Updates za kesi ya mauaji ya Daudi Mwangosi

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Daudi.jpg
img.php

Alhamisi ya Februari 6, 2015, Mahakama Kuu Kanda ya Iringa ilianza kusikiliza kesi ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten, Daud Mwangosi, inayomkabili askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Pacificus Cleofas Simon mwenye namba G 2573.

Kwa wale watu wa matukio ambao walishasahau kilichotokea, Mwangosi aliuawa Septemba 2, mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilaya ya Mufindi wakati akiwa kwenye majukumu yake ya kazi wakati Chadema wanakiandaa kwa ajili ya kufanya maandamano na mkutano mkubwa pamoja na kufungua tawi la chama hicho.

Katika mashtaka hayo, Wakili wa Serikali, Sunday Hyre, anadai kuwa Septemba 2, mwaka 2012, mtuhumiwa (Pacificus Cleofas Simon) alimuua Mwangosi kwa kumpiga kwa bomu kwa makusudi. Hata hivyo, mtuhumiwa amekana shitaka hilo. Mtuhumiwa anatetewa na Wakili Rwezaula Kaijage. Kesi hiyo inasikilizwa mbele ya Jaji Paulo Kihwelo.

Wiki iliyopita Kihwelo aliamuru upande wa utetezi kupokea kielelezo cha gazeti la Septemba 3, mwaka 2012 kama utambuzi wa awali ili kusaidia ushahidi wa keshi hiyo. Jaji Kihwelo alisema kuwa kielelezo hicho ni muhimu kwa sababu kitasaidia kutumika katika ushahidi wa kesi hiyo ya mauaji ya Mwangosi.

Hapa tutakuwa tunaweka updates za kesi hiyo mpaka hukumu itakapotolewa.

PIA SOMA
- TANZIA - Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
 
Shahidi wa kwanza alitoa ushahidi wake katika Mahakama hiyo Alhamisi (12 Februari) ya wiki iliyopita mbele ya Jaji Paulo Kihwelo. Shahidi wa kwanza katika kesi hiyo ni Said Mnunka ambaye ni Ofisa mstaafu wa FFU. Shahidi huyo alidai kuwa hakumtambua aliyedaiwa kufanya mauaji hayo hadi alipotazama picha kwenye gazeti.

"Sikuweza kutambua chochote kuna kitu kilitokea, lakini kama Septemba 3, niliona gazeti ofisini kwa RPC wa Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, ndipo nilibaini kuwa kuna kitu kilitokea jana yake (Septemba 2) baadaye ndipo tulizifuatilia kwa mtu mmoja mmoja kuanzia kwa wale askari walionekana kwenye ile picha hadi kumbaini mtuhumiwa," alidai Mnunka.

Shahidi wa pili alitoa ushahidi wake katika Mahakama hiyo Ijumaa ya wiki iliyopita. Shahidi huyo ni Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya (OCD) cha Mufindi mkoani Iringa, Assel Mwampamba. Alidai kuwa Septemba 1, mwaka 2012, alipigiwa simu na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, na kumuamuru aandae kikosi kwenda Kijiji cha Nyololo kuzuia maandamano na mkutano wa Chama cha Demokraasia na Maendeleo (Chadema).

"Siku hiyo nilitekeleza maagizo kama nilivyoagizwa na RPC kesho (Septemba 2) tulielekea Nyololo nikiwa na kikosi changu, gari la mkoa moja, magari mawili ya askari wa FFU kutoka mjini Dodoma," alidai.

OCD Mwampamba aliendelea kudai kuwa walipofika Mufindi walikutana na magari mawili ya polisi kutoka Wilaya ya Mufindi na kuelekea kwenye eneo la tukio. Alidai walipofika Kijiji cha Nyololo walikuta Chadema wamefunga vinasa sauti kwa ajili ya kuanza mkutano wao na kwamba aliteremka kwenye gari na kuongea na viongozi wa chama hicho, lakini walikaidi na kutamka kuwa liwalo na liwe lazima wafanye mkutano wao.

Alidai kuwa aliamriwa kuzuia maandamano hayo ili kutekeleza amri ya Serikali baada ya kutangaza kuzuia vyama vyote vya siasa visiendelee na mikutano kutokana na zoezi la sensa ya watu na makazi. Aliendelea kudai kuwa baada ya kuona fujo zimetulia, ndipo waliamriwa kuingia kwenye magari kwa ajili ya kurudi kwenye kambi zao.

Hata hivyo, alidai kabla hawajaondoka, alishtukia Mwangosi ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa, amemkamata mikono bila kujua sababu, ndipo alipoamua kupiga yowe kuomba msaada.

Alidai wakati askari wakienda kumsaidia, alisikia mlipuko wa kishindo na kupoteza fahamu. Alidai alipozinduka alijikuta amelazwa Hospitali ya Wilaya Mufindi akipatiwa matibabu bila kujua kilichotokea Septemba 2, mwaka 2012.

Alidai baadae aliambiwa kuwa Mwangosi alifariki dunia. "Sikujua mwandishi huyo alikuwa na dhumuni gani, ndiyo maana nikaamua kuomba msaada kutoka kwa askari wenzangu ili waweze kunisaidia, " alidai Mwampamba.

Jaji Kihwelo aliahirisha kesi hiyo hadi February 16. 2015 atakapoendelea kusikiliza ushahidi huo. Jaji Kihwelo alisema kuwa mashahidi hao wawili watahitajika tena mahakamani hapo kama ushahidi walioutoa haujakamilika. Baada ya shahidi wa pili kumaliza kutoa ushahidi, Jaji Kihwelo alisema kuwa shauri hilo limehairishwa na hakumtaja ni shahidi yupi atatoa ushahidi February 16.

NIPASHE
 
Kesi iliendelea kusikilizwa February 16 kama ilivyopangwa ambapo shahidi wa tatu alikuwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Dodoma, Frola Mhele. Akitoa ushahidi wake, Mhele ameambia Mahakama Kuu kuwa mtuhumiwa alipelekwa kwake kuungama kumuua Daudi Mwangosi kwa bomu bila kukusudia.

Alidai kuwa mtuhumiwa huyo alipelekwa kwake kuungama wakati akiwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mjini Iringa. Alidai Septemba 5, 2012 saa 7:24 mchana, polisi walimpeleka mtuhumiwa huyo katika mahakama hiyo kwa ajili ya ungamo na kuchukua maelezo. Alidai mtuhumiwa huyo alimweleza kuwa amefikishwa mahakamani hapo kwa sababu anatuhumiwa kwa kesi ya mauaji.

Shahidi huyo alidai alimkagua mtuhumiwa mwilini mwake na kumkuta akiwa na jeraha bichi kwenye mkono wake wa kulia katika kidole cha kati kutoka mwisho na majeraha ya zamani. Mhele alidai alipomuuliza kuwa jeraha amelipatia wapi, alimjibu alilipata wakati bomu lilipolipuka na kwamba hakujua kama amepata jeraha hilo.

Alidai mtuhumiwa huyo katika maelezo yake, alimweleza kuwa Septemba 2, 2012 ilitokea kazi kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi ambako kulikuwa na mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao haukua rasmi. Alidai mkutano huo hakuwa rasmi kwa sababu wafuasi wa Chadema na viongozi wao walikaidi amri ya Polisi ya kuzuia kufanyika licha ya kutangaziwa ilani mara tatu.

Alidai mtuhumiwa huyo aliendelea kumweleza kuwa askari waliokuwapo kwenye eneo hilo waliamriwa kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya machozi. Alidai mtuhumiwa huyo alimweleza kuwa yeye na askari wengine walisikia sauti ya askari akipiga yowe kuomba msaada na mlio mkubwa wa kishindo, lakini yeye hakujua mlio ule ulitokea wapi.

"Mshitakiwa katika maelezo yake alieleza kuwa inawezekana ni yeye alipiga bomu bila kujua," alidai na kuongeza: "Baada ya kutoka eneo la tukio na kufika kambini waliitwa kwenye mstari na kugundulika kuwa silaha aliyoibeba yeye ndiyo ilitumika kupiga lile bomu na kumuua Mwandishi Daudi Mwangosi, lakini yeye hakukusudia."

Mahakama hiyo imepokea kielelezo cha kesi hiyo ambacho ni maelezo ya ungamo la mtuhumiwa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Dodoma, Frola Mhele.

NIPASHE
 
Akitoa ushahidi wake February 16, shahidi wa nne, Lewis Tiekya (29) ambaye alikuwa mtunza ghala la silaha msaidizi, alidai kuwa siku ya tukio alipokea simu kutoka kwa Mkuu wa FFU, Said Mnunka, saa 12:30 asubuhi akimweleza kuwa anahitajika haraka katika ghala la silaha kwa sababu kuna dharura imetokea wilayani Mufindi. Tiekya alidai alimwamuru atoe silaha ili kwenda kuweka amani kijijini hapo.

Alidai silaha ya mtuhumiwa iliyokuwa na namba 040824 ilirudi kama ilivyo kwa sababu hakujua kama ndiyo imetumika kupiga bomu hilo. Alidai wakati huo alitoka na mabomu 15 ya kishindo kikubwa na 22 ya moshi ya kurusha kwa mikono, risasi za SMG 60 ambazo hazikurudi hata moja.

Mahakama hiyo imepokea vielelezo vya kesi hiyo ambavyo ni kitabu cha orodha ya majina ya askari wanaochukua na kurudisha silaha ghalani.

Wakili wa Serikali Ladislaus Komanya, alidai kuwa mashahidi wawili wameshindwa kufika kwa sababu hati ya kuitwa haikuwafikia na mmoja ameomba udhuru kwa sababu ameuguliwa ghafla. Komanya aliiomba mahakama kuwa ombi la pili la utuzwaji wa kielelezo cha mashitaka namba nne ambayo ni bunduki mahakama itoe ili itunzwe na Jeshi la Polisi hadi itakapohitajika kwenye kikao kijacho.

Komanya alidai kielelezo namba tano ambacho ni kitabu cha orodha ya kuchukua silaha na kurudisha irejeshwe kwa upande wa mashtaka kwa sababu inatumiwa na jeshi hilo. Aliomba karatasi ambayo ilitumika siku hiyo kwa ajili ya kuchukua silaha, ibaki mahakamani hapo kwa ajili ya ushahidi.

Wakili Kijage hakuweka pingamizi kuhusu kielelezo namba nne kutunzwa na polisi, kadhalika na kielelezo namba tano. Hata hivyo, aliomba shauri lipewe kipaumbele katika kikao kijacho kwa sababu mtuhumiwa yupo rumande.

NIPASHE
 
Hata hivyo, alidai kabla hawajaondoka, alishtukia Mwangosi ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa, amemkamata mikono bila kujua sababu, ndipo alipoamua kupiga yowe kuomba msaada.

Alidai wakati askari wakienda kumsaidia, alisikia mlipuko wa kishindo na kupoteza fahamu.Alidai alipozinduka alijikuta amelazwa Hospitali ya Wilaya
Mufindi akipatiwa matibabu bila kujua kilichotokea Septemba 2,mwaka 2012.shahidi atambue kuwa Mungu alimuona.
 
EMT;

Black/RED: Huyu kuna uwezekano mkubwa anaidanganya mahakama....(kama maelezo yake hayajapindishwa na mwandishi)!
 
Last edited by a moderator:
Hao askari wengine kwenye hiyo picha hawahusiki au walikuwa wanacheza kombolela hapo?

Hii ndio Tanzania kila kitu kinawezekana mradi tu kinahusu wakubwa!
 
Ukiangalia kwa makini, utagundua hao maaskari ambao wapo upande wa mashtaka wanatoa ushahidi dhaifu kwa makusudi ili hukumu itoke kwa namna ambayo itaonekana hakukuwa na ushahidi wa kutosha kumtia mtuhumiwa hatiani. Hebu angalia eti shahidi wako anatoa ushahidi wa mashaka kama huu:
Shahidi wa kwanza .... Shahidi huyo alidai kuwa hakumtambua aliyedaiwa kufanya mauaji hayo hadi alipotazama picha kwenye gazeti.

Shahidi wa pili ... Alidai wakati askari wakienda kumsaidia, alisikia mlipuko wa kishindo na kupoteza fahamu. Alidai alipozinduka alijikuta amelazwa Hospitali ya Wilaya Mufindi akipatiwa matibabu bila kujua kilichotokea Septemba 2, mwaka 2012. Alidai baadae aliambiwa kuwa Mwangosi alifariki dunia.
 
Kamuhanda na Mwigulu wameua Watanzania wenzetu,hatujasahau mpango wa Mwigulu pale Soweto-Arusha.Mungu atatuongoza ktk haya na adhabu inayowafaa,kisasi kipo tu"jino kwa jino"
 
Nadhani hii kesi itakuja kusikilizwa kwa haki siku CCM ikitoka madarakani...
 
Nadhani hii kesi itakuja kusikilizwa kwa haki siku CCM ikitoka madarakani...

Kuna mambo mawili:

1. hao wanaotoa ushaidi wa uongo na huyo jaji au hakimu ambaye atakubali kupokea na kuidhinisha ushaidi wa Uongo, Machozi ya mjane wa Mwangosi hayatawaacha hata kama watajidanganya walikuwa kazini au wataamua kujidai kuwa na KIBURI CHA UZIMA.

2. Hukumu ya kesi hii kama itapendelea wauaji na walioshiriki kutunga ushahidi wa Uongo, utakuwa ni mwendelezo wa wananchi kuendelea kukosa Iman na Mahakama na kuna siku hata kama itakuwa baada ya miaka 100, mahakama hazitaaminika tena, na wale wanaofikiri wako juu ya Haki watakimbia na kusambaratika, Halafu taifa litaanza upya, hiyo ndio nature ya historia
 
Alot of contradictions,upande wa mtuhumiwa wanajikanyaga sana katika harakati za kupindisha ukweli!!!

Hivi tunategemea askari atatoa ushahidi wa kumuweka hatian askari mwenzao kweli?!!,never be so!!!

Na hii delay ili tusahsu sio,ila Mungu hasahau!

Aliua hata angepindusha ukweli hapa duniani ajue ipo sku ukweli utadhihirika machoni pa mwenye Haki!!
 
mwanasheria wa serikali anasimamia kesi inayomhusu mtuhumiwa ambaye ni askari(mwajiriwa)ya ccm,ambao wanatuhumiwa kwa kuelekeza mauaji haya!!!!hakuna kesi hapo.Kuna haja ya kubadili mifumo ya sheria,badala ya jamhuri kumshitaki muuaji kama huyu basi watu binafsi(mjane kwa mfano)ashitaki na aweke wakili mahiri.
 
Back
Top Bottom