Uongozi Chuo Kikuu Dar Es Salaam una matatizo

Well said brother.

English medium sio mkombozi wa tatizo kabisaa ila ni mtaala wetu ndio tatizo.
Mimi napenda kuchangia kidogo mtoa uzi.Mimi ni mwlm tena wa shule ya msingi.Nilianza na ngazi ya chert ila Leo natafuta shahada ya pili.Nimeingia kazini 2010.

Vyuo vikuu tusivilaumu sana kwakuwa vinapata product ambayo imetoka hapa chini.Msingi ambao ndoo elimu ya msingi ni mbovu kupitiliza .Siku hizi wanafunzi wakishafika darasa la saba wanafundishwa past pepers tu mpaka wanafanya mtihani lengo afaulu la saba.

Leo hii mwlm anaingia darasani na kitabu anafundisha kwa kuongea yeye mwanzo mwisho.Akimaliza natoa maswali mwanafunzi anafanya ,atakae kosa atamfnyia masahihisho na kuendelea na mada nyingne.Hakuna kumtengenezea mwanafunzi udadisi,uchunguzi wala ubunifu wowote.

Siku hizi waalimu ndoo wamechoka kabisaa wanawavanyia hadi mtihani wanafunzi ili mradi limtoke asije sumhuliwa kwann hawajafaulu ,mara uandike barua.Ndivyo wakubwa wa ngazi za juu wanavyo taka ,ufaulishe asilimia mia haijalishi umepatikanaje.

Hivyo hivyo shule za English midium,nao wanawakaririsha watoto.Hawana mbinu za kuwafanya watoto wadadisi,wawe wabunifu wala wawe wavumbuzi.Kinacho wasaidia hapo ni lugha na kukrishwa kwa wingi.

Wakitoka hapo wanaenda sekondary huko lugha kingereza na kwakuwa wanamsingi wa ligha wataweza kukariirishwa na kufaulu na jatimae watafika chuo kikuu na hizo one au two.

Tanzania mwanafunzi anae faulu vizuri kidato cha nne na sita akaenda UDSM anacho mzidi mwenzake aliepata 3 au 2 ni kuwa yeye ana uwezo mzuri wa kukariri na kukumbuka kuviandika kwenye karatasi tu ,hana kingine chochote zaidi ya hapo.

Tutazidi kupiga kelele na kuongea sana but mkombozi hayupo.Serikali lazima ikubali ije na mfumo mzima wa utoaji wa elimu utakao tusogeza miaka angalau thelathini mbele sio huu mfumo tulio nao.

Wanachosema serikali wanasema hawana pesa lakini najiuliza si bora wasigharamikie hiyo miradi mikibwa baadala yake wagharamikie elimu iwe bora?

Nisamehe nimeandika marefu sana ila natamani watanzania wajue na waungane kwa pamoja kuishinikiza serikali ibadili huufumo ili watoto wao wapate elimu bora.

Mimi na babaangu mdogo watoto wake wote watatu wamesoma kuanzia nasury mpaka kidato cha sita Tusiime. Chuo kikuu UDSM wote wapo kwake ,alifikiria gharama alioitumia ni kubwa sana na pesa ya kuwa pa mitaji hana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Senzy saana popoma mwenyewe.

Kila mtu yupo huru kusema. Narudia kukwambia kuwa hamna aliyesoma udsm alafu akajilaumu.

Wachache saana.

Ona huyu mwingine anavyoongea Ugoro, unathibitisha kabisa anachokiongea mleta mada, we all know UDSM ni chuo mama na kikubwa nchini na ndio maana mleta uzi kaleta uzi huu sasa kuonesha UPOPOMA wako hilo ndio jibu sahihi uliloliona. Aiseee
Exactly, lakini ukitaka kujua walengwa ni mapopoma, wengi watabase kumuattack mleta uzi as if ni vita.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
serikali ijitaidi pia ilipe mishahara inayoeleweka watu waridhike watulie...unakuta lecture badala ya kukaa chuoni kuandaa kitu cha kufundi yupo uko kwenye plan B anatengeneza cake na kutembeza....anakuja darasani mara moja kwa mwezi au asitokee kabisa...akija anakuambia "mimi hii kazi ya ualimu nafanya tu for funny"...anakwambia nina miradi yangu uko ndio inayonipa pesa...sasa unafkiria kwa mtu kama uyu anategemea afundishe wanafunzi wamuelewe kweli!!!anakuja darasani baada ya lisaa hapo lecture ya masaa mawili...atakaa dk 40 kaondoka...hakuna cha maana alichofundisha zaidi ya kutupigia story za uhaba wa ajira ...kwa hali kama hii kutoka na content inayoeleweka chuoni ni ngumu kwa sababu badala ya mwanafunzi kuwaza chuo unajikuta tena unawaza ya baada ya chuo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
- Miaka inaenda tu na kila mwaka wanachukua vijana wetu wanaojiweza sekondari lakini wanaturudishia uozo. Unakuta mtoto alikua ana akili kweli lakini akimaliza chuo anaanza kuongea pumba, ooh mara " nataka nianzishe kampuni yangu ya software" " nataka nitoe semina ya madini", " nataka niandae semina ya ujasiriamali", ushenzi na uzuzu tu.

- Wakati sisi tunawapeleka watoto pale tunasema mtoto anaenda mlimani, atatoka na kitu pale, kumbe anaenda kutoka na maongezi. Ndio maana hata watu wa taaluma kubwa za sayansi kutoka UDSM wanaishia kuwa wanasiasa. Chuo kimejaa porojo mno.

- Hivi unajua Mwijaku alikua mwanafunzi wa UDSM? that fat fuk should've been the one helping our film industry but he is dying with it. Yani chuo kinachoaminiwa na watanzania wote kinashindwa kuzalisha hata waigizaji wazuri. UDSM ndipo walipotakiwa kutoka first grade Creative writers lakini asilimia 98 ya vitabu vyote vipya Tanzania vinahusu ujasiriamali au ni catalogue za bidhaa mbalimbali. Upumbavu juu ya upumbavu.

- Wazazi hatupendi vijana wetu wawe wanasiasa, tunapenda vijana wetu wawe na taaluma zinazoeleweka.

- UDSM imejaa misifa tu na hamna la maana linalofanyika.

- Chuo kikuu kikubwa kama kile hamna independent course ya Robotics, huwezi kutengeneza lolote miaka hii ya sasa hivi bila kuwa na elimu ya Robotics. Lakini UDSM hamna.

- Kwanini tusichukue waalimu wa nchi za nje walioendelea kielimu kuja kutusaidia kufundisha? ( nchi kama Ujerumani, Uingereza, Norway na Marekani). Tumejaza wasakatonge kama wakufunzi pale badala ya wataalamu. Mtoto anatoka CoICT hata basic commands za Linux hajui.

- Muda umefika wa serikali ya wanafunzi kukomalia taaluma inayotolewa pale, sio kila siku wanafunzi wanagombana na serikali kuu, tafuteni elimu inayoeleweka. Ukiwa na Cheti cha Geology kutoka UDSM halafu huna ajira wewe maisha yako ndio yameisha hivyo lakini haitakiwi kuwa hivyo. Wanafunzi lilieni elimu, mnatoka pale na uwezo mdogo tofauti na matarajio.

Mpaka leo hatuna kampuni binafsi ya mtandao wa simu ya kitanzania, zote zilizopo ni subsidiary ya kampuni za nje, na UDSM ipo tu miaka inaenda. Amkeni serikali ya wanafunzi, chuo kutafute waalimu competent na mazingira yawe wezeshi kusaidia kua na utaalamu wa hali ya juu kabisa kwa kozi husika.
Hasira zako za kukosa admission kwenye chuo kikuu cha taifa zitafutie mahali pa kuzipeleka.
 
Kwenye suala kama hili tupunguze ushabaiki na mizaha jamani

Binafsi naona kuna tatizo siyo udsm peke yake vyuo kibao hazizalishi kile kinatakiwa wazalishe mfano mdogo tu ni kwamba wahitimu wengi vya vyuo vikuu ni tegemezi wa ajira ukiwalinganisha walau na hata wadau wanaotoka vyuo vidogo vya ufundi eg VETA,tuwe wakweli

Huu mfumo unahitaji maboresho kama kweli tunataka kujenga taifa letu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na cha baadae

Majuzi tu niliweka humu uzi namna ambavyo vyuo vingi vikuu vimekuwa vikipika wasaka ajira badala ya kuandaa watalaamu ambao wangelikuwa msaada kwa taifa mwisho tuanze kulaumiana serikali itoe ajira,hivi serikali itaweza ajiri wahitimu wote?

Nadhani kwa sababu lawama zote zaelekezwa kwa serikali ni muda muafaka sasa serikali kujitizama na mitaala yake kwa aidha kuboresha ama kuifumua upya
 
Unakuta mtoto alikua ana akili kweli lakini akimaliza chuo anaanza kuongea pumba, ooh mara " nataka nianzishe kampuni yangu ya software" " nataka nitoe semina ya madini", " nataka niandae semina ya ujasiriamali", ushenzi na uzuzu tu.

😂😂😂😂😂😂
 
achana na hizo habari za admission, Chuo cha taifa kinaisaidiaje nchi?
Kimezalisha wataalamu mbalimbali wanatumikia dunia nzima kama Profesa Muhongo. Kimetoa marais kama Museveni na Magufuli.
Kimetoa wakufunzi wengi sana wanaofanya kazi kwenye vyuo vya mikoa kama Udom
 
Hapa nitashauri kama mpita njia
1. Elimu ya chuo kikuu ni pana sana, mwanachuo hapaswi kutegemea madesa ya darasani pekee. Mkufunzi akishadodosa kidogo ni jukumu lako kwenda deep kupitia vitabu vya maktaba na tutorials nyingine mitandaoni.
WANACHUO MSIPOTEZE MUDA KWENYE KUTAZAMA SERIES NA PORNO.

2. Si ajabu kumkuta mwanachuo wa mwaka wa mwisho anaesomea ualimu hana notes za kufundishia, kila alipokuwa akienda field anabeba daftari lake la O'level alilosomea miaka mitano iliyopita anaenda kuwafundishia vijana, yaani hana muda wa kuboresha kile cha zamani kwa kuzingatia kuwa sasa ameelimika. Hili haliitaji mkufunzi akwambie, linahitaji utashi wa mtu mmoja mmoja, kama huna, huna.

3. Si ajabu kumkuta mwanachuo anaesomea engineering, IT, electronics n.k katika laptop yake ana software nyingi za games kuliko za fani yake. Unamuuliza mwanachuo wa mwaka wa pili anaengia watatu wa fani ya IT kama anajua kutumia framework yoyote katika kutengeneza tovuti, anakuuliza framework ndio nn?
Huyu ni mwanachuo ambae akishafundishwa kile cha darasani ndio kamaliza hatoki nje ya box. Hajihangaishi kujua duniani wataalamu wa fani yake wanatatua changamoto kwa mtindo upi wa kisasa.

4. Maisha magumu ya wanachuo nayo pia yanachangia kupunguza umakini. Si ajabu kumkuta mwanachuo hana laptop, hana smartphone yupo yupo tu na madesa yake, unategemea nini hapo, mkopo wenye asilimia 30, ndugu wanamtegemea, bata hapohapo, aishi kichuochuo, halafu unategemea awe mbunifu, aaa wapi.

5. Chuo kuna katabia kakuaanda project mwaka wa mwisho, project ziwe kila semester, japo ndogondogo, ili mwaka wa mwisho atutengenezee kilicho bora kabisa. Hii system ya sasa inawafanya wazubae zubae sana.

Mpita njia nipo kwenye kimbweta saa hii, nitashuka cafteria ya yombo muda si mrefu niende zangu changanyikeni.
Ciao.
 
Mzumbe ali disco mwijaku.. akaenda kuanza upya udsm na akamaliza degree yake akiwa udsm..

Sasa mtu kasoma archeology unategemea aongee vitu gani vya msingi.. msimpe kiki simkubali ata nukta


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hapa nitashauri kama mpita njia
1. Elimu ya chuo kikuu ni pana sana, mwanachuo hapaswi kutegemea madesa ya darasani pekee. Mkufunzi akishadodosa kidogo ni jukumu lako kwenda deep kupitia vitabu vya maktaba na tutorials nyingine mitandaoni.
WANACHUO MSIPOTEZE MUDA KWENYE KUTAZAMA SERIES NA PORNO.

2. Si ajabu kumkuta mwanachuo wa mwaka wa mwisho anaesomea ualimu hana notes za kufundishia, kila alipokuwa akienda field anabeba daftari lake la O'level alilosomea miaka mitano iliyopita anaenda kuwafundishia vijana, yaani hana muda wa kuboresha kile cha zamani kwa kuzingatia kuwa sasa ameelimika. Hili haliitaji mkufunzi akwambie, linahitaji utashi wa mtu mmoja mmoja, kama huna, huna.

3. Si ajabu kumkuta mwanachuo anaesomea engineering, IT, electronics n.k katika laptop yake ana software nyingi za games kuliko za fani yake. Unamuuliza mwanachuo wa mwaka wa pili anaengia watatu wa fani ya IT kama anajua kutumia framework yoyote katika kutengeneza tovuti, anakuuliza framework ndio nn?
Huyu ni mwanachuo ambae akishafundishwa kile cha darasani ndio kamaliza hatoki nje ya box. Hajihangaishi kujua duniani wataalamu wa fani yake wanatatua changamoto kwa mtindo upi wa kisasa.

4. Maisha magumu ya wanachuo nayo pia yanachangia kupunguza umakini. Si ajabu kumkuta mwanachuo hana laptop, hana smartphone yupo yupo tu na madesa yake, unategemea nini hapo, mkopo wenye asilimia 30, ndugu wanamtegemea, bata hapohapo, aishi kichuochuo, halafu unategemea awe mbunifu, aaa wapi.

5. Chuo kuna katabia kakuaanda project mwaka wa mwisho, project ziwe kila semester, japo ndogondogo, ili mwaka wa mwisho atutengenezee kilicho bora kabisa. Hii system ya sasa inawafanya wazubae zubae sana.

Mpita njia nipo kwenye kimbweta saa hii, nitashuka cafteria ya yombo muda si mrefu niende zangu changanyikeni.
Ciao.
Hiyo no nne inaweza kuwa sababu kubwa inayowagusa wengi.


Kusema ukweli umaskini unachangia hata mwanafunzi kutofanya vzr .



Watu wako mwaka wa pili au wa tatu hawana pc na kama anayo uwezo mdogo.
Wazazi wengi hata ukipata kaboom asilimia 30 wanakuacha na kama ni mwanaume wazazi ndo kabisa wanakutuma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Issue ni mtaala wa elimu ya Tanzania na Africa kwa ujumla umeshindwa kutatua matatizo yetu yanayotukabiri , zaidi ya 60% ya waadhiri na maprofesa wa UDSM PhD zao na Masters zao wamesomea ng'ambo kule tunapoamini elimu yetu ndo ilipochimbuka na wanafaulu vizuri tu kwa grade nzuri, wanaudhuria international conference wanapresent papers kwenye journal za dunia na zinakuwa published . Me binafsi sioni cha kuilaumu UDSM bado is doing better kwenye its core activities of teaching,consulting and Researching. Swala la elimu ni sera ya nchi kuamua itoe elimu ya aina gani kwa ajiri ya manufaa ya wananchi wake. Pia wanafunzi nao inapaswa wajiongeze waende xtra mile thats y ikaitwa "universe" sehemu ya kutafuta maarifa sio kushinda mlimani city na survey unazurura na kuvaa skin jeans, unangoja lecturer akufundishe namna ya kutengeneza app. Unasoma Public admimistration hujawahi hata kuwa kiongozi wa jumuia ya mtaani kwako, utaongozaje watu ukimaliza.Unasoma sheria hujawahi hata kwenda Kisutu kuangalia kesi zinaendehwaje. Tusikurupuke kukishambulia Chuo kuna mambo mengi ya kufanyia kazi. Ni sawa na kusema kwanini Kanisa Katoliki lipo lakini bado dhambi zinaendelea
 
- Miaka inaenda tu na kila mwaka wanachukua vijana wetu wanaojiweza sekondari lakini wanaturudishia uozo. Unakuta mtoto alikua ana akili kweli lakini akimaliza chuo anaanza kuongea pumba, ooh mara " nataka nianzishe kampuni yangu ya software" " nataka nitoe semina ya madini", " nataka niandae semina ya ujasiriamali", ushenzi na uzuzu tu.

- Wakati sisi tunawapeleka watoto pale tunasema mtoto anaenda mlimani, atatoka na kitu pale, kumbe anaenda kutoka na maongezi. Ndio maana hata watu wa taaluma kubwa za sayansi kutoka UDSM wanaishia kuwa wanasiasa. Chuo kimejaa porojo mno.

- Hivi unajua Mwijaku alikua mwanafunzi wa UDSM? that fat fuk should've been the one helping our film industry but he is dying with it. Yani chuo kinachoaminiwa na watanzania wote kinashindwa kuzalisha hata waigizaji wazuri. UDSM ndipo walipotakiwa kutoka first grade Creative writers lakini asilimia 98 ya vitabu vyote vipya Tanzania vinahusu ujasiriamali au ni catalogue za bidhaa mbalimbali. Upumbavu juu ya upumbavu.

- Wazazi hatupendi vijana wetu wawe wanasiasa, tunapenda vijana wetu wawe na taaluma zinazoeleweka.

- UDSM imejaa misifa tu na hamna la maana linalofanyika.

- Chuo kikuu kikubwa kama kile hamna independent course ya Robotics, huwezi kutengeneza lolote miaka hii ya sasa hivi bila kuwa na elimu ya Robotics. Lakini UDSM hamna.

- Kwanini tusichukue waalimu wa nchi za nje walioendelea kielimu kuja kutusaidia kufundisha? ( nchi kama Ujerumani, Uingereza, Norway na Marekani). Tumejaza wasakatonge kama wakufunzi pale badala ya wataalamu. Mtoto anatoka CoICT hata basic commands za Linux hajui.

- Muda umefika wa serikali ya wanafunzi kukomalia taaluma inayotolewa pale, sio kila siku wanafunzi wanagombana na serikali kuu, tafuteni elimu inayoeleweka. Ukiwa na Cheti cha Geology kutoka UDSM halafu huna ajira wewe maisha yako ndio yameisha hivyo lakini haitakiwi kuwa hivyo. Wanafunzi lilieni elimu, mnatoka pale na uwezo mdogo tofauti na matarajio.

Mpaka leo hatuna kampuni binafsi ya mtandao wa simu ya kitanzania, zote zilizopo ni subsidiary ya kampuni za nje, na UDSM ipo tu miaka inaenda. Amkeni serikali ya wanafunzi, chuo kutafute waalimu competent na mazingira yawe wezeshi kusaidia kua na utaalamu wa hali ya juu kabisa kwa kozi husika.
Mliokosa nafasi za kujiunga na UDSM huwa mnakuwa na kahasira ka chini chini
 
Nilisoma udsm na ulo ongea ni kweli kabisa. Ila naona sio udsm pekeee ila ni ugonjwa wa vyuo vyote vya Tanzania sema umelenga Udsm kwani ndo tulipoweka imani ni chuo bora kwa Tz.

Katika vitu nilivyo laumu ni kusoma hadi na maliza hakuna mahali tulipo hitajika kusoma ujasiriamali au kompyuta japo ni Mwalimu wa Sayansi.

Laiti sio kujiongeza kwangu ningetoka mtupu kwenye hayo maswala. Yaaani Elimu yetu imeshindwa kufikiria mbele miaka kumi ijao kuwa dunia itakuwa wapi. Kama umesoma shule za serikali hadi unaingia chuo Kikuu niseme tuu ukweli una hasara sehemu flani katika Maisha hasa kwenye zama hizi. Maana utaambulia kuwa na hiyo Elimu ya makaratasi na vyeti.

Na ujinga mwingine ni wanafunzi wengi kujiskia hasa kipindi wako chuo ,Wanaona kama ndo maisha yameisha hata hii ni kwa wanachuo wote tuu wakishafika chuo duuuh kuna ka kiburi flani hivi kwa wale hawajasoma au kufika na wakiamini maisha ni simple wakishamaliza.

Nilikataa huoo ujinga hasa nilipo kosaga mkopo nikajiongeza ili niweze kujisomesha.. Utamkuta mwanafunzi kavaa likamba la Udsm Student hadi kariakoo ilimradi mumjue anasoma wapi.
Chuo kikuu siyo sehemu ya kuzalisha wachuuzi ni sehemu ya kuzalisha professionals.

Ukienda chuo kikuu hauendi kufundishwa namna ya kuganga njaa unafundishwa kufikiri.

Suala la kutumia hiyo elimu yako linabaki kuwa kwako mwenyewe na siyo kwa chuo.

Watu wanaolalamikia vyuo vikuu ni wale waliofika vyuo vikuu kwa kubahatisha na wakasoma course bila kujua baada ya chuo watakuwa kina nani na kwa sababu gani.

70% ya wanafunzi wa elimu ya juu husoma course ambazo hawana passion na malengo nazo sana sana huzisoma kwa sababu ya kukosa sifa fulani fulani katika course wanazozipenda au pressure kutoka kwa wazazi na ndugu waliosoma hivyo mtu wa namna hii hawezi akajua strength na weakness zake kwenye taaluma husika anayoisomea.

Africa inachangamoto nyingi sana ambazo hazihitaji elimu ya ujasiriamali kuziona kama ni fursa tatizo wanafunzi wengi kwenye universities wako brainwashed kutoka majumbani kuwa wakimaliza kusoma watapata ajira na kuwa matajiri, hiivyo wengi husoma siyo kwa lengo la kupata elimu bali kwa lengo la kupata daraja la kupata ajira.

Mentality kama hii ipo kwa walimu wetu huko mashuleni na kwa wazazi wetu ukimaliza chuo ukaanza mishe zako usipopata kazi unakuwa labled kwamba ulifail bila kujali passion yako.

Najua elimu ya ujasiriamali ina mchango wake katika kufanya vijana wajitegemee lakini msingi mkuu ya ujasiriamali ni taaluma uliyoisomea and your business mind tu.

Tuache kulalamika tuendelee kupambana elimu yenye misingi ya ujamaa haiwezi kuzalisha ujasiriamali badala yake huzalisha ujasiriajira tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tapishana nawewe kidogo. Shule za english medium sio kwamba zinatengeneza products za kjja kujiajri ila wao huwa wanafocus zaidi katika kupata good examination results good caring of pupils basi.

Tatizo lipo kwenye mtaala wetu.

Tatizo lipo pale pale. Hata hao wa english medium mtaan wana hangaika tuu kujiajiri awawez

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati mwingine wanasiasa wamefanikiwa kuwabrainwash wanafunzi wetu kuwa wanatakiwa wajiajri halafu wawaajiri hao wanasiasa wanaowaambia wajiajiri.

Msingi mkubwa wa ujasiriamali ni mtu husika na siyo elimu ya ujasiriamali utakayopewa.

Mtu yeyote anayejitambua kuwa anapaswa kula kwa kutumia taaluma yake lazima atajua taaluma anayosomea inachangamoto zipi katika soko la ajira na yeye atakabiliana nazo vipi au ataweza vipi kutumia taaluma yake kupata kipato.

Tatizo letu vijana wa leo tunataka chuo kitupe na elimu on how to make money, this is wrong vyuo vikuu havizalishi wachuuzi vinazalisha professionals how to make money is up to a professional siyo chuo tena.

Mathalan Mark Zuberck alipata wapi elimu ya ujasiriamali mpaka kuanzisha facebook ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom