Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 754
- 3,097
Akitangaza kuhamia CCM jana January 22, Upendo Peneza amesema kuwa...
"Sasa tuna hoja nzuri sana mezani, Bungeni kuna Miswada mitatu ya Sheria ambayo inabidi ipitishwe na Bunge lakini mmesikia Mwenyekiti Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa) akitangaza maandamano jambo ambalo Mimi naliona (na haya ni mawazo yangu binafsi), Mimi nadhani Viongozi wapo kwenye mshtuko, wanataka kukagua kwa sababu wameshawafanya Wananchi na Wanachama wao ni bidhaa sasa wanataka kutumia maandanamano waangalie hivi tuna bidhaa ngapi na zipi zilizoondoka
Wameshapoteza uhalali wa Kisiasa sasa wanalazimisha uhalali wa Kisiasa wanataka kwenda kwenye maandanamano, wanatumia hoja nzuri sana, na hoja hii naomba niwashukuru sana Viongozi wa Dini na Watu wote ambao wameenda kutoa maoni
Hoja ni nzuri sana lakini inatajwa hoja nzuri ili kuwaaminisha Watu kwamba hiki ndicho wanachokipigania ili Watu kuwaingiza Barabarani lakini lengo ni kuangalia hivi hizo bidhaa bado tunazo au zimeshatukimbia?"
"Sasa tuna hoja nzuri sana mezani, Bungeni kuna Miswada mitatu ya Sheria ambayo inabidi ipitishwe na Bunge lakini mmesikia Mwenyekiti Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa) akitangaza maandamano jambo ambalo Mimi naliona (na haya ni mawazo yangu binafsi), Mimi nadhani Viongozi wapo kwenye mshtuko, wanataka kukagua kwa sababu wameshawafanya Wananchi na Wanachama wao ni bidhaa sasa wanataka kutumia maandanamano waangalie hivi tuna bidhaa ngapi na zipi zilizoondoka
Wameshapoteza uhalali wa Kisiasa sasa wanalazimisha uhalali wa Kisiasa wanataka kwenda kwenye maandanamano, wanatumia hoja nzuri sana, na hoja hii naomba niwashukuru sana Viongozi wa Dini na Watu wote ambao wameenda kutoa maoni
Hoja ni nzuri sana lakini inatajwa hoja nzuri ili kuwaaminisha Watu kwamba hiki ndicho wanachokipigania ili Watu kuwaingiza Barabarani lakini lengo ni kuangalia hivi hizo bidhaa bado tunazo au zimeshatukimbia?"