Updates: VodaCom Premier League 2009/2010

Updates: VodaCom Premier League 2009/2010

TIMU GANI ITAKUWA BINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA(Vodacom Premier League)


  • Total voters
    72
  • Poll closed .
Kama mwaka jana,tutachukua ubingwa siku ya mwisho,waache watangulie
 
Simba, Yanga viwanjani tena leo
Simbba(38).jpg

Timu ya Simba


Vinara Simba watacheza ugenini dhidi ya Polisi kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, lakini macho na masikio mengi yataelekezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambako mahasimu Yanga watajaribu kusahau jinamizi la kupiga mwamuzi katika mechi yao iliyopita uwanjani hapo wakati watakapowakabili African Lyon katika mechi nyingine za Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo.
Simba ambao walishikiliwa kwa sare ya 0-0 dhidi ya Toto African katika mechi yao ya mwisho Jumapili wako kileleni kwa pointi 41 baada ya mechi 19, wakati Yanga wako katika nafasi ya tatu kwa pointi 37 kutokana na kucheza mechi 18.
Nafasi ya pili inashikwa na Azam yenye pointi 41 sawa na Simba ikiwa imezidiwa wastani wa magoli. 'Wana-Lambalamba' wamecheza mechi moja zaidi ya Simba na mbili zaidi ya Yanga.
Yanga inarejea kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa tangu wachezaji wake walipohusika katika vurugu za kumpiga mwamuzi Israel Nkongo aliyewatoa nyota wawo wawili katika mechi dhidi ya Azam waliyolala 3-1 Jumamosi na kupelekea kufungiwa kwa wachezaji watano wa klabu hiyo ya Jangwani.
Adhabu hizo zinamaanisha kwamba Yanga leo itazikosa sura maarufu katika kikosi cha kwanza, Stephano Mwasika aliyefungiwa mwaka mzima, Nadir Haroub 'Cannavaro' aliyefungiwa mechi sita, Nurdin Bakari na Omega Seme waliofungiwa mechi tatu kila mmoja na Haruna Niyonzima, anayetumikia adhabu wa kukosa mechi moja kutokana na kadi mbili za njano alizopewa katika mechi hiyo iliyozua balaa.


Yanga sasa itawategemea nyota wao waliopoteza namba katika kikosi cha kwanza akiwemo kiungo 'jembe' Juma Seif 'Kijiko', beki wa kushoto Oscar Joshua, mlinzi wa kati Chacha Marwa, kiungo mshambuliaji Rashid Gumbo na kiungo wa pembeni Idrissa Rashid.

Viingilio katika mechi ya Yanga itakayoanza saa 10.30 jioni ni Sh. 3,000 kwa viti vya bluu na kijani, Sh. 5,000 viti vya rangi ya chungwa, Sh. 10,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa Sh. 15,000.
Yanga itarejea tena uwanjani Machi 17 kwa pambano dhidi ya wenyeji Villa Squad litakalofanyika Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati siku hiyo hiyo Coastal Union itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.
Machi 18 kutakuwa na mechi tatu ambapo Simba itakuwa ugenini kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro dhidi ya Mtibwa Sugar, Toto African itaikaribisha Polisi Dodoma jijini Mwanza wakati Azam na Ruvu Shooting Stars zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Chamazi.
 
Leo Yebo yebo sijui watapigana tena maana mpira siku hizi hawauwezi kabisa wamebakia mabondia tu....
 
Back
Top Bottom