pandagichiza
JF-Expert Member
- Jul 9, 2013
- 4,643
- 3,020
Tatizo siyo shule wala vyuo, tatizo ni wanafunzi wenyewe. Hata uwapeleke Havard au Stanford university wakirudi Tanzania wanakuwa sawa na wengine tu, hakuna tofauti.
Ndiyo maana nilisema universities siyo sehemu ya kuzalisha wachuuzi ni sehemu ya kuzalisha professionals.Mtoa Mada Naunga mkono hoja. Ngoja na mimi nitie Neno.
Kuna Hawa The So Called walimu wa ujasiriamali Hawa ndo wanatupotosha Sana Vijana. Wanainstill fear kwa Vijana Kisha wanawapiga ela kwa kuwaambia watawafundisha Sijui huo ujasiriamali.
Mwanafunzi hajui ashike kipi masomo au Huo Ujasiriamali. Unakuta Mtu anasoma Political Science lakini ukimuuliza hata Nancy Pelosi Ni Nani Hata Hamjui since most of the time anawaza mradi Wake wa Sabuni aliouanzisha. Anawaza Masoko, Sasa Kama ingekuwa hivo si ungesoma tu kozi Ya Ujasiriamali moja kwa moja. Hapo Kashaambiwa political science haina soko bora uchangamke.
Sasa with that hatuezi kupata Real Experts wanaofaam vitu kwa Undani kwa sababu mwanafunzi kajigawa Mara Mbili. Kashajazwa sumu na motivational speakers.
Akimaliza Chuo Ufaulu wa kawaida au GPA haisomi hata huo mradi wenyewe wa ujasiriamali ambao ni very irrelevant na anachosomea mostly unakuwa haupo Tena.
Kakosa vyote.
Badae ndo anaanzisha nyuzi Humu jukwaani za kusema elimu haisadii kumbe hakuwa collected.
Motivational books na Pseudo Enterpreneurship inareplace our education.
Hiyo ni moja ya sababu, mambo ni kibao.
Iko vizuriUmeongea ukweli mtupu hali ya vyuo ipo hoi.
Lakini utailaumu UDSM bure tu, tatizo linaanzia elimu ya msingi. Watoto wakiwa wadogo hawawekewi msingi mzuri wa kudadisi na kuwa wabunifu mwanzoni kabisa wa safari yao ya elimu. Hata hao mnaowasifia wamesoma English Medium hakuna jipya kule wanameza tu notes na kukaririshwa vitu kibao ilimradi wafaulu mitihani na sio iliwajifunze namna ya kujifunza.
Kama kuna mtu amewahi kusoma mtaala tofauti na huu wa Kitanzania hasa hasa level ya msingi utanielewa ninacho ongelea. Kule mtoto akiwa mdogo anafundishwa namna ya kujifunza, anafundishwa namna ya kufanya brainstorming tangia akiwa standard 3 ili ajifunze mapema namna ya kujiongeza na kuweza kupata mawazo mapya.
Ukikosea kwenye msingi hata aende wapi hata afaulu vipi mtarudi tu kulalamika kuwa watu hawana ubunifu.
Mfano wa haraka ni baadhi ya mawaziri na viongozi waliosoma vyuo vikuu vya nje vikubwa tu lakini bado tunawalalamikia kwamba upeo wao ni mdogo. Sababu ni kwamba msingi wao ni mbovu.
Kurekebisha elimu ya Tanzania ni kufumua kabisa elimu ya msingi ili iwe ya msingi kweli na siyo kuwamezesha watoto wadogo notes na concepts za kutosha ambazo kimsingi hazimsaidai chochote kwa huo umri sana sana zinamdumaza kifikra mpaka kaburini.
Ni kweli vyuo vyetu vinashida kubwa sana lakini wanaokwenda pale wangekuwa tayari wana msingi mzuri wangeweza kuzikabili hizi changamoto na kuzishinda.
Inatoa mkuu, hgl na related comb , o level 3 , high level 1
Huo Ni ukweli mtupuKitu pekee ninachokipata kutoka katika bandiko lako ni kuwa mfumo mzima wa elimu yetu ni hohehahe, uko taabani na haujielewi. Umekitaja UDSM lakini tatizo lipo vyuo vyote vya umma (nataja umma maana sina uzoefu na vyuo binafsi).
Wanafunzi wanaomaliza katika vyuo vyetu (kadiri miaka inavyozidi kwenda) wanazidi kuwa watupu vichwani.
Wacha niweke mambo machache ya kuonesha tulipo sasa (kwa uzoefu wa vyuo vinne; UDSM, UDOM, SUA na Mzumbe).
1. Mhadhiri asipoingia darasani wanafunzi hufurahi
2. Mhadhiri akikazia wanafunzi waelewe (mfano mhadhiri akitumia seminar classes vilivyo huwa anachukiwa na wanafunzi. Na inaweza kwenda mbali kwa wanafunzi wa sasa wakakutengenezea zengwe. Ikumbukwe lecture classes mhadhiri huzitumia kutoa mhadhara wa somo, na seminars kama kupata mrejesho kutoka kwa mwanafunzi).
3. Mhadhiri anayerahisisha mambo "laissez-faire", yaani hatoi kazi kwa wanafunzi, anagawa marks hata pasipo usahihi, ndiye hupendwa na wanafunzi.
4. Ni kosa mwanafunzi kupata marks kidogo hata kama mhadhiri katumia vipindi vyote kwa usahihi. Wanafunzi wa sasa "usiingie darasani lakini toa marks"
Kiufupi elimu ya sasa ni ya marks zaidi kuliko uelewa/maarifa. Nina mifano mingi ya wahadhiri katika vyuo tofauti kuingizwa vikaangoni kutokana na zengwe zinazotengenezwa na wanafunzi.
Nimalizie kwa kusema, elimu ya dunia ya sasa ni maarifa. Inatakiwa hadi mwanafunzi anafika chuoni awe amekwishajua anachotaka kufanya maishani, ajue ni nini anadhani anakikosa (atakapoenda kuanza kukifanya hicho anachotaka) na anadhani kwenda chuo kitasaidia yeye kukipata.
Elimu ya msingi na sekondari inatakiwa iwaandae wanafunzi kwenye hili (tubadili mitaala, na sio kuikumbatia mitaala ya zamani wakati Dunia inazunguuka). Inatia ukakasi sana, hata humu JF huwa naona, mtu kamaliza sekondari anaomba ushauri akasome nini chuoni.
Ni kweli mm ni wa ovyo sana kwa kuwa sikujui na hunijui ila nacho shukuru ujumbe umeuwelewa ma ukaukubali.Muandiko siwaji kutamani kuandika vizuri kwa kuwa sijawahi kumpata aliefanikiwa kwa muandiko.Maisha mema na yenye furaha mpendwaKwamba wewe ni Mwalimu wa shule ya msingi, ulianza na ‘chert’ ila sasa unatafuta ‘shahada’ ya pili... je bado unafundisha shule ya msingi..?
Mkuu wangu nimevumilia sana mwandiko wako mbovu kwa kuheshimu taaluma yako, ila ulivyoandika humo kama kweli wewe ni Mwalimu basi ni wa hovyo sana... ujumbe uliokusudia ni dhahiri ila umeunajisi kwa kujipa sifa za Kihaya mwanzoni kabisa.
Good Friday.
Mzumbe ali disco mwijaku.. akaenda kuanza upya udsm na akamaliza degree yake akiwa udsm..
Jamaa kumbe alidisco halafu uwa anajifanya interlectual kishenzi