ya Lowasa.
Huu ni mpango uliosukwa na kile kile chama kinachoongoza kwa siasa za majitaka, ila njia huwa tofauti katika kufikia malengo yao.
Wametumwa vijana mitandaoni kumvunja nguvu waziri mkuu kupitia thread zao, kwa kujifanya wanampenda na kuchukizwa na kile wanachodai anafanyiwa waziri mkuu, lkn ukweli ni kwamba hawampendi na wala hawana huruma nae. Lengo kuu ni kumtengenezea hisia za kuona kuwa anachukiwa, hivyo aamue kujiuzulu mapema na baadae utokee mvurugano chamani, jamaa wamwite aende kwao kuwa mgombea wao, au ikishindikana basi waone mfurugano ambao baadae unaweza kuwafaidisha wao kisiasa.
Namshauri waziri mkuu awapuuze watu hao, kwani wengi wanatumiwa kwa malengo maalum, japo kuna wengine wanaandika tu ilimrqdi wajitafutie na wao jina haoa mitandaoni kupitia upepo huu wa waziri mkuu ulioanzishwa sasa hivi.
Raisi Samia ana imani nae na anamkubali kwa utendaji wake mzuri wa kazi. Kama angekuwa hamtaki kwa sheria hii ambayo wapinzani wanasema inampa "umungu mtu" raisi, basi angekuwa ameshatumbuliwa kama walivyotumbuliwa kina Bashiru, Pole pole nk na maisha yangeendelea kama yanavyoendelea now.
Utendaji wake unaoibeba serikali, na kufanya wapinzani wa serikali wakose hoja, hivyo wanatafuta njia ya kuhakikisha watendaji wazuri wanatoka kupitia vihoja vya kipuuzi puuzi kama hivi ili wabaki wale wataoharibu na wao iwe rahisi kuwakabili katika uchaguzi mkuu wa 2025. Ukiangalia wanaojenga hoja ya upepo huu ni wale wale vijana wa upande wa pili ambao wanafahamika kwa malengo yao na mipango yao.
Chama hicho kwa sasa ni kama hakina mgombea uraisi wa maana na mwenye ushawishi, hivyo kinachofanyika ni kuangalia namna gani watatengeneza fitina ambazo zitasaidia waziri mkuu kukosana na chama chake na kuhamia katika chama chao ili awe mgombea haswa baada ya kugundua kwamba waziri mkuu huyo hana makando kando na mara nyingi watu huoenda kumpongeza kwa hatua mbali mbali anazochukua dhidi ya waharibifu wa sheria za nchi.
Washaona yule anaeishi na wazungu hawezi kuuzika tena kwa wananchi ukizingatia hana chochote cha kuwaonesha watu kuwa alifanya wakati alipopewa dhamana ya ubunge kwa zaidi ya miaka 10.